Nini chimbuko la Vita vya Uhujumu Uchumi - 1983-84?

Nini chimbuko la Vita vya Uhujumu Uchumi - 1983-84?

Wanabodi,
Sasa naona tunapoteza mwelekeo.. Kama alivyosema Nyani Ngabu hakuna mtu anayesema Tanzania mwaka 1984 ilikuwa katika hali nzuri kiuchumi kuliko leo hii ama Mwalimu hakuweza kukuza mfuko wetu.. laa hasha swala hapa ni mada yenyewe yenye kichwa - Nini chimbuko la vita ya Wahujumu Uchumi!... Na mimi nimeelezea vitu ambavyo vinaonyesha kwamba sisi wananchi na sio viongozi ndio sababu na kulikuwepo na kila haja ya vita vile pamoja na kwamba hatukuweza kufanikiwa hadi mwisho kutokana na Mwinyi kuachana na vita vile..
Sasa tatizo langu kubwa ktk mada hii ni swala la kulaumu na kunyoosha vidole kumsuta mwalimu na Sokoine kuwa ndio sababu na kwamba hapakuwepo na haja ya kufanya hivyo..
It's exactly lawama tunazowashusia wazungu wakoloni ktk kushindwa kwetu kujiendeleza kuwa mkoloni alitufanya hivi ama vile na itasikitisha zaidi ikiwa leo hii tupo huru tunashindwa bado kufanya kitu cha maana tunarudi nyuma kusema sababu ni mkoloni..
Nakumnbukwa mwalimu Nyerere alitumia Mkoloni kama kigezo cha kutuamsha sisi tufanye nini.. Umuhimu wa sisi kujitawala na akaweka mikakati ambayo inapambana na utawala dhalimu wa kikoloni... hivyo hakutumia kabisa mkoloni kuwa sababu ya Tanzania kushindwa kujiendeleza isipokuwa alitumia Mkoloni kuelezea Ugumu wa kasi ya maendeleo yetu..Kwa hiyo mwalimu alioanza kila kitu from the scratch, tuliunda mashirika karibu yote tokea kuweka msingi wake tofauti na nchi nyinginezo kwa sababu mwalimu alizingatia tofauti zilizopo kati yetu na nchi kama Kenya...Mwalimu alitujengea nyumba akaturithisha hata kama kulikuwa hakuna fedha benki lakinii Assets zilikuwepo, miundombinu ilikuwepo ya kulingana na mwanzo wa nchi kujitawala...hiyo pekee ni urithi mkubwa sana..
Yes, Mwalimu alishindwa na sababu inajulikana kwamba hakutaka kupangisha nyumba yetu..Na sote tunafahamu kwamba ni pamoja na Utaifishaji wa mashirika na biashara binafsi zilichangia kushuka kwa uchumi wetu kwa sababu kilichotakiwa tu kuwa mikononi mwa serikali ilikuwa commanding heights which includes all Miundombinu..
He failed economically because of UJAMAA as an economic gateaway! -

Leo hii Tanzania pamoja na maendeleo yote tunayojigamba nayo tumerudi nyuma ktk rank za dunia wakati nchi jirani zetu wote wamepanda.. Tanzania ya Nyerere was ranked nadhani 120 ktk nchi maskini leo hii tunashika mkia sijui wa 147 ikiwa na maana tunazidi kuporomoka wakati wenzetu wanaendelea..Na ajabu ni kwamba tunatumia makuzi ya kimwili kuonyesha maendeleo yetu.. Kila mji duniani una maghorofa siku hizi kila nchi ina vitu toka nje kila nchi ina magari kama yetu lakini hali ya wananchi wake ndio kielelezo safi cha maendeleo..Mtoto aliyezaliwa Tandale uwanja wa fisi mwaka 1961 inawezekana kabisa hakuwahi kuvaa nepi.. akila uji wa ulezi au kande na kadhalika lakini baada ya umri wake kukua iweje tutegemee mtu huyu ataendelea kutembea Uchi.... Kuvaa kwake suruali ya mtumba na T.shirt ya msaada ni moja ya mabadiliko ktk makuzi yake siwezi kuita kuwa ni maendeleo as such..atakula Ugali badala ya Uji na kadhalika ni mabadiliko ya makuzi haya sio maendeleo yake hata kidogo.
Kinachoninda mimi ni pale mnapochukua kuvaa kwa Tanzania suruali ya mtumba mnaita ni maendeleo kwa sababu tu tulipata Uhuru tulikuwa uchi hatukuvaa nguo.. na hakuna mtu kati yenu anayetazama hali ya mtu huyu na mazingira yake kama yamebadilika pia..Kwanza suruali ya mtumba ni Umaskini, T. shirt ya msaada ni Umaskini maisha yake bado ni yale yale ya kuomba msaada...
Binafsi naamini maendeleo ya mtoto huyo Tanzania yatapimwa ktk makuzi yake iwe elimu, afya, malazi yake, Pato (ajira) na ikiwa familia yake imetoka katika umaskini..Mwkaa 1961 mtu akiwa na pato la millioni moja kwa mwaka aliitwa tajiri dunia nzima - as A millionaire..hesabu hizo hazipo tena leo utaonekana mtu wa kawaida tu mwenye fedha ya Usalama..

