Nina mashaka kuna kikundi ndio kinaendesha nchi kwa sasa

Nina mashaka kuna kikundi ndio kinaendesha nchi kwa sasa

Yote kwa yote. Mimi kama raia wa kawaida ningependa rais wetu awe anatokea kwa nadra. Labda kila baada ya miezi mitatu.

Na akitokea nchi inasimama kusikia yaliyofanyika, yanayofanyika na matarajio.

Akitokea anakuja na suluhu za mambo makubwa yenye matokeo makubwa.

Mtindo wa mkuu wa nchi kuonekana kila siku yupo wapi, anafanya nini ni kama kumchosha tu na sisi raia kumzoea kama wa kawaida na kupoteza hamu ya kumsikiliza.

Mawaziri ndio askari wa miavuli, hao ndio wa kuhangaika na kutoa mrejesho na anae kwamisha anasaidiwa inavyo stahili.

Ni maoni tu yanaweza kupuuzwa.
Ilikuwa hivo wakt wa JPM, mawaziri walisikika kila kona ila kwa sasa naona kasi imepungua sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hitaji la Katiba Mpya mwangwi wake unazidi kusikika kuliko wakati mwingine wowote.

Kwa nje tu hivi ni kama kila kitu kinaenda sawa lakini kuna hali fulani ya taharuki ya kimya na sintofahamu kubwa ndani yake.

Ni kama kuna mambo yanapangwa huko halafu yanaletwa upenuni bila hata kueleweshwa vema

Kiongozi mkuu ni kama kawekewa mipaka mingi na kutengwa na hadhira.

Anahangaishwa huko na huko na kuwekwa busy kwa mambo ambayo yalistahili kufanywa na wasaidizi wake.

Kuna hofu fulani miongoni mwetu. Kuna uoga umewashika watu ni kama vile kuna jinamizi kubwa lisiloonekana linatuchungulia na kutufuatilia na kutusikiliza

Si kama nchi iko kwenye auto mode la hasha. Bali kuna kikundi cha wachache ndani ya mfumo pengine ndio kimeyateka mamlaka!
Watu hawasikiki lakini wapo

Watu hawaonekani lakini vitendo vyao unaviona!

Tunanyukwa kimyakimya!

Hii hali haina afya kwa taifa na haipaswi kuendelea kwa muda mrefu. Hawa wanaozungukana huko ndani hawana nia njema na taifa hili. Sinema si kwamba zimeisha bali zinaandaliwa zingine kutuweka busy tena tuyasahau haya!

Kama hizi hisia zangu ni kinyume na uhalisia basi napaswa kuonana na tabibu haraka! Ila kama si kinyume. MUNGU TUSAIDIE
NJOZI NJEMA MWANA WANE,MAMA ANAFUFUA UPYA UCHUMI WA TAIFA LETU MAARIBIFU YALIKUWA NI MAKUBWA MNO TUVUTE SUBIRA KIDOGO TUKUKUMBUKE KILA MAMLAKA PIA NI KIKUNDI,HATA YULE BWANA PIA YALIKUWA NA KIKUNDI CHAKE CHA "WANA"AU ORCHESTRA TETEMESHA
 
Uzuri ni kwamba huyo unayemtaria mabaya pengine anakula zake kiyoyozi kwenye gari yake wewe hapo Unapambana na bomba kwenye dala dala, yaani roho ya kimasikini ni shiidaa..
Kamanda bhana...hamueleweki
 
Unaweza kufanyiwa maombi mabaya apanguswe na kale kaugonjwa... Hivi msaidizi wa mkuu yupo wapi?
Alipigwa pin na system baada ya kuonekana sana front bila maelekezo ya mkuu siku za awali za utawala mpya
 
Kwa Magufuli mlikuwa mnasema ajipangia kwa ubabe!

Ila kwa huyu mnasema anapangiwa na anaonewa!

Ndio maana Lema juzi aliawaita wapumbavu
Kuna vingi hujui na inahitajika muda mwingi kukuelewesha
 
Magu nilikuwa simkubali ila bora angemalizia usheenz wake hafu ndo afe sio kutuachia nchi katika mvurugano na huyu mama.
Tartiiiiiibuuu wakulungwaaa wanaanza kurudi kwenye musitarii wa kumkumbuka jpm....na bado mtaendelea kumkumbukaa nasemaaaa...hapa ndo mwanzo tuu..picha kamilii linaletwaa na kina madiluuuuu
 
Hitaji la Katiba Mpya mwangwi wake unazidi kusikika kuliko wakati mwingine wowote.

Kwa nje tu hivi ni kama kila kitu kinaenda sawa lakini kuna hali fulani ya taharuki ya kimya na sintofahamu kubwa ndani yake.

Ni kama kuna mambo yanapangwa huko halafu yanaletwa upenuni bila hata kueleweshwa vema

Kiongozi mkuu ni kama kawekewa mipaka mingi na kutengwa na hadhira.

Anahangaishwa huko na huko na kuwekwa busy kwa mambo ambayo yalistahili kufanywa na wasaidizi wake.

Kuna hofu fulani miongoni mwetu. Kuna uoga umewashika watu ni kama vile kuna jinamizi kubwa lisiloonekana linatuchungulia na kutufuatilia na kutusikiliza

Si kama nchi iko kwenye auto mode la hasha. Bali kuna kikundi cha wachache ndani ya mfumo pengine ndio kimeyateka mamlaka!
Watu hawasikiki lakini wapo

Watu hawaonekani lakini vitendo vyao unaviona!

Tunanyukwa kimyakimya!

Hii hali haina afya kwa taifa na haipaswi kuendelea kwa muda mrefu. Hawa wanaozungukana huko ndani hawana nia njema na taifa hili. Sinema si kwamba zimeisha bali zinaandaliwa zingine kutuweka busy tena tuyasahau haya!

Kama hizi hisia zangu ni kinyume na uhalisia basi napaswa kuonana na tabibu haraka! Ila kama si kinyume. MUNGU TUSAIDIE
Na badooo..ww c ulikuwa unamnanga jpm..naamn kwenye libichwaaa lako unammsii sanaa jpm..subirr kidogoo utapataa
 
Back
Top Bottom