Nimetelekezwa na ujauzito, natafuta kazi

Nimetelekezwa na ujauzito, natafuta kazi

Joined
Jun 26, 2023
Posts
64
Reaction score
158
Watu wa Mungu mpoo?

Mimi ni member wa JF tangu miaka ilopita nimekuja na ID tofauti ili nieleze yaliyonikuta iwe funzo na ushuhuda kwa wengine.

Niliweka post hapa mika ilopita na kwa bahati tu sijui niseme nzuri au mbaya ila Mungu ndio anajua, nikapata mwanaume ambaye tulianza mahusiano ambayo yalikuwa siriazi kidogo.

Baada ya muda tukapanga mipango ya kuanza mikakati ya kufunga ndoa. Na wakati huo huo ujauzito ukawa umeingia kwangu. Sasa tangu nilipomwambia yule mwanaume kuwa nina ujauzito aliniblock simu na namba zote mawasiliano hakuna. Hadi leo amenitelekezea ujauzito. Alichoniambia mara ya mwisho kabla hajanikimbia ni "wewe ulivyobeba ujauzito si ulijua unabeba ujauzito na sina pesa za kukutunza" kwa maana hiyo nipambane na hali yangu mwenyewe.

Kiukweli maisha kwangu yamekuwa magumu maana ujauzito umefikisha miezi saba na siwezi kufanya kazi nilokuwa nafanya hapo mwanzo. Daktari alinisahuri niachane nayo maana ni kazi ya kusimama zaidi ya masaa saba endapo nitapata wateja mfululizo.

Me nimeleta hili janga lilonipata ili tuendelee kuwa makini humu. Tusikurupukie watu sio wote ni wazuri kama tunavyodhani

Pia nimekuja kuomba kwa yeyote anayeweza kuniajiri kwa kazi yoyote ambayo sio ya kusimama muda mrefu kwa muda wa miezi hii mitatu ya mwishoni nina uhitaji wa kazi ili walao nipate pesa kwa ajili ya kujifungua maana sina msaada wowote wa kifedha wala vifaa vya kujifungulia. Sina matatizo yoyote ya afya hadi sasa yatakayonifanya nishindwe kuhuduria kwenye kazi hiyo nitakayoipata.

Kwa vigezo mimi ni mhitimu wa elimu ya kidato cha sita najua lugha ya kiswahili na kiingereza pia ninajua kutumia komputa vizuri. Naahidi kwamba atakaeniajiri hatajuta licha ya kuwa mimi ni mjamzito.

Mungu awabariki sana.
 
Fuata ushauri wa daktari dada. Hatua ya ujauzito wako na hali uliyonayo hutakiwi tena kufanya kazi za nguswanguswa!

Kwani huyo mvulana aliyekutwisha ujauzito, hajakutambulisha hata kwa dada yake mpaka mahusiano yenu yamemea yakashamiri kiasi cha kujiachia mpaka mimba ikaingia?

Haraka zako kwa huyo mvulana ndo zimekufikisha hapo. Sasa ikitokea hujapata kazi ya kukupush kwa muda uliosalia, watafute ndugu wa huyo chalii wape ukweli lau atatokea mmoja wao mwenye huruma atakusaidia.
NB. Mimba umesema ina miezi saba. Unataka kazi miezi mitatu, inamaana dokta kakwambia utajifungua baada ya miezi kumi...??!!
 
Me nimeleta hili janga lilonipata ili tuendelee kuwa makini humu. Tusikurupukie watu sio wote ni wazuri kama tunavyodhani
Usimchafue kijana wa watu sometimes nyie wadada mnaforce vitu ambavyo ni unreality kabisa km alishakwambia yy hawezi kulea mimba kwann wewe ukajiachia mwaah.. acha kutia watu ubaya!
 
Fuata ushauri wa daktari dada. Hatua ya ujauzito wako na hali uliyonayo hutakiwi tena kufanya kazi za nguswanguswa!
Kwani huyo mvulana aliyekutwisha ujauzito, hajakutambulisha hata kwa dada yake mpaka mahusiano yenu yamemea yakashamiri kiasi cha kujiachia mpaka mimba ikaingia?

Haraka zako kwa huyo mvulana ndo zimekufikisha hapo. Sasa ikitokea hujapata kazi ya kukupush kwa muda uliosalia, watafute ndugu wa huyo chalii wape ukweli lau atatokea mmoja wao mwenye huruma atakusaidia.
NB. Mimba umesema ina miezi saba. Unataka kazi miezi mitatu, inamaana dokta kakwambia utajifungua baada ya miezi kumi...??!!
Nitafanya kazi hadi hapo itakapofikia mwisho na ikitokea nimejifungua nitaendelea na kazi endapo kama bado nafasi itapatikana. Asante wangu
 
Kama unatumia ujauzito kama CV unadhani intaview itafanyikaje na wapi?. Ukipatia njoo ufanye interview kesho upate na kaz kabisa
Sijatumia ujauzito kama CV wangu. Ukiangalia thread vizuri Cv nimeandika mwishoni kabisa. Elimu yangu nimeiandika na vigezo vingine nitavieleza na kuvithibitisha kwenye interview..
Interview nitafanyia ofisi popote nitakapoelekezwa niende Sir Midabwada. Asante
 
Back
Top Bottom