Nimeweka 3M UTT lakin imeongezeka 360 Nimeshtuka?? watalaam mje mnifafanulie

Nimeweka 3M UTT lakin imeongezeka 360 Nimeshtuka?? watalaam mje mnifafanulie

Uwekezaji wa real Estate mfano nyumba za kupangisha unawauwa kwa Pressure wastaafu wengi sana wanaoukurupukia, Huu uwekezaji ni mtamu kama ukiuwahi ukiwa na 20s -Early 30s..

Zaidi ya hapo, Utakua unawawekezea wanao na Wajukuu zako, Return yake ni ndogo mnoo...!!

Noma sana.
 
Nafikiri hapo kwa Albert Einstein, au ni sehemu nyingine ?
Wakuu! Hapana kwa kweli!

Nilikuwa najipanga mwakani niwekeze vijisent vyangu huko UTT baada ya kusoma miongozo ya wakuu huu.

But kwa hiki kilichoibuliwa na mdau, nimeghairi kabisa. Ngoja tu niendelee na biashara zangu hata kama kuna kupomoroka nyakati fulani lakini ni heri biashara na vijisenti navyopata nihifadhi tu akaunt ya kawaida.


Sitaki msongo Mimi.
 
Zile asilimia zinazotajwa huwa ni kwa mwaka sio kwa wiki au siku.
Kwa layman labda tunaweza kujaribu kuchanganua hivi...
Mfano: faida ni 12% = 0.12 × kiasi ulichoweka kwa mwaka.

Ina maana Ukitaka kujua unapata ngapi kwa wiki/siku:
Ni sawa na 0.12÷ siku 366!
Hii hesabu iko Perfect sana 👍🏾
Wakuu! Hapana kwa kweli!

Nilikuwa najipanga mwakani niwekeze vijisent vyangu huko UTT baada ya kusoma miongozo ya wakuu huu.

But kwa hiki kilichoibuliwa na mdau, nimeghairi kabisa. Ngoja tu niendelee na biashara zangu hata kama kuna kupomoroka nyakati fulani lakini ni heri biashara na vijisenti navyopata nihifadhi tu akaunt ya kawaida.


Sitaki msongo Mimi.
Uwekezaji hauhitaji roho nyepesi, jitahidi kuongeza matawi ya biashara kwanza, Walau ukiwa na matawi ma3 hivi unaweza ukaanza kuwekeza..
 
Wakuu! Hapana kwa kweli!

Nilikuwa najipanga mwakani niwekeze vijisent vyangu huko UTT baada ya kusoma miongozo ya wakuu huu.

But kwa hiki kilichoibuliwa na mdau, nimeghairi kabisa. Ngoja tu niendelee na biashara zangu hata kama kuna kupomoroka nyakati fulani lakini ni heri biashara na vijisenti navyopata nihifadhi tu akaunt ya kawaida.


Sitaki msongo Mimi.
Unahitaji kusoma zaidi kuhusu uwekezaji. Kuna uwekezaji wa aina mbili.

1. Active investment
2. Passive investment.

Lakini pia kuna Biashara au kujiajiri.

Kwa mfano umefungua duka unauza mwenyewe na watu kadhaa wa kukusadia una safiri kwenda kufunga bidhaa. Yaani unahusika 100% na hiyo biashara hapo tunasema umejiajiri kwenye biashara. Kwenye pato lako unatakiwa ujilipe mshahara, uwalipe wafanyakazi mshahara, toa matumizi mengine yote ikiwa ni pamoja na kodi, zote kinacho baki ndo faida. Tatizo linaanza wafanyabiashara wengi hawajilipi mishahara. So unaona kila hela iliyobaki baada ya matumizi kama faida. Je unajilipa shs ngapi?

Uwekezaji namba moja yani active investiment unahusisha wewe mwekezaji kushiriki moja kwa moja katika kuendesha na kusimamia huo uwekeziji. Hata kama haupo wakati wote lakini kwa namna moja au nyingine uhai wa hiyo biashara inategemea uwepo wako
Kwa mfano unapita kila siku jioni kufunga hesabu, kufuatilia vibali na makolokolo mengi mengine., kuongea na wateja n.k. hii pia inatakiwa ujilipe mshahara kwa kazi unayoifanya na muda unaotumia. Kinacho baki baada ya kutoa mishahara ya wafnyakazi, kodi na matumizi yote ya biashara ikiwemo mshahara wako ndo faida. Wengi pia hawajilipi mshahara, hivyo huchukulia kila kitu kinachobaki ni faida.

Sasa piga hesabu ya ulichowekeza baada ya kutoa mshahara wako, faida ya mwezi ni % ngapi ya mtaji wako?

Uwekezaji aina ya pili yaani passive investment ni uwekezaji ambao unaweka hela unasubiri faida bila kufanya chochote.

