Nina maswali mengi mno juu ya 'Maelezo Tatanishi' haya kama Critical Thinker, ila naomba Kwanza nanyi muulize yenu ili atujibu mbashara

Nina maswali mengi mno juu ya 'Maelezo Tatanishi' haya kama Critical Thinker, ila naomba Kwanza nanyi muulize yenu ili atujibu mbashara

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Mwanaharakati na mhariri wa kujitegemea, Maria Sarungi, amesema baada ya kuachiwa jana usiku na watekaji, walimtaka asiongee na mtu yeyote na asizungumze chochote kuhusu tukio hilo.

Maria amesema hayo leo, Jumatatu Januari 13, 2025, alipozungumza na waandishi wa habari jijini Nairobi kuhusu utekwaji wake.

“Walivyoniachia ilikuwa usiku—nakumbuka waliniteka kati ya saa 9 alasiri na walivyoniachia, waliniambia nisiongee na yeyote na nisiseme chochote. Ninachokumbuka, walitaka simu yangu na walikuwa wanazunguka nami huku wakisema wanamsubiri bosi wao. Nikawauliza, 'Kumbe mna bosi?' Walikasirika kwa kuhisi nimeanza kujua mipango yao,” amesema Maria.

Maria amedai kuwa watekaji hao walimuachia baada ya vyombo vya habari na taasisi mbalimbali za kimataifa kupaza sauti.

“Nawashukuru vyombo vya habari kwa kupaza sauti, na watu, wanasiasa mbalimbali kwa kupaza sauti, pia nawashukuru mabalozi na Serikali za Umoja wa Ulaya na wanaharakati mbalimbali. Maana sauti zao ziliwafanya watekaji wasite kuendelea na mipango yao,” amesema Maria.

Chanzo: mwananchi_official

Na ndiyo maana Asubuhi ya leo baada ya kuona kuna Kujichanganya Kwingi (hasa Kimaelezo) kutatokea kama Muona Mbali na Mbarikiwa wa kuwa na 6th Sense Kiasili nikamuomba asizungumze kwani ataenda Kuharibu na inaweza hata kumletea matatizo baadae na akaja Kujutia huku wale ambao leo Wanamsifu na kumpa Kichwa wakakaa nae mbali pale yatakapomkuta.
 
Sema script nyepesi sana hii hao wana harakati na serikali ya umoja wa ulaya ndio imedhamini kwenda kuzungumzia kenya.
Pesa zitatuua bongo. Njaa hii mungu aiondoe tuone mengi.
Uchawa kila mahali


"walivyoniachia ilikuwa usiku—nakumbuka waliniteka kati ya saa 9 alasiri na walivyoniachia, waliniambia nisiongee na yeyote na nisiseme chochote. Ninachokumbuka, walitaka simu yangu na walikuwa wanazunguka nami huku wakisema wanamsubiri bosi wao.. . . . . . . . Hawana sehemu walikokubaliana na boss wakutane yaani waliagizwa wakukamate kisha wazunguke na ww hadi boss aseme tukutane kimara au sijaelewa

Nikawauliza, 'Kumbe mna bosi?' Walikasirika kwa kuhisi nimeanza kujua mipango yao,” . . . . . . Kwamba hawa wauaji kuwauliza kama wana boss ndio wakasanuka utajua mambo yao. Halafu walikuteka wakakuacha unazungumza hawakukuziba domo hilo. Au walikuwa wanajifunza kuteka
amesema Maria.

Maria amedai kuwa watekaji hao walimuachia baada ya vyombo vya habari na taasisi mbalimbali za kimataifa kupaza sauti.

“Nawashukuru vyombo vya habari kwa kupaza sauti, na watu, wanasiasa mbalimbali kwa kupaza sauti, pia nawashukuru mabalozi na Serikali za Umoja wa Ulaya na wanaharakati mbalimbali. Maana sauti zao ziliwafanya watekaji wasite kuendelea na mipango yao,” a. . . . Ila walipaza sauti ww ukaachiwa hawajakudhuru ila akina lisu japo walipaziwa sauti na wengine bado walidhuriwa vile vile na kuuliwa. Kwamba watekaji wanaogopa sauti za mabalozi wa serikali za ulaya hata kuacha kufanya wanayoyataka

Au basi wengine najua wameelewa mimo siajaelewa hili tukio naona kama la mchongo hv
 
Back
Top Bottom