Wakuu zangu, tutazunguka weee kuzungumzia mifano ya nchi nyinginezo bila hata aibu kwani wao ni watu na Mazingira tofauti..swala kubwa hapa ni Uhujumu Uchumi ambao tulishindwa kuupiga vita hadi mwisho miaka ile.. Leo hii ni tatizo tata na isijekuwa kuna watu hapa wanafikiri hata Kikwete anapoteza Muda kwa sababu wanataka kuona Ubepari at it's best!.


Mkandara:

Wewe unayezunguka bro. Wengi tunakiangalia kile kipindi cha 1979-1984.

Na wengi hapa sio wajamaa au mabepari. Na kama tungeweza kutoka katika matatizo 1979-1984 bila kolombwezo za IMF, WB na masharti ya wahisani, basi Tanzania ingekuwa nchi yenye kujitegemea.
 
Mkandara,Mwanakijiji,Zakumi
Ndugu zangu lazima tukubali makosa yetu ili tuweze kujirekebisha na hilo ndio tatizo letu la kwanza hatukubali responsibility zetu hadi leo hii na waafrika tuna history ya kung'an'ania madaraka na hilo always limekuwa against sisi wenyewe then mawazo yetu always hayalengi future yetu hebu jamani nielekezeni nina serious broblem ya kuelewa misingi tulioachiwa na Mwalimu mbali na Amani,Amani,Amani.We need to think beyond that.serikali zetu honestly hazina dira na hatufiki kwa sababu hatujui tuendako na ni hatari kubwa sana kuparamia gari bila kujua uendako wanajamii we need to think beyond political parties they don't do good to us rather than divide us I guess because of our culture,I will say the same thing to Zanzibaris na what we call muafaka.Why stress ourself let's use just a little bit of common sense.We need kujua tuendako ili tufike hakuna uchawi utakaotufikisha believe me najua ninalozungumza,hakuna uchawi ni uongozi bora wanajamii.Let's think about our children and grands and forget about ourself because kina Mwalimu wametumaliza and we can not afford kusubiri kulaumiwa na wtoto na wajukuu zetu because you know what ? they will be smarter than us and they will never understand us.We have a lot to answer if we don't make the right decision for their future because ours is done.Karne ya ishirini hatuna hata identification card and let's not compare ourself to other african countries guys because they have the same problems,learn from successful people if you wanna be successful.Thanks

Sahiba:

Katika nchi wanayoua albino kupata utajiri, kufanya vitu kwa kubahatisha ni kitu cha kawaida.

Lakini katika vitu ambavyo Mkandara na Mwanakijiji wanaviita complex, nawaambia wasicheze bahati nasibu ni maarifa tu yatakayotukwamua.
 
Kwa maoni yangu kama uzalishaji ulikuwa ni wa kukidhi demand ya Tz peke yake then hapo ndio makosa na tukiangalia kiundani basi ni sera ya ujamaa na kujitegemea ikipingana na ubepari ambao ulikuwa umetapakaa kwa majirani zetu.Ilikuwa ni vigumu sana kwa mwalimu kuweza kujenga jamii aliyokuwa akiiataka.
Mjadala huu umegusia sehemu mbali mbali zenye hoja ya msingi ila ziko scattered..Mkandara,Zakumi,Rev Kishoka wote kwa pamoja maoni yenu yamekidhi mjadala huu kwa kila namna.

Ila swali moja la msingi kabisa hapa ni je ni kwanini viwanda vyetu vilikufa? Najuwa factor ya vita ya Uganda lazima ilikuwa one of the main impacts to the economy....Ila swali kwa ndugu zangu ni hili...Ni kivipi viwanda vilikufa? Sijasikia mtu akitaja umeme,naelewa hoja hapa ni uhujumu uchumi...Lakini kama tunazungumzia bidhaa zinilizozalishwa nchini mwetu,then tukagusia viwanda hence umeme...Tatizo ambalo ni very sugu.