Kwa mfano kama mtu ni Daktari ameajiriwa analipwa mshahara kwa kazi masaa 8 baada ya hapo anaenda kufanya kazi nyingine kwa masaa 4. Jumla masaa 12 kwa siku. Tuseme Jumla ya kipato chake kwa siku ni Tsh 300,000. Hana muda wa kufungua biashara au active investment. Yeye anaweka hela zake UTT zinaendelea kuzaliana. Tusema anaweka 1m kwa mwezi. Baada ya miezi 12 atakuwa anapata gawio la mwezi ambalo ni karibia 120,000 kwa mezi, baada ya mwaka wa pili atakuwa napata 240,000 kwa mwezi baada ya miaka 5 atakuwa anapata karibia 600,000 kwa mwezi. Na kuendelea.

Kwa hiyo hivi viti ni kwa mahitaji ya watu tofauti. Kama huna kazi ya kufanya na umepata 3M huwezi kwenda kuweka UTT utakuwa huna akili. Lakini. Kwa mtu ambaye tayari mida wake unalipwa pesa nzuri hana sababu ya kukimbizana na vibiashara vya mtaani. Anawekeza sehemu kama UTT.
 
Yes. sijaelewa ulivyo pata 5.5
Nianze kwa kusema Albert Einstein alikua kichwa sana, Maua yake 🌷🌷

Albert Einstein aligundua hii kanuni ya 72 [72 Rule], Hii kanuni inakusaidia kujua iwapo utatumia Muda gani kwa uwekezaji wako kuji double Mara2 kama utatumia njia ya riba mkusanyiko [Compound Interest] .

Kwa lugha nyingine riba mkusanyiko yaani unaiwekeza hela yako bila kutoa, Mwaka ukiisha unaweka tena pesa yote na faida uliyoipata pia, hivyo hivyo miaka na miaka.

Unachukua 72 unagawanya kwa kiwango cha riba unayoitegemea kwa mwaka, Mfano ukiwekeza Milioni 10 vodacom kwa riba ya 13.02% kwa mwaka 👇
Screenshot_20241123-190419~2.png

Sasa ukataka kujua itakuchukua muda gani ili uwe umepata Milioni10 nyingine, Unachukua 72 gawanya kwa riba unayoipata kwa Mwaka.

72%13.02= 5.6

Kwahiyo ukiiacha hiyo pesa iendelee kujizalisha bila kuitoa itakuchukua Miaka5 na miezi6 kupata Milioni 10 nyingine, Tutumie calculator Tuhakiki;

Screenshot_20241123-191310~2.png


Hiyo No.6 ni nusu mwaka, Unajionea hayo Maajabu, Tuwekee mfano mwingine unaoendana na UTT.

Tuseme umewekeza Milioni3 UTT kama mdau hapo, japo hajatuambia riba ya sasa ila Tufanye 14% kwa mwaka.


Kwahiyo achukue 72 ➗14=5.1, Unaona hapo, Itamchukua miaka 5 na na mwezi mmoja kupata Milioni 3 nyingine, Na hapo inaweza ikapanda kidogo au kushuka kidogo kulingana na Mtikisiko wa Uchumi.
 
Nadhani hukuelimishwa vizuri kuhusu uwekezaji. Kama umeambiwa utapata return ya 10% kwa mwaka sio kwamba kila siku hela inaingia, kuna siku itakua zaidi kuna siku itashuka. Subiri mwaka uishe ndo ufanye hesabu zako.

Mifuko ya uwekezaji is not a get-rich-quick scheme. It takes time. Huko unaweka hela na kusahau sio kuangalia kila siku.
 
Mkuu nimekupata sana. Kwa sio muajiriwa nimejiajiri mwenyewe. Kwa kilichojadiliwa humu na pia kwa ushauri wako na mfumo wangu wa maisha....nimegundua kuweka huko fedha hakunifai. Ngoja niendelee na active investment yangu
Unahitaji kusoma zaidi kuhusu uwekezaji. Kuna uwekezaji wa aina mbili.

1. Active investment
2. Passive investment.

Lakini bia kuna Biashara au kujiajiri.

Kwa mfano umefungua duka unauza mwenyewe na watu kadhaa wa kukusadia una safiri kwenda kufunga bidhaa. Yaani unahusika 100% na hiyo biashara hapo tunasema umejiajiri kwenye biashara. Kwenye pato lako unatakiwa ujilipe mshahara, uwalipe wafanyakazi mshahara, toa matumizi mengine yote kinacho baki ndo faida. Tatizo linaanza wafanyabiashara wengi hawajilipi mishahara. So unaona kila hela iliyobaki baada ya matumizi kama faida.

