Nimeyakumbuka maisha yangu ya uyatima; Uyatima ni noma sana ndugu zangu

Nimeyakumbuka maisha yangu ya uyatima; Uyatima ni noma sana ndugu zangu

Jana (Ijumaa) nikiwa kazini Kuna saa nilikosa Kazi (zilikua zimeisha). Nikawazaa, ghafla mawazo ya maisha ya UYATIMA niliyopitia yalinijia.

Ni ndefu sanaa we somaa.!

Japo siwezi kuyaandika yotee, maana UYATIMA wangu ulinipitisha kwenye makubwa sanaa..!!

Nilizaliwa kwenye familia ya watoto 3 tukiwa na baba na mama.
Baba alifariki kwa ku palaryze nikiwa mdogo sanaa.

Baba alikuwa ni mfanyabiashara mwenye mali nyingi ila mama alikua ni mama wa nyumbani.

Kwasababu ya kumkosa mumewe, baada ya baba kufariki mama alikuwa anaumwa umwa Sana.

Hii ilisababisha Mali nyingi kuuzwa na bila kusahau nyengine zilidhulumiwa na ndugu.

Ndugu na marafiki wa baba waligawana mali nyingi sanaa tukaachwa na nyumba tu ya kuishi.

Mama alikua anateseka Sana na mawazo ya kumpoteza mpendwa wake, hii ilisababisha kudhoofisha Kinga ya mwili na hatimae malaria kali ilimjia na kumchukua.

Ilikua ni siku ya jumapili nilipoletewa habari kuwa "Mama yako amefariki".
Aisee Ile siku ilikua nomaa, Mimi na mama tulikua na kijiwe chetu..!! Pale nyumbani (Kona ya barazani kwenye ua alilokuwa analipenda).

Aisee nilikaa pale na kulia sanaa, nilikumbuka ule usia wake, vicheko vyake, sura yake, harufu yake, kifupi niliona dunia imefika mwisho.

Wakati huo nikiwa mdogo sanaa (darasa la 4) ila huwezi amini NAKUMBUKA KILA KITU MPAKA LEO.

Nakuonya mwana JF "Usimfanyie mtoto ubaya" kwamaana "Hawezi sahau".
Mimi japo nilifanyiwa ubaya na ndugu tena nikiwa mdogo ila nakumbuka majina, siku, location yaani kila kitu kwa jambo nililyofanyiwa na ndugu.


Siku ya msiba wa baba watu walijaa wengi na waliiba Mali za pale nyumbani na wezi wote nawakumbuka ""wakina Wajomba zangu""

Baba alikua Tajiri hivyo nyumbani kwetu kulijaa ndugu waliokuja kuomba Msaada.

Ila baada ya baba kufa walipungua sana na baada ya mama kufa ndio kabisaa sikuwaona.

Tulianza kulelewa na dada.

Maisha ya ushua yalipotea na kama upepo, tukaanza shida.

Dada majukumu yalimzidi tuka hamishwa kila mtu kwake.

Mimi nikabaki Dar, mdogo angu mkoani na dada angu akabaki nyumbani.

Huko nilikoenda nilienda kwa mshua mmoja hivi taita Dar pale (rafiki wa baba).

Ila huyu "Mkewe hakunipenda kabisa" sababu mpaka leo huwa siijui.
Nilikua sili Sana, nilifanya Sana Kazi na mengine ila sijui kwanini hakunipenda.

Nilikaa pale miaka miwili, mama akaanda staili moja ili niondoke kwake.

Lile zegwe hausi geli alilijua.
Akanitahadharisha.

Nikamuhadithia shangazi
Shangazi alikuja kunichukua fasta.

Shangazi yangu hakua na maisha mazuri ila nilikomaa hivyohivyo.

Nilikomaa sanaa, chakula hakitoshi, Shule kwenda na miguu tena Dar es salaam, halafu mbali sanaa.
Mwaka mzima hununuliwi nguo mpya..!! Unavaa nguo za kushindia hizohizo mpaka mtaa una kukariri.

Ila nilikomaa.

Shangazi yangu hakuwa na room kwa watoto wa kiume, kwahiyo sometimes nilikua nalala kwenye korido na sometimes nje ya nyumba.

Yaani nje kabisa, milango inafungwa mi nafunga net kibarazani nalala.

Hakua ananitesa na nilikua nina amani.

Kwakuwa chakula kilikuwa hakitoshi nilianza kufanya Kazi kwenye nyumba za watu.

Maisha ya zamani ilikua mwenye hela ndio anabomba la maji la Dawasco.

Hivyo mi nilikua nachotea watu maji wananilipa ndoo moja 50.

Hapo nikawa napata nauli ya kwenda Shule (kipindi hicho mwanafunzi nauli 50).

Na nyengine kabla sijala nyumbani nilikua natanguliza kwanza sambusa, hivyo na kile kidogo cha nyumba nakua nashibaa.

Maisha yalienda mara la 7 nikafaulu.

Miaka ile kufaulu la Saba ilikua dili hasaaa.

Shuleni kwetu tulienda secondary Wa3 tu, yaani tulifaulu Wa3 tu..!!!

Mtaa mzima hongera...!!!

Kufika Shule nikaanza kucheza kamali ili nipate pesa ya kujikimu..!!

Nilikua nawala hasa.

200 inazalisha 3000 mpaka 5000.

Bwana eeeh Kuna siku ikapitishwa karatasi waandikwe majina ya wacheza kamali, na Mimi ndani...!!!

Tulipigwa sanaa siku ile, fimbo kama 100 hivi.
Enzi zile tulikua tunapigwa hasaaa.
Unashika chini huku umebongoa, walimu wanapita na fimbo, ukiishika Tako umefutaa.!!!

Tulipigwa sanaa.

Ila Sasa hata nikiacha kucheza nitapata wapi hela ya kujikimu shule..!!
Shangazi ya kunipa hana, hana uwezo wa kunipa nauli, je madaftari na vitabu atanunua?

Dah maisha yaliendelea, tukawa tunacheza nje ya Shule.

Kufika form 2 nikaongoza wastani kwa Shule nzima.

Ikabidi mwalimu wa darasa aniite "wewe una akili sanaa, kwanini unakua mtundu?"

Nikamuhadithia nayopitia nyumbani, huyu mwalimu niliona kabisa machozi yana mlenga.

Tokea siku hiyo alianza kunichukulia tofauti sanaa.

Form 4 nikaongoza kwa kupata Division 1 Kali sanaaa.

Taarifa zikaenea kwa ndugu na jamaaa + mtaani.

Hongera na masifa kama yoteee.

Ila nyumbani hali ilikua tofauti..!!

Binadamu yangu ye alipata 4 Mimi 1.

