Nimrod Mkono na Mkono Advocates watch

Nimrod Mkono na Mkono Advocates watch

Ninajaribu kuangalia mzazi mwenye watoto wengi ambao wana biashara zao tofauti tofauti; mtoto mmoja ni mwanasheria. Je akija mtu kumtapeli mzee huyu kiuchumi kwa kumtaka aweke sahihi kwenye mkataba ambao kijuu juu ni mzuri lakini kwenye fine print una machungu makubwa sana kwa mzee, je itakuwa ni halali kwa huyu kijana mwanasheria kumsaidia tapeli huyo kuandika mkataba huo wa kumkomoa baba yake?


Kama mkono hakuona ubaya wowote kwenye mikataba ile kisheria ilikuwaje baadaye anaibeza serikali kwama iwe inasoma mikataba kwa makini kabla ya kuisaini? Tukubali kuwa pamoja na mengine mazuri anayofanya jimboni kwake, mzee huyu amechangia kwa kiasi kikubwa kuiweka nchi yetu kwenye mikataba mibaya ingawa hakuwa peke yake; hawezi kuondoa mkono wake kwenye lawama zile.

Kama mkataba haukiuki sheria yoyote na huyo tapeli katengenezewa huo mkataba na mtoto wa huyo mzazi, huyo mtoto atausaini tu (haijalishi kama ni baba yake wala nini). Na baadae atamzodoa baba yake vile vile kwamba kosa ni la kwake, kwa maana anao wataalam wake wa sheria (kama ilivyo serikali) na hakuwatumia kuusoma huo mkataba na kuelewa vifungu vyake vizuri (kama ni kweli). Hivi unashangaa kitu gani hapa. Mteja mfalme, ebo!!

Wanasheria/mawakili hawa hawa wanawatetea majambazi na wauaji (tena wakijua kwamba ni wauaji maana ni lazima useme ukweli wako ili jamaa aangalie jinsi ya kukutetea kwenye kesi) sembuse hili la mkataba ambayo umeutaka mwenyewe. Vinginevyo kwa nini usifanye mwenyewe?

Mkono kama mwanasheria/wakili ana haki ya kuhakikisha mteja wake anapata anachokihitaji kwa kuzingatia sheria zilizopo.
 
Kama mkataba haukiuki sheria yoyote na huyo tapeli katengenezewa huo mkataba na mtoto wa huyo mzazi, huyo mtoto atausaini tu (haijalishi kama ni baba yake wala nini). Na baadae atamzodoa baba yake vile vile kwamba kosa ni la kwake, kwa maana anao wataalam wake wa sheria (kama ilivyo serikali) na hakuwatumia kuusoma huo mkataba na kuelewa vifungu vyake vizuri (kama ni kweli). Hivi unashangaa kitu gani hapa. Mteja mfalme, ebo!!

Wanasheria/mawakili hawa hawa wanawatetea majambazi na wauaji (tena wakijua kwamba ni wauaji maana ni lazima useme ukweli wako ili jamaa aangalie jinsi ya kukutetea kwenye kesi) sembuse hili la mkataba ambayo umeutaka mwenyewe. Vinginevyo kwa nini usifanye mwenyewe?

Mkono kama mwanasheria/wakili ana haki ya kuhakikisha mteja wake anapata anachokihitaji kwa kuzingatia sheria zilizopo.


Basi uanasheria ni kazi mbaya sana. Yaani mwanasheria anaweza kumsaidia mteja wake jinsi ya kuhalisha dhuluma? Hawezi kumshauri mteja wake huyo kuwa ingawa hilo analotaka kufanya linaweza kuhalaishwa kisheria lina repercussion fulani katika jamii?
 
kichuguu,
kati Wabunge ambao wamewahi kupigia kelele hii mikataba ni Mzee Mkono. Actually, Mzee Mkono aliwahi hata kugomea kupokea mchango wa Barick "kusaidia" maendeleo, akidai kwamba ni mdogo kulinganisha na wanachokipata.

