Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani?

Tumestuka

Lakini pia ungemuuliza museveni, nini hasa lilikua lengo lake kutaka kumuondoa Lissu kwenye nyazifa zote na kukataa asigombee Uraisi?
Mbowe ni mfanyabiashara, alitaka kuuza nafasi ya mgombea kutoka ccm
 
Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?

Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.

Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.

Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.

Maasalam.
Kwanini kuna vyama vingi vya siasa?
 
Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?

Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.

Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.

Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.

Maasalam.
Mbowe haondolewi, Kuna uchaguzi wa kikatiba, UPEPO UNAONESHA MBOWE ATAANGUKA, kwamba anaondolewa ndo watu watakuwa wanakusikia wewe!!

Samahani mkuu upo hapa TANZANIA? Au upo Ng'ambo?? Jaribu kushirikisha UBONGO na kufuatilia ukweli wa mambo ulivyo!!

Ni hilo tu!🚴🚴🚴
 
Chadema mnashindwa kabisa kusoma nyakati. Huu sio wakati kabisa wa kupigana marungu kuona Nyumbu wakioneshana ubabe wakati Simba kalala pembeni. Niseme hivi, Lissu na Lema wanabwabwaja hovyo kabisa afadhali ya Heche.

Yaani Mbowe kukutana na rais kalamba Asali lakini Lissu alokutana na rais Ubelgiji akaomba kurudishiwa hela zake nje ya mfumo hakulamba asali? Ile give and take, rais alipata nini kutoka kwa Lissu? Nani anajua.

Haya Lema anaye mpigia simu raus direct akiwa Canada akiomba kama anaweza kurudi nchini na kuhakikishiwa usalama wake nje ya vikao vya chama ilikuwa sawa? Ili apate hayo yeye kaahidiwa nini kwa Mama Samia?

Yaani watu wanavyo bwabwaja hoja ambazo zinawaweka wao mashakani zaidi ndio kweli silaha yao? na naposikia kulikuwa na mpango wa Mapinduzi inanipa shaka zaidi kwao wao kwa nguvu kubwa wanayotumia kuliko Mbowe Mlamba asali..
 
Mbowe haondolewi, Kuna uchaguzi wa kikatiba, UPEPO UNAONESHA MBOWE ATAANGUKA, kwamba anaondolewa ndo watu watakuwa wanakusikia wewe!!

Samahani mkuu upo hapa TANZANIA? Au upo Ng'ambo?? Jaribu kushirikisha UBONGO na kufuatilia ukweli wa mambo ulivyo!!

Ni hilo tu!🚴🚴🚴
Mmhhh
 
Uchaguzi sina tatizo nalo isipokuwa ukiwasikia madai yao ndio utajua ni kampeni. Mgombea ni Lissu kwa nini kila mtu anataka Mbowe aondoke, sijui asigombee, mara mla rushwa, Mbowe ni CCM!
Kweli ndio denokrasia inavyotakiwa? Kwa nini Tundu Lissu asingeweka nia ikaisha bila kuwa na kundi la washabiki nyuma kummaliza kisiasa hata kabla ya Uchaguzi wenyewe? Halafu yanayozungumzwa sii kwamba mapungufu ya itikadi, sera wala misimamo ya Chama bali MBOWE hafai, Mbowe CCM, mzee n.k. Chama cha Siasa hakiongozwi kwa mihemko ya Wanaharakati bali huongozwa na Wanasiasa. Kugombea Urais shauri jingine lakini sio timu moja kumnanga captain wenu. Lissu anazungumza kama Wakili mwanasheria na kesi ya Mbowe ipo mahakamani, kitu ambacho kinaharibu kabisa Demokrasia

.
Hilo swali nililiuliza mapema. Kama kweli watu wanapenda demokrasia kwa nini wanataka mtu wao apite bila kupingwa? Yaani leo wanamlaumu Mbowe kwa kushindwa uchaguzi wa 2020 wakijifanya kusahau mazingira ya wakati ule? Wanazunguka zunguka lakini wana hint kuwa Mbowe alihusika na ubaya wote waliofanyiwa viongozi na makada wa CHADEMA.

Amandla...
 
Hilo swali nililiuliza mapema. Kama kweli watu wanapenda demokrasia kwa nini wanataka mtu wao apite bila kupingwa? Yaani leo wanamlaumu Mbowe kwa kushindwa uchaguzi wa 2020 wakijifanya kusahau mazingira ya wakati ule? Wanazunguka zunguka lakini wana hint kuwa Mbowe alihusika na ubaya wote waliofanyiwa viongozi na makada wa CHADEMA.

