Mwachiluwi
JF-Expert Member
- Mar 10, 2022
- 25,258
- 48,589
“Naanzaje kukataa Joshua? Nipo tayari uniowe hata kesho. Nikikumbuka jinsi tulivyokutana moyo wangu unajawa na furaha na amani sana. Nakupenda pia Joshua” Alisema Noela kisha alimkumbatia Desmond.
Sura ya Desmond ilibadili taswira kutoka kutabasamu hadi kuwa mtu aliye siriazi na jambo lililo akilini mwake.
Majukumu ya kazi yaliendelea kwa pande zote yaani kwa Desmond na kwa upande wa Noela, kumpata Desmond kulimpa furaha sana Noela akawa anachapa kazi zake.
Mchana wa siku hiyo, Desmond alienda Hospitalini kama kawaida, alipewa nafasi ya kumuona Mke wake Mandy. Alikuwa na hasira na Mwanamke huyo. Mandy alikuwa amepoteza fahamu kwa zaidi ya miezi mitano hivyo kwa kipindi chote alikuwa Hospitalini tu, Desmond alisogea akaketi kwenye kiti kimoja ambacho kilikuwa kando ya kitanda cha Mke wake, alikunja nne kisha akamwambia Mandy
“Nina uhakika unanisikia Mandy! Katika vitu sitamani kuona katika Maisha yangu basi ni uhai wako, natamani uwe umekufa na usiamke tena hapo Kitandani” Alisema Desmond akiwa amevalia suti nyeusi zilizomkaa vizuri, alikuwa kijana mwenye muonekano mzuri sana. Desmond alisimama kisha alimsogelea Mandy
“Siri unayoijuwa kuhusu Mama yako ibaki kuwa siri ya Ulimwengu mzima, sipo tayari kuyaharibu Maisha yangu kwasababu yako. Asante kwa utajiri mkubwa ulioniachia Mandy, nasikitika sababu uliyemuamini siku zote hakuwa na mapenzi na wewe, sikuwahi kukupenda Mandy….Nilizipenda pesa zako tu” Alisema Desmond kisha alivuta pumzi zake huku chozi likimlenga, licha ya uamuzi huo mgumu bado alionesha kuumia ndani ya Moyo wake
Ghafla aliona Mandy akitingisha kidole, hii ilimshtua sana Desmond, miezi yote Mandy hakuwahi kutingisha hata kope za macho yake, ilionesha wazi hata alichokizungumza Desmond alikuwa akikisikia. Akiwa anaendelea kushangaa Desmond aliona macho ya Mandy yakifunguka huku yakibubujikwa na mchozi, Mandy alikuwa ni Mwanamke mzuri mwenye weupe wa asili, chozi la Mandy lilionesha wazi kuwa lilibeba maumivu makali sana
“Mandy umeamka? Ina maana siri yangu utaisema!! Hapana Unakufa” Alisema Desmond ndani ya moyo wake huku akiwa amevurugwa sana, aliangalia huku na kule kisha alichukua mto na kumziba pumzi Mandy ili afe pale kitandani. Mandy alihangaika kwa nguvu chache aliyokuwa nayo lakini hakuweza kufanya lolote zaidi ya kuziona pumzi zake zikifika mwisho, Desmond alidhamiria kumuuwa Mandy mchana huo ili hiyo siri yake isijulikane.
Mara Desmond alisikia chupa ikivunjika, alipogeuka alimuona nesi Lucia akiwa anaokota vipande vya vyupa pale mlangoni. Haraka aliacha jaribio la kutaka kumuuwa Mke wake Mandy. Aliuweka mto pembeni, alikuwa akitokwa na jasho jingi kisha alimtazama Mandy alionekana kuzima, Desmond aligeuza macho alimuona nesi Lucia akisogea hapo
“ooh Desmond” Alisema Nesi Lucia huku akiwa anaweka vifaa juu ya meza iliyo pembe ya ukuta, alipomtazama vizuri Desmond alimuona akiwa anatokwa na jasho jingi sana, alishangaa kisha alipeleka macho yake kwenye AC, kisha alirudisha kwa Desmond. Alionekana kushangaa jasho la Desmond lilitoka wapi ikiwa chumba hicho kilikuwa hakina joto kabisa
“Kulikoni Desmond mbona unavuja jasho hivyo” Aliuliza Nesi Lucia akiwa anamtazama kwa makini Desmond
“Aaah- aaah…Jasho….unajuwa!! Lucia sijisikii vizuri naomba nipumzike nje” Alisema Desmond kisha alitoka lakini Nesi Lucia aliendelea kujiuliza maswali yasiyo na majibu, mwisho alipuuzia jambo hilo.