Mimi nadhani badala ya kumlalamikia Mzee Mkono ni bora tuwalaumu hao wanaopanga bei ya mashirika,migodi,etc huko serikalini.
 
Basi uanasheria ni kazi mbaya sana. Yaani mwanasheria anaweza kumsaidia mteja wake jinsi ya kuhalisha dhuluma? Hawezi kumshauri mteja wake huyo kuwa ingawa hilo analotaka kufanya linaweza kuhalaishwa kisheria lina repercussion fulani katika jamii?

Kichuguu,

Sentensi yako ni kali mno.

Kila kazi (kwa maana ya taaluma) inaweza kuwa mbaya kutokana na matumizi yake mabaya. Kama unaitumia kutetea dhuluma dhidi ya haki, obviously itaonekana mbaya. Asilimia kubwa ya wanasheria/mawakili (wawe wa serikali ama binafsi) hapa nyumbani wanaangalia maslahi binafsi zaidi. Wapo wachache ambao wanatetea haki kabla ya kuangalia mambo ya pesa. Lakini hawa hata hizo contracts hawapelekewi kwa maana hawataendekeza upuuzi.

Taaluma zote zinaweza kuwa mbaya iwapo wahusika wataamua kufanya hivyo. Kwa hiyo siyo wanasheria tu. Wahasibu, madaktari, engineers, walimu, etc. wana ubaya wao wakiamua hivyo.

In fact suala la Mkono halina tatizo kwa maana yeye anafanya kazi kwa kutumia kampuni binafsi ambayo nia yake ni kutengeneza faida. Kwa hiyo anahakikisha anabargain big!! Na hapo ndiko kuna tatizo hapa nchini. Na serikali inawategemea wao wawe washauri wake, na wakati huo huo ni washauri wa hao wawekezaji.

Wakati wa mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Sayansi, Technologia na Elimu ya Juu nilisikia baadhi ya wabunge wanalalamika kwamba badala ya kutumia makapuni binafsi katika kuishauri serikali, basi ni vema wakawatumia wataalamu wetu walioko katika Higher Learning Institutions wakiamini kwamba labda hawatahitaji 10% kwa maana hawatakuwa wanafanya kama watu binafsi isipokuwa kama taasisi. Unasemaje hapo?
 
Wakati kesi ya Dito ilipoibuka na Mkono kuwa mmoja wa mawakili tulizua mjadala wa mgongano wa maslahi ya aina fulani. Endapo Mbunge (mtunga sheria) anashiriki katika majadiliano au kushiriki kufanya biashara na makampuni ambayo yana interest na sheria fulani, je haiwezekani kuwa makampuni hayo kumtaka mbunge huyo kupinga/kupitisha sheria fulani kwa ahadi ya kukubali dili fulani la kibiashara? Je, mbunge huyo akipinga/kupitisha sheria fulani ambayo watu wanajua ina madhara kwa jumuiya kubwa lakini itanufaisha watu wachache wakiwemo wafanyabiashara wenzake, je mbunge huyo hatakuwa na mgongano wa kimaslahi?

Mimi nafikiri umefika wakati kwa wabunge wanapochaguliwa kuweka pembeni nafasi zao za uongozi wa makampuni yao hadi watakapomaliza muhula wao ili kuondoa uwepo au kuonekana kuwepo mgongano wa kimaslahi.
 
Kweli kabisa, mgongano wa maslahi ndiyo chanzo kikubwa cha upendeleo, fitina, ubabe, n.k.... With regard to systems in Tanzania, seems like everywhere you go, you gon'meet the same M&*^%"f%rs!!

How small are our judiciary, policing, regulatory systems?! I'm gutted man! It is really depressing me, you couldn't do an investigative work without finding same blood-sucking traits...tentacles of these creatures spread everywhere but belong to the same gene pool! They're really haunting our Nation! Unajua nini, labda tuweke vitunguu saum na kwato za nguruwe milangoni ili yasituingilie tu! But I bet my last dime, they'll be there too!

SteveD.
 
We need a break down to show us (Tanzanians) how did you arrived at that figure of 60 billion shillings.


