Nina kiasi cha shilingi milioni 3. Nataka nifungue sehemu ya chips, kuku, mishkaki, Je mtaji unatosha?

Nina kiasi cha shilingi milioni 3. Nataka nifungue sehemu ya chips, kuku, mishkaki, Je mtaji unatosha?

Sasa kama pango ni laki tatu alafu mtu anataka kodi ya mwaka na inabidi ufanye refurbishment ya mamilioni ya pesa itatosha vipi ?

Lakini kama unaweka mwanvuli na viti vya plastic, kabati la aluminium na jiko la mkaa kwanini isitoshe na kubaki ?

Haya mambo mengine huenda hata pesa sio kigezo unaweza ukawa na laki nne tu unaanza kwa kukodi vitu na kununua viazi mali kauli sokoni na ukapata faida kuliko aliyeweka mamilioni na mzigo unalala daily...
Ndio maana akaja kuomba ushauri kwanza.
 
Hiyo pesa inatosha kuanzia kabisa. Kama ulivyoambiwa,kwanza angalia wapi unaweka biashara yako, umewalenga kina nani: vitu vyote hivyo ulivyoorodhesha, kwa mkupuo utaferi. Kumbuka, kuna kukodi eneo la kazi, kuna mzigo kutoisha. Cha kufanya zunguuka maeneo si chini ya kumi. Kama mteja, soma mazingira,ujue wengine wanafanyaje, ulinotisi kitu gani ambacho kimekuvutia na kimekuwa mfano wa kuigwa. Na labda swali: kwa nini unataka hiyo biashara ya hivo! Wakati zipo nyingine zinazoweza kuzunguusha hela?
 
Lakini hii biashara ili utoboe unahitaji uwe na mtaji mm baada ya kufanya mda kidg mtu akanipa connection mbele ya night club asee na kuna mwamba akanipa connecfion ya kuku kutoka malinyi nkamtafta mama malinyi akawa ananipakia kwenye gari ya master j kipind hicho napokelea town asee kwenye kuku ndio nilipiga hela nkawa nachoma chips kuku kuanzia saa tatu usiku mpka saa tisa alfajir naamsha zangu sema nilifanya ndan ya miez 3 tu nkaswitch kweny mchong mwingine
Mkuuu mimi nimefunga location imeniua, nina vyombo najipanga upya
 
Zingatia kinachouzwa NI chips ambayo NI viazi gunia NI Kama laki moja mafuta NI Kama lakimoja deep fryer ya kuanzia Kama laki 2..sahani 10 chumvi na zaga nyingine...ukiipata chumba au sehemu huo NI mtaji mkubwa japo naamini wateja ndio mtaje he unao...unaweza kuanzia kutafuta wateja huku hujui kazi nenda kajitolee kwa mwamba mmoja hata wale wa club night ...UTAPATA kitu Cha ziada ndio uingie
 
Nina kiasi cha shilingi milioni 3. Nataka nifungue sehem ya chips , kuku, mishkaki samaki juice na vinywaji sio vilevi.

Naombeni ushauri kuhusu mtaji huo unatosha? Na vipi Faida na changamoto zake
Inatosha na chenji kubali, Labda pamoja na vifaa,sahani,jiko,karai,Bado inatosha
 
Back
Top Bottom