Mkandara umesema bidhaa zilizokuwa zinatakiwa zigawanywe kwa wananchi zilifichwa...Swali ni kuwa zilifichwa kabla ya kuuzwa ama baada ya kuuzwa?

Kama ni baada ya kuuzwa,then wenye shida watakuwa ni wananchi ambao walitakiwa wazipate bidhaa hizo...Kwa mantiki hiyo basi serikali ilishapata chake na sioni ni kivipi ilihujumiwa....Kwasababu nasikia kuna wanaosema kuwa wafanya biashara walinunuwa na kuzificha bidhaa hizo na kuzipeleka nje kwa faida zaidi.Hata hivyo kama zilifichwa na viongozi kwasababu zao binafsi then ni kivipi mwalimu alishindwa kuona hilo?

Ninavyoelewa kwa upande mwingine pia serikali ilikuwa ikihujumiwa kwa mapato ya kodi kwa kutowa bidhaa nje na kuingiza nchini kulikokuwa kukifanywa na walanguzi.
Shida kubwa hapa ni siasa,Tanzania kuingizwa vitani haikuwa bahati mbaya,na hata Kenya walifurahia kiaina.

Kwa ujumla chimbuko la vita hii ya uhujumu uchumi kwa maoni yangu limechangiwa na mgongano wa siasa za ujamaa na kujitegemea vs ubepari...Kiutaratibu tulitakiwa tupanue soko la bidhaa zetu nchi za majirani tulibahatika kuwa na TAZARA,tungekuwa mbali kama serikali ingewasaidia wananchi wake na wafanyabiashara na Tanzania labda ingekuwa mbali...Shida ni kwamba hatuwezi kujuwa...Ndugu zetu wakenya nao kama si ukabila wangekuwa mbali,matabaka ndio mojawapo ya matokeo mabaya ya ubepari sasa kwenye kutafuta balance hapo inahitaji Afrika ije pamoja.
 
Last edited:
Zakumi,
Na wengi hapa sio wajamaa au mabepari. Na kama tungeweza kutoka katika matatizo 1979-1984 bila kolombwezo za IMF, WB na masharti ya wahisani, basi Tanzania ingekuwa nchi yenye kujitegemea
Mkuu isingewezekana kwa sababu UJAMAA ulikuwa unakufa kifo cha HIV.. Utamu wa ngono ktk Ujamaa ilfikia kikomo bob haikuwa kazi ya IMF wala WB kutufuata, tulikwenda wenyewe..
Katika nchi wanayoua albino kupata utajiri, kufanya vitu kwa kubahatisha ni kitu cha kawaida.

Lakini katika vitu ambavyo Mkandara na Mwanakijiji wanaviita complex, nawaambia wasicheze bahati nasibu ni maarifa tu yatakayotukwamua.
Hapana wewe ndiye unajaribu kutumia vitabu ktk swala complex kama la kuua Albino.. unatafuta sijui motive cha chuki labda ubaguzi wa rangi na kadhalika... kjwi kwi kwi! Sisi tunaoishi na Wadanganyika wenzetu tunafahamu kuwa ni swala la imani ya Uchawi.. sasa nenda kwamwambie mchumi habari za Uchawi na Utajiri kisha unaanza ku apply maswla ya demand na supply! damn yaani ngozi za Albino zingeweza kuzalishwa zaidi bila shaka demand pia ingepungua... Mkuu wangu acha kutuweka Uchizi.. hawa watu ni criminals na motive yao kubwa ni fedha - kujenga Utajiri by all means..kama walivyokuwa mafisadi wa kuhujumu Uchumi.. books kwao haziwezi kufanya kazi..
 
