Ninawaza kuanzisha kitu kinachoitwa Tantech Association, naomba ushirikiano wenu

Pamoja na maono yako unaweza pia kupitia hapa ether you fight them or join them


 
Dogo wazo lako ni zuri lakin kwa uzoefu wangu hio project yako hutafanikisha kwa Sasa ukiwa upo secondary kwa sababu project inahitaji vitu ving sana.
endelea kutafta ideas tofauti tofauti kuhusiana na hio plan yako ili ukifika chuo uifanye kwa urahisi zaidi kwa sababu utakua na vifaa na muda wa kutisha.
NB: HIO PLAN YAKO ILISHAFANYIKAN TAYARI .
Endelea kutafta ideas tofauti kwa sababu umekua interested.

Nenda google scholar utakuta ideas kibao then we utafanya developing.
 
anawazo zuri
Ila,mtoto wetu simu Katoa wapi umri huo aanze kusoma maandiko yakina to yeye hapa kuhusu kutoolewa
 
onho sawa nimekuelewa ngoja nikuelezee

Shukrani sana kaka maana pia umenipa guides, nitafata ushauri wako
 
Sawa kaka ngoja nakuelezea vizuri
 
Vizuri kwa wazo.

Sasa unajua nini mdogo angu.

Ili hilo wazo lizidi kushika nguvu kichwani na maishani na pia ujiandae kuwakamata wadau wa kuwekeza kama sie (Sahili rnd) fanya kuandaa kitu inaitwa Business plan.

Tena hata kama sio kwa ajili ya wawekezaji hata wewe mwenyewe tu kulitawala wazo lako vizuri andaa hiyo business plan. Kwa maelezo ya namna ya kuandaa huo mpangokazi unaweza kusoma hapa katika blogu hii
 
First nilikuwa nahitaji msaada wenu jinsi ya kukamilisha wazo langu.

Yes nina prototype pia inaweza fanya kazi but wadau wa kutosha sijapata!

Wadau wa kutosha sina ndo maana nimekuja hata kuomba sapoti zetu maana nitahitaji material mbalimbali ambayo yatatoka kweny nyie wadau wa teknolojia
 
sawa kaka nimekueelwa na nitafata ushauri huo
 
Hahaaa ngoja nikuache sidhani kama ulienda shule, walo enda shule wana mwambia asome.
It's not about swala la kubishana kama una wazo kama mdau litoe tu ambayo litanipa mwongozo kama nafanya kitu sahihi au sio sahihi...

sasa unafanya kutoa tu maneno ambayo hayaeleweki🤌🏽
 
Wazo zuri Baraka.

PMC ndiyo Physics Math na Chemistry? Sisi tuliijua kama PCM.

Mimi nilisoma Tambaza kitambo sana.

Kuna kipindi alumni tulijipanga kutoa msaada wa computers.

Hali ya computer lab ikoje shuleni?
 
Okay kwahio unahitaji platform ya kuunganisha wadau katika mambo ya teknolojia (platform sio kazi kuipata na unaweza ukatengeneza kama ni website au App) hilo sio tatizo kabisa issue ni kupata wadau watumiaji na hao watakuja kama kuna content ya kuweza kuinyonya na kuna watu wa kuwasaidie kupata hio content....

Kwahio sababu upo hapo shule na unasomea haya mambo anzisha hata website tena mwanzo unaweza ikawa locked kwa members ambao ni wanafunzi wenzako na mwalimu wenu mkawa mnashare hizo information tofauti tofauti..., na sababu unalenga watanzania na issue za tanzania ni bora ukaifanya ikawa ya kiswahili na ukishajaza wenzako wa mashuleni unaweza kuingia mtaani ukachukua wadau au ni mafundi (simu; computers photocopy n.k.) hao ndio wengi na wengi wao watakuwa wanakutana kuulizana wanapataje information....

Cha maani kuliko vyote its all about Community.....

Ukishatoka hapo utaanza kujiuliza how do you monetize ? Sababu kama utataka uuze information nadhani kwenye dunia ya free info itakuwa ngumu lakini unaweza kutumia indirect ways to monitize
 
Nenda COSTECH pale kuna incubator yakuitwa kaangalie kama inafanana yako cheki changamoto zao uone kama kunakitu chakuboresha kwa idea yako na ukienda pale kafanye research tu usiambie watu idea yako kuna mabro yatakukatisha tamaa
 
Duh kweli mambo hubadilika enzi sisi tunasaka material hilo neno WWW tulikuwa tu tunalisikia kwenye Redio na hapo ni baada ya kuweka battery juani kwa masaa ili nishati ipatikane na kuweka wire (Aerial) mpaka juu ya bati hapo kitabu cha cha physics (mechanical physics) kuna UP (university physics) kipo kwenye Ft na yards kwahio mpaka ufanye conversion kwenye metrics.... Sishangai madogo wa sasa kupata points tatu enzi zetu kungekuwa kuna urahisi wa kupata hizo materials huenda wangesema A iishie 95 na F kuanzia 60
 
Nope website unaweza kufanikisha kwa sekunde tu yaani kipindi cha lunch hour unatengeneza ukirudi darasani tayari upo hewani..., anza kutengeneza community now na sio later watumie marafiki zako na classmates wako tengenezeni kitu kitakuwa pole pole as time goes by...
 
Thanks bro kwa mawazo yako ya dhahabu nitayafata
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…