Ninaumizwa sana na hawa Wachungaji ambao sisi sote tunajua ni matapeli

Ninaumizwa sana na hawa Wachungaji ambao sisi sote tunajua ni matapeli

Upastor ni kazi ya Mungu, kazi yenye heshima katika Imani, lakini wote tunajua Mapastor wanafanya biashara ya kuokota sadaka.

Nina uhakika asilimia mia wale wanaohutubia njiani wanatafuta sadaka.

Hii kitu inaniumiza sana.
Tokeni huko mlipo kabla hamjachelewa.
 
Mnaweza kujadili vile mnavyofikiri kwa sababu ya hizo sadaka lakini mnasahau kuwa kuwa mchungaji hakuondoi mahitaji ya kibinadamu, wanahitaji kusomesha Kama unavyosomesha wewe, wanahitaj kukaa mahali pazuri Kama unavyopambana wewe ukae mahali pazuri

Wakati Mungu anagawa urithi kwa wana waisrael kabila la lawi hawakupata urithi wowote, wao walitakiwa wale vile vinavyoletwa madhabahuni na hao ndugu zao maana wao kazi yao ilikuwa kutumika madhabahuni hawakupaswa kulima au kufanya kazi yoyote ya kiuchumi, kwahiyo walitakiwa kuishi kutikana na hizo sadaka. Sasa mtu unaposema mchungaji ameenda kuhubiri asipewe chochote kwa sababu amehudumiwa unatakiwa kujiuliza alienda na familia yake??... Lakini maandiko yanasema mtenda kazi astahili posho lake.

Hebu tutafakari hapa unamgonjwa ukaenda kumfuata mtumishi amuombee akapona kwani hutakiwi kumshukuru Mungu?? Na ukimshukuru kwa sadaka atachukua nani Kama sio huyo mchungaji aliyekuja?

Huko kwa manabiii mnayataka wenyewe kwenda kupigwa kwasababu nabii huwa hajitangazi anayejitangaza ni tapeli.

Kingine unapotoa sadaka imani yako unaiweka wapi kwa Mungu au kwa anayepokea sadaka yako? Unapotoa sadaka weka imani kwa Mungu usiweke imani kwa anayepokea kwa sababu sadaka haziend mbinguni zinatumika hapa hapa katika kufanya kazi ya Mungu.

Hitimisho huwezi kutumia sadaka kumtambua mchungaji wa kweli au asiye wa kweli mbona kwa waganga mnapeleka sadaka na hamuwalalamikii kwa utapel wa kupokea sadaka?? Bibilia inasema mtawatambua kwa matendo yao.

LINDA SANA IMANI YAKO, KWA SABABU MCHUNGAJI, NABII AU MTUME HANA NAFASI YA KUKUTETEA BALI MUNGU NDIYE ATAKUTETEA
Sadaka ilenge kwa muhitaji wa kweli. Mfano wa anayestahili kutolewa Sadaka ni yule ambaye anashindwa kutimiza hata mahitaji muhimu.
Sasa unapomchangia mchungaji ili akanunue Prado hapo itakua ni kinyume na maana halisi ya sadaka.
By the way wachungaji wasingejishughulisha na mambo ya kidunia mfano marimba ya kifahari magari. Kwani tunafahamu haya ni ya mpito tu maisha yenyewe tutaenda yakuta mbinguni.
 
Kuna uchungaji na wachungaji
Kuna wale ambao baada ya kutafuta ajira zikagoma wanageuza makanisa kuwa ajira mbadala
#akili kichwani
 
Alipofilisha miaka 30 akaanza kuhubiri injili, alikuwa anaendelea na useremala?
Hakuna sehemu ilisemwa aliacha kazi yake ya Useremala. Hata wafuasi wake walipiga kazi. Paulo nasikia alitengeneza mahema. Hata walijisifu kuwa walifanya kazi hawakuwa tegemezi.
 
Upastor ni kazi ya Mungu, kazi yenye heshima katika Imani, lakini wote tunajua Mapastor wanafanya biashara ya kuokota sadaka.

Nina uhakika asilimia mia wale wanaohutubia njiani wanatafuta sadaka.

Hii kitu inaniumiza sana.
Wajinga ni hao wanaoenda, kama wasingewafuata mbona wangeacha huo utapeli wao
 
Upastor ni kazi ya Mungu, kazi yenye heshima katika Imani, lakini wote tunajua Mapastor wanafanya biashara ya kuokota sadaka.

Nina uhakika asilimia mia wale wanaohutubia njiani wanatafuta sadaka.

Hii kitu inaniumiza sana.

Tatizo wale wanaohubiri mitaani huwa wanafanya Kama mradi. Unakuta mtu anahubiri kwenye basi halafu akimaliza anadai sadaka kila siti. Nadhani wanahitaji elimu.
 
Njoo Islam dini ya kweli. Utaenda msikitini kuswali na kuomba buree. Sadaka ni option na ni kidogo. Dini ishatuambia wenye uwezo wachangie.

Bahati wenye wamejaaliwa mali wanatambua hilo wanajenga sehemu za ibada. Wala hawajikadhibishi bali wanamkabithi M. Mungu. sisi tunaingia na kuabudu tu.

Tofautisha dini na imani. Kuna dini ya kiislamu na imani ya kiislamu. Nenda hapo Somalia ndio utajua tofauti ya dini ya kiislamu na imani ya kiislamu.
 
Back
Top Bottom