GODWIN MYOVELA
Daily News; Saturday,September 22, 2007 @00:01

THE Musoma Rural Member of Parliament (CCM), Mr Nimrod Mkono, has defended payments done by the Bank of Tanzania (BoT) to his firm Mkono and Company (Advocates) as legal fees and non fraudulent transaction.

Mr Mkono told reporters in Dar es Salaam yesterday that his firm was paid realistic fees and in accordance with costs that lawyers and law firms charged clients. However, he would not want to reveal exactly how much the BoT paid him.

He was reacting to allegations by Member of Parliament for Karatu, Dr Wilbroad Slaa, (Chadema) at a public rally in Dar es Salaam last Saturday where he mentioned Mr Mkono as one of the major embezzlers of taxpayers money.

My firm has an agreement with BoT as their counsel and we defended the Governor in a disputed payment against a claimant, one Mr Valambhia and his company, Transport Equipment Ltd of a sum totalling 60bn/-, he said.

However, Mr Mkono said he had not yet decided on taking legal action against Dr Slaa, saying he would like first to see how the others who have been mentioned on the so-called list of shame reacted. The MP had mentioned a total of eight people.

Mr Mkono, head of a firm of solicitors with worldwide connections, further said that his firm also defended the Attorney General and the government in general in the case against Mr Valambhia.

Mr Mkono said that Dr Slaa should have first tried to delve deeper into the agreement with BoT before deciding to go public and start accusing his company of embezzlement.

He also rubbished claims that he owned Tanfarms Ltd, Makinyumbi Estates Ltd, Centre Point Investment Ltd, Arusha farms Ltd, Azania Agricultural Enterprises, Oxford Services Ltd and Liberty Leather Shoes Ltd as alleged by the legislator.

Comment on this Story
 
Mkuuu mbona Mkono, hakuigusa hii ishu hapa chini ambayo si ya Dr. Slaaa?


“Kuhusiana na Matumizi Mabaya ya Fedha za Debt Conversion Programme' iliyotolewa Bungeni na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Mheshimiwa Edward Oyombe Ayila mwezi Novemba 1994 ilisema yafuatayo kuhusu Mheshimiwa Nimrod Mkono: "Mhe. Spika si nia yangu kulichosha Bunge lako tukufu na hotuba ndefu lakini ni vizuri nikaelezea juu ya uhusiano unaotia mashaka"
 
Ni wiki moja sasa tangu haya majina ya mafisadi yatangazwe na ni muda wa kutosha kabisa kufanya uamuzi wa kwenda mahakamani kama tuhuma si za kweli. Lakini, anasubiri aone mafisadi wenzake watafanya nini wakati yeye ni mwanasheria.

Halafu, hakueleza ni kiasi gani amelipwa kwa ajili ya hii kesi. This suggests that hizi tuhuma ni za kweli ispokuwa anatafuta mlango wa kutokea.

Kazi kweli kweli.
 
Hizi hoja mbona hakuzigusa?

Hoja ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu ni kuwa kesi hii haina muda maalumu wa kumalizika na hivyo inawezekana kabisa malipo ya wanasheria yakazidi kiasi cha fedha inachodaiwa Benki Kuu.

Lakini hoja nyingine ya kimsingi ni kama malipo haya kwa mawakili yanaruhusiwa chini ya Kanuni za Malipo ya Mawakili na Uamuzi ya Gharama za Kesi za mwaka 1991, Tangazo la Serikali Na. 515 la mwaka 1991 (Advocates Remuneration and Taxation of Costs Rules, 1991). Kanuni hizi zimeweka kiwango cha malipo ya mawakili katika kesi ambazo fedha inayodaiwa ni zaidi ya Shilingi milioni 10 kuwa ni asilimia tatu. Kwa kufuata masharti ya sheria hii ya malipo ya mawakili, kampuni ya Mkono & Co. Advocates ilipaswa kulipwa Shilingi bilioni 1.8.

