figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,724
- 55,906
- Thread starter
-
- #41
Kinondoni mbona mlipata awamu ya kwanza? Hiyo Manyanya hadi kwa Mtogole Manzese pote mitaa imejaaa lami. Bora ungesema upo Mbezi Maramba mawili ningeelewa. Mnataka mpate nyinyi tu. Kinondoni ni kubwa na Sungura ni mdogo. Ila mnaweza kuwauliza Viongozi wenu. Tatizo mnafanya uchaguzi kwa mihemuko na ushabiki matokeo yake mnakosa Watetezi mnabaki kulilia mitandaoni.Asante kwa ufafanuzi ILA mbona kinondoni zipo chache hasa jimbo la kawe ambalo halijawahi guswa na dmdp phase za nyuma????
Nakalekwa -Bwawani (7.32), hii barabara ipo Kawe na imekula km nyingi. Wengine unaona barabara nyingi lakini zina umbali mdogo. Mfano ni Temeke. Barabara ni nyingi Temeke lakini km chache. Barabara za Temeke baadhi ni Markas (0.48), Majimaji (0.32), Keko Machungwa (0.57), Magorofani (0.31), Igome (Yemen) kilomita 0.85, Diwani (0.67), Basri (0.9), Konisaga 1 (0.29), Konisaga (3.4), Kurasini (1.12), Taningira (0.42), Uhasibu (0.44), Kizota (0.91) na Lushoto (0.3).Asante kwa ufafanuzi ILA mbona kinondoni zipo chache hasa jimbo la kawe ambalo halijawahi guswa na dmdp phase za nyuma????
Ustaarabu ilikuwa ni kwenda kuuliza kwenye mjadala husika wa daraja. Usiwe kama unavuta bangi.Oohh, swali hapa JF, lile daraja la Jangwani ni la bilioni 300 au 97?
Kwa nini Kigamboni kama inatengwa hivi?
Hiyo mifumo mnaiingizaje katika bajeti zenu za kila siku, hata kwa kiwango kidogo?
So far, so good.
Hakuna barabara inayoweza kujengwa kwa hizi fedha hadi iwe kwenye mpango wa hizi fedhaBarabara ya kutoka kipati Hadi agape utatusaidia Sana kilasiku nilikuwa naomba hiki kipande kijengwe.
Phase ya tatu wajitahidi kuongeza kilometers Hadi 600 hapa watakuwa wamecheza vizuri
Safi sana Hatimae Msumi inapata Lami...Katika Mwaka wa fedha 2012/13 Serikali ilibuni Mradi wa uendelezaji wa Jiji la Dar es salaam (Dar es Salaam Metropolitan Development Project – DMDP), Madhumuni makubwa ya mradi wa DMDP ni kukabili changamoto zinazolikabili Jiji la Dar es Salaam kwa kutilia mkazo uboreshaji wa huduma za jamii kama miundombinu na kujenga uwezo wa Manispaa za Jiji la Dar es Salaam katika utoaji huduma, kuchangia katika kukabili changamoto za mabadiliko ya tabia nchi na kusaidia katika kukabili matukio makubwa ya dharura kama majanga ambayo yanaweza kulikabili Jiji la Dar es Salaam.
Vipaumbele muhimu vilianishwa kwa kufuata vigezo muhimu bila kuangalia umaarufu wa maeneo au itikadi mbalimbali. Vigezo muhimu vilivyoanishwa ni pamoja na Miradi iwe inayounganisha maeneo ya watu wenye kipato kidogo na yaliyojengwa holela, Miradi iwe inayounganisha Wilaya na Mkoa na Miradi iwe inayounganisha maeneo mbalimbali na ukanda wa mabasi yaendayo haraka (BRT) ili kurahisisha usafirishaji.
