StudentTeacher
JF-Expert Member
- Jan 30, 2019
- 4,153
- 4,301
Hili nalo nenoOgopa sana nguvu ya pesa kuna watu wana pesa ila hawatoki nje na kujitangaza ila michezo wanayoifanya ndani ya system ina athari kubwa sana kwa wananchi wa kawaida kwao ni kama wanacheza game kwenye simu na wanaona ni raha sana.
Kama kawekwa na yeye si atawatupia lawama walimuweka?. Sioni shida hapo.Mama anatakiwa akuamini asimame Kama mkuu wa nchi Mana Mambo yakiharibika hawezikwepa lawama.
Lugha ya kidiplomasia hiyo ili wasikio wasihisi kwamba ye "dikteta". Au unataka awe anafoka?. Usisahau ile ya "ukinizingua tutazinguana"?Hebu imagine ' raisi hana hata kujiamini, kila mara kauli ni ''naombeni mkalifanyie kazi'' je, ni nani wa kufanyia/kutatua matatizo ya wananchi kama sio yeye mwenye mamlaka yote? Aagize jambo na litendeke chap. Sasa ni nani huyu chifu huwa anawaomba wamfanyie kazi?
Mpya ya namna gani?. Ya hovyo zaidi au Nzuri zaidi?Tuamke kichwani na moyoni yapo na yanakuja tujipange kiakili na kimwili pia. Tanzania mpya is coming soon [emoji3589]
Kufanya uchaguzi tena ni gharama mkuu.Tozo kwenye benk zilianza muda ila hawakutaka kuweka wazi, kama una mtu benk muulize.
Kitu ambacho natamani kiondolewe kwenye katiba ni ile rais akifa, maaidizi wake achukue nchi aiseee hii ni kitu ya kipumbavu.
Ila aliecheza hii movie kuanzia kuondoka jpm aliicheza haswa, mwenyewe yupo amekaa anaset mitambo inaenda kama atakavyo dah.
Hitaji la Katiba Mpya mwangwi wake unazidi kusikika kuliko wakati mwingine wowote.
Kwa nje tu hivi ni kama kila kitu kinaenda sawa lakini kuna hali fulani ya taharuki ya kimya na sintofahamu kubwa ndani yake.
Ni kama kuna mambo yanapangwa huko halafu yanaletwa upenuni bila hata kueleweshwa vema
Kiongozi mkuu ni kama kawekewa mipaka mingi na kutengwa na hadhira.
Anahangaishwa huko na huko na kuwekwa busy kwa mambo ambayo yalistahili kufanywa na wasaidizi wake.
Kuna hofu fulani miongoni mwetu. Kuna uoga umewashika watu ni kama vile kuna jinamizi kubwa lisiloonekana linatuchungulia na kutufuatilia na kutusikiliza
Si kama nchi iko kwenye auto mode la hasha. Bali kuna kikundi cha wachache ndani ya mfumo pengine ndio kimeyateka mamlaka!
Watu hawasikiki lakini wapo
Watu hawaonekani lakini vitendo vyao unaviona!
Tunanyukwa kimyakimya!
Hii hali haina afya kwa taifa na haipaswi kuendelea kwa muda mrefu. Hawa wanaozungukana huko ndani hawana nia njema na taifa hili. Sinema si kwamba zimeisha bali zinaandaliwa zingine kutuweka busy tena tuyasahau haya!
Kama hizi hisia zangu ni kinyume na uhalisia basi napaswa kuonana na tabibu haraka! Ila kama si kinyume. MUNGU TUSAIDIE
Ukiona hivyo ujue watanzania wanataka Katiba Mpya itakayowashape viongozi na siyo viongozi kuishape katiba.Ndio maana kila ajaye huonekana hatoshi.Nchi ngumu sana hii, wakati mwingine uwa najiulizaga Watanzania tunataka kitu gani haswa! Ni aina gani ya kiongozi tunayemtaka ambaye atafaa? Nyerere hakufaa, Mwinyi hakufaa,Mkapa hakufaa, Kikwete hakufaa, Magufuli hakufaa,Huyu wa sasa hafai sasa itabidi turekebishe katiba ili ikiwezekana tukakodi kutoka mataifa mengine. Na mara zote hawa watoaji kasoro ubadilika kutokana inategemea ni nani aliyepo madarakani wakati huo hawa watu mara nyingi kama mara zote wanakuwa na sababu zao sirini lakini hadharani utafuta sababu nyingine yoyote kuonesha udhaifu wa huyo wanayempinga ili kutafuta uungwaji mkono.