“Kampuni ya mawakili ya Mkono & Co. Advocates imekuwa ikitajwa kuhusiana na kashfa kubwa za ufujaji na/au ubadhirifu wa fedha za umma kwa muda mrefu. Kwa mfano, Taarifa ya Uchunguzi Kuhusu Tuhuma Dhidi ya Makampuni ya Tanfarms Ltd., Makinyumbi Estates Ltd., Centrepoint Investments Ltd., na Arusha Farms Ltd. Yanayomilikiwa na V.G. Chavda Kuhusiana na Matumizi Mabaya ya Fedha za Debt Conversion Programme iliyotolewa Bungeni na aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, Mheshimiwa Edward Oyombe Ayila mwezi Novemba 1994 ilisema yafuatayo kuhusu Mheshimiwa Nimrod Mkono: Mhe. Spika si nia yangu kulichosha Bunge lako tukufu na hotuba ndefu lakini ni vizuri nikaelezea juu ya uhusiano unaotia mashaka kati ya V.G. Chavda na Mashamba yake na Subash Patel mwenye makampuni ya DECO ART, MM Motors, MM Garage, Hotel Sea Cliff, City Bureau De Change na Nimrod Mkono, Wakili wa kujitegemea ambaye pia ni Mkurugenzi katika makampuni ya AZANIA AGRICULTURAL ENTERPRISES, LIBERTY LEATHER SHOE LTD., AZANIA EXIMCO, n.k. (AIMS GROUP OF COMPANIES)"

“Baada ya kuelezea uhusiano huo ulivyokuwa Mheshimiwa Ayila alimalizia kwa kusema yafuatayo: Mheshimiwa Spika, ni vigumu kabisa katika hali ya kawaida kwa mtu yeyote kuamini kwamba makubaliano haya na uhusiano uliojitokeza hapa haukuwa wa hila."

“Chavda kwa kupitia wakili wake Nimrod Mkono, aliomba Mahakama Kuu kuzuia kabisa shughuli za Kamati (permanent injunction). Aidha ni wakili huyo huyo ambaye ameshuhudia uuzaji wa deni la Deco Art (reassignment) kwa Chavda. Mheshimiwa Spika, hali hii ukiitazama kwa undani utaona kwamba pengine kuna kitu kinafichwa."
 
ukiniuliza nimdefini mkono kwa jina moja ni "Hypocrite", huyu mzee yaani bora nimuache tu amalizie siku zake vizuri.
 
kaka hujajibu kitu.
Dr slaa alichambua kiasi Mkono angelipwa kwa kazi ya kuiwakilisha BOT, sasa atuambie ni wapi si kweli na kwa vigezo gani.

ndio ni malipo hewa ambayo wamegawana kinyemela na sie walia hoi tunalia.

kilichotokea kwenye malipo mbalimbali ni wizi ambao umezoeleka sana wa kulipa zaidi ya kazi halisi na kugawana baadaye.
Ni vigumu sana mkono kukubali au kusema nini kimetokea, lakini vijana waliahoi wamejitahidi kuonyesha jinsi system inavyotuibia.

Kwasasa ni wajibu wa wananchi kuona kuwa mali na maisha ya kifahari ya watu hawa ni wizi wa jasho letu halali. Kitu muhimu kwasasa ni kuwachukia na kuwazomea kwa mayowe ya mwizi kila anayetuibia. Wakijua tunajua wasitunyanyase kwa mali zetu na kujifanya wana tuonea huruma.

Naiona siku mtanzania atakapokwenda kuchukua mali yake kwa nguvu, kwani tumechoka kufa bila dawa, tumechoka kukaa gizani kwa kukosa umeme, tumechoka kurushwa barabarani, tumechoka kupata elimu duni na tumechoka kudanganywa na hawa wezi. sasa tunameanza kuwajua mmoja baada ya mwingine.
 
Kwa mara ya kwanza sasa ninaanza kuamini kuwa Dr. Slaa, ana ushahidi wa kutosha, maana mwanasheria mkubwa kama Mkono, ansema hawezi kwenda mahakamani anasubiri reaction za wenzake?