Ikaibuliwa miradi ya Ujenzi barabara za mlisho (feeder roads) zenye urefu wa kilometa 65.6 katika Manispaa zote za Jiji ili kupunguza changamoto za msongamano. Mradi Mwingine ukawa ni Ujenzi wa mitaro ya kutiririsha maji ya mvua yenye urefu wa kilometa 31.8 katika maeneo ya mto Ng’ombe, Msimbazi, Gerezani Creek, Yombo na Kwashego ili kutatua changamoto za mafuriko.
Kupandisha hadhi makazi yaliyopangwa kiholela katika Kata 14 za Tandale, Mburahati, Mwananyamala, Gongo la Mboto, Kiwalani, Ukonga, Keko, Kilakala, Mbagalakuu, Mbagala, Mtoni, Yombo Vituka, Kijichi na Makangarawe kwa kujenga kilometa 145 kwa kiwango cha lami, kuweka nyenzo za ukusanyaji wa taka ngumu, kujenga mitaro ya kutiririsha maji ya mvua, kuweka taa za barabarani, kujenga njia za watembea kwa miguu, ujenzi wa maeneo ya mapumziko na vituo vya mabasi, ujenzi wa vyoo vya umma na ujenzi wa maeneo ya michezo.
Kuandaa Mpango kabambe wa Mfumo wa Maji ya Mvua na Maji Taka (Storm Drainage and Sewerage Master plan) kwa kushirikiana na DAWASA/DAWASCO ambao utasaidia kupanua wigo wa mifumo kwa asilimia 100% kufikia 2030. Kufunga mfumo wa kisasa wa ukusanyaji wa mapato katika Manispaa zote na kuepuka mianya ya kuvuja na ukwepaji wa kulipa kodi. Na Kujenga uwezo wa mwitikio wa haraka katika kukabiliana na majanga.
UTEKELEZAJI
Katika mwaka wa fedha 2015/16 Serikali iliingia Mkataba na Benki ya Dunia wenye thamani ya dola za Kimarekani 300 milioni za utekelezaji wa mradi wa DMDP kwa kipindi cha miaka mitano. Aidha, mfuko wa maendeleo ya nchi za Nordic (NDF) umechangia dola za Kimarekani 5 milioni kwa ajili ya kukabili changamoto za mabadiliko ya tabia Nchi na Serikali ya Tanzania ina changia dola za Kimarekani 25.3 milioni katika mradi huu.
Katika mwaka fedha 2016/17 utekelezaji wa miradi ya DMDP Awamu ya kwanza ulianza.
Sekretarieti ya Mkoa ndo ilikuwa na jukumu la ushiriki wa pamoja na Ofisi ya Rais TAMISEMI na Manispaa katika maandalizi ya usimamizi wa utekelezaji wa mradi. Kwa sasa Mchakato ya Kuunda Mamlaka ya Jiji la Dar Es Salaam kusimamia miradi huu unaendelea.
Manispaa Bajeti kwa Mwaka 2016/17 (Sh.) Kazi zilizoanza kutekelezwa Temeke 72,804,468,467.00
- Kujenga barabara za mlisho 14.51km
- Ujenzi wa mitaro mikubwa 8.9km
- Ujenzi wa barabara za mitaa 55km
Ilala 43,242,117,826.00
- Kujenga barabara za mlisho 2.84km
- Ujenzi wa mitaro mikubwa
- Ujenzi wa barabara za mitaa 55km
Kinondoni 63,938,175,211.00
- Kujenga barabara za mlisho 14.51km
- Ujenzi wa mitaro mikubwa 8.9km
- Ujenzi wa barabara za Mitaa 55km
Kutekelezwa kwa miradi hii kumeibadilisha sura ya Jiji la Dar es Salaam na kuwa na muonekano. Sasa hivi Ukienda Mbagala, Kijichi, Temeke, Ilala, Tandika nk, Unakuta lami hadi vichochochoroni. Yote hayo ni Matunda ya Miradi ya DMDP.