Mama ake ikawa kila jambo ananipendelea Mimi..!!

Binamu yangu alini mind sanaaa.

Akawa anatanitaka nitoke kwao, hii "Toka kwetu" mwanzo niliiona ya kawaida sanaa ili kufika form 5 ilikolea sanaa.

Kuna siku nilirudi nyumbani nikafungasha nguo na kusepa gheto la masela wapiga misuli.

Shangazi alimind sanaa.

Akaniita tukaongea na kuahidi kila jumapili nikachukue elfu 5 ya matumizi ya wiki.

Yaani kwa wiki utumie elfu 5..!!
Kula mchana, asubuhi, usiku na hela ya pindi mchikichini..!!

Nilikonda hasaa, maana kila siku nashindia miogo ya Shule.
Maana kila siku natakiwa kutumia buku..!!

Maisha yaliendelea taarifa zikamfikia baba mdogo.

Akaniomba niwe naenda kwake kuchukua misaada.

Nilienda kama wiki 4 mfululizo (kila jumamosi).

Nakumbuka Kuna jumamosi nilienda nikamkuta mkewe na baba mdogo hayupo.

Sasa bana Mimi Nina aibu ya kuomba Msaada kwahiyo muda wa kuondoka nikaaga ili niondoke kimya kimya.

Mama mdogo aliniita akanipa maneno makali "Unasababisha sisi tuishi maisha magumu kisa wewe....." aliongea mengi ila mwisho wa siku alinikataza kwenda kwake kuchukua misaada.

Na kama baba mdogo alijua maana hakuwahi kuniuliza lolote juu ya lile jambo.

Nilifika nyumbani siku hiyo nililia sanaa, nilikumbuka maisha ya baba yupo na mama.
Nililia balaaa.

Ghafla mama mdogo (ndugu wa mama) akaniambia niwe naenda kwake.

Huyu nae alinisaidia mara sijui 6 ya 7 nae akanipa dongo "Kwani wengine hawapo" nilibaki mdomo wazi.

Nikarudi gheto nikajisemea "Sitaki tena msaada nitakomaa mpaka nafia humu"

Ile elfu 20 ya mwisho niliyopewa Msaada nikafanya mtaji wa kuuza vitu vidogo vidogo Shule na mitaani.

Nikaacha kwenda mchikichini (tution) NECTA form 6 sikufaulu vizuriiiiii, ila nilipata credit za Degree.

Nilisoma PCB ila nilipenda sanaa mambo ya biashara.
Afya sikuiwaza kabisaa na Wala sikuipenda.

Sasa bana kuomba mkopo na post, post zinatoka chuo UDSM halafu bodi ya mkopo "NO LOAN".

Nani atanisomesha sasa??..!!!!!

Dah nikawazaa, kumbe shangazi yangu anahangaika.

Akanitafutia ufadhili mmoja wa ada.
Chuoni nikawa nalipa 240,000/= ya mambo mengine ya chuo ila ni Diploma.

Nikajisemea "yaani hizi C zangu za PCB naenda kusoma diploma, huku wenye E na D wanaenda degree"
Maisha gani haya...!!!

Nikabeba begi kwenda chuo.

Chuoni sikua na raha Wala amani, nilipenda masomo ya biashara ila nikawa nasomo visivyojulikana na moyo wangu..!!

Nikiwa Diploma 2 mdogo angu akamaliza form 4, akapata ufaulu wa kawaida ila sio wa kwenda advance..!!

Wakumsomesha HAKUNA..!!

UYATIMA nyie, Achana nao kabisaa...!!

Ikabidi nimpe ahadi ya kwamba anisubiri mi mwaka mmoja nimalize Diploma halafu yeye ataingia kwa ada yangu mi nitaishia hapo..!!

Ila kabla ya hapo nikiwa form 4 na 6 nasubiri matokea na post zakuendelea kusoma nilishawahi fanya sehemu tempo.

Kwahiyo lengo langu lilikua ni kumaliza Diploma halafu niende pale kujishikiza, then mdogo angu aingie chuo.

Nikamaliza diploma kufika ile ofisi kuongea na bosi akakubali. Kunipa Kazi.

Nikawa mpiga Kazi pale.

Nilikomaa kuishi maisha magumu hasaa ili tu mdogo angu aingie chuo.

Aisee ni mengi aiseee.

Ile dogo kumaliza Certificate nikamshikiza pale job na kikazi fulani hivi.
Huku Mimi nika apply Kazi serikalini nikapata Mkoani.
Dah hapo ndio ikawa kama nafuu imeanza kuja.

Maisha yalienda, serikalini kazini nikaomba ruhusa ya kwenda Shule kupiga Bachelor nikaunga Masters.

Sikuacha ndoto zangu zife, nilienda kusoma masomo ya biashara.
Ghafla zile ndoto zilizozimwa kisa yatima kakosa ada zikatimia.

Na mwaka huu naingia darasani kusoma PhD yangu..!!!

Na mdogo wangu aliendelea mpaka akapata CPA..!! Na mwaka huu anaingia darasani kusoma Masters.

Mama yetu alikua anatuambia "baba yenu alitaka na kutamani sanaa msome".

Angalau sasa hata tukifa tunaenda kuwaambia wazazi wetu "Tumemaliza yale mlioyatamani kutupa"

Dada yetu yupo na ameolewa na yeye ndio mama yetu.

Huwa tunamlea vizuri ""Japo tunampaga pesa kimya kimya ili shemeji asijue..!!!""

Aisee ni mengi aisee na siwezi kuyaandika yoteee.

Maana pia nilishawahi fukuzwa na shemeji (mke wa kaka - kaka mtoto wa baba mkubwa) bila kujua sababu..!!
Nilikua naendaga kuwasalimia, mkewe sijui akanichoka na kunifukuza ..!!!

Kifupi ndugu walikua wanadhani na hasa wake wa ndugu zangu walikua wanadhani sijui naenda kumaliza hela za waume zao.

Kifupi hakuna aliyenisaidia bila kulalamika, na kunisimanga.
Na wotee waliona Bora kunitimua ili nisiwaletee shida makwao.

Kifupi mpaka leo ndugu huwa siwaelewi.
Huwa wanapiga simu na kiukweli si "save" namba zao.
Na kesho wakipiga Tena na nikiwauliza "nani mwenzangu" huwa wanakata simu na kusema "huyu siku hizi yupo serikalini na kasoma basi anajidai sanaaa"

Na huwa hawaniambii direct ila Wana mwambia dada au shangazi.

Cha ajabu WAMESAHAU YOTEE WALIYOTENDA..!!!

Kifupi sina swaga yoyotee na ndugu YOYOTE.

Siwachukii ila SINA MPANGO NAO KABISAAA.