According to ......Ze Dataz...! Mabalozi wote wa EU na US, waliwaita Zitto na Dr. Slaa, na kukaa nao chini kwa karibu masaaa kadhaa na kuzipitia data zote walizonazo hivi siku za karibuni ,

Wameionya serikali kuwa ijitayarishe kuyajibu rasmi mapigo ya DR. Slaa, ama sivyo watasitisha misaaada anytime, inasemekana kuwa DR. Slaa anaungwa mkono na wabunge karibu 75% wa bunge la UK, na tuhuma zake kutokana na historia yake na dini flani huko UK, ambayo ni ya wabunge wa huko ambao wamechangia kwa kiasi kikubwa kumsaidia kupata data alizonazo........!

Tunaendelea kuzifuatilia!
 
Mkono Slaa ni muongo
Shadrack Sagati
HabariLeo; Saturday,September 22, 2007 @00:05

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM), amejibu tuhuma za ufisadi zilizoelekezwa kwake na kueleza kuwa tuhuma hizo amezushiwa kutokana na wivu wa baadhi ya wanasheria wenzake baada ya yeye kusaidia Benki Kuu (BoT) isilipe mabilioni ya fedha za walipa kodi kwa watu binafsi.

Mkono ambaye ni wakili maarufu na wa kimataifa, alisema madai yote yaliyotolewa na Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa (Chadema) ni ya uongo yenye lengo la kuchafua jina lake.

Amemtaka Mbunge huyo aliyemwelezea kuwa ni ‘Padri wa Kanisa Katoliki' kutubu mbele ya Mungu kutokana na kumzushia madai ya ufisadi. Dk. Slaa aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).

Akizungumzia tuhuma moja moja kati ya tatu zilizoelekezwa kwake, Mkono alikiri kulipwa fedha ambazo alidai ni malipo yake halali katika kesi ya Benki Kuu Tanzania (BoT) ya kudaiwa Sh bilioni 60 na Valambhia. Lakini alisema tangu aanze kutetea BoT mwaka 2003, amefanikiwa kuepusha gavana asifungwe na kuokoa mabilioni ya fedha kulipwa kwa waliofungua kesi hiyo.

Wapinzani wanamtuhumu Mkono kuwa amelipwa Sh bilioni 8.1 sawa na asilimia ya 15 fedha ambazo BoT inadaiwa.

Mkono katika kujibu hoja hiyo hakutaja kiasi cha fedha ambacho amelipwa hadi sasa, lakini alitoa mchanganuo wa Sh bilioni 2.1 ambazo mawakili wake wa nje ya nchi wamelipwa kutokana na kushiriki kwenye kesi hiyo kuanzia mwaka 2004 hadi Juni mwaka jana.

Alisema katika kesi hiyo kampuni yake inawakilishwa na mawakili wanane. Mawakili wanne wa hapa nyumbani na wawili wa Ireland na wengine wawili kutoka iliyokuwa Czechoslovakia. Alisema wakili wa hapa nyumbani akisimama mahakamani analipwa dola 500 za Marekani kwa saa moja wakati dola za Marekani 1,000 kwa saa moja zinalipwa kwa mawakili wa nje ambao wanasaidia kwenye kesi hiyo.

Mbunge huyo wa Musoma Vijijini alisema kesi hiyo iko katika nchi tatu, Czech, Ireland na hapa nchini. Alisema ndiyo maana kampuni yake inatumia mawakili wa kigeni kuitetea Tanzania katika kesi zinazotajwa katika nchi hizo za nje.

Hata hivyo, alisema mkataba wa malipo kati yake na BoT uko wazi na haujavunja kanuni ya malipo ya uwakili kama ilivyodaiwa na wapinzani.

"BoT ni lazima watulipe fedha kila mwezi kutokana na mkataba tulioingia. Walikuja kuniomba niwasaidie baada ya mahakama kutoa hukumu ya kufungwa gavana. Sasa tumefanikiwa gavana hafungwi tena na tayari tumegundua kuwa kulikuwa na njama za kughushi," alisema Mkono.