Wanajamii suala la viwanda kufa Mwalimu was very smart and that is why I don't understand alot of his decisions and the problem was no one could open his/her mouth and say anything at the time.Wajameni mnamtafuta mchawi wakati mchawi mnamjua guys let's be real and just say it.I think is fare to speak out if you don't do it know then when.Mwalimu alipokwenda kudai uhuru Malkia alimuuliza Julius baada ya kukupa uhuru unataka nikusaidie nini ?na hili ndio jibu la Mwalimu 'nanukuu 'NATAKA WATU WAKO WOTE WAONDOKE'Yes ndivyo alivyojibu matokeo yake tunayaona leo.Professionals wote madoctor,engineers wote wakaondoka wakatuacha matokeo yake wanaomtetea wanasema ati kachukua nchi ikiwa na madokta wazalendo wanne,sasa si umefukuza wote ulitegemea nini waganga wa kienyeji.haya wakati wa ukoloni kulikuwa na vifo vichache na madokta wanne na sasa tuna madokta bwerere na vifo mahospitalini kila dakika hadi pamba ya kidonda uwende nayo hospitali,rushwa kibao huna mshiko utakufia reception na madokta wengine vihiyo mgonjwa wa mguu anapasuliwa kichwa wakuu hii ndiyo misingi yetu.
 
Sahiba,
Haya maneno unayazungumza kwa kunukuu maneno ya watu au unazungumza tu kufurahisha baraza..
Je, unajua ni muda gani transition ya Uhuru wetu ilichukua?.. unajua hata jeshi letu liliendelea kuwa chini na Malkia hadi kina sarakikya walipoanza kugoma na kum force mwalimu kuanzisha JWTZ..Nambie sehemu ambayo wazungu waliondoka mara tu baada ya Uhuru kwa sababu ya majibu ya mwalimu..
Mkuu ni hadi Azimio la Arusha ndipo mabadiliko mengi yalifanyika meaning up to 1967 wazungu walikuwepo nchini..
Kisha hizi Imani za wazungu. mbona ni akili za kushikiwa. hao wazungu walipoondoka sijui madoctor ulisikia tatizo la vifo au tumeshindwa kuendesha kitu...zaidi ya hapo unaweza kunambia huyo Malkia alijenga kitu gani kwetu..hao ma engineer walikuwa wakiendesha kitu gani..
Mwalimu alijenga almost everything from the ground.. kitu poekee ni reli ya Mjarumani na shirika la meli la huyo malkia na Nyerere alipoingia tuliweza kuongeza meli mara tatu ya zile alizoacha Muingereza..nambie shirika hata moja la Muingereza ambalo tulishindwa kuliendeleza toka Mkoloni alipoondoka..
Yes, tunakubali yalifanyika makosa ya kutaifisha kila kitu hata biashara binafsi ambazo hazikuwa commanding Heights, na biashara hizi hazikuwa na Muingereza ila wazungu wa kila Kabila zipo za Wataliani, Wajarumani, waarabu, wahindi na hata waafrika wenyewe.. Haya ni makosa ya siasa za Ujamaa ambazo leo unakuja jutia..lakini above all hazikutuacha vilema isipokuwa zilivunja mifupa ya uchumi wetu na tukaanza kutembelea magongo..
Toka wakati ule hatujafanya tiba yoyote kiuchumi kufikiria kuondokana na magongo...Tunachofanya leo hii ni ku hire msaidizi wa kutuburuza ktk viti vya vilema wakati mifupa imeisha unga na tunaweza kufanya therapy ya kiuchumi kutuwezesha kutembea tena bila magongo..
 
Kwa maoni yangu kama uzalishaji ulikuwa ni wa kukidhi demand ya Tz peke yake then hapo ndio makosa na tukiangalia kiundani basi ni sera ya ujamaa na kujitegemea ikipingana na ubepari ambao ulikuwa umetapakaa kwa majirani zetu.Ilikuwa ni vigumu sana kwa mwalimu kuweza kujenga jamii aliyokuwa akiiataka.
Mjadala huu umegusia sehemu mbali mbali zenye hoja ya msingi ila ziko scattered..Mkandara,Zakumi,Rev Kishoka wote kwa pamoja maoni yenu yamekidhi mjadala huu kwa kila namna.

Ila swali moja la msingi kabisa hapa ni je ni kwanini viwanda vyetu vilikufa? Najuwa factor ya vita ya Uganda lazima ilikuwa one of the main impacts to the economy....Ila swali kwa ndugu zangu ni hili...Ni kivipi viwanda vilikufa? Sijasikia mtu akitaja umeme,naelewa hoja hapa ni uhujumu uchumi...Lakini kama tunazungumzia bidhaa zinilizozalishwa nchini mwetu,then tukagusia viwanda hence umeme...Tatizo ambalo ni very sugu.

Mkandara umesema bidhaa zilizokuwa zinatakiwa zigawanywe kwa wananchi zilifichwa...Swali ni kuwa zilifichwa kabla ya kuuzwa ama baada ya kuuzwa?

