Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani?

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.
Nilipoona ID yako nikafurahi kwa kujua uwezo wako wa kuchambua hoja tangu enzi zile za 'nondo za moto'....kumbe hola!!

Hili hitimisho limeweka dhahiri wewe ni ccm unayetaka FAM abaki uongozini kwa maslahi yenu mnayoyajua wenyewe.⁹
 
lengo kuu ni ili wapate mtu ambaye hatakuwa analamba asali. uwepo upinzani halisi utakaoiwajibisha serikali inayouza nchi kwa mwarabu.
1. Una hakika Lissu haonji Asali? Kama Lissu hana Biashara, hana Ubunge, hana hata Usafiri wake anaishije mjini? Naomba nambie source ya Imcome ya Tundu Lissu happ mjini.
2. Ya Abdul ukisikiliza kwa makini utetezi wa Lissu unajua wazo alikuwa anamjua ana amekuja nyumbani kwake kufanya nini!
3. Kisha sio Lissu alokutana na Mama Samia Ubelgiji? Waliongea nini hadi karudi Tz, TISS wasimguse maana alisema Usalama wa Taifa walitaka kumuua.
4. Usalama wa Taifa wanaweza kweli futa kesi zao ikiwa kuna hatari ya Usalama wa nchi? Ghafla tunaona Lissu analiamsha ndani ya Chadema muda huu ambao Chadema wanajipanga kuikabiri CCM.
5. Ebu wewe nipe time line yaani pale ashinde au ashindwe Lissu Uenyekiti kutakalika?
 
1. Una hakika Lissu haonji Asali? Kama Lissu hana Biashara, hana Ubunge, hana hata Usafiri wake anaishije mjini? Naomba nambie source ya Imcome ya Tundu Lissu happ mjini.
2. Ya Abdul ukisikiliza kwa makini utetezi wa Lissu unajua wazo alikuwa anamjua ana amekuja nyumbani kwake kufanya nini!
3. Kisha sio Lissu alokutana na Mama Samia Ubelgiji? Waliongea nini hadi karudi Tz, TISS wasimguse maana alisema Usalama wa Taifa walitaka kumuua.
4. Usalama wa Taifa wanaweza kweli futa kesi zao ikiwa kuna hatari ya Usalama wa nchi? Ghafla tunaona Lissu analiamsha ndani ya Chadema muda huu ambao Chadema wanajipanga kuikabiri CCM.
5. Ebu wewe nipe time line yaani pale ashinde au ashindwe Lissu Uenyekiti kutakalika?
unauliza swali hilo kwa mtu aliyekuwa mbunge miaka mingi sana, na hela za ubunge alizokuwa amezuia ndugai alilipwa zote, unafikiri aatalala njaa? au unataka tusemeje?
 
Nilipoona ID yako nikafurahi kwa kujua uwezo wako wa kuchambua hoja tangu enzi zile za 'nondo za moto'....kumbe hola!!

Hili hitimisho limeweka dhahiri wewe ni ccm unayetaka FAM abaki uongozini kwa maslahi yenu mnayoyajua wenyewe.⁹
U CCM wala Uchadema niliisha acha siasa siku nyingi maana niliona Siasa za Bongo ni sawa na debe linalovuja. Watu wakipenda hawaoni chongo
 
unauliza swali hilo kwa mtu aliyekuwa mbunge miaka mingi sana, na hela za ubunge alizokuwa amezuia ndugai alilipwa zote, unafikiri aatalala njaa? au unataka tusemeje?
Alaaa alipewa na nani?
 
Wale Team Lisu wanajiona wana uwezo mkubwa sana kifikra kumbe ni kakikundi kadogo kaliko jawa na wivu, na uchu wa madaraka wanayohisi watayapata kupitia Lisu, waliyakosa kuputia Mbowe.

Nashauri kamati kuu ikimjadili Lisu na wapiga kelele wenzake wamfukuze kutoka chamani, ilu wapate fursa kuanzisha na kusajiri chama chao cha harakati.

