Ninawezaje kuifungulia mashtaka Benki ya NMB kwa dhuluma hii ya fedha zangu?

Ninawezaje kuifungulia mashtaka Benki ya NMB kwa dhuluma hii ya fedha zangu?

Mgaa gaa upwa

Senior Member
Joined
Jan 11, 2024
Posts
180
Reaction score
281
Poleni na majukumu ya Kila siku.

Mwezi wa tano nilimfungulia biashara ya uwakala mke wangu, nikajenga duka na lilipokamilika nikawa nimebakiwa na fedha kidogo Kama mtaji, baada ya biashara kuanza nikaona Umuhimu wa kupanua biashara.

Nikawahi Benki ya NMB na kupata mkopo wa fedha kidogo ili kukuza biashara nilichukua kidogo ili kuendana na upepo.

Upepo ukakubali hivyo nikaamua kuongeza mkopo (top up).

Hilo lilikuwa kosa kubwa kwani Mara baada ya fedha za top up kuingia tu matatizo yakaanza..

1:-Akaunti yangu ikafungiwa na kiasi changu Cha fedha zangu za akiba, matumizi binafsi na mkopo wenyewe zikafungiwa.

2:- Nikaanza kukatwa mkopo Mara mbili yaani nakatwa mkopo wa Kwanza ule mdogo nilioulipa (kwenye top up) na mkopo wa pili (mkopo mkuu uliobeba Deni lote) nakatwa pia.

3:- Mkopo wa Kwanza haujafutwa (Maana nimeulipia kwenye top up)

Nimefuatilia Sana tatizo langu hapa tawini Hadi branch manager akanichukia na kuanza kunitisha kuwa atanishtaki kwa mkurugenzi ili nifukuzwe kazi.

Nikaamua kuingia kwenye emails (NMB makao makuu,huduma kwa wateja na BOT huduma kwa wateja) nikatembelea tawi la NMB mkoani Ila tatizo lipo pale pale.

Kuanzia mwezi wa Tisa Hadi mwezi wa kumi na mbili bado namekatwa makato zaidi na fedha zangu zimezuiliwa.

Msaada wanajf maana mwaka unaelekea ukingoni na Mimi sijatimiza adhima ya kumuwezesha mke.

Nitumie mbinu gani, watu gani na njia gani kuchukua pesa zangu.

Nimeweka ushahidi wa emails hapo chini.

Emails kwenda BOT

Emails kwenda NMB
Screenshot_20241228-143342.png
Screenshot_20241228-144542.png
 
Pole kwa kukatwa mara mbili!

Nakushauri nenda mahakama ya kibiashara ukafungue madai yako!

Hakikisha una vielelezo vyako mhimu!

Shitaki na claim fidia na usumbufu wa hasara walizokuingizia!
Ukikosa wakili weka namba mawakili wazuri wapo waliobebea kwenye kesi kama hizo.

Ifahamike hata kucheleweshewa pesa kwa wakati ni kosa taasisi inatakiwa ishitakiwe!

Kama wao walivyo na haki yankukutoza riba ukichelewa na wao unaweza kuwashitaki kwa kukucheleweshea malipo!

Mimi maishani mwangu sitambui samahani! Nachojua ni kusudi na uzembe!
 
Unaweza Ila Kaa ukijua unaingia vitani na taasisi kubwa! Uwe na wanasheria wazuri ambao watakuwa na uhakika kwamba utashinda kutokana na maono yao yatakayotengenezwa na hoja au malalamiko yako.
Hiyo ndiyo changamoto kubwa inayonikabil mbele yangu, sijui nitumie mbinu gani maana ya maridhiano Kama imefika ukingoni.
 
Be smart Dai fidia wakulipe ela ya maana. Ukichora plan nzuri unaweza kunja atleast 100M

Kusanya ushahidi wowote ule kimya kimya (Bank statement n.k) alafu tafuta wakili mwelewa then mwandishi wa habari (Jambo TV ...) Ukimaliza watumie email ya kudai fidia then push plan yako kismart soon account itasoma kuanzia 100+M
 
Pole kukatwa mara mbili!
Nakushauri nenda mahakama ya kibiashara ukafungue madai yako! Hakikisha una vielelezo vyako mhimu!

Shitaki na claim fidia na usumbufu wa hasara walizokuingizia!
Je hizi mahakama zipo mikoani?
 
