Nimeweka 3M UTT lakin imeongezeka 360 Nimeshtuka?? watalaam mje mnifafanulie

Nimeweka 3M UTT lakin imeongezeka 360 Nimeshtuka?? watalaam mje mnifafanulie

Mjadala huu umetoa mwanga kwamba watu wengi hawana Elimu ya uwekezaji na hawajui kitu kinaitwa UTT(Mifuko ya uwekezaji wa pamoja)
Sitaki kusema mambo mengi, wewe binafsi kama mwekezaji mtarajiwa tafuta Elimu juu ya haya masuala. Kwa urahisi ingia YOUTUBE kisha search kwa neno UTT zitakuja video ambazo ukisikiliza zitajibu maswali mengi. UTT ni sehemu salama sana.
poa
 
Uwekezaji wa 100ml utakupatika kati ya 8ml na 13ml kwa mwaka siyo 90ml.

Huu uwekezaji si wa kila mtu. Ni wa watu ambao hawawezi kufanya vitu vingine kama biashara ambazo zinahitaji uwepo wao.

Tuchukue mfano; ndugu yako amefariki akaacha madogo wa darasa la 6 na 4. Mirathi zao zikawa 200mil. Sasa hawa madogo utawapa hizo hela watafanyia nini?

Ukiziweka UTT mil 100 kwa kila dogo wana uhakika wa kupata mil 2.5 hadi 3 kila baada ya miezi 3 kwa kila dogo. Hiyo ni hela ambayo inaweza kuwasomesha hadi chuo kikuu na bado wakapata mtaji wa kuanzia maisha watakapo maliza vyuo.

Usiseme ni mafisadi ndo wanawekeza huko.
mtoe uvundo huyo jamaa
 
Muwe mnapata elimu in details kuhusu UTT kabla hamjajiunga..elimu zimetapakaa huko Youtube.
unafikiri sijapata

Ningekua sijapata ningeamua vip maamuzi.
Badala ya kucomment comment hela ungetumia muda huo kutoa ufafanuzi wa kimahesabu kama wewe unajua
 
Iko hivi ukiwekeza kwenye mfuko wa UTT Liquid funds kikawaida huu mfuko hutoa Ongezeko la asilimia 7-10 kwa mwaka, Makadirio tuweke 8% .


Kwa uwekezaji wako wa 3,000,000/= Nikikupigia hesabu kwa mwaka kwa Interest rate ya 8% kwa mwaka inakuja 3240,000/= 👇
View attachment 3159720

Sasa nikikupigia hesabu ya Mwezi utakua na 3,20,000/=
View attachment 3159723
Kwa maana hiyo kwa wiki ilitakiwa isome 3,05,000/=, Mwanzo hua ina shake hivyo hivyo mpaka walau utulie Miezi3 .


Kwanza nikuulize, kwenye muda wa kuwekeza umeweka malengo ya Miezi mingapi au Miaka mingapi?
Ila huu uwekezaji unataka moyo sana au mtu mwenye pesa nyingi au kama una hela unahisi utaiharibu kwa matumizi ambayo hukupanga.

Kuweka milioni tatu nikae mwaka mzima nasubiri laki mbili na ushee inahitaji moyo sana au labda pengine mimi ndio sijaelewa.

Milioni tatu ukiwekeza eneo zuri kwenye biashara return yake ikipungua kwa mwaka ni nzuri kuliko huko.

Niko tayari kurekebishwa.
 
Ila huu uwekezaji unataka moyo sana au mtu mwenye pesa nyingi au kama una hela unahisi utaiharibu kwa matumizi ambayo hukupanga.

Kuweka milioni tatu nikae mwaka mzima nasubiri laki mbili na ushee inahitaji moyo sana au labda pengine mimi ndio sijaelewa.

Milioni tatu ukiwekeza eneo zuri kwenye biashara return yake ikipungua kwa mwaka ni nzuri kuliko huko.

Niko tayari kurekebishwa.
Uko sahihi mkuu, Kitaalamu wanashauri kama unataka kufanya huu uwekezaji ni Condition mbili tu:

1. Kuwekeza ili kupata faida, hapa inatakiwa kuweka mpunga mrefu kweli kweli, Inashauriwa ukitaka ufanye uwekezaji wa aina hii bhasi hakikisha walau una vyanzo vya kipato vya uhakika vinavyokulipa vizuri na ambavyo unavyovisimamia vizuri walau vi2,3 na zaidi ...


2. Kutumia hii mifuko kama kibubu na njia ya kustawisha nidhamu yako ya pesa, hapa hata kama bado unajitafuta badala ya kucheza michezo ya mwezi, weka huko, unajifunza kutunza fedha zako mwenyewe. Unabana matumizi yasiyo lazima mf. Soda, Keki, Biskuti, Kubeti, Beer, Unatupia huko, ukipata kafaida asilimia kidogo unatupia huko..


Baada ya miezi 6 hivi utajionea maajabu ya pesa uliyojiwekea, unaweza ukaitoa ukaanzisha mradi, uzuri hii mifuko pesa haikatwi zaidi inapanda, pia huwezi kuitoa mpaka muda uliopanga ufike..



Lakini si lazima uweke pesa huko, Ziko savings account nyingi tu za bank tofauti tofauti, Ni wewe tu uamuzi wako, unapendelea nini .
 
Uko sahihi mkuu, Kitaalamu wanashauri kama unataka kufanya huu uwekezaji ni Condition mbili tu:

1. Kuwekeza ili kupata faida, hapa inatakiwa kuweka mpunga mrefu kweli kweli, Inashauriwa ukitaka ufanye uwekezaji wa aina hii bhasi hakikisha walau una vyanzo vya kipato vya uhakika vinavyokulipa vizuri na ambavyo unavyovisimamia vizuri walau vi2,3 na zaidi ...


2. Kutumia hii mifuko kama kibubu na njia ya kustawisha nidhamu yako ya pesa, hapa hata kama bado unajitafuta badala ya kucheza michezo ya mwezi, weka huko, unajifunza kutunza fedha zako mwenyewe. Unabana matumizi yasiyo lazima mf. Soda, Keki, Biskuti, Kubeti, Beer, Unatupia huko, ukipata kafaida asilimia kidogo unatupia huko..


Baada ya miezi 6 hivi utajionea maajabu ya pesa uliyojiwekea, unaweza ukaitoa ukaanzisha mradi, uzuri hii mifuko pesa haikatwi zaidi inapanda, pia huwezi kuitoa mpaka muda uliopanga ufike..



Lakini si lazima uweke pesa huko, Ziko savings account nyingi tu za bank tofauti tofauti, Ni wewe tu uamuzi wako, unapendelea nini .
Mkuu asante sana, nimeelewa vyema sana
 
Ila huu uwekezaji unataka moyo sana au mtu mwenye pesa nyingi au kama una hela unahisi utaiharibu kwa matumizi ambayo hukupanga.

Kuweka milioni tatu nikae mwaka mzima nasubiri laki mbili na ushee inahitaji moyo sana au labda pengine mimi ndio sijaelewa.

Milioni tatu ukiwekeza eneo zuri kwenye biashara return yake ikipungua kwa mwaka ni nzuri kuliko huko.

Niko tayari kurekebishwa.
let say magaiwio yakawa 12%

12% x 3,000,000= 360,000

ni kama lak 3 na 60 siyo laki mbili lakini inategemea na riba yabmwaka huo
 
Back
Top Bottom