Ninachokijua kuhusu Miradi ya DMDP na Ujenzi wa Miundombinu Mkoani Dar

Ninachokijua kuhusu Miradi ya DMDP na Ujenzi wa Miundombinu Mkoani Dar

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
Salaam Wakuu,

Mwaka wa fedha 2012/13 Serikali ilibuni Mradi wa uendelezaji wa Jiji la Dar es salaam (Dar es Salaam Metropolitan Development Project – DMDP), Madhumuni makubwa ya mradi wa DMDP ni kukabili changamoto zinazolikabili Jiji la Dar es Salaam kwa kutilia mkazo uboreshaji wa huduma za jamii kama miundombinu na kujenga uwezo wa Manispaa za Jiji la Dar es Salaam katika utoaji huduma, kuchangia katika kukabili changamoto za mabadiliko ya tabia nchi na kusaidia katika kukabili matukio makubwa ya dharura kama majanga ambayo yanaweza kulikabili Jiji la Dar es Salaam.

Vipaumbele muhimu vilianishwa kwa kufuata vigezo muhimu bila kuangalia umaarufu wa maeneo au itikadi mbalimbali. Vigezo muhimu vilivyoanishwa ni pamoja na Miradi iwe inayounganisha maeneo ya watu wenye kipato kidogo na yaliyojengwa holela, Miradi iwe inayounganisha Wilaya na Mkoa na Miradi iwe inayounganisha maeneo mbalimbali na ukanda wa mabasi yaendayo haraka (BRT) ili kurahisisha usafirishaji.

Ikaibuliwa miradi ya Ujenzi barabara za mlisho (feeder roads) zenye urefu wa kilometa 65.6 katika Manispaa zote za Jiji ili kupunguza changamoto za msongamano. Mradi Mwingine ukawa ni Ujenzi wa mitaro ya kutiririsha maji ya mvua yenye urefu wa kilometa 31.8 katika maeneo ya mto Ng’ombe, Msimbazi, Gerezani Creek, Yombo na Kwashego ili kutatua changamoto za mafuriko.

Kupandisha hadhi makazi yaliyopangwa kiholela katika Kata 14 za Tandale, Mburahati, Mwananyamala, Gongo la Mboto, Kiwalani, Ukonga, Keko, Kilakala, Mbagalakuu, Mbagala, Mtoni, Yombo Vituka, Kijichi na Makangarawe kwa kujenga kilometa 145 kwa kiwango cha lami, kuweka nyenzo za ukusanyaji wa taka ngumu, kujenga mitaro ya kutiririsha maji ya mvua, kuweka taa za barabarani, kujenga njia za watembea kwa miguu, ujenzi wa maeneo ya mapumziko na vituo vya mabasi, ujenzi wa vyoo vya umma na ujenzi wa maeneo ya michezo.

Kuandaa Mpango kabambe wa Mfumo wa Maji ya Mvua na Maji Taka (Storm Drainage and Sewerage Master plan) kwa kushirikiana na DAWASA/DAWASCO ambao utasaidia kupanua wigo wa mifumo kwa asilimia 100% kufikia 2030. Kufunga mfumo wa kisasa wa ukusanyaji wa mapato katika Manispaa zote na kuepuka mianya ya kuvuja na ukwepaji wa kulipa kodi. Na Kujenga uwezo wa mwitikio wa haraka katika kukabiliana na majanga.

UTEKELEZAJI

Mwaka wa fedha 2015/16 Serikali iliingia Mkataba na Benki ya Dunia wenye thamani ya dola za Kimarekani 300 milioni za utekelezaji wa mradi wa DMDP kwa kipindi cha miaka mitano. Aidha, mfuko wa maendeleo ya nchi za Nordic (NDF) umechangia dola za Kimarekani 5 milioni kwa ajili ya kukabili changamoto za mabadiliko ya tabia Nchi na Serikali ya Tanzania ina changia dola za Kimarekani 25.3 milioni katika mradi huu.

Katika mwaka fedha 2016/17 utekelezaji wa miradi ya DMDP Awamu ya kwanza ulianza.

ManispaaBajeti kwa Mwaka 2016/17 (Sh.)Kazi zilizoanza kutekelezwa
Temeke72,804,468,467.00
  • Kujenga barabara za mlisho 14.51km
  • Ujenzi wa mitaro mikubwa 8.9km
  • Ujenzi wa barabara za mitaa 55km
Ilala43,242,117,826.00
  • Kujenga barabara za mlisho 2.84km
  • Ujenzi wa mitaro mikubwa
  • Ujenzi wa barabara za mitaa 55km
Kinondoni63,938,175,211.00
  • Kujenga barabara za mlisho 14.51km
  • Ujenzi wa mitaro mikubwa 8.9km
  • Ujenzi wa barabara za Mitaa 55km
Sekretarieti ya Mkoa ndo ilikuwa na jukumu la ushiriki wa pamoja na Ofisi ya Rais TAMISEMI na Manispaa katika maandalizi ya usimamizi wa utekelezaji wa mradi. Kwa sasa Mchakato ya Kuunda Mamlaka ya Jiji la Dar Es Salaam kusimamia miradi huu unaendelea.