Kama ni baada ya kuuzwa,then wenye shida watakuwa ni wananchi ambao walitakiwa wazipate bidhaa hizo...Kwa mantiki hiyo basi serikali ilishapata chake na sioni ni kivipi ilihujumiwa....Kwasababu nasikia kuna wanaosema kuwa wafanya biashara walinunuwa na kuzificha bidhaa hizo na kuzipeleka nje kwa faida zaidi.Hata hivyo kama zilifichwa na viongozi kwasababu zao binafsi then ni kivipi mwalimu alishindwa kuona hilo?

Ninavyoelewa kwa upande mwingine pia serikali ilikuwa ikihujumiwa kwa mapato ya kodi kwa kutowa bidhaa nje na kuingiza nchini kulikokuwa kukifanywa na walanguzi.
Shida kubwa hapa ni siasa,Tanzania kuingizwa vitani haikuwa bahati mbaya,na hata Kenya walifurahia kiaina.

Kwa ujumla chimbuko la vita hii ya uhujumu uchumi kwa maoni yangu limechangiwa na mgongano wa siasa za ujamaa na kujitegemea vs ubepari...Kiutaratibu tulitakiwa tupanue soko la bidhaa zetu nchi za majirani tulibahatika kuwa na TAZARA,tungekuwa mbali kama serikali ingewasaidia wananchi wake na wafanyabiashara na Tanzania labda ingekuwa mbali...Shida ni kwamba hatuwezi kujuwa...Ndugu zetu wakenya nao kama si ukabila wangekuwa mbali,matabaka ndio mojawapo ya matokeo mabaya ya ubepari sasa kwenye kutafuta balance hapo inahitaji Afrika ije pamoja.


Jmushi:

Suala la umeme tumeligusa sana humu ndani. Lakini focus ilikuwa 1979-1984.

Katika kipindi hiki umeme ulikuwa sio tatizo kubwa sana. Tatizo kubwa lilikuwa ni viwanda kujengwa katika sehemu zisizo za umeme. Mfano ulikuwa nikiwanda cha nguo Musoma. Umeme wa kuzalishwa na maji ulifika Mwanza na Musoma miaka ya 90. Lakini tayari sehemu hizo zilichakuwa na viwanda vya nguo vyenye kutumia umeme mkubwa katika miaka ya 70 na 80. (najua hapa watakuja wakina Mkandara kubisha). Hivyo maamuzi ya kisiasa ya kujenga viwanda yalitawala mikakati ya kiuchumi.

Kuhusu matumizi ya reli ya TAZARA, nadhani hapo watanzania ni uzembe wetu mkubwa unaouonyesha.

China ilikuwa ndio inaanza kujitangaza duniani kuwa inaweza kufanya vitu lakini kwa sababu ya dominance ya nchi za magharibi katika masoko ya dunia ya tatu, China ilipata kazi kujitangaza. Hivyo TAZARA ni mradi wa kwanza mkubwa uliochuliwa na China ili kujitangaza nje kuwa inaweza kufanya kazi. Lakini kama kawaida yetu, tukaona kuwa KAKA zetu wajamaa wametusaidia, hivyo tukabweteka. Baada ya TAZARA, China ilianza kupata tenda kutoka katika nchi zingine za dunia ya tatu kujenga miradi mingi.

Kwa sisi tuliuchulia kama mradi wa kisiasa hili Zambia isitegemee sana South Africa. Na hatujafanya juhudi zozote zile za kufanya TAZARA itumike katika mazingira ya sasa ya kisiasa. Na vilevile reli hiyo inaathirika sana na ukiritimba wa Bandari ya DSM.

Hivyo tunaweza kujibu maswali mengi lakini tunaweza kutoka nje ya mada.
 
Wanajamii suala la viwanda kufa Mwalimu was very smart and that is why I don't understand alot of his decisions and the problem was no one could open his/her mouth and say anything at the time.Wajameni mnamtafuta mchawi wakati mchawi mnamjua guys let's be real and just say it.I think is fare to speak out if you don't do it know then when.Mwalimu alipokwenda kudai uhuru Malkia alimuuliza Julius baada ya kukupa uhuru unataka nikusaidie nini ?na hili ndio jibu la Mwalimu 'nanukuu 'NATAKA WATU WAKO WOTE WAONDOKE'Yes ndivyo alivyojibu matokeo yake tunayaona leo.Professionals wote madoctor,engineers wote wakaondoka wakatuacha matokeo yake wanaomtetea wanasema ati kachukua nchi ikiwa na madokta wazalendo wanne,sasa si umefukuza wote ulitegemea nini waganga wa kienyeji.haya wakati wa ukoloni kulikuwa na vifo vichache na madokta wanne na sasa tuna madokta bwerere na vifo mahospitalini kila dakika hadi pamba ya kidonda uwende nayo hospitali,rushwa kibao huna mshiko utakufia reception na madokta wengine vihiyo mgonjwa wa mguu anapasuliwa kichwa wakuu hii ndiyo misingi yetu.