Wanajivunia chadema kwasababu ya uongozi mahili wa FAM, Wakichukua chama kina kufa, na ndiyo nia yao hawa mahodari wa kuongea bila mipaka.
 
Mtoa hoja ama ni mnafiki, au ana uelewa mdogo.

Labda kwakumpa faida, tuamini kuwa ana uelewa mdogo, na hivyo tumpe shule kidogo ili aanze kuuendea weledi taratibu.

1) Baada yaminong'ono mingi kuwa Mbowe ameikalia hiyo nafasi kwa muda mrefu sana, na kuifanya CHADEMA kusemwa vibaya na wapinzani wake, Mbowe mwenyewe kwa kinywa chake, alitamka kuwa kipindi chake cha uongozi kikiisha, hatagombea tena. Uamuzi wake wa kugomvea tena, huku tayari ameishikilia nafasi hiyo kwa miaka 21, ni jambo linalomshamgaza kila mwenye akili. Maana anatengeneza mazingira ya CHADEMA kusemwa kwa ubaya na washindani wake.

2) Mwakajana ulikuwa ni mwaka wa uchaguzi wa ndani ya chama, kikatiba, lakini haukumalizika, na hivyo kusogezwa mbele kidogo. Kama akili inacheza kidogo, utakuwa umepata jibu la swali lako kwa nini siyo juzi au jana. Haya siyo mapinduzi bali uchaguzi. Hivyo kudai kuwa kuna watu wanataka kumwondoa Mbowe kwenye nafasi ya umwenyekiti, ni uwongo mkubwa, na inadhihirisha kuwa wewe kwenye haya mambo ni mtupu kabisa. Mbowe anamaliza kipindi chake cha uongozi, na kisha atakabidhi kwa atakayekuwa amechaguliwa, kumpokea.
Member since 2006 hajui kwa nini mwaka juzi na mwaka jana hakukua na kumuondoa mbowe kwenye uenyekiti. Sijui wangemuondoa vipi bila uchaguzi

Hata hivyo mbowe mwaka 2021 alisema hatagombea tena uenyekiti
 
Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?

Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.

Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.

Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.

Maasalam.
Lengo chama kirudi katika mstari wake kupitia mawazo mapya , wala sio kwamba mbowe hajafanya makubwa
 
Mzee mkandara umeamua kuja kupima upepeo Kama Mbowe bado anafaa .

Huyo mtu wenu hana nafasi tena
 
hata kama alipewa na samia, si ilikuwa halali yake? unataka afumbe mdomo kwa sababu alipewa haki yake na samia? au
Sheria ya Bunge inasemaje ikiwa mbunge akifutwa Ubunge?
Kabla sijakujibu....nini lilikua lengo la FAM kuhakikisha LISSU anakoswa Umakamu??.
Hayo ni madai ya Lissu anatapatapa tu. isikilize vizuri hotuba yake kisha jiulize what if ni Wenje aloomba ushauri kugombea, ulitaka Mbowe aseme usigombee? Kwani nafasi hiyo imezuiwa kugombewa isipokuwa Lissu peke yake?
Na kwa nini Lissu aseme Mbowe alimtuma agombee nafasi yangu basi na mimi nagombea nafasi ya huyo alomtuma!
Huoni kama ni Uchizi huo?
 
Mbowe kataka mwenyewe kuondolewa madarakani, kwa kujifanya yeye ni Masta wa siasa na propaganda, Anajifanya yeye ndo mpanga safu ya uongozi Chamani

Safari hii kakutana na kisiki
 
Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?

Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.

Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.

Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.

Maasalam.
Hakuna mpango wowote wa kumuondoa Mbowe madarakani, kinachoendelea ndani ya CHADEMA ni kufanya uchaguzi wa kupata viongozi wa kuendesha chama kipindi kinachofuata baada ya kipindi cha Mbowe kwisha. Hiyo ni fursa inayotolewa kwa mwanachama yoyote yule, sio lazima awe Mbowe au Lissu.
 
Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?

Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.

Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.

Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.

Maasalam.
Mwamko wa raia dhidi ya hadaa za watawala kupitia kivuli cha vyama kupitia mapandikizi yao.
 
Back
Top Bottom