MIRADI YA DMDP II INAYOJENGWA KUANZIA 2024
Mwaka 2024, Miradi ya DMDP II inaanza tena ambapo, Mkoa wa Dar es Salaam, barabara za awali zitakazoanza kujengwa kwenye awamu ya kwanza ya utekelezaji na zimeshafanyiwa usanifu zitakuwa zina urefu wa kilomita 150.74.
Kwa wilaya ya Ubungo, jumla ya kilomita 36.11 zitajengwa kwenye maeneo zaidi ya 20 kwa umbali tofauti.
Katika maeneo yote barabara ndefu zaidi ni kilomita 9.83 ya Msumi, na Goba Wakorea kilomita 7.76, huku barabara fupi ni ile ya kilomita 0.28 ya Tiptop na barabara ya Shule.
Nyingine ni Hondogo Shija (4.16), Makoka (4.04), Posta Matembe (0.82), Sheikh Bofu (1.13), Msikitini (0.37), Sinza KKKT (0.27), Segesera (0.77), Lion (0.84), Juma Ikangaa (0.97), Mbegani (0.28), Namnani (0.66), Chimwaga (0.34) na Mikindani (0.45)
Zimo barabara za Ubungo NHC (0.6), Midizini (0.99) na Binti Kayenga (1.27). Jumla ni kilomita 36.11.
Manispaa ya Kinondoni
Kilomita 20.34 zitajengwa katika manispaa hii. Zipo barabara za Nakalekwa -Bwawani (7.32), Umoja (3.86), Mivumoni (4.79), Tegeta Polisi - Silver- Binti Matola (0.77), na Amiri/Leni Tatu (Dawasa) kilomita 0.68.
Nyingine ni Togo (0.36), Togo 2 (0.36) na Togo 3 (0.2).
Jiji la Dar es Salaam(Wilaya ya Ilala)
Jumla ya kilomita 29.8 zitajengwa zikijumuisha barabara ya Banana Kitunda- Kivule -Msongola kilomita (16.31), Barakuda- Changombe -Majichumvi (3.27), Majumba Sita - Segerea (3.31), Migombani (1.57), Tabata Mawenzi - Kisiwani 2.12 na Bombom Market (0.12).
Barabara nyingine ni Community Park 2 (0.38), Community Park 2 Road 2 (0.56), Community Park 2 Road 3 (0.11), Community Park 2 Road 4 (0.11), Community Park 1 (0.35), Community Park 2 (0.11), Kigilagila Market 2 (0.28), Kigilagila Market (0.76), Kigilagila Market 3 (0.44).
Temeke
Kilomita 32.09 zitajengwa zikigusa barabara ya Ndunguru (1.64), Masaki (3.91) Masuliza (4.04) Kipati (0.72), Agape (1.07), Kilimahewa -Toangoma (6.17), Msikitini (0.45), Mwembeni (Nyika) (0.44), Malawi (0.28), Songambele (0.32), Mwakalinga Road 1.07.
Nyingine ni Markas (0.48), Majimaji (0.32), Keko Machungwa (0.57), Magorofani (0.31), Igome (Yemen) kilomita 0.85, Diwani (0.67), Basri (0.9), Konisaga 1 (0.29), Konisaga (3 0.4), Kurasini (1.12), Taningira (0.42), Uhasibu (0.44), Kizota (0.91) na Lushoto (0.3).
Pia zimo barabara za Pendamoyo (0.56), Pendamoyo 1 (0.2), Mandera (0.85), Mkumba - Miburani (0.39).
Kigamboni
Kwa upande wa Manispaa ya Kigamboni, zitaboreshwa barabara za kilomita 32.4.
Hizi zitajumuisha MC Full Shangwe (1.38), Gofingo - Shangwe (1.77), Kibada Plot (2.91), Lingia - Nyakwale (3.75), Gezaulole (Mivumoni) (7.05), Geza Juu - Eddah Avenue (2.92), Muongozo P/S (2.85), Pengo Simba (2.47), Dege Mbutu (1.6) na Atani Dege (1.76).
