Nina tatizo la sikio kuunguruma au kama kuna maji sikioni

Nina tatizo la sikio kuunguruma au kama kuna maji sikioni

E

Exactly mkuuu........ Nenda popote tu Wana kakipimo flani na Wala sio gharama na hakamalizi hata dk 3 kujua kama ishu ni uchafu..... Hilo ya miayo nilikua nalo, au ukikimbia au kubonyeza sikio Kwa nje linazibuka.......

Jaribu nilichoeleza hapo mkuuu Mimi limeisha kabisaaaa aseee
Nashukuru mkuu ila hiyo dawa ya macho uliyotumia Ndio sijui
 
Tinnitus ndio unaitwa huo ugonjwa kuna nyuzi nyingi za zamani na kuna mdau alisema kuna hospital Mwanza inatibu ila sijaenda
Mimi nina tatizo hilo pia kelele na muungurumo upande mmoja hasa kukiwa kimya
 
Kuna hali moja ambayo ninatamani apatikane mtaalamu aitolee maelezo mazuri. Hapo awali nilimuuliza mleta mada kama aliwahi kuugua mafua kabla ya kutokewa na hilo tatizo.

Nawakilisha mchango wangu kwa kurejea tatizo kama hilo lililomtokea ndugu yangu. Yeye baada ya uchunguzi iligundulika kuwa bakteria walishambulia ngoma yake sikio na kuleta madhara. Chanzo cha bakteria hao ni mafua aliyoyapata.

Hapa nimetumia akili bandia kupata maelezo zaidi

Swali langu kwenda Bard: Je bakteria watokanao na mafua wanaweza kuleta madhara katika masikio?

Jibu: Ndiyo, bakteria watokanao na mafua wanaweza kuleta madhara katika masikio. Maambukizi ya sikio yanayosababishwa na bakteria mara nyingi hujulikana kama uvimbe wa sikio la kati (AOM). AOM ni hali ya kawaida sana, haswa kwa watoto wadogo. Inakadiriwa kwamba takriban asilimia 75 ya watoto watapata AOM angalau mara moja kabla ya kufikia umri wa miaka 3.

Maambukizi ya sikio yanaweza kusababishwa na bakteria mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Streptococcus pneumoniae, Haemophilus influenzae, na Moraxella catarrhalis. Bakteria hizi zinaweza kuingia kwenye sikio la kati kupitia kijifereji cha Eustachian, ambacho huunganisha sikio la kati na pua na koo. Kijifereji cha Eustachian kinaweza kuziba kwa sababu ya msongamano wa pua au koo, ambayo inaweza kutokea wakati wa mafua.

AOM inaweza kusababisha dalili mbalimbali, ikiwa ni pamoja na:

Maumivu makali ya sikio
Kuvimba kwa sikio
Homa
Kichefuchefu na kutapika
Kupoteza uwezo wa kusikia
AOM mara nyingi huponywa yenyewe bila matibabu, lakini katika hali nyingine, matibabu ya antibiotiki yanaweza kuhitajika.

Madhara yanayoweza kutokea ya AOM ni pamoja na:

Uvimbe wa sikio la kati wa muda mrefu (OME)
Uvimbe wa sikio la kati ulio na usaha (CSOM)
Maambukizi ya ubongo
Upotevu wa kusikia wa kudumu
Ikiwa unapata dalili za AOM, ni muhimu kuonana na daktari. Matibabu ya haraka yanaweza kusaidia kuzuia matatizo.

Kuna mambo kadhaa ambayo unaweza kufanya ili kupunguza hatari yako ya kupata AOM, ikiwa ni pamoja na:

Kusafisha pua yako mara kwa mara kwa kutumia chumvi ya bahari
Kunywa maji mengi
Kuepuka kuvuta sigara
Kuweka mtoto wako mchanga aliyelala juu ya tumbo lake
Ikiwa una mafua, unaweza kuchukua hatua kadhaa ili kupunguza hatari yako ya kupata AOM, ikiwa ni pamoja na:

Kunywa maji mengi
Kutumia dawa za kutuliza maumivu na homa
Kutumia dawa za kupunguza msongamano wa pua na koo
Kuepuka kuvuta sigara


Credit: Bard
 
Hii hali na mimi huwa inanitokea ila nimetambua ni earwax au uchafu wa masikioni unaojaa na kusababisha sikio kuziba Kwa muda , mimi siku nyingine hata siku nzima linaziba kesho yake lifunguka .

Mwaka jana ndio nilianza kuhisi hili tatizo lilipo anza kama double sound Kwa sikio la kulia yaani kama mwangwi hivi nilipanick kinoma baada ya wiki likaacha.

Kwenye kufuatilia niligundua ni tatizo linalosababishwa na blocked earwax .
Uko sahihi kabisa mkuu, shida ni kwamba hizo earwax zinakuwa kwa ndani kabisa ya sikio na ndio zinablock kabisa mtu unapoteza usikivu.

Sasa nilikuwa nataka kujua ni njia gani ya kuondoa hizo earwax ili sikio lizibuke na lirudi katika usikivu wa kawaida.
 
Mafuta ya kitunguu saum tumia kuweka matone 3 usku kla ukitaka kulala kwa sku 3 tu utapona mkuu
 
Nenda Ekenywa hospital mkuu. Ipo Dar es salaam -Magomeni.
 
Back
Top Bottom