Nina wazo ambalo linaweza kutunufaisha mimi na wewe kama una kipato kidogo na hujui pa kuwekeza

Nina wazo ambalo linaweza kutunufaisha mimi na wewe kama una kipato kidogo na hujui pa kuwekeza

NyegereBOY

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2021
Posts
225
Reaction score
328
Nawasalimu Kwa jina la muungano wana JF wote

Kifupi nisikuchoshe wala tusichoshane nitaenda moja Kwa moja kwenye maada kama kichwa kinavyoeleza

Mtanisamehe Kwa uandishi wangu Mimi sio muandishi mzuri

Kwa kifupi Mimi ni kijana Wa kitanzania mkazi Wa jijini Dar es Salaam. Katika harakati za kutafuta mkate Wa kila siku Na kujiinua kiuchumi kuna changamoto tunazipitia sisi sote ila hizo changamoto ndio fursa Kwa namna nyingine.

Sasa kuna hii fursa nilipata kuiona mda mrefu Na kuanza kuifanyia uchunguzi kukusanya taarifa za kutosha kuhusu hii fursa nivipi naweza kufaidika na nini changamoto zake kiujumla.

Fursa yenyewe ni utafutaji Wa masoko ya bidhaa kidigitali Kwa njia ya mtandao yaani (online business marketing) Kwa kuanzisha soko LA kimtandao ambalo litawakutanisha wafanyabiashara Na wateja mbalimbali wenye uhitaji Wa kufanya manunuzi kwanjia ya mtandao kirahisi Na salama.

Waswahili wanasema fursa siku zote ni changamoto zilizotuzunguka. Labda niweke uzoefu wangu kidogo Na namana nilivoiona fursa

Kiuzoefu mimi ni sales and marketing consultant (yaani mtaalamu Wa mauzo Na masoko ) nina uzoefu Wa miaka 6 na nikazi imekuwa ikiniweka mjini mpaka sasa Kwa kuhudumu kama sales officer au freelancer ambae nimefanikiwa kufanya kazi na makampuni mbalimbali katika nyanja ya utafutaji masoko ya bidhaa Na huduma (product and services) zilizotolewa Na makampuni niliowahi Kufanyia kazi Na ninayofanyia kazi mpaka sasa.

Sasa kuna hii kazi ya kutoa huduma (service) inayotolewa Na Kampuni moja wapo ya Mawasiliano hapa nchini imekuwa ikinikutanisha sana Na wafanyabiashara wengi hasa katika soko letu maarufu la Kariakoo Na vitu nilivyoweza kubaini Na kuona fursa ndani yake.

A) Kariakoo ndio soko pekee nchini lenye kuhudumia mpaka nje ya mipaka ya Tanzania Na kukutanisha watu mbalimbali

B) Sio kila mfanyabiashara unaemuona Kariakoo anamiliki bidhaa ktk duka wengi ni Mali kauli Na huchukua Kwa wafanyabiashara wenzao ambao ni wenye mzigo Wa kutosha

C) Sio kila bidhaa inauzika Na pia sio kila mfanyabiashara pale kariakoo anafanya biashara licha ya kuonekana Kwa macho kariakoo kuwa Na utitiri mkubwa Wa watu kuna wafanya biashara hawauzi hata bidhaa moja mpaka duka linafungwa jioni. Kuna Vingi vya kueleza ila tuishie hapo

Sasa nilifanya mchanganuo Na kulipata hili wazo pale nilipoona nimekuwa nikipata watu wengi wakiulizia bidhaa mbalimbali katika hili soko hiyo yote kwakuwa nimekuwa nakutana Na watu wengi lakini kiuhalisia mimi similiki biashara yoyote hapa mjini ila nimekuwa nikipata wateja wengi sana Wa bidhaa mbalimbali kutokaana Na uzoefu nilionao hivo nikakaa chini kulitengeneza wazo kuwa fursa

Wazo lenyewe ni kuanzisha soko LA kimtandao kama nilivoeleza hapo juu najua hii sio mimi Wa kwanza kuwa Na hili wazo ila ubora Wa wazo ndio hutofautisha wazo moja Na lingine nilifanya uchunguzi Kwa walioanzisha wazo kama langu Na mapungufu yao kiujumla Na kuona kuwa ni wakati sahihi Na Mimi kulileta wazo language katika uhalisia.

Safari ya majaribio La wazo langu lilikuwa Nzuri Na lenye mafanikio changamoto zifuatazo ndio zikanifanya niandike Uzi huu ili kutafuta mdao mwenye uhitaji Wa kuwekeza ila amekosa wazo LA kibiashara ili liweze kutunifaisha Kwa pamoja.