Be smart Dai fidia wakulipe ela ya maana. Ukichora plan nzuri unaweza kunja atleast 100M

Kusanya ushahidi wowote ule kimya kimya (Bank statement n.k) alafu tafuta wakili mwelewa then mwandishi wa habari (Jambo TV ...) Ukimaliza watumie email ya kudai fidia then push plan yako kismart soon account itasoma kuanzia 100+M
Ila kumbuka napambana na taasisi kubwa inayopitisha mishahara asilimia kubwa ya watumishi wa serikali.
 
Ila kumbuka napambana na taasisi kubwa iliyoshikilia mishahara asilimia kubwa ya watumishi wa serikali.
Acha ujinga,toka lini NMB inashikilia mishahara ya watumishi???
Mishahara ya Watumishi hulipwa na HAZINA kupitia Bank yoyote iliyoshinda tenda katika Mwaka wa Fedha husika,na kazi ya hiyo bank ni kuingiza kiasi cha pesa katika akount yako.
 
Be smart Dai fidia wakulipe ela ya maana. Ukichora plan nzuri unaweza kunja atleast 100M

Kusanya ushahidi wowote ule kimya kimya (Bank statement n.k) alafu tafuta wakili mwelewa then mwandishi wa habari (Jambo TV ...) Ukimaliza watumie email ya kudai fidia then push plan yako kismart soon account itasoma kuanzia 100+M
Mpaka anachezewa hivyo maana yake wamemuona hayuko smart,hiki anacho mshauri ndio anaweza kufanya?
 
Atakushtaki kwa mkurugenzi akufukuze kazi??? yani huyo meneja amechanganyikiwa au na wew unafanya kazi hapo nmb.
Sifanyi kazi nmb na Wala hatufahamiani naye sijui alinichukuliaje Hadi kunitisha hivyo.

Tena alikuwa kasimama na loan officers wake wakiwa na sura za chuki Kama Kuna maslahi wanayatetea
 
Hiyo ndiyo changamoto kubwa inayonikabil mbele yangu, sijui nitumie mbinu gani maana ya maridhiano Kama imefika ukingoni.
Kuna wenzako walikuwaga wanamuziki leo hii ni mabilionea… waliwashtaki TIGO na kwa bahati nzuri walikuwa wanajulikana, wakapataga na mwanasheria mzuri na uzuri wao wenyewe shule wanayo na familia walizotoka si haba. Wakasimamiwa kesi yao na DC alberto Msando kipindi hicho na yeye anajitafuta ila alikuwa vizuri kwenye sheria.

Wakashinda, wakapataga 3B, ndio mwanzo wa kuwa matajiri. Na wakaachana na muziki, wanafanya for fun tu. Mmoja naibu waziri…, mmoja mfanyabiashara tajiri sana! Na bongo anakaaga mara mojamoja tu.

Na huyo mwanasheria wao saiv ni mkuu wa wilaya fulani hapa nchini. Maisha yao ni raha tu
 
Acha ujinga,toka lini NMB inashikilia mishahara ya watumishi???
Mishahara ya Watumishi hulipwa na HAZINA kupitia Bank yoyote iliyoshinda tenda katika Mwaka wa Fedha husika,na kazi ya hiyo bank ni kuingiza kiasi cha pesa katika akount yako.
Asante.

Ila ingekuwa rahisi hivyo kuhama Benki hiyo kutoka na kupokea tu fedha kutoka hazina na kupitishwa kwa watumishi ningehama Benki maana mkopo mmoja wanaukata direct kutoka kwenye akaunti baada ya kutoka hazina.
 
Kuna wenzako walikuwaga wanamuziki leo hii ni mabilionea… waliwashtaki TIGO na kwa bahati nzuri walikuwa wanajulikana, wakapataga na mwanasheria mzuri na uzuri wao wenyewe shule wanayo na familia walizotoka si haba. Wakasimamiwa kesi yao na RC alberto Msando kipindi hicho na yeye anajitafuta ila alikuwa vizuri kwenye sheria.

Wakashinda, wakapataga 3B, ndio mwanzo wa kuwa matajiri. Na wakaachana na muziki, wanafanya for fun tu. Mmoja naibu waziri…, mmoja mfanyabiashara tajiri sana! Na bongo anakaaga mara mojamoja tu.

Na huyo mwanasheria wao saiv ni mkuu wa mkoa fulani hapa nchini. Maisha yao ni raha tu
Ungenisaidia Mambo mawili.


1:- Niweze kumfahamu aliyekuwa mwanasheria wao.

2:-Kufahamu zaidi kuhusu kesi hiyo tafadhari.
 
Back
Top Bottom