Mama Mdogo
JF-Expert Member
- Nov 21, 2007
- 2,967
- 2,147
Hekaya za Abunwasi............................................
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nakujibu kutokana na uzoefu binafsi. Huyo ni changudoa. Na ukimuendekeza kuna siku atakuumbua utajuta sana. Machangudoa kitabia hawana heshima hata chembe, na silaha yao kubwa hasa kwa mtu anayeonekana ana 'heshima zake' ni blackmail.Ni wiki chache zimepita tangu nihamie kwenye kibanda chungu nilichojenga nje ya mji. Kwa sababu ya umbali wa ninakokaa na foleni za magari, inanilazimu kuondoka nyumbani kumi na mbili kasoro kuwahi traffic jam. Siku ya kwanza nikiwa kwenye gari yangu nilikutana na huyu binti aliyesababisha leo niombe ushauri. Alikuwa anajitembelea pembeni ya barabara akielekea kazini. Kwa kuwa sikumfahamu, nilimpita.
Kesho yake muda kama huo nilikutana naye tena, aliniangalia sana, lakini nikampita. Siku ya tatu nikamkuta tena kwa huruma nikasimama, na kumkaribisha lifti mpaka mjini ambako kila mtu alielekea kzn kwake. Basi tangu siku hiyo ikawa ndo kupeana lifti na mazungumzo ya ndani yalikuwa ni salamu tu.
Juzi amehamia jirani mwingine mdada ambaye amejenga nyumba karibu na kwangu kabisa. Baada ya kutambulishana na jirani huyu, akaomba nayeye awe anapata lifti ya kwenda kazn. Nilimkubalia.
Cha kushangaza, leo nilimpa lifti jirani yangu huyu mpya ambaye alikaa siti ya mbele ya gari. Hatua chache mbele kidogo nikakutata na huyu mdada wa siku zote, kama kawaida nikasimama.
Akaja, akafungua mlango wa mbele, baada ya kugundua kuwa kuna dada mwingine amekaa siti ya mbele, akafyonza na kufunga mlango kisha akazira na kukataa kupanda gari.
Nauliza waungwana kosa langi ni lipi? Na nimtendeje huyu dada? Nahisi maenidhalilisha kwa jirani yangu!
Wasalaam,
HP
Chief acha umalaya, kwa nini uwape lift kina dada tu, acha ufataki utakufa.
hii ni kali!
Nimesoma hadithi nyingi, huwa zinaelekeana lakini ya kwako hii ni ya aina yake!
Wanawake wana wivu sana na ni roho mbaya kichizi!
Lakini wewe mwenyewe huenda hujatulia, unaweza kukuta unajieleza mambo mazuri tu, usikute ushalikoroga sana na huyo mdada wa watu siku za nyuma!...kwanini asonye wakati hajui kuwa huyo ni dada yako au shangazi yako?
Anaijua tabia yako huyo mkuu!..badilika!