Ngoja nitanabaishe kidogo......
Mara nyingi ibilisi shetani huwa anatafuta chanzo ili kukuchochea kwenye uovu ambao kwa wakati huo hata hilo wazo hukuwa nalo kabisa......
Hata wale wanaolala na Shemeji zao, ndugu zao wa damu, watoto wao wa kuwazaa, walimu kulala na kuwalawiti wanafunzi wao wengi wa watendaji wa haya matukio asilimia kubwa hapo hawali hawakuwa na fikra hizo na wengi wamekuwa wenye kujuta.....
Namna bora ya kuzieupuka hila na ghiriba za ibirisi shetani ni kukaa mbali na vishawishi hata viwe vidogo kiasi gani......chunga Sana mipaka yako kwa maana Sisi wanadamu tuna mapungufu na ni wadhaifu........
Haya anayoyasema mtoa mada kwa hali ya kawaida yanaweza kuonekana kama uhayawani kumdhania mabaya shemeji yake lakini tukirudi kwenye ubinadamu na mapungufu yetu inawezekana akafanya kwani hayo matukio yapo na yanafanywa na binadamu kama yeye......
Si jambo jema watu wa jinsia mbili au mtu mzima kulala au kutumia faragha pamoja ikiwa hakuna uhalali baina yao unless kuwe na dharula labda ya maradhi au namna nyingine..... wanadamu lazima tuwe na mipaka ya kifaragha na sio kuishi kama wanyama........
Wapo watu wamefanya mambo mabaya na kujifunza mambo mabaya yasiyofaa kwa kujiweka karibu na watu wabaya au vitu vibaya.....