Nimetoka ukweni Kigoma, ila kama hii ndiyo aina ya wazee acha wabaki na watoto wao!

Sio kila kitu Ni Cha kufuata kisa ni Cha zamani Kuna sababu gani ya kuozesha mwanao Kama unamuuza ,kwani lazima baba uwe mafia?tuache vingine vipite na wakati kikubwa tuwaombee watoto waishi kwa amani milioni 4 mahari ya mtu mmoja sio fair
Kumbe hujui hata maana ya mahari bure kabisa mahari ni shukrani kwa wazazi kwa kumtunza mwanamke ambaye ni mke wako
 
Nachojua umeambiwa utoe million 4 mahari ukaandaa uzi wa malalamiko nawakati hio ni case ya kawaida kwenye maisha hakuna jambo rahisi
Upuuzi mtupu, kama ulishindwa kukomaa ukiwa na nguvu basi komaa tu na uzee wenye stress, lakini sio stress zako unazimalizia kwa vijana wanaokuja kuoa kwako
 
Kumbe hujui hata maana ya mahari bure kabisa mahari ni shukrani kwa wazazi kwa kumtunza mwanamke ambaye ni mke wako
Wewe ndo hujui kitu sasa, hizo shukrani za kutunza zilikuwa mahususi wakati ambao mabinyi walikuwa wabakutwa wangali bikra, sasa unakuta mzee amefeli kwenye kulinda bikra za watoto wake halafu anataka kulazimisha mambo ya enzi za ubikra, inakaaje hiii???
 
Pole sana, makosa yapo pande mbili, kwako na kwa familia ya Binti. Makosa yalishafanyika kwako kuishi na binti wa watu bila kufuata utaratibu, hilo lilishapita. Mzee wa Binti ameshindwa kuling'amua Hilo, amesimamia kwenye misimamo ambayo itamfanya akose vyote. Inaonyesha Mzee Hana mtu anayeweza kumshauri, kama yupo basi hapo kwenye kikao hakuwepo.

Ushauri wangu, usije ukamwacha huyo mke wako kwa sababu ya mzazi wake mmoja. Inaonyesha wazi mama wa mke wako amechukia hicho kitendo, unaweza kujenga ukaribu naye akakusaidia baadhi ya mambo namna ya kuliweka jambo lako vizuri.

Tafuta kiasi cha mahari kile ulicho na uwezo nacho, wape wazazi wake. Endelea kuishi na mke wako na fuata taratibu za Sheria upate cheti cha ndoa.
 
Mwache mwanamke wa watu kama unamuogopa baba mkwe au kama una ona million 4 ni nyingi sio unakuja kulalami lalamika mambo magumu ni kwa ajili ya wanaume na sio wavulana
 
Upuuzi mtupu, kama ulishindwa kukomaa ukiwa na nguvu basi komaa tu na uzee wenye stress, lakini sio stress zako unazimalizia kwa vijana wanaokuja kuoa kwako
Mambo magumu ni kwa ajili ya wanaume na sio wavulana
Seriou unataka usikie maneno kama unaonewa, mara baba mkwe kakosea, mara achana nae maisha ni mapambano

Mwanaume ambaye sio mwoga wa maisha hilo ni jambo kama mwanamke hana shida, mama yake hana shida ni baba yake tu imetokea kutokuelewana alafu unaamua kuzira kuishi na mwanamke ambaye hana shida yeyote
Sasa ukiwa baba wa familia unaweza ipigania familia yako siku ukikutana na changamoto utaizira familia yako au kuisusa

Mwanaume akimbii changamoto anazikabili kwa ujasiri
 
Mwache mwanamke wa watu kama unamuogopa baba mkwe au kama una ona million 4 ni nyingi sio unakuja kulalami lalamika mambo magumu ni kwa ajili ya wanaume na sio wavulana
Huo uanaume wa kuumizana na kufurahisha wakwe ni wa kipumbavu!

Uanaume wa kutafuta pesa kwa ajili ya familia yangu (mke na watoto wangu) ni sawa kabisa!
 