Mwendazake alikuwa hajali kelele?. Nadhani huyu wa sasa ndio hajali. Ukimsema kwamba anasafisafiri hovyo ndio kwanza kesho yake yupo Rwanda huko.Ukilalamikia tozo anakwambia "tozo ziendelee". Yule alikuwa analalamikia hadi katuni za akina Masudi.Dah, yaani acha tu mkuu! Wakati mwingine unatafakariii mwishowe unaamua kunyamaza tu ili maisha yaendelee.
Ili uongoze bila presha nchi hii inabidi usiwe mtu wa kujali.....yaani we fanya yako tu. Mwendazake alifanikiwe sana katika hilo. Ye alikuwa anakanyaga tu; kelele za kutojua kiingereza, sijui hana exposure n.k aliwaachia wenyewe wazungumzaji na alipoamua kuwalipa basi alilipa kwa 'vitendo' tu wakati wa uchaguzi. Nafarijika kuona na mama nae kama anafuata njia hiyo hiyo ya kutokujali.......
‐ mwanzo ilianza kikwete ndo anaongoza nchi, naona limekufa sasa na mama anaendelea tu na yake!
‐ likaja eti 'haijui nchi', mama akaendelea na yake na limekufa!
‐ mara nchi imerudi kwa mafisadi, kwamba kwenda kwake Kenya n.k ni kwenda kusaini mikataba ya kinyonyaji (eti hajui lolote). Mama kimya anaendelea na yake
‐ Royal tour hamna kitu, kwanza mliona wapi raisi anatangaza utaliii! Mama kimya na ndo kwanza anazidi kutembelea vivutio! Safi kabisa.
‐ na leo hili, kwamba kuna kikundi kinaongoza nchi 'bila raisi kujua'! Hahahahaaaaa!!!
Wakati tunayaongea, hayo mama analipa vitendo;
1. Tozo (‐ or +)
2. Sgr
3. Umeme wa rufiji
4. Vituo vya afya n.k.
Mimi sijui nikoje?. Mtu asipokuwa na utu hata ajitape kwa lipi katu siwezi kumuelewa.Hatimaye watu wameanza kukubali kuwa Magufuli alikuwa shujaa na kiongozi mwenye maono.
Muache atafute hela aajiri vijana. Machinga wapungue aisee. Huku kwenye sekta binafsi vijana wananyanyasika sana.This is not right..sio kwa manguo hayaView attachment 1929671View attachment 1929672
Kushoot muvi haja-decide?Ndio ilivyo , Ni ukweli mtupu , mama ni symbolic leader , wamemblock kuongea na marais wastaafu , pia wamemfanyia enslavement , she has no authority or anything to decide .
Hivi kuna mtu mwenye akili timamu hawezi kuwa Rais wa nchi hii?sio hakujiandaa kuwa rais hata angejiandaaa alikuwa hawezi na hata weza
Kuna wakati nailaumu sana Corona kushindwa kuwapangusa hawa wajinga hapo angetembea na miskafu ya benderaMkuu nchi iko mikononi mwa kikundi kinachoitwa Axis of Evil na Kiongozi wao ni gaidi Mwigulu Nchemba kwenye kundi hilo yuko Majaliwa, Ndugai, Mpango, Msigwa, Diwani wa TISS, Ndugulile. Hawa watu ni watu hatari sana na sijui nchi itakuwa mikononi mwa hawa kwa kipindi gani.
Kirahisi ivooo mkuu??Nina mashaka tutampoteza CDF siku si nyingi
Umewahi kumwambia hitaji lako na akakusikiliza? Au wasaidizi wake wanaropoka na yeye hasemi kitu na kushindilia tu wananchi wamekubali.Kikundi hicho ni sisi wananchi ambao kiongozi wetu ni Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan. Una jengine?