Kutekelezwa kwa miradi hii kumeibadilisha sura ya Jiji la Dar es Salaam na kuwa na muonekano. Sasa hivi Ukienda Mbagala, Kijichi, Temeke, Ilala, Tandika nk, Unakuta lami hadi vichochochoroni. Yote hayo ni Matunda ya Miradi ya DMDP.

MIRADI YA DMDP II INAYOJENGWA KUANZIA 2024

Mwaka 2024, Miradi ya DMDP II inaanza tena ambapo, Mkoa wa Dar es Salaam, barabara za awali zitakazoanza kujengwa kwenye awamu ya kwanza ya utekelezaji na zimeshafanyiwa usanifu zitakuwa zina urefu wa kilomita 150.74.

Wilaya ya Ubungo

Kwa wilaya ya Ubungo, jumla ya kilomita 36.11 zitajengwa kwenye maeneo zaidi ya 20 kwa umbali tofauti.

Katika maeneo yote barabara ndefu zaidi ni kilomita 9.83 ya Msumi, na Goba Wakorea kilomita 7.76, huku barabara fupi ni ile ya kilomita 0.28 ya Tiptop na barabara ya Shule.

Nyingine ni Hondogo Shija (4.16), Makoka (4.04), Posta Matembe (0.82), Sheikh Bofu (1.13), Msikitini (0.37), Sinza KKKT (0.27), Segesera (0.77), Lion (0.84), Juma Ikangaa (0.97), Mbegani (0.28), Namnani (0.66), Chimwaga (0.34) na Mikindani (0.45)

Zimo barabara za Ubungo NHC (0.6), Midizini (0.99) na Binti Kayenga (1.27). Jumla ni kilomita 36.11.

Manispaa ya Kinondoni

Kilomita 20.34 zitajengwa katika manispaa hii. Zipo barabara za Nakalekwa -Bwawani (7.32), Umoja (3.86), Mivumoni (4.79), Tegeta Polisi - Silver- Binti Matola (0.77), na Amiri/Leni Tatu (Dawasa) kilomita 0.68.

Nyingine ni Togo (0.36), Togo 2 (0.36) na Togo 3 (0.2).

Jiji la Dar es Salaam(Wilaya ya Ilala)

Jumla ya kilomita 29.8 zitajengwa zikijumuisha barabara ya Banana Kitunda- Kivule -Msongola kilomita (16.31), Barakuda- Changombe -Majichumvi (3.27), Majumba Sita - Segerea (3.31), Migombani (1.57), Tabata Mawenzi - Kisiwani 2.12 na Bombom Market (0.12).

Barabara nyingine ni Community Park 2 (0.38), Community Park 2 Road 2 (0.56), Community Park 2 Road 3 (0.11), Community Park 2 Road 4 (0.11), Community Park 1 (0.35), Community Park 2 (0.11), Kigilagila Market 2 (0.28), Kigilagila Market (0.76), Kigilagila Market 3 (0.44).

Temeke

Kilomita 32.09 zitajengwa zikigusa barabara ya Ndunguru (1.64), Masaki (3.91) Masuliza (4.04) Kipati (0.72), Agape (1.07), Kilimahewa -Toangoma (6.17), Msikitini (0.45), Mwembeni (Nyika) (0.44), Malawi (0.28), Songambele (0.32), Mwakalinga Road 1.07.

Nyingine ni Markas (0.48), Majimaji (0.32), Keko Machungwa (0.57), Magorofani (0.31), Igome (Yemen) kilomita 0.85, Diwani (0.67), Basri (0.9), Konisaga 1 (0.29), Konisaga (3 0.4), Kurasini (1.12), Taningira (0.42), Uhasibu (0.44), Kizota (0.91) na Lushoto (0.3).

Pia zimo barabara za Pendamoyo (0.56), Pendamoyo 1 (0.2), Mandera (0.85), Mkumba - Miburani (0.39).

Kigamboni

Kwa upande wa Manispaa ya Kigamboni, zitaboreshwa barabara za kilomita 32.4.

Hizi zitajumuisha MC Full Shangwe (1.38), Gofingo - Shangwe (1.77), Kibada Plot (2.91), Lingia - Nyakwale (3.75), Gezaulole (Mivumoni) (7.05), Geza Juu - Eddah Avenue (2.92), Muongozo P/S (2.85), Pengo Simba (2.47), Dege Mbutu (1.6) na Atani Dege (1.76).

Nyingine ni Machava Njama (0.7), Mtaa wa Maji - Posta (1.28), Orasa (0.89), Mzee Msomi (0.65) na Polisi Pikori.

ujio wa DMDP awamu ya pili ni kicheko na furaha kwa Wananchi ambao hawakufikiwa na awamu ya kwanza.

Je, Umenufaikaje na miradi hii Sehemu unayoishi? Nini maoni yako?

Asanteni sana. Mjadala upo wazi karibuni
 
Oohh, swali hapa JF, lile daraja la Jangwani ni la bilioni 300 au 97?

Kwa nini Kigamboni kama inatengwa hivi?

Hiyo mifumo mnaiingizaje katika bajeti zenu za kila siku, hata kwa kiwango kidogo?

So far, so good.
 
Barabara ya kutoka kipati Hadi agape utatusaidia Sana kilasiku nilikuwa naomba hiki kipande kijengwe.
Phase ya tatu wajitahidi kuongeza kilometers Hadi 600 hapa watakuwa wamecheza vizuri
 
Back
Top Bottom