Nina Virusi vya UKIMWI ila naogopa kumwambia mume wangu maana yeye yupo salama

Nina Virusi vya UKIMWI ila naogopa kumwambia mume wangu maana yeye yupo salama

Watoto wawili mmepata, ina maana mlipiga mechi kavukavu, na naamini kwa vile hajui, bado anaendelea kudemka.
Sasa miaka minne yote anademka na hujamgawia virusi, aisee hapo na sisi umetudanganya!
Hiyo inawezekana mkuu Kirokonya, kuna watu duniani ni gifted, yaani hata uwadunge sindano ya damu ya mtu mwathirika wa HIV,kamwe hawawezi kupata ngoma.Kuna watu nimeshakutana nao ambao wapo ktk hali hiyo.
 
Hospitali ya wapi wauguzi wapuuzi namna hiyo, acha kuchafua taaluma za watu…..
Hospitali kibao tu hawasemagi ukweli! Unaweza kuta mtu ana VVU kwa kulingana na cheti tu wame refer CTC!
Ila dokta anamwambia yuko freshi tu hana shida.

Akija anashangilia sema kama mwana namkaukia tu sababu sio poa yani maana anakuwa haelewi!
 
Watoto wawili mmepata, ina maana mlipiga mechi kavukavu, na naamini kwa vile hajui, bado anaendelea kudemka.
Sasa miaka minne yote anademka na hujamgawia virusi, aisee hapo na sisi umetudanganya!
Hili swala la jamaa kuishi na mwanamke mwenye VVu bila ya yeye kuambukizwa ni kweli inatokeaga, nilishaona bro mmoja kaishi na mke wake kwa miaka 30 mke ana VVU afu jamaa hana lakini walipopima wakasema yule jamaa ana grp O sasa hpo skumbuki ni O+ au O- ko kati ya hayo magrp hapo kuna grp halipati maambukizi ya ukimwi kwama watu wengine tunavyopataga Afu na watu wa Afya wakamwambia aendelee tu kuishi na mke wake hamna shida yoyte itakayo mtokea basi ikaisha hv, So hii ishu mmi sizan km niuongo
 
Mwanachama #001

Tafadhali ficha kitambulisho changu Mheshimiwa.

Najua nimemkosea Mungu na ubinadamu..pole pole napoteza akili yangu...sikutaka yoyote haya...Nina miaka 25, mama na mke , nina VVU lakini mume wangu hajui.

mwanzoni mimi nilidhania alijua.maana nilihisi nilipata kwake... Nilikutana naye 2016, kisha nikabainika kuwa na VVU wakati nilienda klinic kwa
pole Dada yangu, huwez jua mipengo ya Mungu kat yako wewe mwenye vvu na mumeo Nan atatangulia mbele ya haki.

Hivyo basi kwa kuwa dhamila yako haitaki apate magonjwa mumeo, nakushauri ufanye mambo yafuatayo:-

Kwanza tambua Mungu anasamehe ata Kama ulidanga au vyovyote, Muombe msamahaa then acha kabisaaa kila siku kujihukum. Jikabidhi kwake na familiya yako mkaombe rehema za Mungu. Atasikia

Pili, miaka 4 ambayo umemaliza mumeo hajapata ugonjwa ni waz Kuna ulinzi Mungu amemuwekea ili kusudi mlee watoto wenu kwa pamoja.

Tatu, ushauri wangu naona watoto wenu bado wadogo ukimwambia ndo kwanza ndoa itavunjika, baba ataoa mke mwingine au atapata kipozeo Cha mtaani na huyo mke mwingine ndo anaweza kumpa maradhi na hivyo watoto wakapata shida Sana

Hivyo basi kwa mtazamo wangu na ushauri, usimwambie kwanza subiria watoto wakue kidogo.

Lakin wakati unasubiria watoto wakue, fanya mambo yafuatayo kwa uhaminifu Sana:-

1. Meza dawa kwa ratiba kikamilifu, kula vizuri, hacha mawazo kabisaaa na uwe mtu wa kuchangamka.

2.Usikubali kabisa kabisa kabisa yaan hata kidogo, kufanya mapenzi na mumeo kabla hajakuandaa, nadhan unanielewa kuandaliwa kupi namahanisha.

Na akianza kukuandaa, weka akili yote kwake ili kuruhusu..........kulainika, ukiona wakati mwingine hauna mudi kabisa, nunua mafuta yanayofaa kitaalam ya kuweka kule chin......, Uweke kabla ya mumeo haja anza shughuri. Hii yote ni kumkinga asichubuke akiwa kwenye tendo.