Kwa upande wangu bado naona nafasi ya kurekebisha unayo!!

Binti anasema nini kuhusu wewe akiwa kwao?? Labda anakunadi wewe ni tajiri.

Tafuta wazee wa huko uwaelezee scenario wakusaidie kuongea nae.
 
Nimemshangaa sana jamaa kutaka kumkimbia mwanamke ambae anaonekana ni jasiri na mwenye kutumia akili na sio hisia kama jamaa.
 
Huo uanaume wa kuumizana na kufurahisha wakwe ni wa kipumbavu!

Uanaume wa kutafuta pesa kwa ajili ya familia yangu (mke na watoto wangu) ni sawa kabisa!
Swala sio kuumizana ndo maana unatakiwa ndoa ni kwa ajili ya watu ambao wako tayari kupambana

Nikusaidie watu wengi hayo mamahari yenye fugure kubwa wanalipaga tu sehemu wengi hawalipi yote kwenye maisha jifunze kutumia akili na sio hisia wewe ni wa kiume na acha tabia ya kuzirazira kila unapokutana na changamoto
 
Nimemshangaa sana jamaa kutaka kumkimbia mwanamke ambae anaonekana ni jasiri na mwenye kutumia akili na sio hisia kama jamaa.
Tukubali tunakizazi cha wanaume waoga sana ambao kila wakikutana na changamoto kidogo wanakimbilia kuzira au kususa
Somo la ujasiri ikiwezekana inabid ifundishwe huko mashuleni mtu anataka kufanya jambo pasipokuwa na changamoto yeyote ile ikitokea tu anasusa aiseeee
Yaan naisha sio marahisi hivyo
 
Hamna jambo lisilo na suluhu. Itafte uoe huyo mwanamke. Naamini ni bora sana kwako kuliko kuja kuanza moja hawa wala shisha. Utakuja kujutia kumwacha huk mbele,itunze hii msg.
 
Nipambane na changamoto za kuandaa maisha ya watoto wangu, then bado nipambane na changamoto za wazee wenye shari shari kama huyu, hapana!

Kwangu nadhani kuanzisha familia ni jambo la kheri, halipaswi kufanywa kama kutafuta kazi, kwamba unafanya interview na michujo ! Haifaiiii
 
Mkuu kataa kabisa unyonge wa kipumbavu. Na usijaribu kabisa kutoa million 4 kuhamisha mtu kuja kwako. Bora uwekeze milioni tatu halafu hiyo moja utafute pisi nyingine uoe. Kama huyo mzee anaendeleza itikadi za kipumbavu basi mwambie amuoe yeye huyo binti yake. Kutishiwa kurogwa sio rahisi, ni ngumu sababu wataloga baba wa mjukuu wao. Do you think what next mtoto anakua halafu aambiwe baba alirogwa na babu? Kama huyo mzee hatabadilika basi atamnyima haki mtoto wake wa kike ambae kiuhalisia anakupenda sana tu.
 
Kama changamoto ya mtu mmoja inakushinda ndo za maisha na purukushani za watoto utaziweza kweli
 
Iliwahi nikuta scenario kama hiyo hiyo mwaka 2018 ,japo nashukuru Mungu nipo na binti yao mpaka leo

Mzee ujinga aliacha siku hizi aliniheshimu
 
Kama changamoto ya mtu mmoja inakushinda ndo za maisha na purukushani za watoto utaziweza kweli
Hii sio changamoto ni upumbavu tu, yaani kama mtu anaweza kuona mimi n'a ndugu yangu kusafiri zaidi ya kilomita 1200 kutafuta undugu wenye nia njema kabisa kuwa ni upuuzi na kuamua kucheza na akili yangu kwa makusudi, halafu nijibembelezeshe kwa kuitazama kama changamoto, kwa kweli HAPANA!

Nampenda binti yao, nilifanya wajibu wangu kwa kadri ya uwezo wangu,mzee ameidharau dhamira yangu, basi nitamuacha mtoto wake, sio kwa sababu simpendi, ila kwa sababu sitaki kutengeneza familia yenye misingi ya ugomvi na udhalilishaji!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…