Ila mdogo angu anamsemo wake "Atavuna aliyepanda kwenye maisha yangu tu, kwani wakati hatuna wazazi na tunateseka walikua wapi"

Kifupi hatuna connection na ndugu wa upande wa mama woteeeeee yaani hata mmoja sijui yuko wapi.

Ila Kwa baba ni shangazi yangu ndio aliyepambana tukafika hapa..!!!
Tupo nae karibu na tunampenda sanaaa.

Baba yangu kwao walizaliwa Wa2 tu.
Yeye na dada ake ambae alitulea.

Nampenda sanaa shangazi yangu na namuheshimu sanaa.

Siwezi kufika Dar bila kumuona Wala kumletea Zawadi ni Mungu wangu aisee hapa duniani.

Ila ndugu wa mama HAPANA KWA KWELI.

Siwachukii ila HATA SIJUI WAKO WAPI NA SINA MPANGO NAO KABISAAA.
Waliamua kunitupa na Mimi nimejitupa mazima.

Dah tuishie hapo.....

YANAYONITAWALA KICHWANI.

1. Natamani kumuuliza yule mama wa mshua, kwanini alipanga kunifanyia lile tukio ili mumewe anifukuze?

2. Natamani kuwauliza wajomba zangu, kwanini mliamua kutudhulumu mali zetu?

3. Natamani kuwauliza mama wadogo, kwanini mliamua kumuacha dada yao (mama yetu) atulee kwa shida wakati wao walikua wanakuja kwake kulia shida?

Kifupi natamani tu nikae na walionifukuza halafu niwahojii kwanini walinifanyia vile.
Yaani tuhojianee weee mpaka moyo ukaridhika.

Natamani nikae na walionipitisha kwenye shida niwahojiiii mpaka niridhike.

KITU NILICHOSHINDWA NI KUWATAFUTA NA KUONGEA NAO.
Najua watakua wanamiliki simu ila hata kutafuta namba zao NIMESHINDWA ..

Na nimepitia mengi siwezi kuyaandika yoteee mengine yanauma na kuumiza.

Tuishie hapa.

Miss you Daddy and Mammy.

UYATIMA ni nyokooooo sanaaaa.
Kuna kale kamsemo kanasemaga adui yako ni mtu wa karibu... Au ule msemo mtegemea cha nduguye hufa masikini, ndugu wana maajabu yao na wanaweza kukuacha mdomo wazi
 
jamaa hajui kama hao ndugu zake, yawezekana wameshatubu kwa Mungu, wanaendelea na Mungu maishani, yeye amebaki na kinyongo na mzigo moyoni, na zigo hilo linamuumiza yeye zaidi ya hao ndugu zake, na akifa leo hii na zigo hilo anaenda moja kwa moja motoni. Mungu anasema ukitaka akusamehe dhambi, na wewe samehe wenzako, usipowamehe wengine hata Mungu hatakusamehe. kwahiyo kama yeye ni msafi kabisa hajawahi kumtenda Mungu dhambi basi asiwasamehe hao ndugu zake, ila kama na yeye ni mwanadamu kama tulivyo sisi wenzake, ni lazima asamehe na ajue kuwa mwanadamu mbaya wa jana anaweza kuwa mzuri wa kesho na akakusaidia kesho hata kama jana hakukusaidia. kukusaidia sio lazima pesa, kiburi cha uzima alichonacho sasaivi ndicho kinamdanganya ajione hawahitaji ndugu zake, Mungu akikipiga hicho kiburi utahitaji hata ndugu yako mmoja tu akutembelee hata kukutembelea tu. kuna siku atakuja kujua hili.
 
Aisee pole sana kaka, imenibidi nichimbue nijue nini kilijiri kwako. Mimi ni yatima pia 80% uliyoyasema nimepotia....uyatima unaumiza sana. Mno mno
 
Aisee pole sana kaka, imenibidi nichimbue nijue nini kilijiri kwako. Mimi ni yatima pia 80% uliyoyasema nimepotia....uyatima unaumiza sana. Mno mno
Mungu Mkubwa kwa maana TUMEFIKA japo sio juu ila ANGALAU TUMEFIKA.

#YNWA
 
jamaa hajui kama hao ndugu zake, yawezekana wameshatubu kwa Mungu, wanaendelea na Mungu maishani, yeye amebaki na kinyongo na mzigo moyoni, na zigo hilo linamuumiza yeye zaidi ya hao ndugu zake, na akifa leo hii na zigo hilo anaenda moja kwa moja motoni. Mungu anasema ukitaka akusamehe dhambi, na wewe samehe wenzako, usipowamehe wengine hata Mungu hatakusamehe. kwahiyo kama yeye ni msafi kabisa hajawahi kumtenda Mungu dhambi basi asiwasamehe hao ndugu zake, ila kama na yeye ni mwanadamu kama tulivyo sisi wenzake, ni lazima asamehe na ajue kuwa mwanadamu mbaya wa jana anaweza kuwa mzuri wa kesho na akakusaidia kesho hata kama jana hakukusaidia. kukusaidia sio lazima pesa, kiburi cha uzima alichonacho sasaivi ndicho kinamdanganya ajione hawahitaji ndugu zake, Mungu akikipiga hicho kiburi utahitaji hata ndugu yako mmoja tu akutembelee hata kukutembelea tu. kuna siku atakuja kujua hili.

Sijakwambia Nina NINA KINYONGO ila nimekwambia NAHITAJI TU KUWAULIZA.

ila pia NILISHAWA DELETE na hasa NDUGU WA MAMA Hawa ndio nadhani ni woteee NISHAWA DELETE.

Na Wala sina kisasi nao, ila waliamua kunitupa basi tuendeleze ile life style ya KUTUPANA.

#YNWA
 
Kuna Mambo mengi omba kuyasikia tu. kwa sehemu kuna baadhi ya mambo nimepitia kama wewe ikiwa ni pamoja na kutengwa na upande wa mzazi wetu aliefariki na upande wa ndugu waliyebaki hai walikuwa wanakuja kujibebea vitu kwa siri. ila mwisho wa siku nilikuja kujua ilikua ni umaskini tu. ILA UMASKINI NI MBAYA SANA mshua wenu alistahili kuwainua wengine kiuchumi maudhi ya dizaini hiyo yangepungua ila inaonekana ni kama yeye ndo alikuwa anategemewa na wengine wote hapo tatizo ndo lilipoanzia sasa.
 