Sahiba:

Chunga sana unapomtaja Mwalimu. Kuna walinzi wa historia hapa.
icon10.gif
 
Mtu anaweza kusema uongo kwa muda mrefu, akawa wa kwanza kuaamini, mwisho anauita historia!
 
Kishoka:

Anzisha topiki nyingine kama vile kuchambua paper ya Prof. Wangwe.
 
Sahiba:

Chunga sana unapomtaja Mwalimu. Kuna walinzi wa historia hapa.
icon10.gif

Ni lazima wawepo ili kuweka historia sawa sawa.

Mkandara sina jinsi ya kukupongeza lakini wewe ni moja kati ya vichwa vinavyojua kuchambua mada na kutoa mifano barabara. Nyerere hakuwa malaika lakini alifanya mengi makubwa katika mazingira magumu ambapo hakuna raiswa tanzania tunayeweza kumlinganisha naye kwa sasa.
 
Sahiba,
Haya maneno unayazungumza kwa kunukuu maneno ya watu au unazungumza tu kufurahisha baraza..
Je, unajua ni muda gani transition ya Uhuru wetu ilichukua?.. unajua hata jeshi letu liliendelea kuwa chini na Malkia hadi kina sarakikya walipoanza kugoma na kum force mwalimu kuanzisha JWTZ..Nambie sehemu ambayo wazungu waliondoka mara tu baada ya Uhuru kwa sababu ya majibu ya mwalimu..
Mkuu ni hadi Azimio la Arusha ndipo mabadiliko mengi yalifanyika meaning up to 1967 wazungu walikuwepo nchini..
Kisha hizi Imani za wazungu. mbona ni akili za kushikiwa. hao wazungu walipoondoka sijui madoctor ulisikia tatizo la vifo au tumeshindwa kuendesha kitu...zaidi ya hapo unaweza kunambia huyo Malkia alijenga kitu gani kwetu..hao ma engineer walikuwa wakiendesha kitu gani..
Mwalimu alijenga almost everything from the ground.. kitu poekee ni reli ya Mjarumani na shirika la meli la huyo malkia na Nyerere alipoingia tuliweza kuongeza meli mara tatu ya zile alizoacha Muingereza..nambie shirika hata moja la Muingereza ambalo tulishindwa kuliendeleza toka Mkoloni alipoondoka..
Yes, tunakubali yalifanyika makosa ya kutaifisha kila kitu hata biashara binafsi ambazo hazikuwa commanding Heights, na biashara hizi hazikuwa na Muingereza ila wazungu wa kila Kabila zipo za Wataliani, Wajarumani, waarabu, wahindi na hata waafrika wenyewe.. Haya ni makosa ya siasa za Ujamaa ambazo leo unakuja jutia..lakini above all hazikutuacha vilema isipokuwa zilivunja mifupa ya uchumi wetu na tukaanza kutembelea magongo..
Toka wakati ule hatujafanya tiba yoyote kiuchumi kufikiria kuondokana na magongo...Tunachofanya leo hii ni ku hire msaidizi wa kutuburuza ktk viti vya vilema wakati mifupa imeisha unga na tunaweza kufanya therapy ya kiuchumi kutuwezesha kutembea tena bila magongo..

Mkandara,
Mzee naona majibu yana jazba kumbe Azimio la Arusha lilikuwa ni la kuwafukuza wazungu hilo mimi sina uhakika nalo maana asilimia kubwa sana ya mali zilizotaifishwazilimilikiwa na wahindi,waarabu na wazalendo sasa hili la wazungu vipi hapa wakubwa.Na ikiwa unasema hakuna viwanda vilivyotushinda kuviendeleza na tukaviua inabidi mjadala tuufunge maana naona Bwana mkandara mapenzi yamezidi na mwisho kama huoni walivyojenga wazungu mimi nakumbuka maana hata zile parking meter tu tulizivunja mzungu alipoondoka tu hatukujua manufaa yake na loe tunafunga magari yetu kwa machuma haya nipe logic bwana mkubwa.
 
