Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani?

Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?

Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.

Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.

Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.

Maasalam.
Hakuna harakati za kumuondoa Mbowe bali kuna mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa kitaifa wa Chadema. Box la kura ndiyo msema kweli,mengine uliyoelezea ni upambe na matamanio yako.
 
Unashangaza aisee, unauliza kwanini siyo mwaka jana au juzi kwani mwaka jana au mwaka juzi kulikuwa na uchaguzi mkuu wa chama!? Kwa mujibu wa katiba yao hiki ndo kipindi cha uchaguzi kwahiyo ndo nafasi pekee ya maamuzi. Hata hivyo kwa akili ya kawaida tu nikuulize: unahisi Mbowe hata akiachwa/Akishinda uchaguzi anaweza kuiongoza CHADEMA kuitoa CCM madarakani kwenye uchaguzi wa mwaka huu? Zoezi hilo chini ya Mbowe limeshashindikana na mbaya zaidi graph inazidi kushuka hivyo chama kinahitaji hamasa na uongozi mpya usio na makando kurudisha imani kwa Watanzania.
Mleta uzi bila shaka yoyote ni nyumbu wa Mbowe
 
Kama unaona habari hazikuhusu zipotezee tu. Hujalazimishwa kuzifuatilia.

Wanaoona zinawahusu watafuatilia.

Hizi ni habari za kuendesha chama cha kitaifa, si habari za mke na mume kulala.

You are comparing apples to oranges.
Mkuu hujui kama ukituma clip ya mambo ya chumbani kwako itatazamwa na kila mtu na ita trend na kuzungumziwa sana? Ndio hayo yotokea kwa Chadema
 
1. Una hakika Lissu haonji Asali? Kama Lissu hana Biashara, hana Ubunge, hana hata Usafiri wake anaishije mjini? Naomba nambie source ya Imcome ya Tundu Lissu happ mjini.
2. Ya Abdul ukisikiliza kwa makini utetezi wa Lissu unajua wazo alikuwa anamjua ana amekuja nyumbani kwake kufanya nini!
3. Kisha sio Lissu alokutana na Mama Samia Ubelgiji? Waliongea nini hadi karudi Tz, TISS wasimguse maana alisema Usalama wa Taifa walitaka kumuua.
4. Usalama wa Taifa wanaweza kweli futa kesi zao ikiwa kuna hatari ya Usalama wa nchi? Ghafla tunaona Lissu analiamsha ndani ya Chadema muda huu ambao Chadema wanajipanga kuikabiri CCM.
5. Ebu wewe nipe time line yaani pale ashinde au ashindwe Lissu Uenyekiti kutakalika?
Tunajua maccm mnataka Mbowe aendelee kwa vile amefika bei.
 
Mkuu hujui kama ukituma clip ya mambo ya chumbani kwako itatazamwa na kila mtu na ita trend na kuzungumziwa sana? Ndio hayo yotokea kwa Chadema
CHADEMA ni chama cha kitaifa, si habari za chumbani.

Unapolinganisha vitu, linganisha vinavyolinganishika.

Again. You are comparing apples to oranges.
 
Mkuu hujui kama ukituma clip ya mambo ya chumbani kwako itatazamwa na kila mtu na ita trend na kuzungumziwa sana? Ndio hayo yotokea kwa Chadema
Hiyo ni minyukano ya ndani tu ndani ya vyama nyakati za uchaguzi
 
Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?

Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.

Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.

Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.

Maasalam.
Umeandika as if ni hila, No ni utaratibu wa chama, itapigwa kura kuona nani atafaa kuwaongoza

Mbowe amefanya kazi nzuri, but kwa sasa chama hakihitaji mwanasiasa wa taratibu, kinataka aggresive politics, ili watoke hapo
 
Wale Team Lisu wanajiona wana uwezo mkubwa sana kifikra kumbe ni kakikundi kadogo kaliko jawa na wivu, na uchu wa madaraka wanayohisi watayapata kupitia Lisu, waliyakosa kuputia Mbowe.

Nashauri kamati kuu ikimjadili Lisu na wapiga kelele wenzake wamfukuze kutoka chamani, ilu wapate fursa kuanzisha na kusajiri chama chao cha harakati.

Wanajivunia chadema kwasababu ya uongozi mahili wa FAM, Wakichukua chama kina kufa, na ndiyo nia yao hawa mahodari wa kuongea bila mipaka.
Na nyumbu wa Sultan Mbowe mnajiona hii Chadema kama kampuni yenu binafsi.
 
