Nina $ 23,000 ila sijui biashara gani inanifaa

Kila biashara inamitihani yake. Usifikiri hardware hawafirisiki mkuuu. Au usifikiri wote waiofanya biashara za kusafirisha maliasili walifilisika. Kila mmoja katika field yake na kwa bahati mbaya au nzuri kila aina ya biashara au shuguli inamatajiri wa kutupwa na pia inamasikini wa kutupwa.
Tazama kilimo, madini, wauza mandazi etc utangundua kuna matajiri na masikini
 
Ni sawa ulichoongea ndio maana nimekupa like. Lakini milioni 20 kwa hardware ni ndogo sana mkuu
 
Wazanzibari nao wanatolea macho hizo fursa hapo "kwao" sasa wewe "Chogo" ndo ukajidai unajua kukamata fursa kwao. Hawachelew kukutoa dv
Kujaribu ndio kila kitu mimi niko huku mbona hakuna swala kama hilo huwa nakodi magari sometimes kazi yangu inajumuisha sana watu so vipindi kadhaa inabidi nipate magari ya ziada hapo nakodi kwa watu , so naona sana uwanja wa wanaokodisha magari kikubwa kua na mtu wa kumpa abc, tena hata usimamii unazikabidhi kwenye kampuni mnakubaliana kiasi zinakua kwenye kampuni husika wewe unakaa kando unakula hela yako tu taratibu. Kikiwa kipindi cha high season ambayo kwa Zanzibar ni kuanzia mwezi wa saba mpaka mwezi wa nne kama hujawahi booking na kama hujulikani basi hata magari hupati yote yanakua occupied
 
Mi nikopeshe $3000 kwa mwaka nakupa 20% mkataba wa miaka miwili. Meaning after 2yrs narudisha $4200
 
Unamzungumzia Abdillahi Lali (kibabu)??
 
Huu ushauri mzuri mkuu nitaufanyia kazi siku nikikamilisha hlo duka nitarudi kwako
Ushauri wangu ni huu mkuu: Usimwamini mtu YOYOTE kwenye suala la fedha hata awe ndugu yako labda uwe una uhakika naye. Simamia kila kitu peke yako kama inawezekena. Usipofuata ushauri wangu nina uhakika utarudi hapa ukiwa umeshalizwa! Kila la kheri.
 
Nimepitia Uzi huu mwanzo mwisho. Nipo kwenye ujasiriamali since my graduation in 2013 ninaweza nika recommend with my greatest experience all are here are just ideal and will remain Ideas. Any one can try but does not guarantee success. Kwa mawazo mengi yaliyoko hapa yanaeleza kuwa tatizo pekee linalokwamisha success ni mtaji na kwa kuwa unao no any problems litakukwamisha. Mtaji wako ni mkubwa sana na ni mdogo sana itategemea na wazo utakalochagua. But kumbuka biashara au miradi iliyofanikiwa imetegemea sana muongoza njia katika mafanikio hayo. Ndiyo maana wasitafu wengi au watu wanaopata mtaji kwa namna yeyote na wasiwe na uwezo wa kuongoza njia ya miradi yao huwa wanaishia kukwama.


All the best kwa kupata mtaji but mtaji pekee siyo kikwazo cha mafanikio.
 
Asikudanganye mtu na taxi. Biashara ya taxi huwa inamnufaisha dereva tu. Ninao uzoefu huo. Ni uzoefu mbaya. Mwenye mali anakuwa mtu wa kumfanyia service na matengenezo dereva.
N kazi nzur mkuu ila kwa mimi uwa nna amini nyumba kuliko ngari,
 
Ukitaka kulia kwenye biashara basi vamia biashara ya magari. Hayo mahesabu uliyopiga; kwenye field hayaendi smooth namna hiyo. Ni watu wengi wanalia kuhusu hii biashara kwani madereva wengi si wa kuaminika kabisa.
 
Ukitaka kulia kwenye biashara basi vamia biashara ya magari. Hayo mahesabu uliyopiga; kwenye field hayaendi smooth namna hiyo. Ni watu wengi wanalia kuhusu hii biashara kwani madereva wengi si wa kuaminika kabisa.
Unatoa gari kwa kila Mtu? Mi natoa Gari kwa mtu mwenye Familia ambaye hata kwa muonekano awe decent
 
Buy Bitcoin
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…