Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?
Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?
Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?
Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.
Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.
Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.
Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.
Maasalam.
Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?
Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?
Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.
Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.
Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.
Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.
Maasalam.