Alienda kumtazama Mandy, alionekana kupowa huku mapigo ya moyo yakienda sawa kwa maana Desmond hakufanikiwa jaribio la kuondoa uhai wa Mandy, alibadilisha dripu na kufanya mambo mengine kisha naye alitoka. Hali ya Mandy haikujulikana kwa wakati huo kuwa ataamka lini wala saa ngapi laiti kama taarifa ya kuamka kwake ingewafikia madaktari basi tumaini lingekuwa kubwa sana.
Akiwa nje ya wodi ile, Desmond aliendelea kutafakari kuhusu usalama wa Mandy, alifikiria kama Mandy alikuwa amekufa au alikuwa hajafa na kama hajafa basi siri yake iliyojificha kuhusu Mama yake Mandy ingefichuka, akiwa hapo alisikia sauti ikimuita
“Mr Desmond” Alipogeuka alimuona Mtu mmoja akiwa amemsimamia, alishtuka sana sababu hakutarajia kumuona Mtu huyo kwa wakati huo
“Mbona umeshtuka au hukutarajia kuniona?” Alihoji Mtu huyo aliyekuwa Mwanaume mwenye sauti nzito
“Hapana ila nilikuwa mawazoni ndiyo maana nimeshtuka” Alisema Desmond kisha aliketi vizuri ili Mwanaume huyo naye aketi
“Hali ya Mkeo vipi?” Aliuliza Mwanaume huyo
“Mke wangu anaendelea…Hali yake bado ipo vile vile” Alijibu Desmond
“Mkeo ni shahidi namba moja wa kifo cha Mama yake, mara ya mwisho alituma ujumbe kituo cha polisi kuwa anamjuwa Muuwaji wa Mama yake, baada ya hapo ndiyo tukio la wewe kupigwa risasi na Mke wako kupigizwa ukutani lilipotokea, Mkeo ni Mtu muhimu zaidi katika kesi ile” Alisema Mwanaume huyo ambaye sasa alitambulika kuwa ni askari
“Yaah! Ni kweli, ilikuwa ni siku ngumu sana katika Maisha yangu ni kama nilimpoteza Mke wangu tokea siku ile hadi hivi leo” Alijikakamua Desmond kisha alijibu, huyu Desmond alionekana wazi kutambua juu ya kifo cha Mama yake Mandy lakini kwanini hakutaka ukweli uwekwe wazi? Au yeye ndiye aliyemuuwa Mama yake Mandy? Kwanini Amuuwe? TUSONGE MBELE
“Kwa lolote usisite kutujulisha Mr. Desmond” Alisema Askari huyo kisha aliondoka hapo. Kumbe nesi Lucia alikuwa anamuangalia Desmond akizungumza na polisi kisha alipoondoka yeye alimfuata Desmond alipokaa
“Desmond najuwa unavyojisikia, najuwa unaumia sana lakini Mkeo atakuwa sawa tu siku moja mtarudi kuwa kama zamani” Alisema Nesi Lucia, Desmond alimtazama Lucia kisha alijisemea moyoni
“Ungejuwa ninavyotamani afe wala usingesema hayo maneno” Kabla hajamjibu chochote Lucia alipokea simu ya Noela
“Hello” Alisema Desmond baada ya kupokea simu hiyo
“Desmond nakusubiria Mgahawani” Alisema Noela kisha Desmond alijibu
“Sawa nakuja”
“Unaenda wapi?” Alihoji Lucia
“Mjini”
“Hata mimi ninaenda huko kwa ajili ya chakula, tafadhali nipe lifti” Alisema Lucia
“Haya sawa!” alisema Desmond kisha waliongozana hadi kwenye gari ya Desmond na safari ya Kuelekea Mjini ilianza.
Wakiwa barabarani Nesi Lucia macho yake yote yalikuwa kwa Desmond, alimpenda sana Mwanaume huyo lakini alishindwa kumwambia sababu alikuwa Mume wa Mtu istoshe alikuwa akimuuguza Mke wake huyo.
Desmond aligundua hilo akamuuliza Lucia
“Kwanini unaniangalia hivyo?”
“Desmond wewe ni Mzuri sana, Hakika Mke wako anajivunia kuwa na Mwanaume kama Wewe” Alisema Lucia kisha Desmond alitabasamu kidogo alafu hakusema chochote kile hadi anafika eneo ambalo Lucia alikuwa akienda. Ilikuwa ni kwenye mgahawa huo huo ambao Desmond alienda kukutana na Mpenzi wake Noela
“Eeeh ajabu kumbe nawe ulikuwa unakuja hapa?” Aliuliza
“Yaah! Kuna Mtu naonana naye mara moja kisha niendelee na majukumu mengine”
“Haya asante kwa Lifti” Alisema Lucia kisha alishuka akaingia kwenye mgahawa huo ambao ulikuwa wenye hadhi kubwa na pia ulikuwa mkubwa mno, Desmond alienda mahali ambapo alipanga kuonana na Noela.
