Una milioni 12 unataka kununua gari. Je, nyumba yako binafsi unayo?
Ila mkuu naweza kutofautiana na wewe kidogo.Nafikiri hapa unazungumzia waajiriwa..kwa nin usinunue nyumba badala ya kununua kiwanja na kujenga hizo nyumba its very funny watanzania tuna hama mijini na kuhamia mwishoni mwa miji? Hatunaga tofauti na wazaramo..gari ndo mpango mzima maisha ni kujipanga tu nyumba ndo kitu cha mwisho kukifanya..!!!
Ila mkuu naweza kutofautiana na wewe kidogo.
Sijali sana kujenga nyumba kwa sababu ni upuuzi na upotwevu wa maliasili kwa kutaka sifa kutoka kwa wazee ambao ndiyo waliotuharibu kimawazo na bado wanatutawala.
Ila kiwanja ndiyo mpango mzima. Kwa Tanzania, kukodisha nyumba ni rahisi kuliko kujenga nyumba. Mtanzania wa kawaida huishi miaka 80, kukodisha nyumba milioni mbili kwa mwaka kwa miaka 55 ni milioni 110.
Kwa sasa hivi viwanja vinapanda sana gharama, kiwanja cha milioni 5 Mbweni miaka mitano iliyopita ni milioni 10 sasa hivi. Nyumba nyingi baada ya miaka 20 zitakuwa rent to own i.e Mortagaged na mabenki, ambapo automatically unakatwa kwenye mshahara kwa miaka 25 au 30 au 15 kama unataka.
Kuwa na kiwanja kwanza, hata shamba .... then nunua gari kurahisisha maisha yako na watoto halafu ndiyo labda uamue kuanza kujenga.
Hayo ni maoni yangu. N a kama maoni yangu yangekuwa sahihi angalau asilimia 70, ningekuwa mbali sana kimaisha. Mimi sioni mantiki ya kuwa na nyumba wakati maisha yanakugonga, mkeo anachakaa haraka na watoto hawapati elimu na maisha yaliyotulia.Mkuu, tafadhali futa hiyo kauli ya kwenye red!..hapo kwenye blue fafanu.
Mambo ya kipi kianze kati ya gari na nyumba inategemea na mtu mwenyewe, mazingira aliyopo, na kazi anazofanya, lazima kila mtu ana vipaumbele vyake, na anaangalia ni kitu kipi kitafanya maisha yake yawe rahisi zaidi. Mfano mmachinga mwenye kufanya biasara ndogondogo mkoani itamuwia rahisi zaidi akijenga kwanza kibanda cha kuishi, kuliko kununua gari (gari linahitaji pesa nyingi za pamoja, nyumba unaweza kununua vitu kwa kadri unavyopata senti na baada ya miaka mitatu minne ukahamia kwako), nyumb hiyo itamrahisishia hata kupata mkopo wa kupanua biashara. Hali ni tofauti kidogo kwa wafanyakazi kama wewe kaka, wanakopa wananunua gari, baada ya miaka mitatu amemaliza kulipa mkopo mtumba wake wa gari umeshachoka anakopa tena anaenda kununua nyingine!!!!
Nachotaka kusema ni kwamba, maisha ni kama mtihani wa hesabu wenye maswali tofauti kwa akila mtahiniwa, ukiangalizia formular anayotumia mwenzio wakati swali lako ni tofauti itakula kwako. SOLVE MTIHANI WAKO.