3. Tatu Kama unafanya kazi, jitahidi sana kuweka akiba kubwa, kwa Siri kubwa, namahanisha ata Kama utapata hela ya kiwanja nunua kwa Siri, jina la kiwanja andika watoto wako, hati tunza kwa Siri. Hii itakusaidia ata pale utakapo kuja kumwambia baada ya watoto wenu kukua kidogo, ata Kama hatakuelewa, kale ka kiwanja katakusaidia upate pa kuishi.

Dada yangu Amin usiamin kuwa na virusi siyo mwisho wa maisha, bado unaweza kuishi mpaka ukaona wajukuu wako Kama utajikubali na kumtegemea Mungu.

Mwisho.usisimulie watu wengi, ili kusudi Siri isitoke haraka. Mungu uangalia nia ya moyo inadhamilia nini.

Naomba nisihukumiwe kwa mawazo yangu na Samahan kwa uandishi mbaya nimeandika nikiwa safarin

Barikiwa.
 
[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji1426]pole tafuta muda kaa naye mweleze kwa mwanaume mwelewa atakusifia namuona unamthamini atakutunza na pengne akaongeza upendo Mara dufu.
 
Yawezekana hauna huo ugonjwa...!

Mawazo uliyonayo sasa yatachangia sana kushusha kinga yako ya mwili / stress zinaleta shida sana kwenye akili na moyo wa binadamu jaribu kuzingatia hayo..
usiumize sana kichwa chako,

jali watoto wako waone kama baraka , furahia maisha yako kwa kila muda unaoupata...


Pima sehemu tatu tofauti..
 
pombe iliyokuw kichwan imekata ghafla,sijui kwa nn nmeufungua huu uzi,baada ya kusoma huu uzi akili yangu imeanza kuhisi vibaya kwa wife sijui kama nitaperfom task leo
 
Kusema uongo nacho ni kipaji ila wewe huna kipaji hicho,hiyo story yako peleka kwenye vijiwe vya kahawa ili ukawachangamshe,

Acha kutafuta umaarufu JF kwa story za kutunga zisizokua na kichwa wala miguu.
 
Mute tu, kama anakukunja kunja zaidi ya miaka minne na yupo fit.
Nashangaa sana unaogopa huo ugonjwa miaka hii, ingekuwa dawa zake azitaki pombe ndio ningesikitika.
Kikubwa anza dozi kwa siri ili usimwambukize kabisa.
Asante
 
Kuna baba mmoja,kashaoa zaidi ya wanawake watatu mpaka sasa na wote wamekufa kwa Ukimwi.

Yeye mzima kabisa,na akioa mkewe akishajijua ameathirika yeye ndo anakuwa anamsimamia kumeza dawa,na clinic anamsindikiza

Wakeze wengi wanakufa kwa Sonona wanajifikiria wao ndo malaya,kumbe ukimwi wameukuta ndani

Acha kujiletea Sonona mtoa mada utakufa siku si zako,kama mapito yako unaamini yako fresh

Basi tambua kuna mijanaume mi career
Yenyewe ukitembea nalo linakuambukiza,ila lenyewe likipimwa lizima kabisa.

Kama mumeo ni mtu wa kupanic ishi nae tu,usimwambie wala nini
Lakini mlinde kwa kumeza dawa zako vizuri kwa wakati.hutomuambukiza.
kama ni wa kuambukizwa
Lakini kama ni hayo ma career hata usipokunywa dawa huliambukizi ng'oooo.wewe ndo utazorotesha afya yako.
 
Watoto wawili mmepata, ina maana mlipiga mechi kavukavu, na naamini kwa vile hajui, bado anaendelea kudemka.
Sasa miaka minne yote anademka na hujamgawia virusi, aisee hapo na sisi umetudanganya!
Kakangu ninaemfuata alipimwa na kupatikana na UKIMWI 2013 na mke wake hakua na maambukizi; tokea kipindi hicho hadi sasa wameshapata mtoto mwingine mmoja.
Hadi leo mke wake hajapata maambukizo na wanashiriki ngono kila mara ndiyo maana walizaa mtoto wao wa nne. Kwakweli shemeji wangu ni mwanamke kwelikweli; hua anamsindikiza mme wake kuchukua dawa na yeye kufanya vipimo kila baada miezi mitatu
 
Watoto wawili mmepata, ina maana mlipiga mechi kavukavu, na naamini kwa vile hajui, bado anaendelea kudemka.
Sasa miaka minne yote anademka na hujamgawia virusi, aisee hapo na sisi umetudanganya!
Udanganywe vipi ilhali mtu anatumia dawa ipasavyo hivo vidudu viko na nguvu kidogo
 
Back
Top Bottom