Kwanza kabisa muundo Wa kazi nilikuwa nikiufanya nilikuwa nikipokea oda kutoka Kwa watu mbali mbali wakihitaji kuwanunulia bidhaa hapo kariakoo hivo nikawa nawapelekea wateja wafanyabiashara nikitegemea kupata percent % kadhaa kama kamishen ya kuleta Mteja changamoto ikawa uswahili mwingi Wa wafanyabiashara

Hivyo nikapata wazo LA kufungua KAMPUNI ili nifanye kazi kisheria Na kihalali. Changamoto ni kuwa sikuwa Na mtaji Wa kufanikisha hili zoezi kama mnavyojua mchakato Wa kufungua Kampuni Na sheria zilizowekwa

Hivyo basi nilikuwa nahitaji mdau mwenye mtaji walau Wa kufungua Kampuni tu ya ubia yaani Mimi Na yeye au kama tayari ana Kampuni Na hana project ya kufanya tuweze kuwa Na makubaliano ya namna tutakavyoweza kunufaika Kwa pamoja Na wazo hili kumbuka wazo langu haliitaji mtaji mkubwa ni pesa tuu ya kufungua Kampuni ili kufanya kazi kihalali au kama una kampuni basi inatosha sana kuweza kugawana keki hii nilioiona mtanzania mwenzenu

Nimeandika Uzi huu kwakuwa katika ridhki Na vipato tumetofautiana hivo naimani kuna watu wamejaliwa kidogo Na wangependa kuwekeza

MCHANGANUO WA KILICHONIFELISHA
1) kufungua kampuni yaani (LIMITED COMPANY) approximately cost )1000,000/= hii ni kwaajili ya brela Na consultation cost za wanasheria ili kukamilisha Usajili

2) Kwa sheria ya Tanzania ukihitaji kufanya kazi kama kampuni inapendekeza kutambulishwa office ya Kampuni itakapo kuwepo hapa ndipo unapata cost ya office au frem japo Kwa kazi au huduma itakayotolewa itafanyika online hivo akuna ulazima Wa physical location ila kisheria hakuna budi kuwepo cost zake kama fremu itakuwa ( 150k au 250k per month basi Kwa miezi 6 itakuwa 1.5M )

Cost ya mwisho ni branding ya huduma ambayo unaweza kugharimu 1M.
hivo kufanya uwekezaji jumla kugharimu 3.5M au 4M hii ni Kwa muwekezaji ambae atapendelea tuanzishe kampuni ila Kwa ambae anakampuni tayari ni cost ya branding tyuuu nafkri Na makubaliano baina yetu ili kuongozana jinsi kazi itakavyofanyika Na maslahi ya pande zote kiujumla

So kama kuna mdau anaweza kuwa interest Na wazo Na anahitaji kuekeza namkaribisha au kama kuna ushauri wapi naweza Ku present hili wazo Kwa washika dau wakawezesha huu mchakato nipo kusoma comment kama kuna swali pia nipo kujibu kuhusu mchakato Wa wazo ila Kwa maelezo zaidi kuhusu wazo
Mawasiliano yangu ni haya

+255746367002

Asanteh Kwa muda wako.
 
Huo mchanganuo wa kampuni mbona gharama ni kubwa
Hii ni Kwa limited company yenye mtaji mkubwa ambayo fees take nikama laki 5 hiv plus gharama za kuandaa memorandum kama 150k Na Kwa sharia za TZ huandai wewe binafsi wanaanda wanasheria hapo unakutana Na service chaji ya mwanasheria so minimum unaweza kuwa 800k ila maximum ni 1000M
 
Wazo zuri lkn haujaeleza kampuni itavyofanya kazi ili mshirika wako nae anufaike,mfano mm. Siko Dar lkn Nina mtaji ila wewe uko Dar,tumefanya makubaliano yote,mm narudi nyumbani kuangalia kampuni inaendaje,nitafahamu biashara na shughuli zetu zinakwendaje?
 
Mkuu kuelezea mlolongo mzima tunaweza jazz kurasa ndio mana Kwa ufupisho nikaweka namba ya simu kama kuna swali La ziada iwe rahisi kujibiwa ila kiufupi iko hivi

Kama itakuwa imefunguliwa kampuni baina mwenye mtaji na mwenye wazo kutakuwa na makubaliano Kwa kila faida itakayokuwa inapatikana kulingana na his a katika kampuni hiyo moja

Pili kama umefatilia vizuri andika nikwamba inaenda kufanyika biashara ya kuuza bidhaa mbalimbali Kwa njia ya mtandao hivo basi kuna mfumo utawekwa ambao utaratibu manunuzi yote yatakayo kuwa yanafanyika Kwa kampuni hivo kujua kilichouzika ni kipi na faida ni IPI Kwa kuwa sheria ya kwanza ni kutokupokea pesa kwenye hili wazo jinsi lilivopangiliwa ili kuweka kumbukumbu ya mauzo yote uatakayo fanyika hiii itamsaidia hata mbia Wa kampuni kuona mauzo ya kampuni kupitia simu yake na kujua faida ilioingia Kwa mda husika

Nafkr nimejibu swali lako mkuu
 
Back
Top Bottom