Nina miaka 45, nimeshafungua maduka 11 sasa nimefilisika

Nina miaka 45, nimeshafungua maduka 11 sasa nimefilisika

Ninaomba kusaidiwa mchango wa mawazo tatizo ni nini mpaka muda huu nimefilisika kabisa. Mwisho ndani ya miaka mitatu nimefilisika maduka 5. Ambayo nilikuwa nalipia kodi laki 5 kwa mwezi.

Nina mkosi gani au ndio majaliwa yangu au mipango ya Mungu ama shetani.

Situmii kilevi na sijawahi kuhonga hata 30000.
Pole brother muombe sana mungu
 
Maduka 11 umefilisika kizembe sana moja tu likianzakudorora inabidi ushtuke ,nakuanza kutafuta pancha ilipo uzibe upepo usitoke, tena haraka ukipunguza matumizi kwa asilimia 50 mpaka utakaporejea sawa, sasa maduka 11 yanaisha upo tu,. Basi kuna mawili unanyota ya umaskini huo utajiri ulilazmisha, pili umemkosea Mungu sana, tatu uchawi, kama ni kwaakili yako timamu hayo hayapo maduka 11 yakaisha wewe ni bwege sana,. Nipo kwenye shida ila siwezi kuwa na maduka matano tu alafu nifilisike eti.
Ulishawahi kufanya biashara japo yakuuza karanga?Kwa namna ulivyoandika sidhani kama unauzoefu wa biashara yoyote.
Wakati mwingine bora unyamaze ujifunze kwa wengine
 
Ahsante mkuu
Mkuu Pole na napenda nikuambie haya.

Mungu ni mwenye Rehema.
Usijihesabu mkosaji mbele za Mungu ikiwa unatambua makosa uliyotenda na kukiri mbele zake toka moyoni, anasamehe. Umeshasamehewa. Jisamehe mwenyewe pia na usamehe waliokukosea. Usihukumu wengine.

Usihusishe Uchawi kwenye biashara.
Ikiwa ulitumia ushirikina katika biashara zako mafanikio uliyopata yasingekuwa ya kudumu. Shetani hukuvuta akishakumiliki anakupiga. Atakupa mafanikio ya muda kisha anakugeuka. Lakini Mungu ni mwema rejea kwake uanze upya.

Kushindwa usimamizi wa biashara.
Biashara kuwa nyingi hivyo kukosa usimamizi wa mapato na shughuli zako.

Hofu na mashaka.
Hii ni karakana ya shetani inayochakata na kuharibu mambo ya watu wengi. Hofu na mashaka ya mambo usiyoyajua na hayapo. Hapa humtegemei Mungu unategemea akili zako mwenyewe. Hii karakana imeleta majanga na vilio kwa wengi kwani ukishakuwa na hofu tayari umeshafilisika hata kabla ya kufilisika kiuhalisia. Hapa ndipo hasa wewe ndugu ulipoangukia.

Mahusiano mabaya ndani ya ndoa.
Kukosa mahusiano mazuri kwenye ndoa ni janga lingine shetani amewekeza kuharibu maendeleo na ustawi wa kazi zetu. Ukiondoka nyumbani unasononeko na kuwaza naenda kutafuta kwa ajili ya nini sasa hupati na hata ulicho nacho kinaondoka kwani haukihitaji. Hapa kuna siri kubwa shetani kawekeza.

Ni mengi ndugu ila hapo napiga kuzunguka kichaka kama nimekugusa sema hapo hapo. Ila ikiwa tunaongea ana kwa ana kupata mtiririko wewe mwenyewe utajua umeangukia wapi.

Lakini pia ikiwa kuna watu wanaanza kutoka zero na kuwa matajiri, iweje wewe mwenye uzoefu na biashara uanze kujikabidhi kwa shetani katika mfumo wa kufilisika? La! hasha. Ondoa hilo kichwani, hauna cha kupoteza, kataa shetani, chagua mafanikio na Mungu.
 
Mkuu sikuweza kuweka kumbukumbu izo kipindi hiki cha mwisho wa kufilisika lakin nina historia nzuri tangu nianze biashara mwaka 94 mpaka nilipofilisika mwaka 2016
Hili ndio chanzo cha yote yaliokufika...muwe munaendesha biashara kwa kufata principle za biashara kwa kutfuta mtu mwenye elimu ya uhasibu akusaidie.
 
Pole kwa maswahibu. Nataka kujua ukweli . Je wakati ulioanza harakati zako za kufungua yao maduka11. Ulishawayi kutenga muda kumuomba na kumshukuru munguu imani yako? Je hicho kipato uliokua unazalisha ndani ya biashara zako. Ulishawahi kutenga angalau theluthi yake kurudisha shukran kwa kutoa Sadaka ndani ya nyumba ya mungu iliosimamisha imani yako?

Kama ndio yote ulikua unayatekeleza baci kuna njia za kukurudishia hizo mali ulizopoteza. njoo ntakusaidia utaweza . ila kama hujawahi kumkumbuka baci ujue umeshagongwa mihuri ya safari ya kupotea duniani. Siku zote utakua Binadamu wakupoteza hadi mwisho wa pumzi zako...
acha kumdanganya mwenzako isee .. biashara ni mipango na kusimamia hiyo mipango kwa umakini kama hakufanya hivyo au ata wewe hautafanya hivyo utafilisika tu.
 
