Nini hasa kinafanya gharama za kuchimba kisima kuwa mil 8, 10, 12? What is so special?

Nini hasa kinafanya gharama za kuchimba kisima kuwa mil 8, 10, 12? What is so special?

Kuna bei za vitu vya ajabu ajabu sana bongo,

Kuna huu urembo wa Tv shiw case kwa kutumia panel kuna mdau pale sinza alisema kazi yote ni 6m

Nikaingia mtaani nikanumua material na fundi iligota laki 8.

Chamber zisizo jaa kuna fundi famous mtandaoni akasema 4m, nikasaka fundi wengine wakafanya 1m

Kisima niliambuwa futi 12 milion 9,

Kuna fundi wengine wakaja na kimtambo chao wanazunguka nacho kinachimba, nikapata maji ya kutosha hayasumbui niliwapa laki 6
Msaada mkuu wa contact huku tuna shida ya maji zaidi ya jangwani mkuu
 
Kazi ya uchimbaji visima imejaa udalali mkubwa wa kupindukia, ukitaka kuchimbiwa kisima kwa bei ambayo ni rahisi na halali bila ya kuwepo mtu wa katikati hakikisha unachimbiwa na kampuni ya mwenye mashine au unafanya biashara noja kwa moja na mmiliki wa mashine ya uchimbaji.
Hao Nao wamekua kama wenye nyumba za kupangisha hawafanyi.kazi Bila Dalali inchi hii wananchi wanapigwa sana
 
Na
Bei za wapi izo njoo Tabata kuna kampuni ya kichina million 4 tu unachimbiwa mpaka mita 60..wanakuja na wataalamu wao wanapima kabisa..usifanye mchezo na wachina..wanachimba mpaka kwa mkopo unatoa 2million inayobaki mnaandikishinana unaimalizia lini..Watu mambo ya dawasco tulishayasahau.
Omba namba zao boss
 
Mzee sinutoe
Filter wapi wachina wanadawa zao wanamwagia kwenye kisima sema inatakiwa wiki 1 kisima kisitumike toka muda walipoweka dawa..baada ya apo ukikutana na chumvi sijui magadi niite mbwa..mimi nilishawai kumchukua senior graduated kutoka chuo cha maji aje anipigie survey kabla ya kuchimba akasema apa maji yapo kuanzia mita 100 na kuendelea..kuna jamaa yangu akaniletea survey wa iyo kampuni ya kichina MR LIU akasema apa tunachimba mita30 tu maji yapo ya kumwaga..
Mzee Si utoke Namba uwasaidie wadau
Filter wapi wachina wanadawa zao wanamwagia kwenye kisima sema inatakiwa wiki 1 kisima kisitumike toka muda walipoweka dawa..baada ya apo ukikutana na chumvi sijui magadi niite mbwa..mimi nilishawai kumchukua senior graduated kutoka chuo cha maji aje anipigie survey kabla ya kuchimba akasema apa maji yapo kuanzia mita 100 na kuendelea..kuna jamaa yangu akaniletea survey wa iyo kampuni ya kichina MR LIU akasema apa tunachimba mita30 tu maji yapo ya kumwaga..
 
Gharama ya kuchimba kisima inategemea aina ya kisima, kina (urefu kwenda chini), aina ya mwamba eneo la kisima (geology), aina ya mashine itakayochimba na mabomba yatakayotumika.

VISIMA VIFUPI
Visima hivi huchimbwa kwenye michanga/udongo

1. Kisima kifupi aina ya ring well ndiyo bei rahisi kuliko vyote kwani uchimbaji wake ni wa mikono. Bei ni kama laki tano na kushuka chini.

2. Kisima kifupi aina ya tube well inaweza kuchimbwa kwa mashine ya mkono au ya mafuta (diesel/petroli). Kina cha kisima ni chini ya mita 20. Bei ni kama 2 milioni inategemea kina na mabomba yatakayotumika.

VISIMA VYA KATI
Visima hivi huchimbwa kwa mashine (rig) kwenye mchanga (Maeneo ya pwani na mabonde/mbuga na miamba laini)
Visima vya aina hii hufikia kina cha mita 50. Bei yake hufikia milioni 5.

VISIMA VIREFU

Visima hivi huchimbwa kwa mashine kubwa (rig) kwenye michanga, miamba laini na miamba migumu. Kwa Tanzania visima hivi hufikia kina cha mita mpaka 300. Bei ya kuchimba kisima hufikia hadi zaidi ya milioni 20.

