Nimetongozwa na Mwalimu wa kike

Nimetongozwa na Mwalimu wa kike

Bundakwetu

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2022
Posts
551
Reaction score
1,014
Habari zenu wakuu, leo nimerudi kutoka mishe mishe zangu za ufundi, ile nafika nyumbani baada ya watoto wangu kunipokea na kusalimiana nao mwanangu akaniambia baba Mwalim Joyce amesema ukifika umpigie anashida na wewe nikamjibu sawa.

Ikumbukwe mimi ninaishi na mabinti zangu wawili baada ya kushindwana na mama yao na mimi kuamua kumuachia mji na kuanza upya, sasa niliona baada ya kufanikiwa kuwahamisha shule toka kule Mwanza hadi hapa Morogoro na hawa ni watoto wa kike na niwadogo bado mkubwa ana miaka 11 na mdogo miaka 8 basi hapa shuleni wanaposoma kwa sasa nikaona ni bora niwakabidhishe kwa mwalim ambae anafundisha shule hiyo wanaposomea watoto wangu, na huwa anakuja hapa nyumbani kwa ajili ya kuwafundisha masomo ya ziada (Tution) na nilishamsimulia mkasa wangu na mke tuliyeachana na akanipa pole nyingi sana,

Nirudi kwenye mada sasa baada ya kumpigia kuwa nimeambiwa na watoto kuwa nikifika nimpigie nikafanya hivyo na Madam kaja kwakweli amefunguka mwanzo mwisho kuwa ananipenda na yupo tayar kuanzisha mahusiano na ikibidi tuoane kabisa, yeye ni mwenyeji wa Lindi na ni muajiriwa wa serikali Mwalimu na hajazaa na hana mume wala mchumba, kiukweli sijampa jibu nimemwambia ngoja nitafakar kwakuwa sina hamu tena ya kuoa kwa sasa, na amesisitiza kuwa hawa watoto wangu wanahitaji malezi ya mama ambae ni yeye kiukweli nipo njia panda sijampa jibu la ndio au hapana, ila kiujumla yeye na watoto wangu wako vizur sana sijajua nimkubalie au vipi na Madam ananiambia ananitegemea nitampa jibu zuri nipo njia panda sijajua nimjibu nini Madam.
 
Mkuu kwanza pole sana. Huyu mwanamke hana nia mbaya na watoto wako. Ameona nafasi ipo wazi angeweza kumtongoza mwanaume fresh asiye na watoto. Nakushauri fikiria nenda naye kwa makini kwanza kama mpenzi hata mchunguze mwaka hivi kama ukiona watoto wanampenda basi muoe
 
Usijaribu...weee. Pona na kaa vizuri kwanza. Jijenge, simamia watoto wako mwenyewe. As long as umetoka kutengana na mwanamke na huyu nae ni mwanamke. Utakaribisha drama na hiz zitakumaliza maana kazi ya kudeal na mwanamke mwngne mpya na akuletee visanga akati wewe tayari umevikimbia huko..nehii. Afu kwa sabbu amejua mapito yako anataka kwenda na upepo. Jitafute upya ndo uanze kuwaza sketi.
 
Vipi nae akizingua utamuachia Kila kitu!?maana ni given kuwa mtakuja tofautiana
Anyway sikiliza moyo wako fanya maamuzi ikiwa utamuoa basi chukua watoto wako peleka kwa bibi Yao we na yeye anzisheni familia yenu ila kusema atapenda watoto wako never!!!
 
Wapo my dear. Nimewaona kwa macho yangu. Hawezi kuwapenda kama kawazaa lakini kama mzazi na mlezi wapo wanawake wanaoweza. Sema asilimia kubwa ni wale wa kizazi cha kuanzia 79 kurudi nyuma. Very few though.
So long as ni "very few" basi ni kusema hakuna nami nasema hakuna kabisa kuwaolea watoto mama mpya ni kuwatesa
 
Habari zenu wakuu, leo nimerudi kutoka mishe mishe zangu za ufundi, ile nafika nyumbani baada ya watoto wangu kunipokea na kusalimiana nao mwanangu akaniambia baba Mwalim Joyce amesema ukifika umpigie anashida na wewe nikamjibu sawa. Ikumbukwe mimi ninaishi na mabinti zangu wawili baada ya kushindwana na mama yao na mimi kuamua kumuachia mji na kuanza upya, sasa niliona baada ya kufanikiwa kuwahamisha shule toka kule Mwanza hadi hapa Morogoro na hawa ni watoto wa kike na niwadogo bado mkubwa ana miaka 11 na mdogo miaka 8 basi hapa shuleni wanaposoma kwa sasa nikaona ni bora niwakabidhishe kwa mwalim ambae anafundisha shule hiyo wanaposomea watoto wangu, na huwa anakuja hapa nyumbani kwa ajili ya kuwafundisha masomo ya ziada (Tution) na nilishamsimulia mkasa wangu na mke tuliyeachana na akanipa pole nyingi sana, nirudi kwenye mada sasa baada ya kumpigia kuwa nimeambiwa na watoto kuwa nikifika nimpigie nikafanya hivyo na Madam kaja kwakweli amefunguka mwanzo mwisho kuwa ananipenda na yupo tayar kuanzisha mahusiano na ikibidi tuoane kabisa, yeye ni mwenyeji wa Lindi na ni muajiriwa wa serikali Mwalimu na hajazaa na hana mume wala mchumba, kiukweli sijampa jibu nimemwambia ngoja nitafakar kwakuwa sina hamu tena ya kuoa kwa sasa, na amesisitiza kuwa hawa watoto wangu wanahitaji malezi ya mama ambae ni yeye kiukweli nipo njia panda sijampa jibu la ndio au hapana, ila kiujumla yeye na watoto wangu wako vizur sana sijajua nimkubalie au vipi na Madam ananiambia ananitegemea nitampa jibu zuri nipo njia panda sijajua nimjibu nini Madam.
Nenda karipoti kwenye vyombo husika huo ni unyanyasaji wa kijinsia mkuu fanya haraka
 
Back
Top Bottom