Sahiba, mkuu sizungumzi kwa jazba hata kidogo, ndio lugha yangu na wengi hapa JF wanafahamu kuwa mimi huandika kwa msisitizo tu zaidi ya jazba kiasi kwamba ukisoma juu ya gamba unaweza fikiria ni jazba au nachoandika hakina makosa..
Huu ni mjadala ambao kila mmoja wetu huweka hoja zake pinzani au zinazokubaliana kutokana na Ufahamu wetu iwe kwa elimu au Experience...

Mimi nimejibu tu hoja yako kulingana na usemi wako kuwa mwalimu aliulizwa na Malikia asaidiwe nini akakataa, hivyo wazungu wakaondoka.. hao wazungu madaktari na wengine umewasema wewe sikuandika mimi.. Na jibu langu limekuonyesha wazungu hawakuondoka kama madai yako na mimi ndiye niliyeongeza raia wengine wa nje zaidi ya Muingereza ambao waliathirika na Azimio la Arusha..
sasa unapokuja na madai ambayo yanapindisha ukweli sijui unachojaribu kusema hapa.. Bila shaka Azimio la Arusha liliathiri watu wengi ikiwa ni pamoja na wazalendo wananchi weusi wenye mali zao.
Uendeshaji wa viwanda sio swala kabisa kwa sababu Muingereza hajkujenga kiwanda hata kimoja isipokuwa ni wafanya biashara wa mataifa tofauti.. Muingereza alikuwa akichuma kodi tu kuuza mali zetu nje.. tena basi infrustructure yote alijenga Mjarumani, hivyo kutawaliwa na Muingereza hakukuleta mafanikio yoyote ambayo leo hii tunaweza kusimama na kusema Unaona muundombinu uleee... umejengwa na Muingereza!..
Kwa hiyo mwalimu alijenga karibu kila kitu from scratch tofauti na nchi kama Kenya..inasikitisha tu Watanzania tunaposhindwa ku recognize that!...
Na uchovu kama huu ndio maana watu kama Lowassa, Chenge na Mramba wanatunukiwa na kuitwa mashujaa kwa sababu ni mila yetu kumsifia mwizi, jambazi maadam analisha familia yake kwa Ujambazi.
 
Sahiba, mkuu sizungumzi kwa jazba hata kidogo, ndio lugha yangu na wengi hapa JF wanafahamu kuwa mimi huandika kwa msisitizo tu zaidi ya jazba kiasi kwamba ukisoma juu ya gamba unaweza fikiria ni jazba au nachoandika hakina makosa..
Huu ni mjadala ambao kila mmoja wetu huweka hoja zake pinzani au zinazokubaliana kutokana na Ufahamu wetu iwe kwa elimu au Experience...

Mimi nimejibu tu hoja yako kulingana na usemi wako kuwa mwalimu aliulizwa na Malikia asaidiwe nini akakataa, hivyo wazungu wakaondoka.. hao wazungu madaktari na wengine umewasema wewe sikuandika mimi.. Na jibu langu limekuonyesha wazungu hawakuondoka kama madai yako na mimi ndiye niliyeongeza raia wengine wa nje zaidi ya Muingereza ambao waliathirika na Azimio la Arusha..
sasa unapokuja na madai ambayo yanapindisha ukweli sijui unachojaribu kusema hapa.. Bila shaka Azimio la Arusha liliathiri watu wengi ikiwa ni pamoja na wazalendo wananchi weusi wenye mali zao.
Uendeshaji wa viwanda sio swala kabisa kwa sababu Muingereza hajkujenga kiwanda hata kimoja isipokuwa ni wafanya biashara wa mataifa tofauti.. Muingereza alikuwa akichuma kodi tu kuuza mali zetu nje.. tena basi infrustructure yote alijenga Mjarumani, hivyo kutawaliwa na Muingereza hakukuleta mafanikio yoyote ambayo leo hii tunaweza kusimama na kusema Unaona muundombinu uleee... umejengwa na Muingereza!..
Kwa hiyo mwalimu alijenga karibu kila kitu from scratch tofauti na nchi kama Kenya..inasikitisha tu Watanzania tunaposhindwa ku recognize that!...
Na uchovu kama huu ndio maana watu kama Lowassa, Chenge na Mramba wanatunukiwa na kuitwa mashujaa kwa sababu ni mila yetu kumsifia mwizi, jambazi maadam analisha familia yake kwa Ujambazi.