Nyingine ni Machava Njama (0.7), Mtaa wa Maji - Posta (1.28), Orasa (0.89), Mzee Msomi (0.65) na Polisi Pikori.
ujio wa DMDP awamu ya pili ni kicheko na furaha kwa Wananchi ambao hawakufikiwa na awamu ya kwanza.
Je, Umenufaikaje na miradi hii Sehemu unayoishi? Nini maoni yako?
Asante.
Ni kweli Mkuu, nimeangalia nikakuta ilitengewa fedha na tenda ilishatangazwa kwenye bajeti ya 2021/22 kwenye awamu ya kwanza ya DMDP. Sijajua kwanini haijaanza kujengwa hadi sasa.Huko nyuma niliwahi kusoma kwamba barabara ya Mvuti - Dondwe imo DMDP phase two. Ila sasa sijaiona hapo juu. Jee iliondolewa?
Hata mnaofatilia michango yenu ndio hii, nanyi bado mnaziwaza simba ya yanga, kweli tuna safari ndefu mkuu.Mada kama hizi tunafatilia wachache, wengi akili ipo kwa yanga na simba, tuna safari ndefu sana
Ndipo CCM ilipofikisha taifa lote ili iwe rahisi kutawala na kuiba. Maandishi kama haya hayana maana yoyote kwa sababu ni bla bla bla tu.Mada kama hizi tunafatilia wachache, wengi akili ipo kwa yanga na simba, tuna safari ndefu sana
Ungefupisha haya maelezo kwa maneno machache sana. CCM ime fail kwa hali zote na bila mabadiliko ya mfumo na viongozi hakutakuwa na ufanisi.Ni kweli Mkuu, nimeangalia nikakuta ilitengewa fedha na tenda ilishatangazwa kwenye bajeti ya 2021/22 kwenye awamu ya kwanza ya DPDP. Sijajua kwanini haijaanza kujengwa hadi sasa.
Ila kwa uzoefu unakuta watu wanagoma kupisha miundombinu ya Barabara na kwenda Mahakamani hasa waliojenga katibu na barabara. Miradi mingine inachelewa kutokana na uzembe wa Mkandarasi. Wengine wanachelewesha miradi kutokana na Serikali kutokutoa hela. Unakuta fungu la hela linahamishwa kutoka mradi A kwenda B. Mfano hela za Barabara ya Bonyokwa huko Kimara zilihamishwa zikaenda kujenga barabara lililobomoka kipindi cha mvua za el nino.
Nyie wakazi wa huko muwe mnahudhuria Mikutano ya Serikali ili kuwauliza maswali kama haya.
Tenda ya hiyo barabara hii hapa
We hujapita uzi wa kula tundra kimasihara?acha kuwasingizia Simba na Yanga.Mada kama hizi tunafatilia wachache, wengi akili ipo kwa yanga na simba, tuna safari ndefu sana
Ipo Wilaya ya Temeke kabla hujafika Mbagala. Kituo kabla ya Zakhem.Kipati ipo wilaya gani ?
Inaweza kujengwa hata kama haipo kwenye mradi. Sababu sio kila barabara inayojengwa na Tarura ipo DMDP. Ila watu wa Viwege kazi mnayo. Upite ile Barabara hadi Utoboe kwa Muhaya, lazima utubu🤣🤣🤣Majohe Viwege sijaiona. Kuna mpuuzi kaninunulisha kiwanja huko kwa kuniaminisha soon lami inapita kupitia DMDP.
Asante kwa ufafanuzi ILA mbona kinondoni zipo chache hasa jimbo la kawe ambalo halijawahi guswa na dmdp phase za nyuma????