Uyatima hauna mazoea..pole na hongera kwa kufika hapo ulipo.
Umeniliza aisee..wazazi wapumzike kwa amani
 
Mateso sio ishu saana, yatima kinachowaumizaga ni kunyanyaswa kukosa kupewa upendo, huwezi kumsaidia usimtamkie maneno mabaya, yupo mtu hapo anaumia akikumbuka ameishi maisha ya mtaani ili Hali yupo mkoa wa chimbuko lake kwenye ndugu zake. Jamaa alilala kwenye korido na kwenye Baraza ila rohoo kwatu sababu shangazi alimpenda. Huyo mke wa ba mdogo alipungukiwa nini mpaka a mwambie maneno Yale, yule alosema huoni ndugu wengine, siyo maneno ya kumuambia mtu. Ndo hayo hayafutiki kwenye kumbukumbu, watu hawalaumu ila wanaona kwa nini hawakuchukuliwa kama watu. Muonyeshe muhitaji upendo hatosahau na utabarikiwa. Ahimidiwe MUNGU baba wa yatima.
 
Kamwe hawezi kusahau, na siyo kusahau tu, ubaya ule unaweza ukamfanya aje kuwa mtu mbaya katika maisha yake, Hakuna aliyefilisika kwa kumsaidia muhitaji.
 
Jana (Ijumaa) nikiwa kazini Kuna saa nilikosa Kazi (zilikua zimeisha). Nikawazaa, ghafla mawazo ya maisha ya UYATIMA niliyopitia yalinijia.

Ni ndefu sanaa we somaa.!

Japo siwezi kuyaandika yotee, maana UYATIMA wangu ulinipitisha kwenye makubwa sanaa..!!

Nilizaliwa kwenye familia ya watoto 3 tukiwa na baba na mama.
Baba alifariki kwa ku palaryze nikiwa mdogo sanaa.

Baba alikuwa ni mfanyabiashara mwenye mali nyingi ila mama alikua ni mama wa nyumbani.

Kwasababu ya kumkosa mumewe, baada ya baba kufariki mama alikuwa anaumwa umwa Sana.

Hii ilisababisha Mali nyingi kuuzwa na bila kusahau nyengine zilidhulumiwa na ndugu.

Ndugu na marafiki wa baba waligawana mali nyingi sanaa tukaachwa na nyumba tu ya kuishi.

Mama alikua anateseka Sana na mawazo ya kumpoteza mpendwa wake, hii ilisababisha kudhoofisha Kinga ya mwili na hatimae malaria kali ilimjia na kumchukua.

Ilikua ni siku ya jumapili nilipoletewa habari kuwa "Mama yako amefariki".
Aisee Ile siku ilikua nomaa, Mimi na mama tulikua na kijiwe chetu..!! Pale nyumbani (Kona ya barazani kwenye ua alilokuwa analipenda).

Aisee nilikaa pale na kulia sanaa, nilikumbuka ule usia wake, vicheko vyake, sura yake, harufu yake, kifupi niliona dunia imefika mwisho.

Wakati huo nikiwa mdogo sanaa (darasa la 4) ila huwezi amini NAKUMBUKA KILA KITU MPAKA LEO.

Nakuonya mwana JF "Usimfanyie mtoto ubaya" kwamaana "Hawezi sahau".
Mimi japo nilifanyiwa ubaya na ndugu tena nikiwa mdogo ila nakumbuka majina, siku, location yaani kila kitu kwa jambo nililyofanyiwa na ndugu.


Siku ya msiba wa baba watu walijaa wengi na waliiba Mali za pale nyumbani na wezi wote nawakumbuka ""wakina Wajomba zangu""

Baba alikua Tajiri hivyo nyumbani kwetu kulijaa ndugu waliokuja kuomba Msaada.

Ila baada ya baba kufa walipungua sana na baada ya mama kufa ndio kabisaa sikuwaona.

Tulianza kulelewa na dada.

Maisha ya ushua yalipotea na kama upepo, tukaanza shida.

Dada majukumu yalimzidi tuka hamishwa kila mtu kwake.

Mimi nikabaki Dar, mdogo angu mkoani na dada angu akabaki nyumbani.

Huko nilikoenda nilienda kwa mshua mmoja hivi taita Dar pale (rafiki wa baba).

Ila huyu "Mkewe hakunipenda kabisa" sababu mpaka leo huwa siijui.
Nilikua sili Sana, nilifanya Sana Kazi na mengine ila sijui kwanini hakunipenda.

Nilikaa pale miaka miwili, mama akaanda staili moja ili niondoke kwake.

Lile zegwe hausi geli alilijua.
Akanitahadharisha.

Nikamuhadithia shangazi
Shangazi alikuja kunichukua fasta.

Shangazi yangu hakua na maisha mazuri ila nilikomaa hivyohivyo.

Nilikomaa sanaa, chakula hakitoshi, Shule kwenda na miguu tena Dar es salaam, halafu mbali sanaa.
Mwaka mzima hununuliwi nguo mpya..!! Unavaa nguo za kushindia hizohizo mpaka mtaa una kukariri.

Ila nilikomaa.

Shangazi yangu hakuwa na room kwa watoto wa kiume, kwahiyo sometimes nilikua nalala kwenye korido na sometimes nje ya nyumba.

Yaani nje kabisa, milango inafungwa mi nafunga net kibarazani nalala.

Hakua ananitesa na nilikua nina amani.

Kwakuwa chakula kilikuwa hakitoshi nilianza kufanya Kazi kwenye nyumba za watu.

Maisha ya zamani ilikua mwenye hela ndio anabomba la maji la Dawasco.

Hivyo mi nilikua nachotea watu maji wananilipa ndoo moja 50.

Hapo nikawa napata nauli ya kwenda Shule (kipindi hicho mwanafunzi nauli 50).

Na nyengine kabla sijala nyumbani nilikua natanguliza kwanza sambusa, hivyo na kile kidogo cha nyumba nakua nashibaa.

Maisha yalienda mara la 7 nikafaulu.

Miaka ile kufaulu la Saba ilikua dili hasaaa.

Shuleni kwetu tulienda secondary Wa3 tu, yaani tulifaulu Wa3 tu..!!!

Mtaa mzima hongera...!!!

Kufika Shule nikaanza kucheza kamali ili nipate pesa ya kujikimu..!!

Nilikua nawala hasa.

200 inazalisha 3000 mpaka 5000.

Bwana eeeh Kuna siku ikapitishwa karatasi waandikwe majina ya wacheza kamali, na Mimi ndani...!!!

Tulipigwa sanaa siku ile, fimbo kama 100 hivi.
Enzi zile tulikua tunapigwa hasaaa.
Unashika chini huku umebongoa, walimu wanapita na fimbo, ukiishika Tako umefutaa.!!!

Tulipigwa sanaa.

Ila Sasa hata nikiacha kucheza nitapata wapi hela ya kujikimu shule..!!
Shangazi ya kunipa hana, hana uwezo wa kunipa nauli, je madaftari na vitabu atanunua?