Upuuzi kama huu ndio ulonifanya nipumzike #Jamiiforums kwa sababu hamsomi content mkazielewa bali mnakurupuka na kutukana watu wazima pengine wazazi wanu. Na ndio.maana sidhangai kuona watu kama wewe mnashangilia Lissu bila kujiuliza uwezo wake bali kwa sababu analipiza kisasi.
Ukipumzika jamii forums hiyo ni hasara kwa nani?
 
Kujipanga kwa ajili ya uchaguzi mkuu hakutaisha 2025, kuna 2030, 2035, 2040 etc. Je mleta mada unata Mbowe aendelee kutawala mpaka afie kwenye kiti simply because kuna uchaguzi nchini kila baada ya 5years?
 
Kujipanga kwa ajili ya uchaguzi mkuu hakutaisha 2025, kuna 2030, 2035, 2040 etc. Je mleta mada unata Mbowe aendelee kutawala mpaka afie kwenye kiti simply because kuna uchaguzi nchini kila baada ya 5years?
Kuongoza Chama sii sawa na Kuongoza NCHI. Nitarudia kusema Kujenga Chama ni sawa na contactor wa ujenzi wa nyumba ya kujitolea. Haihitaji kubadilisha Mwenyekiti au safi na viongozi maana ni kazi ya Kujitolea haina malipo. Na kama kuna mmoja wao hafai ataondolewa na Mkutano Mkuu au Kamati kuu kama walivyoondolewa kina Zitto, Kitila, Dr. Slaa na wengineo, labda nikuulize alipoondoka Dr.Slaa au Zitto Chadema kulifanyika Uchaguzi? Kifungu gani cha Sheria kilimuondoa Zitto lakini hakiwezi kumuondoa Mbowe?

Halafu unasikia watu wanasema Mbowe asingeweza kuondolewa bila Uchaguzi.
Rudini nyuma issue ya kija Zitto nani alokuwa mpambe wa Mbowe? Sii huyu huyu Lissu mpaka wakatukanana matusi mazito, Zitto akisema haongei na kitu kama mbwa bali mwenye mbwa au nakosea? Issue ya Dr. Slaa alokuwa akimpiga madongo Slaa muda wote nani kama sio Lissu huyu huyu?

Leo Lissu kamgeuka Kiongozi wake tena basi aliomba kikao cha faragha yeye Mbowe na Mnyika wagawane vyeo. Mbowe alikataa, yeye akataka sijui Urais, Uenyekiti au vyote. Yote haya yanavuja sasa hivi na Lissu atakataa yote mbele za watu kwa sababu anajua sana kujifanya mhanga. Labda nianze kuwamiminia clip zake mpime wenyewe..
 
lengo kuu ni ili wapate mtu ambaye hatakuwa analamba asali. uwepo upinzani halisi utakaoiwajibisha serikali inayouza nchi kwa mwarabu.
Lakini nchi ikiuzwa vatican au kwa mjrumani au kwa mbelgiji hakuna nenoi.
 
Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?

Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.

Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.

Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.

Maasalam.
Ni bora CCM iwe marakani milele kuliko wakina Mbowe ndio wao wawakilishi wa demokrasia mavi.
Chama kimejaa ukabila,kazi kubwa ni kula ruzuki, hadi leo hamna ofisi,............yeye mbowe KAZI yake ni kuona namna gani nzuri anapaya pesa kupitia siasa na sio kuwakomboa wananchi,.
Yes tunataka kuona wakina Lissu wanavunja huu upumbavu,ama CCM iendelee kutawala milele na sio eti kushabikia SACCOS YA kina mbowe
 
Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?
Diligency
 
Kwani uchaguzi wa CDM unafuata ratiba ya uchaguzi mkuu wa nchi? Kama wana uchaguzi wao kwanini ushangae muda kuwa sasa kama muda wake umefika?
 
Kwani uchaguzi wa CDM unafuata ratiba ya uchaguzi mkuu wa nchi? Kama wana uchaguzi wao kwanini ushangae muda kuwa sasa kama muda wake umefika?
Uchaguzi upi wa CCM? Mkuu wangu CCM Uchaguzi wa Mgombea Urais ndio hufanyika na anayeshinda ndiye automatically anakuwa Mwenyekiti wa Chama kwa sababu mgombea ni yeye pekee. Anapigiwa kura ya ndio au Hapana. Kwa hiyo ni baada ya kuwa rais ndio unapata Mwenyekiti wa CCM, siku wakishindwa Urais sijui Mwenyekiti atakuwa nani..😁😁😁
 
Uwazi kwa wahusika tu, hata ukiwa na mkeo unafunga milango na madirisha, uwazi unabakia kwenu pekee 😁😁
Acha hizo mzee mwenzetu, tumefika hapa tulipo kama taifa kwa sababu ya UNAFIKI. Unafiki umekuwa kama ugonjwa wa kuambukiza na muda umefika wa kuiita kolea kwa jina lake na si kijiko kikuubwa!