Katika mwaka wa fedha 2015/16 Serikali iliingia Mkataba na Benki ya Dunia wenye thamani ya dola za Kimarekani 300 milioni za utekelezaji wa mradi wa DMDP kwa kipindi cha miaka mitano. Aidha, mfuko wa maendeleo ya nchi za Nordic (NDF) umechangia dola za Kimarekani 5 milioni kwa ajili ya kukabili changamoto za mabadiliko ya tabia Nchi na Serikali ya Tanzania ina changia dola za Kimarekani 25.3 milioni katika mradi huu.
Katika mwaka fedha 2016/17 utekelezaji wa miradi ya DMDP Awamu ya kwanza ulianza.
Tanzania sio Dar pekee kwamba Kila kitu ni huko hukoKatika Mwaka wa fedha 2012/13 Serikali ilibuni Mradi wa uendelezaji wa Jiji la Dar es salaam (Dar es Salaam Metropolitan Development Project – DMDP), Madhumuni makubwa ya mradi wa DMDP ni kukabili changamoto zinazolikabili Jiji la Dar es Salaam kwa kutilia mkazo uboreshaji wa huduma za jamii kama miundombinu na kujenga uwezo wa Manispaa za Jiji la Dar es Salaam katika utoaji huduma, kuchangia katika kukabili changamoto za mabadiliko ya tabia nchi na kusaidia katika kukabili matukio makubwa ya dharura kama majanga ambayo yanaweza kulikabili Jiji la Dar es Salaam.
Vipaumbele muhimu vilianishwa kwa kufuata vigezo muhimu bila kuangalia umaarufu wa maeneo au itikadi mbalimbali. Vigezo muhimu vilivyoanishwa ni pamoja na Miradi iwe inayounganisha maeneo ya watu wenye kipato kidogo na yaliyojengwa holela, Miradi iwe inayounganisha Wilaya na Mkoa na Miradi iwe inayounganisha maeneo mbalimbali na ukanda wa mabasi yaendayo haraka (BRT) ili kurahisisha usafirishaji.
Ikaibuliwa miradi ya Ujenzi barabara za mlisho (feeder roads) zenye urefu wa kilometa 65.6 katika Manispaa zote za Jiji ili kupunguza changamoto za msongamano. Mradi Mwingine ukawa ni Ujenzi wa mitaro ya kutiririsha maji ya mvua yenye urefu wa kilometa 31.8 katika maeneo ya mto Ng’ombe, Msimbazi, Gerezani Creek, Yombo na Kwashego ili kutatua changamoto za mafuriko.
Kupandisha hadhi makazi yaliyopangwa kiholela katika Kata 14 za Tandale, Mburahati, Mwananyamala, Gongo la Mboto, Kiwalani, Ukonga, Keko, Kilakala, Mbagalakuu, Mbagala, Mtoni, Yombo Vituka, Kijichi na Makangarawe kwa kujenga kilometa 145 kwa kiwango cha lami, kuweka nyenzo za ukusanyaji wa taka ngumu, kujenga mitaro ya kutiririsha maji ya mvua, kuweka taa za barabarani, kujenga njia za watembea kwa miguu, ujenzi wa maeneo ya mapumziko na vituo vya mabasi, ujenzi wa vyoo vya umma na ujenzi wa maeneo ya michezo.
Kuandaa Mpango kabambe wa Mfumo wa Maji ya Mvua na Maji Taka (Storm Drainage and Sewerage Master plan) kwa kushirikiana na DAWASA/DAWASCO ambao utasaidia kupanua wigo wa mifumo kwa asilimia 100% kufikia 2030. Kufunga mfumo wa kisasa wa ukusanyaji wa mapato katika Manispaa zote na kuepuka mianya ya kuvuja na ukwepaji wa kulipa kodi. Na Kujenga uwezo wa mwitikio wa haraka katika kukabiliana na majanga.