Dah maisha yaliendelea, tukawa tunacheza nje ya Shule.

Kufika form 2 nikaongoza wastani kwa Shule nzima.

Ikabidi mwalimu wa darasa aniite "wewe una akili sanaa, kwanini unakua mtundu?"

Nikamuhadithia nayopitia nyumbani, huyu mwalimu niliona kabisa machozi yana mlenga.

Tokea siku hiyo alianza kunichukulia tofauti sanaa.

Form 4 nikaongoza kwa kupata Division 1 Kali sanaaa.

Taarifa zikaenea kwa ndugu na jamaaa + mtaani.

Hongera na masifa kama yoteee.

Ila nyumbani hali ilikua tofauti..!!

Binadamu yangu ye alipata 4 Mimi 1.

Mama ake ikawa kila jambo ananipendelea Mimi..!!

Binamu yangu alini mind sanaaa.

Akawa anatanitaka nitoke kwao, hii "Toka kwetu" mwanzo niliiona ya kawaida sanaa ili kufika form 5 ilikolea sanaa.

Kuna siku nilirudi nyumbani nikafungasha nguo na kusepa gheto la masela wapiga misuli.

Shangazi alimind sanaa.

Akaniita tukaongea na kuahidi kila jumapili nikachukue elfu 5 ya matumizi ya wiki.

Yaani kwa wiki utumie elfu 5..!!
Kula mchana, asubuhi, usiku na hela ya pindi mchikichini..!!

Nilikonda hasaa, maana kila siku nashindia miogo ya Shule.
Maana kila siku natakiwa kutumia buku..!!

Maisha yaliendelea taarifa zikamfikia baba mdogo.

Akaniomba niwe naenda kwake kuchukua misaada.

Nilienda kama wiki 4 mfululizo (kila jumamosi).

Nakumbuka Kuna jumamosi nilienda nikamkuta mkewe na baba mdogo hayupo.

Sasa bana Mimi Nina aibu ya kuomba Msaada kwahiyo muda wa kuondoka nikaaga ili niondoke kimya kimya.

Mama mdogo aliniita akanipa maneno makali "Unasababisha sisi tuishi maisha magumu kisa wewe....." aliongea mengi ila mwisho wa siku alinikataza kwenda kwake kuchukua misaada.

Na kama baba mdogo alijua maana hakuwahi kuniuliza lolote juu ya lile jambo.

Nilifika nyumbani siku hiyo nililia sanaa, nilikumbuka maisha ya baba yupo na mama.
Nililia balaaa.

Ghafla mama mdogo (ndugu wa mama) akaniambia niwe naenda kwake.

Huyu nae alinisaidia mara sijui 6 ya 7 nae akanipa dongo "Kwani wengine hawapo" nilibaki mdomo wazi.

Nikarudi gheto nikajisemea "Sitaki tena msaada nitakomaa mpaka nafia humu"

Ile elfu 20 ya mwisho niliyopewa Msaada nikafanya mtaji wa kuuza vitu vidogo vidogo Shule na mitaani.

Nikaacha kwenda mchikichini (tution) NECTA form 6 sikufaulu vizuriiiiii, ila nilipata credit za Degree.

Nilisoma PCB ila nilipenda sanaa mambo ya biashara.
Afya sikuiwaza kabisaa na Wala sikuipenda.

Sasa bana kuomba mkopo na post, post zinatoka chuo UDSM halafu bodi ya mkopo "NO LOAN".

Nani atanisomesha sasa??..!!!!!

Dah nikawazaa, kumbe shangazi yangu anahangaika.

Akanitafutia ufadhili mmoja wa ada.
Chuoni nikawa nalipa 240,000/= ya mambo mengine ya chuo ila ni Diploma.

Nikajisemea "yaani hizi C zangu za PCB naenda kusoma diploma, huku wenye E na D wanaenda degree"
Maisha gani haya...!!!

Nikabeba begi kwenda chuo.

Chuoni sikua na raha Wala amani, nilipenda masomo ya biashara ila nikawa nasomo visivyojulikana na moyo wangu..!!

Nikiwa Diploma 2 mdogo angu akamaliza form 4, akapata ufaulu wa kawaida ila sio wa kwenda advance..!!

Wakumsomesha HAKUNA..!!

UYATIMA nyie, Achana nao kabisaa...!!

Ikabidi nimpe ahadi ya kwamba anisubiri mi mwaka mmoja nimalize Diploma halafu yeye ataingia kwa ada yangu mi nitaishia hapo..!!

Ila kabla ya hapo nikiwa form 4 na 6 nasubiri matokea na post zakuendelea kusoma nilishawahi fanya sehemu tempo.

Kwahiyo lengo langu lilikua ni kumaliza Diploma halafu niende pale kujishikiza, then mdogo angu aingie chuo.

Nikamaliza diploma kufika ile ofisi kuongea na bosi akakubali. Kunipa Kazi.

Nikawa mpiga Kazi pale.

Nilikomaa kuishi maisha magumu hasaa ili tu mdogo angu aingie chuo.

Aisee ni mengi aiseee.

Ile dogo kumaliza Certificate nikamshikiza pale job na kikazi fulani hivi.
Huku Mimi nika apply Kazi serikalini nikapata Mkoani.
Dah hapo ndio ikawa kama nafuu imeanza kuja.

Maisha yalienda, serikalini kazini nikaomba ruhusa ya kwenda Shule kupiga Bachelor nikaunga Masters.

Sikuacha ndoto zangu zife, nilienda kusoma masomo ya biashara.
Ghafla zile ndoto zilizozimwa kisa yatima kakosa ada zikatimia.

Na mwaka huu naingia darasani kusoma PhD yangu..!!!

Na mdogo wangu aliendelea mpaka akapata CPA..!! Na mwaka huu anaingia darasani kusoma Masters.

Mama yetu alikua anatuambia "baba yenu alitaka na kutamani sanaa msome".

Angalau sasa hata tukifa tunaenda kuwaambia wazazi wetu "Tumemaliza yale mlioyatamani kutupa"

Dada yetu yupo na ameolewa na yeye ndio mama yetu.

Huwa tunamlea vizuri ""Japo tunampaga pesa kimya kimya ili shemeji asijue..!!!""

Aisee ni mengi aisee na siwezi kuyaandika yoteee.

Maana pia nilishawahi fukuzwa na shemeji (mke wa kaka - kaka mtoto wa baba mkubwa) bila kujua sababu..!!
Nilikua naendaga kuwasalimia, mkewe sijui akanichoka na kunifukuza ..!!!

Kifupi ndugu walikua wanadhani na hasa wake wa ndugu zangu walikua wanadhani sijui naenda kumaliza hela za waume zao.