Hii ni JF where we dare, remember? Umesahau jinsi baadhi yetu nyakati zote tumemkoma nyani giledi bila kumuangalia usoni? Hizo siasa zako kwa sasa zimepitwa na wakati...Unafiki basi, CCM has to go!
 
Uchaguzi upi wa CCM? Mkuu wangu CCM Uchaguzi wa Mgombea Urais ndio hufanyika na anayeshinda ndiye automatically anakuwa Mwenyekiti wa Chama kwa sababu mgombea ni yeye pekee. Anapigiwa kura ya ndio au Hapana. Kwa hiyo ni baada ya kuwa rais ndio unapata Mwenyekiti wa CCM, siku wakishindwa Urais sijui Mwenyekiti atakuwa nani..😁😁😁

Wapi nimeuliza uchaguzi wa CCM? You lack comprehension skills.

Nimesema uchaguzi wa CHADEMA (CDM) ni kila baada ya muda gani? Huu uchaguzi wa sasa ni muda wake au wameforce kufanya uchaguzi muda wakati muda haujafika?
 
Acha hizo mzee mwenzetu, tumefika hapa tulipo kama taifa kwa sababu ya UNAFIKI. Unafiki umekuwa kama ugonjwa wa kuambukiza na muda umefika wa kuiita kolea kwa jina lake na si kijiko kikuubwa!

Hii ni JF where we dare, remember? Umesahau jinsi baadhi yetu nyakati zote tumemkoma nyani giledi bila kumuangalia usoni? Hizo siasa zako kwa sasa zimepitwa na wakati...Unafiki basi, CCM has to go!
Kwanza nitoe shukran zangu kwako kumbe bado mpo? Mkuu nadhani unakumbuka sana kwamba mada nyingi zamani mlikuwa mnakataa mwisho wa siku mnakutana na ukweli nilousema. Toka wakati ule kina Zitto, January, Maria Sarungi, Kitila, Nape, Mnyika wakiwa hapa mara nyinti nilikuwa upande msoupenda.

Sasa kumkoma nyani sii lazima iwe Mbowe wakati najua fika Lissu ndiye hafai kuwa Kiongozi bali ni Mwanaharakati na wakili mtetezi wa hata Jambazi. Lissu anaweza mtetea jambazi alokamatwa na nyala za Serikali na akashinda kesi. Ni mjuzi wa kujenga hoja za UONGO na akashinda.


Mimi mwananchi siwezi kutetea Ushindi huo, nitasema Ukweli ninao uona na naoujua. Siandiki kitu kama sina hakika nacho. Niliwahi sema humu zamani kuwa namjua Lissu kuliko mnavyodhania. Alisomeshwa Marekani na LEAT ambayo wafadhili wake ni Ford Foundation ni tapeli mpenda sifa na majivuno kuwa yeye ndiye Alfa na Omega hakuna zaidi yake.

Hata wakati wa Magufuli, Lissu alipinga Sheria mpya ya mikataba ya madini na nishati akisema mikataba hiyo ni ya Kimataifa hatuwezi kuivunja. Lakini haada ya mwendazake akarudi nchini tukaanza kudaiwa madeni hayo ili mradi tu muendelee kumchukia Magufuli - Nawaelewa.

Kule west Bukina Faso, Chad, Mali n.k wamefuta mikataba ya zamani, wamekubali kulipa madeni yote, leo wako HURU na mfano bora kwa viongozi wa KiAfrika kila mtu anawaona hawa ndio Viongozi tunaowataka.
Senegal inafuata na baadhi ya nchi chini ya Wafaransa wanafuata njia hiyo ya Magufulification. Huku kwetu sisi ni malumbano tu wenyewe kwa wenyewe. Haya kama sii matunda ya Umaskini na Ujinga kitu gani kimetusibu?
 
Wapi nimeuliza uchaguzi wa CCM? You lack comprehension skills.

Nimesema uchaguzi wa CHADEMA (CDM) ni kila baada ya muda gani? Huu uchaguzi wa sasa ni muda wake au wameforce kufanya uchaguzi muda wakati muda haujafika?
Samahani nime qoute vibaya, hoja sii Uchaguzi nachozungumzia ni haya malumbano baina ya Lissu na Wapambe wake kumshusha Mbowe kiasi hiki hata kabla ya kusimama mbele ya wapiga kura na kuomba kura zao. Mbona zamani haikuwa kutokea hivi? Kuna mgombea alikatazwa kugombea? Sioni sababu kabisa ya malumbano na character assassination ndani ya Chama kimoja
Hakutakuwa na AMANI baada ya Uchaguzi Mkuu.
 
Back
Top Bottom