UTEKELEZAJI
Katika mwaka wa fedha 2015/16 Serikali iliingia Mkataba na Benki ya Dunia wenye thamani ya dola za Kimarekani 300 milioni za utekelezaji wa mradi wa DMDP kwa kipindi cha miaka mitano. Aidha, mfuko wa maendeleo ya nchi za Nordic (NDF) umechangia dola za Kimarekani 5 milioni kwa ajili ya kukabili changamoto za mabadiliko ya tabia Nchi na Serikali ya Tanzania ina changia dola za Kimarekani 25.3 milioni katika mradi huu.
Katika mwaka fedha 2016/17 utekelezaji wa miradi ya DMDP Awamu ya kwanza ulianza.
Sekretarieti ya Mkoa ndo ilikuwa na jukumu la ushiriki wa pamoja na Ofisi ya Rais TAMISEMI na Manispaa katika maandalizi ya usimamizi wa utekelezaji wa mradi. Kwa sasa Mchakato ya Kuunda Mamlaka ya Jiji la Dar Es Salaam kusimamia miradi huu unaendelea.
Manispaa Bajeti kwa Mwaka 2016/17 (Sh.) Kazi zilizoanza kutekelezwa Temeke 72,804,468,467.00
- Kujenga barabara za mlisho 14.51km
- Ujenzi wa mitaro mikubwa 8.9km
- Ujenzi wa barabara za mitaa 55km
Ilala 43,242,117,826.00
- Kujenga barabara za mlisho 2.84km
- Ujenzi wa mitaro mikubwa
- Ujenzi wa barabara za mitaa 55km
Kinondoni 63,938,175,211.00
- Kujenga barabara za mlisho 14.51km
- Ujenzi wa mitaro mikubwa 8.9km
- Ujenzi wa barabara za Mitaa 55km
Kutekelezwa kwa miradi hii kumeibadilisha sura ya Jiji la Dar es Salaam na kuwa na muonekano. Sasa hivi Ukienda Mbagala, Kijichi, Temeke, Ilala, Tandika nk, Unakuta lami hadi vichochochoroni. Yote hayo ni Matunda ya Miradi ya DMDP.
MIRADI YA DMDP II INAYOJENGWA KUANZIA 2024
Mwaka 2024, Miradi ya DMDP II inaanza tena ambapo, Mkoa wa Dar es Salaam, barabara za awali zitakazoanza kujengwa kwenye awamu ya kwanza ya utekelezaji na zimeshafanyiwa usanifu zitakuwa zina urefu wa kilomita 150.74.
Kwa wilaya ya Ubungo, jumla ya kilomita 36.11 zitajengwa kwenye maeneo zaidi ya 20 kwa umbali tofauti.
Katika maeneo yote barabara ndefu zaidi ni kilomita 9.83 ya Msumi, na Goba Wakorea kilomita 7.76, huku barabara fupi ni ile ya kilomita 0.28 ya Tiptop na barabara ya Shule.
Nyingine ni Hondogo Shija (4.16), Makoka (4.04), Posta Matembe (0.82), Sheikh Bofu (1.13), Msikitini (0.37), Sinza KKKT (0.27), Segesera (0.77), Lion (0.84), Juma Ikangaa (0.97), Mbegani (0.28), Namnani (0.66), Chimwaga (0.34) na Mikindani (0.45)
Zimo barabara za Ubungo NHC (0.6), Midizini (0.99) na Binti Kayenga (1.27). Jumla ni kilomita 36.11.
Manispaa ya Kinondoni
Kilomita 20.34 zitajengwa katika manispaa hii. Zipo barabara za Nakalekwa -Bwawani (7.32), Umoja (3.86), Mivumoni (4.79), Tegeta Polisi - Silver- Binti Matola (0.77), na Amiri/Leni Tatu (Dawasa) kilomita 0.68.
Nyingine ni Togo (0.36), Togo 2 (0.36) na Togo 3 (0.2).