Kifupi hakuna aliyenisaidia bila kulalamika, na kunisimanga.
Na wotee waliona Bora kunitimua ili nisiwaletee shida makwao.

Kifupi mpaka leo ndugu huwa siwaelewi.
Huwa wanapiga simu na kiukweli si "save" namba zao.
Na kesho wakipiga Tena na nikiwauliza "nani mwenzangu" huwa wanakata simu na kusema "huyu siku hizi yupo serikalini na kasoma basi anajidai sanaaa"

Na huwa hawaniambii direct ila Wana mwambia dada au shangazi.

Cha ajabu WAMESAHAU YOTEE WALIYOTENDA..!!!

Kifupi sina swaga yoyotee na ndugu YOYOTE.

Siwachukii ila SINA MPANGO NAO KABISAAA.

Ila mdogo angu anamsemo wake "Atavuna aliyepanda kwenye maisha yangu tu, kwani wakati hatuna wazazi na tunateseka walikua wapi"

Kifupi hatuna connection na ndugu wa upande wa mama woteeeeee yaani hata mmoja sijui yuko wapi.

Ila Kwa baba ni shangazi yangu ndio aliyepambana tukafika hapa..!!!
Tupo nae karibu na tunampenda sanaaa.

Baba yangu kwao walizaliwa Wa2 tu.
Yeye na dada ake ambae alitulea.

Nampenda sanaa shangazi yangu na namuheshimu sanaa.

Siwezi kufika Dar bila kumuona Wala kumletea Zawadi ni Mungu wangu aisee hapa duniani.

Ila ndugu wa mama HAPANA KWA KWELI.

Siwachukii ila HATA SIJUI WAKO WAPI NA SINA MPANGO NAO KABISAAA.
Waliamua kunitupa na Mimi nimejitupa mazima.

Dah tuishie hapo.....

YANAYONITAWALA KICHWANI.

1. Natamani kumuuliza yule mama wa mshua, kwanini alipanga kunifanyia lile tukio ili mumewe anifukuze?

2. Natamani kuwauliza wajomba zangu, kwanini mliamua kutudhulumu mali zetu?

3. Natamani kuwauliza mama wadogo, kwanini mliamua kumuacha dada yao (mama yetu) atulee kwa shida wakati wao walikua wanakuja kwake kulia shida?

Kifupi natamani tu nikae na walionifukuza halafu niwahojii kwanini walinifanyia vile.
Yaani tuhojianee weee mpaka moyo ukaridhika.

Natamani nikae na walionipitisha kwenye shida niwahojiiii mpaka niridhike.

KITU NILICHOSHINDWA NI KUWATAFUTA NA KUONGEA NAO.
Najua watakua wanamiliki simu ila hata kutafuta namba zao NIMESHINDWA ..

Na nimepitia mengi siwezi kuyaandika yoteee mengine yanauma na kuumiza.

Tuishie hapa.

Miss you Daddy and Mammy.

UYATIMA ni nyokooooo sanaaaa.
Pole sana yatima mwenzangu , ifike mahali basi sisi yatima tuungane tuwe na umoja wa kuwakomboa ndugu zetu , huko mtaani na pia kuwatetea mahali popote pale wanapoguswa maana ukipita kwenye familia nyingi , hakika yatima wanazalilishwa sana .[emoji24][emoji24][emoji24], watoto wa mtaani wengi ni yatima, hao panya roads wengi ni ndugu zetu , itoshe kusema kuna haja ya kuungana kukifariji kizazi cha watoto wanaoachwa na wazazi wao., financially , psychologically na responsible towards their future life.[emoji120][emoji120]

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Nimesoma hii nmejikuta tu nalia sijui hata nalia nini maana sijapitia hayo maisha nina wazazi wote wawili mpaka sasa ila maisha yalikua magumu tu wakati wa kusoma.
 
QURAN 4: 6

6. "Na wajaribuni mayatima mpaka wafike umri wa kuoa. Mkiwaona ni werevu, basi wapeni mali yao. Wala msiyale kwa fujo na pupa kwa kuwa watakuja kuwa watu wazima. Na aliye kuwa tajiri na ajizuilie(asiguse kabisa mali ya yatima), na aliye fukara basi na ale kwa kadri ya ada. Na mtakapo wapa mali yao wekeni mashahidi. Na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa Mhasibu."


 
QURAN 4: 9-10

9. "
Na wachelee (wasile mali ya yatima) wale ambao lau kuwa na wao wangeli acha nyuma yao watoto wanyonge wangeli wahofia. Basi nao wamche Mwenyezi Mungu, na waseme maneno yaliyo sawa"


10. Hakika wanao kula mali ya mayatima kwa dhuluma, hapana shaka yoyote wanakula matumboni mwao moto, na wataingia Motoni"
 
Jana (Ijumaa) nikiwa kazini Kuna saa nilikosa Kazi (zilikua zimeisha). Nikawazaa, ghafla mawazo ya maisha ya UYATIMA niliyopitia yalinijia.

Ni ndefu sanaa we somaa.!

Japo siwezi kuyaandika yotee, maana UYATIMA wangu ulinipitisha kwenye makubwa sanaa..!!

Nilizaliwa kwenye familia ya watoto 3 tukiwa na baba na mama.
Baba alifariki kwa ku palaryze nikiwa mdogo sanaa.

Baba alikuwa ni mfanyabiashara mwenye mali nyingi ila mama alikua ni mama wa nyumbani.

Kwasababu ya kumkosa mumewe, baada ya baba kufariki mama alikuwa anaumwa umwa Sana.

Hii ilisababisha Mali nyingi kuuzwa na bila kusahau nyengine zilidhulumiwa na ndugu.

Ndugu na marafiki wa baba waligawana mali nyingi sanaa tukaachwa na nyumba tu ya kuishi.

Mama alikua anateseka Sana na mawazo ya kumpoteza mpendwa wake, hii ilisababisha kudhoofisha Kinga ya mwili na hatimae malaria kali ilimjia na kumchukua.

Ilikua ni siku ya jumapili nilipoletewa habari kuwa "Mama yako amefariki".
Aisee Ile siku ilikua nomaa, Mimi na mama tulikua na kijiwe chetu..!! Pale nyumbani (Kona ya barazani kwenye ua alilokuwa analipenda).

Aisee nilikaa pale na kulia sanaa, nilikumbuka ule usia wake, vicheko vyake, sura yake, harufu yake, kifupi niliona dunia imefika mwisho.

Wakati huo nikiwa mdogo sanaa (darasa la 4) ila huwezi amini NAKUMBUKA KILA KITU MPAKA LEO.

Nakuonya mwana JF "Usimfanyie mtoto ubaya" kwamaana "Hawezi sahau".
Mimi japo nilifanyiwa ubaya na ndugu tena nikiwa mdogo ila nakumbuka majina, siku, location yaani kila kitu kwa jambo nililyofanyiwa na ndugu.


