Ninapitia msongo mkali wa mawazo baada ya kusimamishwa kazi kisa vyeti feki. Naomba ushauri niweze kujikwamua

Ninapitia msongo mkali wa mawazo baada ya kusimamishwa kazi kisa vyeti feki. Naomba ushauri niweze kujikwamua

Nimesoma UDSM miaka hiyo ya 2000s haikuwa na Diploma. Ni Degree ,Masters na PHD.

Huyu mhusika anaweza kuwa ni mwanaume anatafuta kuwaibia watu au mwanamke anatafuta pia sympathy awapige watu.

Script yake haikuandaliwa vizuri kabisa. Angeomba tumsaidie jinsi ya kuandika. Huyu could be tapeli. Na huku ndani tuna MISS NATAFUTA. Huyu kabadilisha jina kawa MISS NATAFUTWA.
Usiwe mwepesi wa kuhukumu bado Kuna baadhi ya maelezo yanaeleweka vizuri, mpe moyo maisha yanabadilika.
 
Naamini ulivyo andika juu ya Kaka Max

Ukienda ofisini kwake aka kuona na kutoa taarifa hapa bila kukutana au kuweka picha yako kama hautaki

Basi mdogo wako atapataja pesa za kusomeshwa na Mahitaji mengine kama yeye

Taja shule anasoma na Mahitaji watu wanunue apewe

Ila hakuna ada si ndio so hayo mengineyo

If unataka kweli naamini ukiwa umesema umatafufa kazi nawe utakuwa unajiongeza kivyako
 
Dada acha haya majadiliano, unaanza kunikwaza; endelea na mengine niweze kuendelea kukusitiri!
Utttoh unataka kumsaidia kusoma jambo zuri sana. Je kama hataki...angalia historia ya elimu yake na miaka yake hapo anaweza asiwepo rahisi sana kusoma. Vilevile ktk suala la elimu yake na wewe unataka kumpeleka kusoma hoping degree kma ni ya TCU huwa Wana link data za NECTA Sasa huyu atapita kweli hapo na anacheti fake.l Cha PDGE aliyoipata kwa cheti Cha form four tena fake. Kwanza PDGE ni post graduate ktk elimu. Sasa alifikaje kuwa graduate na kwenda kusomea elimu. Maana yake huyu ana degree nyingine au diploma nyingine isiyokuwa ya elimu. Sasa sula la vyeti fake linatoa ukakasi. Application zote za vyuo zinapitia kwa TCU kwa ku link form four index number. Anyway, elimu yake inanukakasi. Ni bora kuomba msaada au kutoa msaada bila kuzingatia details. Kuna details ametoa hazilink up.
 
udsm diploma.jpg
 
Pole na changamoto unayopitia...

Huyo mdogo wako anasoma Shule za binafsi (Kulipia) ama Shule za Serikali?

Tukijua mahitaji yake ya kusoma kwasasa, na tukathibitisha, tunaweza kumchangia japo yeye aendelee na masomo

Umesema uliondolewa Kazini kutokana na ile skendo ya Vyeti feki, Rudi Kwa mwajiri wako wa zamani (Halmashauri) wakupe barua ya kukufukuza kazi kisha uitumie kwenda kwenye Taasisi uliyokuwa unachangia pension ili wakupe fao la kukosa ajira ili walau liku-boost wakati huu mgumu unaopitia.

Mungu akupe uvumilivu ili usije kufanya maamuzi ambayo yanaweza kukutengenisha naye.

Kila la heri Mkuu
 
Habari wana Jf kwa ujumla.
Sina muda mrefu tangu nijiunge na jumuia hii chini ya kaka Max.

Ni hivi, napitia msongo mkali sana wa mawazo yaani nikisema ni mkali namaanisha.

First of all nilikuwa muajiriwa serikalini na likapita suala la vyeti feki hapo nilikuwa natumia cheti cha mtu na kazi ikawa ndio basi.

Sababu nilipoteza wazazi ikabidi ile akiba niliyojiwekea kipindi nafanya kazi niitumie kwa ajili ya kumsomesha mdogo wangu ambae niliachiwa na wazazi pamoja na kununua kiwanja tu. Hali ikazidi kuwa mbaya zaidi, ikabidi niingie kwenye kazi ya kujiuza.

Nilichokuwa nafanya ni kumuandalia mdogo wangu sare za shule na pesa ya matumizi usiku ili hata kama nitarudi asubuhi au kama sitarudi kabisa basi apate kujiandaa na kwenda shule (shule na nyumbani ni kama km 1 tu) mwenyewe.

Nilifanya hiyo kazi kwa miaka 6, nikapata pesa na kuanza ujenzi wa nyumba yangu ya kuishi pamoja na mdogo wangu.

Shida imeanza tena, nyumba haijakamilika na pesa zote nimemaliza na mdogo wangu mwaka huu anaingia kidato cha 3.
Sitaki tena kurudi kule nilipotoka (kujiuza). Nahitaji mdogo wangu akue bila kujua nafanya nini. Pia nahitaji kumalizia nyumba

Kama kuna mtu ana uhitaji wa mtu wa kufanya kazi naomba nipewe ajira.

1. Nina diploma ya Education niliyoipata pale UDSM kabla sijatumbuliwa.

2. Nina uzoefu katika kulea watoto na pia ninajua sana upishi (nilisomea hotel management kabla sijaenda kusomea ualimu), Umri wangu ni miaka 42 na niko Morogoro.

Asanteni.
Umeongea ukweli ambao pia kwa namna fulani ni kama umetubu uliyowahi kuyafanya. Nakupa pole kwa uliyoyapitia na hata sasa unayopitia.
 
Pope sana dada, Natumai wenye uhitaji wata kusikia.

Mzee wangu Ushimen, Shimba ya Buyenze, Grahams, Mshana Jr msikilizeni dada yetu hapa
Nimeona andiko lake, Kuna vitu nimeshauri kupitia maoni niliyoyatoa hapo juu,

Kama ataweza atuletee uthibisho wa nyaraka ili tuweze kumchangia ili mdogo wake aendelee na masomo.

Na Kwa kuwa JF ni pool kubwa, natumai wenye uwezo wa kumwajiri watafanya hivyo

Najua Kuna baadhi yetu humu ndani, tunafanya biashara ya Shule(tunamiliki) kwahiyo ni rahisi wakiona ana sifa hasa ya uzoefu wampe ajira
 
Back
Top Bottom