Aliongeza kuwa katika kesi hiyo BoT ilitakiwa kumlipa Valambhia malipo ya aina tatu ambayo ni asilimia 45 ya fedha zinazodaiwa, dola za Marekani milioni 160, riba na gharama za mahakama.

Mkono alisema yeye kwa kutumia juhudi zake alizuia gavana asifungwe kama ilivyosema hukumu ya awali kabla ya yeye kuanza kushiriki kwenye kesi hiyo.

"Sasa baada ya kuzuia fedha za umma nyingi zisitolewe, mimi naambiwa fisadi. Lakini ninachotaka kusema ni kwamba walioungana na wapinzani kunichafua ni mawakili wa Valambhia kwa sababu tayari mteja wao amefariki dunia na wao wanataka malipo kutoka BoT.

"Angalia wakati kesi inaanza hawa mawakili walidai walipwe dola za Marekani milioni 9.9 (Sh bilioni 10 na sasa hivi mawakili hao akiwamo Marando (Mabere) wanaomba walipwe dola za Marekani milioni 19.8 ( Sh bilioni 23.7).

"Je, kati yangu na hawa ni wapi mafisadi?" alihoji huku akitoa vielelezo vinavyoonyeshwa kuandikwa na kampuni ya uwakili ya Marando & Mnyele ya Dar es Salaam, za kutaka malipo hayo.

Alidai baada ya yeye kuisaidia hadi BoT ikazuia malipo hayo, ndiyo maana Marando yuko mbele kushabikia madai hayo ya ufisadi yaliyoelekezwa kwake yeye Mkono.
"Hawa ni wivu tu ndiyo unaowasumbua, wanaona mimi ni wakili maarufu na nina uwezo wa kuwa na ofisi nzuri kama hii, jambo ambalo wao hawaliwezi," alidai Mkono akiwa ofisini kwake, Jengo la PPF Towers.

Marando alipoulizwa kuhusiana na tuhuma hizo, alikiri kuwa wanamwonea wivu Mkono kwa vile wamemshinda katika kesi zote ambazo yeye amekuwa anaitetea BoT, lakini ajabu ni kwamba Mkono analipwa fedha na wao wanaoshinda kesi zote, hawajalipwa hata senti moja.

Alihoji kuwa katika kesi hiyo walimshinda Mkono hadi mahakama ikaamuru gavana Daud Ballali afungwe au alipwe faini kwa kudharau mahakama. Alilipa faini ya Sh 400,000 akaponyeka kwenda jela.

Marando aliongeza kuwa kampuni yake na ya Moses Maira zina haki ya kulipwa fedha hizo kwa vile wao ndiyo wameshinda katika kesi hiyo.

"Sio siri tunamwonea wivu huyu Mkono… iweje yeye anashindwa katika kesi analipwa fedha na sisi tulioshinda hatulipwi. Angalia katika mashauri yote mahakama iliamuru tulipwe baada ya kushinda na mwenye kutulipa ni BoT, lakini mkono hataki tulipwe fedha hizo," alisema Marando.

Hata hivyo, Marando alikanusha kuwatumia wapinzani, bali alisema Dk. Slaa aliona nyaraka hizo za Kampuni ya Mkono kulipwa Sh bilioni nane kutoka kwa ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Mkono pia alikanusha tuhuma kuwa ni mkurugenzi wa kampuni mbalimbali zilizotajwa na Dk. Slaa. Aliwataja wakurugenzi wa kampuni anazotuhumiwa kama kampuni ya Azania Agricultural ambayo alisema kwa mujibu wa Wakala wa Msajili wa Makampuni (Brela) wakurugenzi wake ni Jayantikumar Chandubhai Patel, Sarbjitsingh Bharya na Alex Khalid.

Kuhusu kampuni ya Viatu ya Liberty Leather wakurugenzi wake ni Patel, Bhara na Robert Feruzi ambao pia ni wa wakurugenzi wa kampuni ya Azania Eximco.