Siku ya msiba wa baba watu walijaa wengi na waliiba Mali za pale nyumbani na wezi wote nawakumbuka ""wakina Wajomba zangu""

Baba alikua Tajiri hivyo nyumbani kwetu kulijaa ndugu waliokuja kuomba Msaada.

Ila baada ya baba kufa walipungua sana na baada ya mama kufa ndio kabisaa sikuwaona.

Tulianza kulelewa na dada.

Maisha ya ushua yalipotea na kama upepo, tukaanza shida.

Dada majukumu yalimzidi tuka hamishwa kila mtu kwake.

Mimi nikabaki Dar, mdogo angu mkoani na dada angu akabaki nyumbani.

Huko nilikoenda nilienda kwa mshua mmoja hivi taita Dar pale (rafiki wa baba).

Ila huyu "Mkewe hakunipenda kabisa" sababu mpaka leo huwa siijui.
Nilikua sili Sana, nilifanya Sana Kazi na mengine ila sijui kwanini hakunipenda.

Nilikaa pale miaka miwili, mama akaanda staili moja ili niondoke kwake.

Lile zegwe hausi geli alilijua.
Akanitahadharisha.

Nikamuhadithia shangazi
Shangazi alikuja kunichukua fasta.

Shangazi yangu hakua na maisha mazuri ila nilikomaa hivyohivyo.

Nilikomaa sanaa, chakula hakitoshi, Shule kwenda na miguu tena Dar es salaam, halafu mbali sanaa.
Mwaka mzima hununuliwi nguo mpya..!! Unavaa nguo za kushindia hizohizo mpaka mtaa una kukariri.

Ila nilikomaa.

Shangazi yangu hakuwa na room kwa watoto wa kiume, kwahiyo sometimes nilikua nalala kwenye korido na sometimes nje ya nyumba.

Yaani nje kabisa, milango inafungwa mi nafunga net kibarazani nalala.

Hakua ananitesa na nilikua nina amani.

Kwakuwa chakula kilikuwa hakitoshi nilianza kufanya Kazi kwenye nyumba za watu.

Maisha ya zamani ilikua mwenye hela ndio anabomba la maji la Dawasco.

Hivyo mi nilikua nachotea watu maji wananilipa ndoo moja 50.

Hapo nikawa napata nauli ya kwenda Shule (kipindi hicho mwanafunzi nauli 50).

Na nyengine kabla sijala nyumbani nilikua natanguliza kwanza sambusa, hivyo na kile kidogo cha nyumba nakua nashibaa.

Maisha yalienda mara la 7 nikafaulu.

Miaka ile kufaulu la Saba ilikua dili hasaaa.

Shuleni kwetu tulienda secondary Wa3 tu, yaani tulifaulu Wa3 tu..!!!

Mtaa mzima hongera...!!!

Kufika Shule nikaanza kucheza kamali ili nipate pesa ya kujikimu..!!

Nilikua nawala hasa.

200 inazalisha 3000 mpaka 5000.

Bwana eeeh Kuna siku ikapitishwa karatasi waandikwe majina ya wacheza kamali, na Mimi ndani...!!!

Tulipigwa sanaa siku ile, fimbo kama 100 hivi.
Enzi zile tulikua tunapigwa hasaaa.
Unashika chini huku umebongoa, walimu wanapita na fimbo, ukiishika Tako umefutaa.!!!

Tulipigwa sanaa.

Ila Sasa hata nikiacha kucheza nitapata wapi hela ya kujikimu shule..!!
Shangazi ya kunipa hana, hana uwezo wa kunipa nauli, je madaftari na vitabu atanunua?

Dah maisha yaliendelea, tukawa tunacheza nje ya Shule.

Kufika form 2 nikaongoza wastani kwa Shule nzima.

Ikabidi mwalimu wa darasa aniite "wewe una akili sanaa, kwanini unakua mtundu?"

Nikamuhadithia nayopitia nyumbani, huyu mwalimu niliona kabisa machozi yana mlenga.

Tokea siku hiyo alianza kunichukulia tofauti sanaa.

Form 4 nikaongoza kwa kupata Division 1 Kali sanaaa.

Taarifa zikaenea kwa ndugu na jamaaa + mtaani.

Hongera na masifa kama yoteee.

Ila nyumbani hali ilikua tofauti..!!

Binadamu yangu ye alipata 4 Mimi 1.

Mama ake ikawa kila jambo ananipendelea Mimi..!!

Binamu yangu alini mind sanaaa.

Akawa anatanitaka nitoke kwao, hii "Toka kwetu" mwanzo niliiona ya kawaida sanaa ili kufika form 5 ilikolea sanaa.

Kuna siku nilirudi nyumbani nikafungasha nguo na kusepa gheto la masela wapiga misuli.

Shangazi alimind sanaa.

Akaniita tukaongea na kuahidi kila jumapili nikachukue elfu 5 ya matumizi ya wiki.

Yaani kwa wiki utumie elfu 5..!!
Kula mchana, asubuhi, usiku na hela ya pindi mchikichini..!!

Nilikonda hasaa, maana kila siku nashindia miogo ya Shule.
Maana kila siku natakiwa kutumia buku..!!

Maisha yaliendelea taarifa zikamfikia baba mdogo.

Akaniomba niwe naenda kwake kuchukua misaada.

Nilienda kama wiki 4 mfululizo (kila jumamosi).

Nakumbuka Kuna jumamosi nilienda nikamkuta mkewe na baba mdogo hayupo.

Sasa bana Mimi Nina aibu ya kuomba Msaada kwahiyo muda wa kuondoka nikaaga ili niondoke kimya kimya.

Mama mdogo aliniita akanipa maneno makali "Unasababisha sisi tuishi maisha magumu kisa wewe....." aliongea mengi ila mwisho wa siku alinikataza kwenda kwake kuchukua misaada.

Na kama baba mdogo alijua maana hakuwahi kuniuliza lolote juu ya lile jambo.

Nilifika nyumbani siku hiyo nililia sanaa, nilikumbuka maisha ya baba yupo na mama.
Nililia balaaa.

Ghafla mama mdogo (ndugu wa mama) akaniambia niwe naenda kwake.

Huyu nae alinisaidia mara sijui 6 ya 7 nae akanipa dongo "Kwani wengine hawapo" nilibaki mdomo wazi.

Nikarudi gheto nikajisemea "Sitaki tena msaada nitakomaa mpaka nafia humu"

Ile elfu 20 ya mwisho niliyopewa Msaada nikafanya mtaji wa kuuza vitu vidogo vidogo Shule na mitaani.

