Nimetoka ukweni Kigoma, ila kama hii ndiyo aina ya wazee acha wabaki na watoto wao!

Kaka angu usimlipie mamilioni huyo mwanamke. Kama anakupenda kweli nendeni mkaishi tu. Hizi tamaduni za mahari ni tamaduni za kisheni. Na wanaume wengi hamstuki. Wenzako wamemla buuuure na wataendelea kumla pengine. Wewe unaenda kulipa mamilioni? Hebu amkeni.
 
We jamaa ni mpumbafu sana,unakaa na binti wa watu unamzalisha hovyo hujawahi kwenda hata kwao kujitambulisha halafu unataka wakuchekee,boya kweli wewe.
 
Unajaribu kuwatetea lakini unafahamu kabisa, kuna watu wanazalishwa na wenye watoto hawatumi pesa za malezi wala kwenda kujitambulisha!

Sisi kwa kujua kwamba hatujui mila na desturi zao, tuliomba mzee mwenyeji atuongoze, na tulipata pre information kwa mahari zao huwa hazizidi Milioni moja, tunajiandaa hivyo, na tulienda kwa nia njema!
That is why, mshenga wetu (ambaye ni mwenyeji wa huko) alishangaa kuona aina ile ya reaction, na mahari iliyotajwa, akasema wana lao jambo, na akasisitiza tuwe wapole ili tusimpe nafasi!

As long as tumeshatoka huko salama, basi ntalazimika kuamua tu, kama kurogwa basi nirogwe tu!
 
Huko ni walozi, utarogwa, na huyo binti atahakikisha anabeba mimba tena akukomoe.

Hayo majadiliano ujue walipanga na binti yao ambaye anaujua uchumi wako vizuri.

Tafuta tu hiyo hela, mengine utajua huko mbele
 
afu mahali milioni 4 huyo binti hatarudi kwao??? sema sishangai bro wangu alitajiwa mahali 6M akalia lia wakapunguza mpaka 4M[emoji23][emoji1787][emoji174][emoji174] mama angu ana hasira mpaka leo na hiyo pesa mwanae katajiwa[emoji119][emoji119]
Kabila gani hii?
 
Mfano wewe mtoto wako azalishwe bila ndoa itafurahia ? Na aje kuishi na mwanaume bila kumjua na aje kwako kujitambulisha na vizawadi vya kuwadanganya kama watoto au familia yenye dhiki sana.
Wewe ni mjinga, mtu kukuletea zawadi ni kudanganywa 🚮 au mtaonekana mnadhiki..?

Kuna watu waliacha kuoa kisa hayo mamilioni waliaga wakenda mazima
 

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ndo mana matatizo kama hayo yanawakuta watu wanaoweza kutatatua tu[emoji113] siku zote hasira hasara sasa atakaeteseka ni mwanao yani damu yako ety akiamua kunitafuta atanitafuta loooh[emoji28][emoji28][emoji706] hivii kabisa unajua una mtoto wako mahali hujui anakula nini analala vp unishi kwa amani kabisa kisa wamekutajia mahali bei[emoji1787][emoji1787] pesa inatafutwa mkuu tunaishi mpaka siku tunakufa tunatafuta helaa tuu[emoji119] ila ukiwa na mawazo ya kwamba sisi wote ni binadamu na yote yanapita wala hutateseka na vitu vya kijinga kama pesa[emoji174]
 
Kwa tabia na hiyo, nakuhakikishia watoto wako watazalishwa na hutokaa uone sura za waliowazalisha, achilia mbali kuwapiga makofi...
Utalea vijukuu visivyo na baba na cha kufanya hautakuwa nacho!

Yaani mtu kuja kuyajenga ili kurekebisha makosa unaleta upumbavu wa kujifanya una hasira nyingi?
 
Mpenzi wako ndio kakuchoma bro, siku nyingine uwe na akili uwo mchongo ni wa binti na wazazi wake ila kwakuwa love is blind unawaparua wazazi badala ya binti.
 
Mkuu kila jamii inatamaduni zake jaribu kujua hilo,mfano huyo binti uliye mzalisha angekuwa Mzanzibari leo hii ungeleta habari mbaya, yan ingekuwa umeenda Zanzibar cha kwanza ungewekwa mahabusu na kufunguliwa kesi ya kutorosha na kuishi na binti wawatu kutoka chini ya uangalizi wa wazazi na kesi ya kubaka na kumpa binti ujauzito kwa Zanzibar yake kukuta hayo.
 
Kwa hiyo kwa mtazamo wako sisi kutoka Dar mpaka Kigoma kwenda kuyajenga tulikuwa wapumbavu?
Ilikuwa busara kuona dhamira yetu na kuwa muungwana, ila kwa réaction aliyoonyesha atabaki n'a mtoto wake tu, siwezi kuwa n'a baba mkwe wa aina yake
Ama binti akaongee na wazazi wake, kuwa wewe HUNA HELA
 
Tafuta hela mkuu, Kigoma wala siyo mbali. Ni mwendo wa around saa mbili tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…