Sababu kubwa ya bei ya visima kuwa ghali ni kwa kuwa vifaa vya kuchimbia ni kubwa. Vifaa hivyo ni Rig, mabomba ya chuma, mabomba ya kuweka ndani ya kisima, bits za kuchimbia, hammer, bentonite (matope ya kuchimbia), diesel na mafuta mengine kama hydraulic oil nk.
Matope ya kuchimbia? Mzee hii ndio kitu gani pamoja na yote uliposema still gharama za kuchimba ziko juu sana
 
Matope ya kuchimbia? Mzee hii ndio kitu gani pamoja na yote uliposema still gharama za kuchimba ziko juu sana
Unapochimba sehemu yenye mchanga wenye maji ni dhahiri kuwa mchanga utakuwa unabomokea ndani ya kisima. Ili kuzuia mchanga usibomokee ndani ya shimo la kisima, matope (drilling mud inayotengenezwa kwa mchanganyiko wa maji na bentonite) hutumika kusiliba kingo za shimo la kisima. Baada ya kukamilika uchimbaji na maeneo yenye maji kuainishwa mabomba (casings na screens) huwekwa na kazi ya kusafisha tope lililosiliba kingo za kisima huanza. Tope likiisha na maji kuwa masafi na upimaji wa wingi wa maji (pumping test) kufanyika ndipo tunasema kisima kimekamilika na miundombinu ya ku-pump maji inaweza kujengwa.

Hivyo gharama hutokana na uchimbaji, tope la kuchimbia, mabomba (casings na screens), usilibaji na usafishaji wa tope na upimaji wa wingi wa maji (pumping test).
 
Halafu wakikutana na mwamba wanasepa wanakuachia shimo!
Wanatoboa mwamba.
Mwaka huu wametuchimbia home wakafika kwenye mwamba kukawa na moshi unafuka (mvuke mwingi kama moshi) wakaomba tuwatafutie mashine ya kupumulia,wakaunganisha na umeme wakashuka nayo mpaka chini wakamalizia kutoboa mwamba. Maji yakapatikana kwa wingi sana.
Gharama zao ndogo mno!!!

Sent from my SM-G970U using JamiiForums mobile app
 
Kuna baadhi ya maeneo hapa Dar kama ukanda wa Kimara, Mbezi, Kibamba, Ubungo usipoteze hela yako kuchimba kisima

Water table ya hayo maeneo maji yake yana magadi maana ile sio chumvi imagine hata wanyama wanayasusa

Natamani hii comment ungeandika 2014.

Maana mwaka 2015 nilichimba kisima ubungo. Nilipata maji yana magadi balaa
 
Kwa wakazi wa Bagamoyo na maeneo jirani tupeni uzoefu wa kuchimba visima maeneo hayo..
 
Tatizo udalali. Zamani 14+year nilichimba 3m mita 80 kila kitu kwao, mpka Leo pump inapiga kazi. Strange zamani annual service ilikuwa 200,000, latest 150,000 tu. Lakini najua bado kuna udalali tu.
 
Wanatoboa mwamba.
Mwaka huu wametuchimbia home wakafika kwenye mwamba kukawa na moshi unafuka (mvuke mwingi kama moshi) wakaomba tuwatafutie mashine ya kupumulia,wakaunganisha na umeme wakashuka nayo mpaka chini wakamalizia kutoboa mwamba. Maji yakapatikana kwa wingi sana.
Gharama zao ndogo mno!!!

Sent from my SM-G970U using JamiiForums mobile app
Fanya Mpango nipate mawasiliano Yao boss
 
Kwangu mimi udalali ndio umeharibu Kwa asilimia kubwa bei za vitu na huduma,middle man ni wengi sana na hawa ndio kichefuchefu cha bei.Hata hivyo visima wamesababisha wao kupandisha bei,na Si vifaa
 
Katika vitu ambavyo Kila nikifikiria nakosa majibu ni gharama ya kuchimba kisima na Ile mitambo yao kiujumla, Sote tunajua kuwa katika mitambo inayouzwa bei ghali ni mitambo ya kutengeneza Barabara na ya migodini, ikiwemo Wheel loader, Excavator, Bull dozer (mashine ya kipekee ambayo ukiwa Dar unaweza kuiwasha kuweka mafuta na kuweka gia na kuielekezea Mwanza Kisha ukapanda ndege na baada ya muda litafika tu Mwanza lenyewe maana Kila mahali linapita). Sasa hii mitambo gharama ya kukodisha Kwa siku ni kati ya laki 8 Hadi milioni.

Sasa twende huku kwenye visima vya maji, wao wanakuambia Kwa MITA 50,000 Hadi 85,000 hivyo mpaka kisima unamaliza ni milioni 10+.

Sasa je ni Nini hasa kinachokuwa gharama kwao mpaka kupelekea gharama ishoot milioni 10 Kwa kisima, maana haiingii akilini, Nilielewa hii nitakaa kimya.
Kumbe mwalimu wangu alikuwa boya, alinifundisha eti mita 1,000 sawa na kilomita moja! Huku nakuta watu wanachimba kisima mita 50,000! Yaani kilomita 5 kwenda chini ya ardhi! JF imenifumbua macho na masikio.
 
Back
Top Bottom