Akizungumzia kutajwa kuhusiana na kashfa kubwa ya ufujaji au ubadhirifu wa fedha za umma kwa kushirikiana na kampuni mbalimbali za V. Chavda, Mkono alikanusha madai hayo na akaeleza kuwa yeye alikuwa wakili wa Chavda baada ya kutakiwa kuondoka nchini.


Mkono alisema yeye kama wakili ana leseni ya kutetea wahalifu hata awe muuaji, lakini kamwe hawezi kuwa mhusika kwenye tuhuma za mteja wake. Alikiri kuwa yeye alimtetea Chavda asifukuzwe nchini, hali iliyosababisha achukiwe na kulaaniwa, lakini alikuwa anatekeleza wajibu wake.

"Huyu Dk. Slaa kafunguliwa kesi kule kwenye jimbo lake, hivi wakili wake naye alihusika kwenye tuhuma anazotuhumiwa? Sasa anawaambia watu milioni 35 waamini uongo wake, anasema uongo wakati yeye ni Padri! Kwa kweli sijawahi kusikia wakili akitetea kesi naye anakuwa mtuhumiwa," alisema.
Kuhusu tuhuma kuwa yeye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Oxford Service Ltd na Marcus Ltd ambazo zilifaidika kupata Sh bilioni 4.5 chini ya utaratibu wa uuzaji wa madeni (Debt Conversion Programme), Mkono alisema hizo ni kampuni za kigeni ambazo zilikuwa wateja wake katika mpango huo wa DCP.

Alisema mpango wa kuuza madeni kwa dola ulisaidia taifa kupata fedha za kigeni "Sijui nisingekuwa mimi hii nchi ingekuwa wapi leo hii, maana mimi nilisaidia kuwa wakili wa kampuni hizi na mpango huo ukafanikiwa. Je, kuwa wakili ni ufisadi, ufisadi wangu uko wapi hapa?" alihoji.

Alisema anashangaa kwamba ‘Padri' Dk. Slaa anaomba Mungu majina yabadilishwe kwenye kampuni hizo na jina la Mkono liwamo. Alisema Mbunge huyo alipaswa kwenda kumuuliza yeye Mkono kuhusiana na kuhusika kwake na kampuni hizo na siyo kukurupuka kumtangaza kuwa yeye ni fisadi wakati yeye anafanya kazi ya uwakili.

Pia alimshangaa Dk. Slaa kumdhalilisha Rais Jakaya Kikwete kuwa ni fisadi. Alisema demokrasia ya vyama vingi inatumiwa vibaya na akahoji kutokuwapo kwa sheria ambayo inapiga watu marufuku ya kumtukana rais.

"Angalia rais yuko Marekani anasaka fedha kidogo zije zitusaidie, lakini kuna watu huku nyuma wanamtukana, hiyo ndiyo demokrasia kweli?" alihoji Mbunge huyo.

Mkono ni miongoni mwa viongozi 10 waliotajwa na Dk. Slaa wakituhumiwa kuwa ni mafisadi ambao wanaitafuna nchi. Mbunge huyo aliwataja kwa kushirikiana na Tundu Lissu ambaye ni mwanasheria kama njia ya kuwashtaki viongozi hao kwa wananchi.
 
Kiini cha mgogoro ni Serikali kumlipa Nolan badala ya Marehemu Valambhia.

So In the first place, why pay Nolan , wakati commission agent alikuwa Valambhia, Kwanini serekali imli amua kuingia ktk internal conflict kati ya nolan na valambhia badala ya kusubiri arbitration au uamuzi wa competent court, na ukitilia manani hii ni kesi ya kimataifa , then ingekuwa international court or arbitration, badala ya mahakama zetu za bongo
 
Hapo tusingekuwa tume tumia fedha nyingi, because we were not part of the Problem, labda cost ya filing cost of the issue na postage, lakini hao ndugu zetu kwa kuwa wana penda kutafuta njia za kutolea hela, basi hutengeneza Bomu wenyewe , then wana lilipua wenyewe, then wanakwenda kuzima wenyewe.

