Nina miaka 45, nimeshafungua maduka 11 sasa nimefilisika

Nina miaka 45, nimeshafungua maduka 11 sasa nimefilisika

Nimesoma mwanzo mwisho sijaona sababu za kufilisika!
-Wateja walipungua?
-Ushindani uliongezeka?
-Gharama za biashara ziliongezeka?
-Ulishindwa kusimamia (usimamizi mbovu)?
-Au figisu/uchawi/umefilisiwa kimkakati?
 
Jambo la ibada sikuwahi kulizingatia sana nilikua naona muda haunitoshi kufanya sala 5 mara nyongine zilikua zinanipita na kuhisu kutoa nilianza nilipoona mambo yamenikubali kibiashara na mzunguko ulikua mzuri lakin saiv niko bench nafanya sala zote na nimejifunza utamaduni wa kutoa kila ninachokipata.
Ulikuwa unakumbuka asilimia 2.5 ya zakka? Maana ile ni muhimu sana kwetu sisi waislamu.

Aidha kuwa na maduka mengi siyo jibu la biashara hasa kwa kwetu maana unaweka ndugu zako ambao ndiyo wanakufilisi kwa vile wanaona mali ya kaka au baba mdogo haina hesabu.
 
Kama ulifilisika 2016 kipindi cha kuanza upya ni sasa...nakushauri yafuatayo....
1.Badili Marafiki kabisa...
2.Usiongee Mambo yako kabisa kwa mtu hata ndugu yako
3.Biashara ya simu imebadilika kidogo tafuta mtaji tafuta simu used za Dubai...uza kwa oda na uzia wateja waKo..
4.Naamini ulikua na asset uza moja iwe mtaji...


Pole ila Pambana mm utawala 2016-2021 march hali ilikua mbaya ila nimekaza kuna hatua nimepiga...
Haaaaa Haaaaa 😂, hili janga lilitupitia wote, isitoshe kusema kuwa hali ngumu ya biashara imefanya kuongezeka kwa wafanyabiashara wengi na bidhaa nyingi zinafanana
 
Ulikuwa unakumbuka asilimia 2.5 ya zakka? Maana ile ni muhimu sana kwetu sisi waislamu.

Aidha kuwa na maduka mengi siyo jibu la biashara hasa kwa kwetu maana unaweka ndugu zako ambao ndiyo wanakufilisi kwa vile wanaona mali ya kaka au baba mdogo haina hesabu.
Zaka ngumu sana sadaka inawezekana
 
Zaka ngumu sana sadaka inawezekana
Hapana, zaka ni lazima ili uweze kupata mafanikio. Siku nyingine utakapojipanga vyema Inshallah, weka hiyo kama vile unavyoweka kodi ya TRA.

Bila ya hivyo utakuwa unafanya kazi ya kujaza maji kwenye ndoo mbovu.
 
Hapana, zaka ni lazima ili uweze kupata mafanikio. Siku nyingine utakapojipanga vyema Inshallah, weka hiyo kama vile unavyoweka kodi ya TRA.

Bila ya hivyo utakuwa unafanya kazi ya kujaza maji kwenye ndoo mbovu.
Hamna hata bahresa hatoi zaka anatoa anavopenda mwenyewe kama sadaka.
 
Nilianza biashara pemba mwaka 94 nikahamia dar mwaka 2007 mambo yaliponichanganyia.
Sasa nimekuelewa na nimeelewa chanzo cha "kushindwa" kwako kwenye hiyo biashara ya maduka; ulikuwa kijana mdogo wakati unaanza hizo biashara, kimahesabu naona ulianza biashara ukiwa na miaka kumi na nane! Sasa ukianza biashara, utashinda tu! Anza usikate tamaa.
 
Nimesoma mwanzo mwisho sijaona sababu za kufilisika!
-Wateja walipungua?
-Ushindani uliongezeka?
-Gharama za biashara ziliongezeka?
-Ulishindwa kusimamia (usimamizi mbovu)?
-Au figisu/uchawi/umefilisiwa kimkakati?
Mkuu jibu hili kwanza halafu tuendelee.
 
Awamu ile nilisema ngoja nijaribu biashara. nikafungua duka la kawaida la jumla lilifilisika kabisa na kuniachia baadhi ya madeni.
Baadae niligundua kosa kubwa ilikua sina rekodi nzuri ya mwenendo wa biashara, sina kumbukumbu ya matumizi na mapato, nilikua nachanganya hela yangu na ya biashara, nilikua sifuatilii vizuri benki nimetoa nini na nimebakisha nini na mwisho nilikua na matumizi binafsi yasiozingatia bajeti wala ukubwa wa biashara. kwa ufupi kwa mtazamo wangu nilifilisi biashara yangu kwa (Poor management of my business)
Pole
 
Back
Top Bottom