Sura ya Desmond ilibadili taswira kutoka kutabasamu hadi kuwa mtu aliye siriazi na jambo lililo akilini mwake.
Majukumu ya kazi yaliendelea kwa pande zote yaani kwa Desmond na kwa upande wa Noela, kumpata Desmond kulimpa furaha sana Noela akawa anachapa kazi zake.
Mchana wa siku hiyo, Desmond alienda Hospitalini kama kawaida, alipewa nafasi ya kumuona Mke wake Mandy. Alikuwa na hasira na Mwanamke huyo. Mandy alikuwa amepoteza fahamu kwa zaidi ya miezi mitano hivyo kwa kipindi chote alikuwa Hospitalini tu, Desmond alisogea akaketi kwenye kiti kimoja ambacho kilikuwa kando ya kitanda cha Mke wake, alikunja nne kisha akamwambia Mandy
“Nina uhakika unanisikia Mandy! Katika vitu sitamani kuona katika Maisha yangu basi ni uhai wako, natamani uwe umekufa na usiamke tena hapo Kitandani” Alisema Desmond akiwa amevalia suti nyeusi zilizomkaa vizuri, alikuwa kijana mwenye muonekano mzuri sana. Desmond alisimama kisha alimsogelea Mandy
“Siri unayoijuwa kuhusu Mama yako ibaki kuwa siri ya Ulimwengu mzima, sipo tayari kuyaharibu Maisha yangu kwasababu yako. Asante kwa utajiri mkubwa ulioniachia Mandy, nasikitika sababu uliyemuamini siku zote hakuwa na mapenzi na wewe, sikuwahi kukupenda Mandy….Nilizipenda pesa zako tu” Alisema Desmond kisha alivuta pumzi zake huku chozi likimlenga, licha ya uamuzi huo mgumu bado alionesha kuumia ndani ya Moyo wake
Ghafla aliona Mandy akitingisha kidole, hii ilimshtua sana Desmond, miezi yote Mandy hakuwahi kutingisha hata kope za macho yake, ilionesha wazi hata alichokizungumza Desmond alikuwa akikisikia. Akiwa anaendelea kushangaa Desmond aliona macho ya Mandy yakifunguka huku yakibubujikwa na mchozi, Mandy alikuwa ni Mwanamke mzuri mwenye weupe wa asili, chozi la Mandy lilionesha wazi kuwa lilibeba maumivu makali sana
“Mandy umeamka? Ina maana siri yangu utaisema!! Hapana Unakufa” Alisema Desmond ndani ya moyo wake huku akiwa amevurugwa sana, aliangalia huku na kule kisha alichukua mto na kumziba pumzi Mandy ili afe pale kitandani. Mandy alihangaika kwa nguvu chache aliyokuwa nayo lakini hakuweza kufanya lolote zaidi ya kuziona pumzi zake zikifika mwisho, Desmond alidhamiria kumuuwa Mandy mchana huo ili hiyo siri yake isijulikane.
Mara Desmond alisikia chupa ikivunjika, alipogeuka alimuona nesi Lucia akiwa anaokota vipande vya vyupa pale mlangoni. Haraka aliacha jaribio la kutaka kumuuwa Mke wake Mandy. Aliuweka mto pembeni, alikuwa akitokwa na jasho jingi kisha alimtazama Mandy alionekana kuzima, Desmond aligeuza macho alimuona nesi Lucia akisogea hapo
“ooh Desmond” Alisema Nesi Lucia huku akiwa anaweka vifaa juu ya meza iliyo pembe ya ukuta, alipomtazama vizuri Desmond alimuona akiwa anatokwa na jasho jingi sana, alishangaa kisha alipeleka macho yake kwenye AC, kisha alirudisha kwa Desmond. Alionekana kushangaa jasho la Desmond lilitoka wapi ikiwa chumba hicho kilikuwa hakina joto kabisa
“Kulikoni Desmond mbona unavuja jasho hivyo” Aliuliza Nesi Lucia akiwa anamtazama kwa makini Desmond
“Aaah- aaah…Jasho….unajuwa!! Lucia sijisikii vizuri naomba nipumzike nje” Alisema Desmond kisha alitoka lakini Nesi Lucia aliendelea kujiuliza maswali yasiyo na majibu, mwisho alipuuzia jambo hilo.