Kwa hiyo ndo kusema kwamba hiyo kesi tulijitakia wenyewe? Ama kweli hela za Bongo ziko nje nje na hazina mwenyewe. Ndiyo maana kesi inasemekana haina mwisho.

Kwa mwendo wa kulipwa dollar 500 kwa saa, nadhani within the next 10 yrs jamaa atakuwa ameishalipwa fedha nyingi kuliko hata deni linalotetewa na hatuji outcome ya kesi!
 
Mkono mtamlipa na at the end of the day Marehemu Valambhia naye atapata chake so tutakuwa tumelipa twice.

How do you find it. very sweet to Mkono and his Friends, then watakwambia from then hakuna Rushwa na Biashara ni ya ushindani, kazi ni za Ushindani , Siasa ni za Ushindani, maana wao kianzio wanacho
 
Give us that break down please! So how many hours did you charge BOT to arrive at that figure of approximately $8 million? Do you charge other clients the same rate or you overstated your hourly rate just because of the financial ability of BOT? Colleagues in your field do they charge the same rate?

I don't come cheap - Mkono: Going rate is up to $1,000 an hour

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

PROMINENT Dar es Salaam lawyer Nimrod Mkono yesterday publicly admitted that his legal fees are truly expensive, and declared that his law firm was actually 'underpaid' by the Bank of Tanzania with regard to services rendered in the long-running Valambhia case.

''Yes, I am expensive and I use expensive lawyers�I charge my fees based on individual cases,'' Mkono, managing partner of Mkono & Company Advocates, told a news conference at the firm's city offices.

He told reporters that the firm's going rates range between $500 (local legal fees) and $1,000 (international fees) per hour - amounts which he personally described as still being somewhat low.

''The BoT was at liberty to hire me or go for somebody else who is a lot cheaper. But my client is so far comfortable with my services,'' said Mkono, who is also Member of Parliament for Musoma Rural Constituency on a ruling party CCM ticket.

The lawyer-cum-businessman-cum-politician called the news conference to respond to his inclusion in a list of prominent Tanzanians alleged by opposition legislator Dr Wilbrod Slaa (Karatu-CHADEMA) to have been involved in various, multi-billion shilling shady deals with the government over the past seven years alone.

He denied Dr Slaa's assertion that he (Mkono) had overcharged the BoT for services rendered in relation to the Valambhia case, stating that the payments were well within legal limits.

When asked to state the total amount of legal fees paid by the central bank to his law firm so far, Mkono would not give an exact figure, but estimated it to be around $8m (approx. 10bn/-).

Out of this, he claimed, the law firm paid a total of 2,184,890,934.93 euros (approx. 4bn/-) to external consultants on the case between 2004 and last year.

According to regulations under the Advocates' Remuneration and Taxation of Costs Rules, 1991, legal fees are not allowed to exceed the equivalent of 3 per cent of the principal amount in cases where the amount in dispute is more than 10m/-. In the case being defended by Mkono's company, the BoT is challenging payment of $55,099,171.66 (approx. 72bn/-) to Devram Valambhia in civil case number 210 of 1989.

Mkono also distributed a document to journalists showing that the principal amount and interest in the amount being demanded by Valambhia had by September 3 this year accumulated to $111.881m (over 141bn/-).

Frequently referring to Dr Slaa as 'Father Wilbrod', Mkono said the CHADEMA MP had declined an invitation to his office to discuss the matter of his being included in the widely publicised 'List of Shame', ''so that we can reach some sort of a common understanding on this thing''.

The latest report of the government controller and auditor-general (CAG) has raised audit queries on a total of 8,128,375,237/- paid by the BoT to Mkono & Company Advocates in stated legal fees up to the end of last year.

The CAG report described the fees as 'excessive' and advised the BoT management and governor Daudi Ballali to ditch Mkono in favour of a much cheaper law firm.
 
Kwa hiyo ndo kusema anatucheka ujinga kwa kumlipa those carzy money eeh...
 
OOH yes, he's not a cheap thief, for he's only involved in high calibre public funds swindles!

SteveD.
 
Back
Top Bottom