Jiji la Dar es Salaam(Wilaya ya Ilala)
Jumla ya kilomita 29.8 zitajengwa zikijumuisha barabara ya Banana Kitunda- Kivule -Msongola kilomita (16.31), Barakuda- Changombe -Majichumvi (3.27), Majumba Sita - Segerea (3.31), Migombani (1.57), Tabata Mawenzi - Kisiwani 2.12 na Bombom Market (0.12).
Barabara nyingine ni Community Park 2 (0.38), Community Park 2 Road 2 (0.56), Community Park 2 Road 3 (0.11), Community Park 2 Road 4 (0.11), Community Park 1 (0.35), Community Park 2 (0.11), Kigilagila Market 2 (0.28), Kigilagila Market (0.76), Kigilagila Market 3 (0.44).
Temeke
Kilomita 32.09 zitajengwa zikigusa barabara ya Ndunguru (1.64), Masaki (3.91) Masuliza (4.04) Kipati (0.72), Agape (1.07), Kilimahewa -Toangoma (6.17), Msikitini (0.45), Mwembeni (Nyika) (0.44), Malawi (0.28), Songambele (0.32), Mwakalinga Road 1.07.
Nyingine ni Markas (0.48), Majimaji (0.32), Keko Machungwa (0.57), Magorofani (0.31), Igome (Yemen) kilomita 0.85, Diwani (0.67), Basri (0.9), Konisaga 1 (0.29), Konisaga (3 0.4), Kurasini (1.12), Taningira (0.42), Uhasibu (0.44), Kizota (0.91) na Lushoto (0.3).
Pia zimo barabara za Pendamoyo (0.56), Pendamoyo 1 (0.2), Mandera (0.85), Mkumba - Miburani (0.39).
Kigamboni
Kwa upande wa Manispaa ya Kigamboni, zitaboreshwa barabara za kilomita 32.4.
Hizi zitajumuisha MC Full Shangwe (1.38), Gofingo - Shangwe (1.77), Kibada Plot (2.91), Lingia - Nyakwale (3.75), Gezaulole (Mivumoni) (7.05), Geza Juu - Eddah Avenue (2.92), Muongozo P/S (2.85), Pengo Simba (2.47), Dege Mbutu (1.6) na Atani Dege (1.76).
Nyingine ni Machava Njama (0.7), Mtaa wa Maji - Posta (1.28), Orasa (0.89), Mzee Msomi (0.65) na Polisi Pikori.
ujio wa DMDP awamu ya pili ni kicheko na furaha kwa Wananchi ambao hawakufikiwa na awamu ya kwanza.
Je, Umenufaikaje na miradi hii Sehemu unayoishi? Nini maoni yako?
Asanteni sana. Mjadala upo wazi karibuni
Kwani hapo Kuna ishu gani spesho zaidi ya reporting Kwa Umma?Mada kama hizi tunafatilia wachache, wengi akili ipo kwa yanga na simba, tuna safari ndefu sana
DMDP awamu ya kwanza ilifanyika wakati wa Mwendazake na hakuna mradi wowote wa DMDP mwaka ulioutaja weweNi kweli Mkuu, nimeangalia nikakuta ilitengewa fedha na tenda ilishatangazwa kwenye bajeti ya 2021/22 kwenye awamu ya kwanza ya DMDP. Sijajua kwanini haijaanza kujengwa hadi sasa.
Ila kwa uzoefu unakuta watu wanagoma kupisha miundombinu ya Barabara na kwenda Mahakamani hasa waliojenga katibu na barabara. Miradi mingine inachelewa kutokana na uzembe wa Mkandarasi. Wengine wanachelewesha miradi kutokana na Serikali kutokutoa hela. Unakuta fungu la hela linahamishwa kutoka mradi A kwenda B. Mfano hela za Barabara ya Bonyokwa huko Kimara zilihamishwa zikaenda kujenga barabara lililobomoka kipindi cha mvua za el nino.
Nyie wakazi wa huko muwe mnahudhuria Mikutano ya Serikali ili kuwauliza maswali kama haya.
Tenda ya hiyo barabara hii hapa