Nina miaka 45, nimeshafungua maduka 11 sasa nimefilisika

Nina miaka 45, nimeshafungua maduka 11 sasa nimefilisika

Ninaomba kusaidiwa mchango wa mawazo tatizo ni nini mpaka muda huu nimefilisika kabisa. Mwisho ndani ya miaka mitatu nimefilisika maduka 5. Ambayo nilikuwa nalipia kodi laki 5 kwa mwezi.

Nina mkosi gani au ndio majaliwa yangu au mipango ya Mungu ama shetani.

Situmii kilevi na sijawahi kuhonga hata 30000.
Kama ulikuwa auhongi au kutumia pombe lazima ufilisike
 
Kwa nilichojifunza kwenye biashara izi kipindi biashara imekunyookea jaribu kuwaza biashara mpya au uwekezaji mpya wengi waljofanya ivyoo wamesavaivu sana pindi biashara zikiyumba au kufilisika mf Una maduka na biashara imechangaya embu wekeza kwenye hisa au mashamba au mifugoo usiwekeze tena kwenye Duka au Una mifugo na Duka embu wekeza tena kwenye nyumba za kupangisha au udalali kubadili uelekeo WA shughuli zako unasaidia sna niliona Kwa mjimba wangu alikuwa na Duka kama 3 apo buguruni za mbao na hardware Ila vilipotea kama utani kilichomsaidia ni mashamba na mifugoo
Kitaalam tunaita portfolio diversification.
 
Yaani makosa ninayoyaona hapo ni mengi mno, yaani natamani nikukalishe chini nikupe somo la biashara. Lakini pole tumia muda huu kutafakari ulipoanguka, fanya hivi
1.chukua kalamu na daftari anza kuandika kila kosa unalofikiri ulilifanya kwenye biashara yako mpaka ukafilisika alafu kwa kila kosa andika suluhisho lake ni lipi.... usijaribu kuanza upya bila kujua ulipokosea na utatuzi wake la sivyo utaanguka tena.
2. Kumbuka mara ya kwanza kabisa ulipoanza biashara ulianza vipi mpaka ukaweza kutoka.
3. Sasa angalia ni biashara gani ukiifanya sasa hivi itakusaidia hata kama ni ya mtaji mdogo. Anza nayo tena.
4. Usihof kuhusu swala la umri miaka 45 ni mdogo sana hasa kwa sisi waafrika. Namfahamu mtu ambaye ana miaka 67 na bado anafungua biashara mpya kila siku.
5. Anza upya ila angalia usirudie makosa
 
Yaani makosa ninayoyaona hapo ni mengi mno, yaani natamani nikukalishe chini nikupe somo la biashara. Lakini pole tumia muda huu kutafakari ulipoanguka, fanya hivi
1.chukua kalamu na daftari anza kuandika kila kosa unalofikiri ulilifanya kwenye biashara yako mpaka ukafilisika alafu kwa kila kosa andika suluhisho lake ni lipi.... usijaribu kuanza upya bila kujua ulipokosea na utatuzi wake la sivyo utaanguka tena.
2. Kumbuka mara ya kwanza kabisa ulipoanza biashara ulianza vipi mpaka ukaweza kutoka.
3. Sasa angalia ni biashara gani ukiifanya sasa hivi itakusaidia hata kama ni ya mtaji mdogo. Anza nayo tena.
4. Usihof kuhusu swala la umri miaka 45 ni mdogo sana hasa kwa sisi waafrika. Namfahamu mtu ambaye ana miaka 67 na bado anafungua biashara mpya kila siku.
5. Anza upya ila angalia usirudie makosa
Amin
 
Maduka 11 with same line of products? Anyways 2016-2020 wafanyabiashara wengi walipitia changamoto sana. Mabadiliko ya kisiasa, covid, sera za fedha.
 
Awamu ile tulifilisika kwa nguvu, awamu hii ni automatically unajikuta nje ya mfumo, nasubri ushauri na mimi
Awamu ile nilisema ngoja nijaribu biashara. nikafungua duka la kawaida la jumla lilifilisika kabisa na kuniachia baadhi ya madeni.
Baadae niligundua kosa kubwa ilikua sina rekodi nzuri ya mwenendo wa biashara, sina kumbukumbu ya matumizi na mapato, nilikua nachanganya hela yangu na ya biashara, nilikua sifuatilii vizuri benki nimetoa nini na nimebakisha nini na mwisho nilikua na matumizi binafsi yasiozingatia bajeti wala ukubwa wa biashara. kwa ufupi kwa mtazamo wangu nilifilisi biashara yangu kwa (Poor management of my business)
 
Kama ulifilisika 2016 kipindi cha kuanza upya ni sasa...nakushauri yafuatayo....
1.Badili Marafiki kabisa...
2.Usiongee Mambo yako kabisa kwa mtu hata ndugu yako
3.Biashara ya simu imebadilika kidogo tafuta mtaji tafuta simu used za Dubai...uza kwa oda na uzia wateja waKo..
4.Naamini ulikua na asset uza moja iwe mtaji...


Pole ila Pambana mm utawala 2016-2021 march hali ilikua mbaya ila nimekaza kuna hatua nimepiga...
 
Ninaomba kusaidiwa mchango wa mawazo tatizo ni nini mpaka muda huu nimefilisika kabisa. Mwisho ndani ya miaka mitatu nimefilisika maduka 5. Ambayo nilikuwa nalipia kodi laki 5 kwa mwezi.

Nina mkosi gani au ndio majaliwa yangu au mipango ya Mungu ama shetani.

Situmii kilevi na sijawahi kuhonga hata 30000.
mimi naomba kazi ya Shop Manager. Hayo maduka yatainuka tena kwa kasi ya ajabu.
 
Mkuu sikuweza kuweka kumbukumbu izo kipindi hiki cha mwisho wa kufilisika lakin nina historia nzuri tangu nianze biashara mwaka 94 mpaka nilipofilisika mwaka 2016
Ulikuwa unafanya biashara gani kwenye hayo maduka yako na kuanzia 1994 hadi 2016 ulikuwa ukijihusisha na biashara gani na wapi? Kwa kujua hayo machache, naweza kujua wapi nianzie kwa ajili ya kukupa ushauri wangu.
 
Back
Top Bottom