Nikaacha kwenda mchikichini (tution) NECTA form 6 sikufaulu vizuriiiiii, ila nilipata credit za Degree.

Nilisoma PCB ila nilipenda sanaa mambo ya biashara.
Afya sikuiwaza kabisaa na Wala sikuipenda.

Sasa bana kuomba mkopo na post, post zinatoka chuo UDSM halafu bodi ya mkopo "NO LOAN".

Nani atanisomesha sasa??..!!!!!

Dah nikawazaa, kumbe shangazi yangu anahangaika.

Akanitafutia ufadhili mmoja wa ada.
Chuoni nikawa nalipa 240,000/= ya mambo mengine ya chuo ila ni Diploma.

Nikajisemea "yaani hizi C zangu za PCB naenda kusoma diploma, huku wenye E na D wanaenda degree"
Maisha gani haya...!!!

Nikabeba begi kwenda chuo.

Chuoni sikua na raha Wala amani, nilipenda masomo ya biashara ila nikawa nasomo visivyojulikana na moyo wangu..!!

Nikiwa Diploma 2 mdogo angu akamaliza form 4, akapata ufaulu wa kawaida ila sio wa kwenda advance..!!

Wakumsomesha HAKUNA..!!

UYATIMA nyie, Achana nao kabisaa...!!

Ikabidi nimpe ahadi ya kwamba anisubiri mi mwaka mmoja nimalize Diploma halafu yeye ataingia kwa ada yangu mi nitaishia hapo..!!

Ila kabla ya hapo nikiwa form 4 na 6 nasubiri matokea na post zakuendelea kusoma nilishawahi fanya sehemu tempo.

Kwahiyo lengo langu lilikua ni kumaliza Diploma halafu niende pale kujishikiza, then mdogo angu aingie chuo.

Nikamaliza diploma kufika ile ofisi kuongea na bosi akakubali. Kunipa Kazi.

Nikawa mpiga Kazi pale.

Nilikomaa kuishi maisha magumu hasaa ili tu mdogo angu aingie chuo.

Aisee ni mengi aiseee.

Ile dogo kumaliza Certificate nikamshikiza pale job na kikazi fulani hivi.
Huku Mimi nika apply Kazi serikalini nikapata Mkoani.
Dah hapo ndio ikawa kama nafuu imeanza kuja.

Maisha yalienda, serikalini kazini nikaomba ruhusa ya kwenda Shule kupiga Bachelor nikaunga Masters.

Sikuacha ndoto zangu zife, nilienda kusoma masomo ya biashara.
Ghafla zile ndoto zilizozimwa kisa yatima kakosa ada zikatimia.

Na mwaka huu naingia darasani kusoma PhD yangu..!!!

Na mdogo wangu aliendelea mpaka akapata CPA..!! Na mwaka huu anaingia darasani kusoma Masters.

Mama yetu alikua anatuambia "baba yenu alitaka na kutamani sanaa msome".

Angalau sasa hata tukifa tunaenda kuwaambia wazazi wetu "Tumemaliza yale mlioyatamani kutupa"

Dada yetu yupo na ameolewa na yeye ndio mama yetu.

Huwa tunamlea vizuri ""Japo tunampaga pesa kimya kimya ili shemeji asijue..!!!""

Aisee ni mengi aisee na siwezi kuyaandika yoteee.

Maana pia nilishawahi fukuzwa na shemeji (mke wa kaka - kaka mtoto wa baba mkubwa) bila kujua sababu..!!
Nilikua naendaga kuwasalimia, mkewe sijui akanichoka na kunifukuza ..!!!

Kifupi ndugu walikua wanadhani na hasa wake wa ndugu zangu walikua wanadhani sijui naenda kumaliza hela za waume zao.

Kifupi hakuna aliyenisaidia bila kulalamika, na kunisimanga.
Na wotee waliona Bora kunitimua ili nisiwaletee shida makwao.

Kifupi mpaka leo ndugu huwa siwaelewi.
Huwa wanapiga simu na kiukweli si "save" namba zao.
Na kesho wakipiga Tena na nikiwauliza "nani mwenzangu" huwa wanakata simu na kusema "huyu siku hizi yupo serikalini na kasoma basi anajidai sanaaa"

Na huwa hawaniambii direct ila Wana mwambia dada au shangazi.

Cha ajabu WAMESAHAU YOTEE WALIYOTENDA..!!!

Kifupi sina swaga yoyotee na ndugu YOYOTE.

Siwachukii ila SINA MPANGO NAO KABISAAA.

Ila mdogo angu anamsemo wake "Atavuna aliyepanda kwenye maisha yangu tu, kwani wakati hatuna wazazi na tunateseka walikua wapi"

Kifupi hatuna connection na ndugu wa upande wa mama woteeeeee yaani hata mmoja sijui yuko wapi.

Ila Kwa baba ni shangazi yangu ndio aliyepambana tukafika hapa..!!!
Tupo nae karibu na tunampenda sanaaa.

Baba yangu kwao walizaliwa Wa2 tu.
Yeye na dada ake ambae alitulea.

Nampenda sanaa shangazi yangu na namuheshimu sanaa.

Siwezi kufika Dar bila kumuona Wala kumletea Zawadi ni Mungu wangu aisee hapa duniani.

Ila ndugu wa mama HAPANA KWA KWELI.

Siwachukii ila HATA SIJUI WAKO WAPI NA SINA MPANGO NAO KABISAAA.
Waliamua kunitupa na Mimi nimejitupa mazima.

Dah tuishie hapo.....

YANAYONITAWALA KICHWANI.

1. Natamani kumuuliza yule mama wa mshua, kwanini alipanga kunifanyia lile tukio ili mumewe anifukuze?

2. Natamani kuwauliza wajomba zangu, kwanini mliamua kutudhulumu mali zetu?

3. Natamani kuwauliza mama wadogo, kwanini mliamua kumuacha dada yao (mama yetu) atulee kwa shida wakati wao walikua wanakuja kwake kulia shida?

Kifupi natamani tu nikae na walionifukuza halafu niwahojii kwanini walinifanyia vile.
Yaani tuhojianee weee mpaka moyo ukaridhika.

Natamani nikae na walionipitisha kwenye shida niwahojiiii mpaka niridhike.

KITU NILICHOSHINDWA NI KUWATAFUTA NA KUONGEA NAO.
Najua watakua wanamiliki simu ila hata kutafuta namba zao NIMESHINDWA ..

Na nimepitia mengi siwezi kuyaandika yoteee mengine yanauma na kuumiza.

Tuishie hapa.

Miss you Daddy and Mammy.

UYATIMA ni nyokooooo sanaaaa.
Nimesoma hadi nikajisikia uchungu pole sana mkuu
 
Back
Top Bottom