Nimpeleke mtoto shule ya milioni 1.5 au hela nimuwekezee UTT au hisa?

Nimpeleke mtoto shule ya milioni 1.5 au hela nimuwekezee UTT au hisa?

Ndio maana nimekushangaa mno hadi nikakuuliza milioni 3 kabisa???? Nikajua labda kaka umeshinda Biko kwahiyo unatenda wema 🤣🤣🤣🤣
Ahh wapi, yaani huo mchezo Sina sio leo au kesho.
labda mzazi awe total incapacitated.

Beside suala lako lile la kujutia, liko Lina fanyiwa kazi.
 
Wakuu kuna mtoto wangu kaanza shule mwaka huu, chekechea ada yake ni milioni 1.5 ukijumlisha na vikorokoro vingine inaweza fika jumla milioni 1.7

Sio muumini sana wa hizi shule, ila mama yake ndio aling'ang'ania sana tumpeleke huko baada ya kuona rafiki zake nao wamepeleka watoto wao shule za private na wanaongea kiingereza kingi wakiwa na umri mdogo na pia anasema mtoto tukimpeleka shule za serikali atateseka6

Sasa nimefikiria, kumpeleka mtoto hadi amalize shule ya msingi, then sekondari, je hizo pesa za ada badala ya kumlipia shule ya private nikamhamishia serikalini ambako hata hivyo atakua ananuliwa vitabu na materials nyingine , halafu hiyo ada ya private nikawa naiwekeza kwenye mfuko wa UTT au kununua hisa za kampuni inayofanya vizuri tu kila mwaka, au kuiwekeza kwenyw kununua ardhi

Baaadae mtoto akiwa na miaka 20 ama 25 huko atakuwa na mtaji wa kuanzia maisha halafu connection nitampa mimi kwenye biashara zangu

Pia nimefikiria kumpeleka mtoto shule za kawaida kutamjenga awe 'mgumu' awe na kuweza kumudu mazingira halisi ya mtaano baada ya kumaliza masomo, kuliko mazingira ya kupelekwa na kurudishwa na school bus ambayo hayamjengi

Mimi mwenyewe ni msomi mwenye degree, lakini kazi ninyoifanya haihusiani kabisa na elimu yangu, na ilinibidi ni adapt mtaani japo kwa maumivu na hofu yangu ni kuwa mwanangu naweza kumsomesha kwa gharama kubwa halafu elimu isimsaidie kwenye maisha kama mimi, na akawa hana hata skills za kutoboa mtaani, mimi kutokusoma hizo shule za gharama naamimi kumenisaidia kidogo

Dunia inabadilika, wasomi wengi mtaani kazi hakuna na mbaya zaidi kazi nyingi zitaenda kuwa automated miaka ijayo,
Kaka hapo umemalza kila kitu kabisa... Just go ahead I mean Proceed with the Plan!
 
Kwa walio wengi wanaosomesha watoto wao shule za Kayumba ni kutokana na uchumi wao kutetereka. Si kwamba wanapenda. Ila katika kujifariji ndipo utawakuta wakiibuka na hoja ya kuzisifia wakati hata matokeo ya kitaifa ya kila mwaka na kila level yanathibitisha shule hizo kutokuwa na ubora wowote.
Maisha hayako kwenye matokeo makubwa ya shule
 
Kupanga ni kuchagua shirikishaneni na Mwenza wako mueleweshane pro and cons za kufanya yote hayo; ingawa ni vema mkafanya kile ambacho kipo within your means.., Kwa Serikali ya sasa huo ni msingi tu bado huko mbeleni pia panahitaji pesa ndefu sana, kwahio angalia usije ukajenga msingi wa ghorofa kwa kutumia zege alafu ukamalizia juu kwa nyumba ya tope, wakati huenda ungeweza kuanza na kupaliza kwa kutumia tofari za kuchoma ambazo ni durable sometimes hata zaidi ya simenti.
 
usipoteze hela kulipa english medium primary school

HIZO HELA WEKEZA KWENYE HISA,MASHAMBA,VIWANJA PERI URBAN AREAS

📌FOCUS IANZE KWA KUWEKEZA PESA ZA KUJA KUWAPA MITAJI NA URITHI WA MALI KWA HAO AKINA JUNIOR WENU.KUPOTEZA MAMILIONI HUKO EMS KISHA ANAKUJA KUGOMBANIA INTERVIEW ZA TAMISEMI NI "UKICHAA".

MABASI YA NJANO NA TABU ZA TAMISEMI WAPI NA WAPI ACHIENI KAYUMBA HUKO TAMISEMI NDO MAZINGIRA YAO TANGU WADOGO.NYIE WAZUNGU PORI😄😄😄ANZISHENI MIRADI!!!
Asante
 
S

Sijakataa , private schools walimu Wana bidii kuliko wanafunzi Ila serikali wanafunzi Wana bidii kuliko walimu yaani Iko vice versa. Mie topic ya water mwalimu aliingia darasani akauliza kuwa Kuna nani hayajui maji, darasa kimya, Kuna mtu hajui maji Yana rangi ama harufu Gani , tukawa kimya mwalimu akasema kuwa topic imeisha iyo. N kweli ikaisha mtihani ukaja na tunafaulu mno.
Mie nachoomba mwanangu awe na bidii ,kiu,ari ,shauku etc ya kusoma basi. Mie nakumbuka nimeokota sh 500 zamani nikanunua kitabu, mwingine anaenda kununua soda ama kuchezea game yaani ukiwa na mtt akawa anatambua jambo Bora kwangu ni greatest gift pia na kwake
Una watoto?
Vijana wengi huwa mnawaza hivi ila mkipata watoto mnawaza vingine.

Kuna jamaa alikuwa anaponda sana hizi shule za private tena kwa nguvu zote.

Na kutoa maapio hatapeleka mtoto huko.
Amekuja kupata watoto, juzi anauzilia anawezaje kupata nafasi kwenye shule zenye michepuo ya Cambridge. 🤣🤣
 
Hivi Hawa private students wanafanya kazi maofisi yapi jaman, au ndio wafanyabiashara wengi wao ?. Maana walioko huku ofisini ni wakawaida sana uwezo wao.
Unazungumzia Ofisi zipi?
Inawezekana uko kwenye ofisi za kawaida sana pia.
 
Acha Kumsumbua mtoto mwache tu asome kwa raha.
Hivi kwenda shule na fagliò na kudumu unaona kazi ndogo

Mungu akubariki uweke na hisa zake,
Nimepeleka mwanangu private baada ya kuona kile choo cha ile shule ya serikali pale jirani yetu
 
Back
Top Bottom