Alienda kumtazama Mandy, alionekana kupowa huku mapigo ya moyo yakienda sawa kwa maana Desmond hakufanikiwa jaribio la kuondoa uhai wa Mandy, alibadilisha dripu na kufanya mambo mengine kisha naye alitoka. Hali ya Mandy haikujulikana kwa wakati huo kuwa ataamka lini wala saa ngapi laiti kama taarifa ya kuamka kwake ingewafikia madaktari basi tumaini lingekuwa kubwa sana.
Akiwa nje ya wodi ile, Desmond aliendelea kutafakari kuhusu usalama wa Mandy, alifikiria kama Mandy alikuwa amekufa au alikuwa hajafa na kama hajafa basi siri yake iliyojificha kuhusu Mama yake Mandy ingefichuka, akiwa hapo alisikia sauti ikimuita
“Mr Desmond” Alipogeuka alimuona Mtu mmoja akiwa amemsimamia, alishtuka sana sababu hakutarajia kumuona Mtu huyo kwa wakati huo
“Mbona umeshtuka au hukutarajia kuniona?” Alihoji Mtu huyo aliyekuwa Mwanaume mwenye sauti nzito
“Hapana ila nilikuwa mawazoni ndiyo maana nimeshtuka” Alisema Desmond kisha aliketi vizuri ili Mwanaume huyo naye aketi
“Hali ya Mkeo vipi?” Aliuliza Mwanaume huyo
“Mke wangu anaendelea…Hali yake bado ipo vile vile” Alijibu Desmond
“Mkeo ni shahidi namba moja wa kifo cha Mama yake, mara ya mwisho alituma ujumbe kituo cha polisi kuwa anamjuwa Muuwaji wa Mama yake, baada ya hapo ndiyo tukio la wewe kupigwa risasi na Mke wako kupigizwa ukutani lilipotokea, Mkeo ni Mtu muhimu zaidi katika kesi ile” Alisema Mwanaume huyo ambaye sasa alitambulika kuwa ni askari
“Yaah! Ni kweli, ilikuwa ni siku ngumu sana katika Maisha yangu ni kama nilimpoteza Mke wangu tokea siku ile hadi hivi leo” Alijikakamua Desmond kisha alijibu, huyu Desmond alionekana wazi kutambua juu ya kifo cha Mama yake Mandy lakini kwanini hakutaka ukweli uwekwe wazi? Au yeye ndiye aliyemuuwa Mama yake Mandy? Kwanini Amuuwe? TUSONGE MBELE
“Kwa lolote usisite kutujulisha Mr. Desmond” Alisema Askari huyo kisha aliondoka hapo. Kumbe nesi Lucia alikuwa anamuangalia Desmond akizungumza na polisi kisha alipoondoka yeye alimfuata Desmond alipokaa
“Desmond najuwa unavyojisikia, najuwa unaumia sana lakini Mkeo atakuwa sawa tu siku moja mtarudi kuwa kama zamani” Alisema Nesi Lucia, Desmond alimtazama Lucia kisha alijisemea moyoni
“Ungejuwa ninavyotamani afe wala usingesema hayo maneno” Kabla hajamjibu chochote Lucia alipokea simu ya Noela
“Hello” Alisema Desmond baada ya kupokea simu hiyo
“Desmond nakusubiria Mgahawani” Alisema Noela kisha Desmond alijibu
“Sawa nakuja”
“Unaenda wapi?” Alihoji Lucia
“Mjini”
“Hata mimi ninaenda huko kwa ajili ya chakula, tafadhali nipe lifti” Alisema Lucia
“Haya sawa!” alisema Desmond kisha waliongozana hadi kwenye gari ya Desmond na safari ya Kuelekea Mjini ilianza.
Wakiwa barabarani Nesi Lucia macho yake yote yalikuwa kwa Desmond, alimpenda sana Mwanaume huyo lakini alishindwa kumwambia sababu alikuwa Mume wa Mtu istoshe alikuwa akimuuguza Mke wake huyo.
Desmond aligundua hilo akamuuliza Lucia
“Kwanini unaniangalia hivyo?”
“Desmond wewe ni Mzuri sana, Hakika Mke wako anajivunia kuwa na Mwanaume kama Wewe” Alisema Lucia kisha Desmond alitabasamu kidogo alafu hakusema chochote kile hadi anafika eneo ambalo Lucia alikuwa akienda. Ilikuwa ni kwenye mgahawa huo huo ambao Desmond alienda kukutana na Mpenzi wake Noela
“Eeeh ajabu kumbe nawe ulikuwa unakuja hapa?” Aliuliza
“Yaah! Kuna Mtu naonana naye mara moja kisha niendelee na majukumu mengine”
“Haya asante kwa Lifti” Alisema Lucia kisha alishuka akaingia kwenye mgahawa huo ambao ulikuwa wenye hadhi kubwa na pia ulikuwa mkubwa mno, Desmond alienda mahali ambapo alipanga kuonana na Noela.