Uwekezaji namba moja yani active investiment unahusisha wewe mwekezaji kushiriki moja kwa moja katika kuendesha na kusimamia huo uwekeziji. Hata kama haupo wakati wote lakini namna moja au nyingine uhai wa hiyo biashara inategemea uwepo wako
Kwa mfano unapita kila siku jioni kufunga hesabu, kufuatilia vibali na makolokolo mengi mengine., kuongea na wateja n.k. hii pia inatakiwa ujilipe mshahara kwa kazi unayoifanya na muda unaotumia. Kinacho baki baada ya kutoa mishahar ya wafnyakazi, kodi na matumizi yote ya biashara ikiwemo mshahara wako ndo faida. Wengi pia hawajilipi mshahara, hivyo huchukulia kila kitu kinachobaki ni faida.

Uwekezaji aina ya pili yaani passive investment ni uwekezaji ambao unaweka hela unasubiri faida bila kufanya chochote.

Kwa mfano kama mtu ni Daktari ameajiriwa analipwa mshahara kwa kazi masaa 8 baada ya hapo anaenda kufanya kazi nyingime kwa masaa 4. Jumla masaa 12 kwa siku. Hana muda wa kufungua biashara au active investment. Yeye anaweka hela zake UTT zinaendelea kuzaliana. Tusema anaweka 1m kwa mwezi. Baada ya miezi 12 atakuwa anapata gawio la mwezi ambalo ni karibia 120,000 kwa mezi, baada ya mwaka wa pili atakuwa napata 240,000 kwa mwezi baada ya miaka 5 atakuwa anapata karibia 600,000 kwa mwezi. Na kuendelea.

Kwa hiyo hivi viti ni kwa mahitaji ya watu tofauti. Kama huna kazi ya kufanya na umepata 3M huwezi kwenda kuweka UTT utakuwa huna akili. Lakini. Kwa mtu ambaye tayari mida wake unalipwa pesa nzuri hana sababu ya kukimbizana na vibiashara vya mtaani. Anawekeza sehemu kama UTT.
 
Nianze kwa kusema Albert Einstein alikua kichwa sana, Maua yake 🌷🌷

Albert Einstein aligundua hii kanuni ya 72 [72 Rule], Hii kanuni inakusaidia kujua iwapo utatumia Muda gani kwa uwekezaji wako kuji double Mara2 kama utatumia njia ya riba mkusanyiko [Compound Interest] .

Kwa lugha nyingine riba mkusanyiko yaani unaiwekeza hela yako bila kutoa, Mwaka ukiisha unaweka tena pesa yote na faida uliyoipata pia, hivyo hivyo miaka na miaka.

Unachukua 72 unagawanya kwa kiwango cha riba unayoitegemea kwa mwaka, Mfano ukiwekeza Milioni 10 vodacom kwa riba ya 13.02% kwa mwaka 👇View attachment 3159766
Sasa ukataka kujua itakuchukua muda gani ili uwe umepata Milioni10 nyingine, Unachukua 72 gawanya kwa riba unayoipata kwa Mwaka.

72%13.02= 5.6

Kwahiyo ukiiacha hiyo pesa iendelee kujizalisha bila kuitoa itakuchukua Miaka5 na miezi6 kupata Milioni 10 nyingine, Tutumie calculator Tuhakiki;

View attachment 3159772

Hiyo No.6 ni nusu mwaka, Unajionea hayo Maajabu, Tuwekee mfano mwingine unaoendana na UTT.

Tuseme umewekeza Milioni3 UTT kama mdau hapo, japo hajatuambia riba ya sasa ila Tufanye 14% kwa mwaka.


Kwahiyo achukue 72 ➗14=5.1, Unaona hapo, Itamchukua miaka 5 na na mwezi mmoja kupata Milioni 3 nyingine, Na hapo inaweza ikapanda kidogo au kushuka kidogo kulingana na Mtikisiko wa Uchumi.
Kwa investiment kama UTT ni sawa. Ila kwa investment ya Hotel, hela unayopoata unaiwekeza wapi? Hakuna compounding pale unless kama faidayote unaiwekeza kwenye bond au UTT.
 
Kwa investiment kama UTT ni sawa. Ila kwa investment ya Hotel, hela unayopoata unaiwekeza wapi? Hakuna compounding pale unless kama faidayote unaiwekeza kwenye bond au UTT.
Nashukuru kuniambia hilo, Uko Sahihi , Nilitaka nimpigie hesabu ingekua ameweka UTT hizo M430 badala yake angepata kiasi gani...

Anyway nishai-
edit Imekaa clear mkuu..
 
Mkuu nimekupata sana. Kwa sio muajiriwa nimejiajiri mwenyewe. Kwa kilichojadiliwa humu na pia kwa ushauri wako na mfumo wangu wa maisha....nimegundua kuweka huko fedha hakunifai. Ngoja niendelee na active investment yangu
Ni kweli uwekezaji wa UTT au Bond ni kwa watu ambao tayari masaa 24 ya siku wanayatumia kwa mambo mengine yenye tija, lakini wana mitaji ambayo wanaogopa kufungua biashara zikakosa usimamizi.

Hivyo ni afadhali apate hicho kidogo kuliko kuwekeza akamwachia ndugu, baada ya muda zinaanza story.
 
Back
Top Bottom