Nilianza na mtaji wangu mwenywe baadae nikakop

Mwaka 94 nilianza duka langu la kaseti za radio zikaja cd nikaweka nikabadili biashara mwaka 99 nikapigisha simu nikabadili biashara mwaka 2002 nikauza simu na accessory mpaka nimefilisika mwaka 2016 niko kwenye maduka ya simu tu. Nilikua nasimamia mwenyewe biashara mpaka 2010 ndio nilianza kuajiri hapo ndio biashara ilinichanganyia sana nikawa nasafiri mwenyewe kodi zote nilikua nalipa vizuri maduka 3 ndio niliyokua nikiyaendesha kwa pamoja mwaka 2010 mpaka 2015 baadae hapo ndio nikafilisika nikafungua jengine na jengine mpaka ikafika hesabu ya maduka 11.
Mi nadhani hata utitiri wa ofisi nyingi umekukwamisha.

Kikawaida ukishaona mambo yameyumba,
Unatakiwa baadhi ya branch uzisimamishe mpka utakapokaa sawa.

Hapo mi nadhan Ni hesabu TU ya mapato vs matumizi ilikuangusha
 
Hukusoma vizuri mwenendo wa biashara yako. ulitakiwa ubadilishe mapema biashara au kuongeza huduma nyingine mfano kutoka kuuza simu na vifaa vyake na utoe huduma za kifedha kupitia simu, uza vocha au utengeneze simu hata kwa kumlipa fundi akae hapo. Inafika wakati kila mmoja anamiliki simu je hapo utafanya kweli biashara?
 
acha kumdanganya mwenzako isee .. biashara ni mipango na kusimamia hiyo mipango kwa umakini kama hakufanya hivyo au ata wewe hautafanya hivyo utafilisika tu.
Na hapo ndo unapozidi kupotea. Unapojifanya ww ni bingwa wa fikra na mipango. Mwisho wa siku unajikuta umepoteza kila kitu. Kwa kosa la kumsahau na kumtanguliza mungu kwanza.... Angalia Marekani pexa yao inaongoza ulimwengu mzima ( Soma meneno yalioandikwa ndani ya us $)
 
Na hapo ndo unapozidi kupotea. Unapojifanya ww ni bingwa wa fikra na mipango. Mwisho wa siku unajikuta umepoteza kila kitu. Kwa kosa la kumsahau na kumtanguliza mungu kwanza.... Angalia Marekani pexa yao inaongoza ulimwengu mzima ( Soma meneno yalioandikwa ndani ya us $)
Unajua ni Mungu gani wanaye muamini..
Au wewe ukisikia Mungu tu unaweweseka.
-Mungu wao anaruhusu ushoga na usagaji.
-mungu wao anaruhusu mapenzi hadharani na Wala hakuna shida.
-mungu wao anaruhusu uasi na n.k

Siku nyingine dokie kabla ya praise tu..
 
Unajua ni Mungu gani wanaye muamini..
Au wewe ukisikia Mungu tu unaweweseka.
-Mungu wao anaruhusu ushoga na usagaji.
-mungu wao anaruhusu mapenzi hadharani na Wala hakuna shida.
-mungu wao anaruhusu uasi na n.k

Siku nyingine dokie kabla ya praise tu..
Je kwa upande wako ww binafsi umemuani mungu gani ?
 
Ulishawahi kufanya biashara japo yakuuza karanga?Kwa namna ulivyoandika sidhani kama unauzoefu wa biashara yoyote.
Wakati mwingine bora unyamaze ujifunze kwa wengine
Nilipokua miaka 9 niliuza biashara ya njugu miwa na mahindi mpaka nimefika miaka 15 nikafungua duka
 
Hukusoma vizuri mwenendo wa biashara yako. ulitakiwa ubadilishe mapema biashara au kuongeza huduma nyingine mfano kutoka kuuza simu na vifaa vyake na utoe huduma za kifedha kupitia simu, uza vocha au utengeneze simu hata kwa kumlipa fundi akae hapo. Inafika wakati kila mmoja anamiliki simu je hapo utafanya kweli biashara?
Mkuu biashara ya simu mpaka leo inalipa kwa mfano simu jumla 15000 unauza 20000

Simu jumla 150000 unauza 160000

Mtaji wa milioni 10 unaweza kuuza hata pc 10 au 15 kwa siku

Biashara iliopo kariakoo
 
Kwa nilichojifunza kwenye biashara izi kipindi biashara imekunyookea jaribu kuwaza biashara mpya au uwekezaji mpya wengi waljofanya ivyoo wamesavaivu sana pindi biashara zikiyumba au kufilisika mf Una maduka na biashara imechangaya embu wekeza kwenye hisa au mashamba au mifugoo usiwekeze tena kwenye Duka au Una mifugo na Duka embu wekeza tena kwenye nyumba za kupangisha au udalali kubadili uelekeo WA shughuli zako unasaidia sna niliona Kwa mjimba wangu alikuwa na Duka kama 3 apo buguruni za mbao na hardware Ila vilipotea kama utani kilichomsaidia ni mashamba na mifugoo
 
Back
Top Bottom