Mkandara:

Basi acha basi kuwa spin-doctor kwa muda fulani. Waingereza nao waliacha vitu tena muhimu tu. Matatizo yako unaangalia viwanda tu.

Waingereza waliongoza mfumo wa utawala unaotumika mpaka sasa. Waliacha bunge. Sheria za nchi. Serikali za mitaa zilizokuwa zinaendeshwa na wananchi wenyewe.

Hata miundo mbinu aliyoacha mjerumani, mwingereza aliisimamia vizuri tu.

Mambo yote aliyofanya Nyerere yalitegemea miundombinu aliyoacha mwingereza.
 
Zakumi,
Mkuu umesema niache kuwa spin doctor sawa!.. Na wewe umefanya nini yaani hizo sheria za nchi na sheria za mitaa ndio urithi unaweza kuuweka hapa mkuu wangu!..
Kibaya zaidi umefikia kusema Miundombinu aloacha Mjarumani ati Muingereza aliisimamia vizuri bila hata aibu mkuu wangu, Hapa unatazama kusimamia mradi au unatazama mjenzi nani..
Hivi ndivyo visingizio vya kuspin..read my lips..nimesema Muingereza hakutupa wala kutuachia kitu ambacho leo hii sisi wananchi tungeweza kujivunia hata kama tusingekuwa na Azimio la Arusha, Muingereza bila kufukuzwa, aliondoka kwa sababu muda wa Protectorate kufikia mwisho wake..hawakwa na kitu nchini zaidi ya bendera zao na kukusanya kodi za kichwa kwa Malkia..Kutawala tu kama Warumi walivyomwejka Herod kule Israel na middle east.
Sheria kitu gani cha kujivunia wakati tulijenga constitution yetu wenyewe.. Kufanana sio hoja kwani hata yeye aliiga mengi toka kwa Mfaransa! labda useme sisi Ndivyo Tulivyo mahakimu wetu waliiga hata kuvaa majoho na nywele za bandia blonde ili sijui tufanane na Wazungu...
 
Zakumi,
Mkuu umesema niache kuwa spin doctor sawa!.. Na wewe umefanya nini yaani hizo sheria za nchi na sheria za mitaa ndio urithi unaweza kuuweka hapa mkuu wangu!..
Kibaya zaidi umefikia kusema Miundombinu aloacha Mjarumani ati Muingereza aliisimamia vizuri bila hata aibu mkuu wangu, Hapa unatazama kusimamia mradi au unatazama mjenzi nani..
Hivi ndivyo visingizio vya kuspin..read my lips..nimesema Muingereza hakutupa wala kutuachia kitu ambacho leo hii sisi wananchi tungeweza kujivunia hata kama tusingekuwa na Azimio la Arusha, Muingereza bila kufukuzwa, aliondoka kwa sababu muda wa Protectorate kufikia mwisho wake..hawakwa na kitu nchini zaidi ya bendera zao na kukusanya kodi za kichwa kwa Malkia..Kutawala tu kama Warumi walivyomwejka Herod kule Israel na middle east.
Sheria kitu gani cha kujivunia wakati tulijenga constitution yetu wenyewe.. Kufanana sio hoja kwani hata yeye aliiga mengi toka kwa Mfaransa! labda useme sisi Ndivyo Tulivyo mahakimu wetu waliiga hata kuvaa majoho na nywele za bandia blonde ili sijui tufanane na Wazungu...

Bro:

Ukishindwa lazima utafute mbaya wako na visingizio. Hizo nchi zilizoachwa pazuri ziko wapi?

Na hata kama angetuachia vitu unavyotaka wewe, unafikiri tungekuwa mbele?

Niambie kitu gani ungeachiwa ungekuwa mbali?
 
Ni lazima wawepo ili kuweka historia sawa sawa.

Mkandara sina jinsi ya kukupongeza lakini wewe ni moja kati ya vichwa vinavyojua kuchambua mada na kutoa mifano barabara. Nyerere hakuwa malaika lakini alifanya mengi makubwa katika mazingira magumu ambapo hakuna raiswa tanzania tunayeweza kumlinganisha naye kwa sasa.


Watu tunataka good time. Hayo mambo ya rais kufanya mambo kibao na kukuacha na msuli kama mgogo, hayana mpango.
 
Zakumi,
No bob, mpango wa Ushanga theory hata haupandi! - kwi! kwi! kwi!
 
Back
Top Bottom