Amandla...
Mbowe mstaarabu sana aisee jamaa anampaka vibaya sana hata kwenye mdahalo.
Nimemsikia Tundu Lissu akidai Mbowe alipotoka jela alibadilika kalamba asali!,
Najiuliza hivi, yeye aliporudi nchini alifanya nini? Upi mchango wake mkubwa baada ya kurudi nchini kutoka Ubelgiji ambao tunaweza sema Tundu Lissu aliyeondoka ndiye huyu aliyerudi. Mimi niko huku nilisikia haya
1. Tumesikia alikutana na Abdul nyumbani kwake arudishiwe fedha zake za maribabu nje ya utaratibu. Inakuwaje mpokea rushwa ni Wenje sio yeye au kwa sababu hakupata fedha hizo ndio kageuka?
2. Tulisikia CCM wakimchagia kupata gari lake na akasema wakimpa atalichukua, ilitokeaje?
3. Tundu Lissu akiwa Ubelgiji alimuomba Mama Samia kumlipa hela zake nje kabisa ya mfumo wa malipo ya fedha na akalipwa.
Katika fikra za kawaida utajiuliza Je, Mama Samia alitaka nini kutoka kwa Lissu mpaka akampa fedha hizo nje ya utaratibu wa Bunge?
Nina hakika angekuwa Kiongozi mwingine yeyote Tundu Lissu asingemuacha.
 
Wale Team Lisu wanajiona wana uwezo mkubwa sana kifikra kumbe ni kakikundi kadogo kaliko jawa na wivu, na uchu wa madaraka wanayohisi watayapata kupitia Lisu, waliyakosa kuputia Mbowe.

Nashauri kamati kuu ikimjadili Lisu na wapiga kelele wenzake wamfukuze kutoka chamani, ilu wapate fursa kuanzisha na kusajiri chama chao cha harakati.

Wanajivunia chadema kwasababu ya uongozi mahili wa FAM, Wakichukua chama kina kufa, na ndiyo nia yao hawa mahodari wa kuongea bila mipaka.
Huna hoja, tulia unyolewe pamoja na huyo sultani.
Mliifanya cdm shamba la bibi
 
Mbowe mstaarabu sana aisee jamaa anampaka vibaya sana hata kwenye mdahalo.
Nimemsikia Tundu Lissu akidai Mbowe alipotoka jela alibadilika kalamba asali!,
Najiuliza hivi, yeye aliporudi nchini alifanya nini? Upi mchango wake mkubwa baada ya kurudi nchini kutoka Ubelgiji ambao tunaweza sema Tundu Lissu aliyeondoka ndiye huyu aliyerudi. Mimi niko huku nilisikia haya
1. Tumesikia alikutana na Abdul nyumbani kwake arudishiwe fedha zake za maribabu nje ya utaratibu. Inakuwaje mpokea rushwa ni Wenje sio yeye au kwa sababu hakupata fedha hizo ndio kageuka?
2. Tulisikia CCM wakimchagia kupata gari lake na akasema wakimpa atalichukua, ilitokeaje?
3. Tundu Lissu akiwa Ubelgiji alimuomba Mama Samia kumlipa hela zake nje kabisa ya mfumo wa malipo ya fedha na akalipwa.
Katika fikra za kawaida utajiuliza Je, Mama Samia alitaka nini kutoka kwa Lissu mpaka akampa fedha hizo nje ya utaratibu wa Bunge?
Nina hakika angekuwa Kiongozi mwingine yeyote Tundu Lissu asingemuacha.
Pumba tupu, huyo sultani wenu kafika mwisho.
Nyakati zimemkataa
 
Pumba tupu, huyo sultani wenu kafika mwisho.
Nyakati zimemkataa
Jibu hoja, sio kunishambilia mimi, nina haki ya kusema, kuhoji na kuuliza kama ulokuwa nayo wewe unayempigia chabu Lissu.
CHadema ilipoteza Wanachama wengi wakati yeye akiwa mgombea wa Urais, mkasema wamehongwa na CCM, leo mmebadilika ni kwa sababu ya Mbowe, kwa nini isiwe sababu ni Lissu aloshindwa Urais akakimbia nchi?
 
Mbowe mstaarabu sana aisee jamaa anampaka vibaya sana hata kwenye mdahalo.
Nimemsikia Tundu Lissu akidai Mbowe alipotoka jela alibadilika kalamba asali!,
Na anadai kuwa ishara ni kuwa Mbowe hakuwaomba wenzake kibali kabla ya kwenda kumuona Samia. Yeye mbona hakumfukuza Samia alipoenda kumpa pole Nairobi?
Najiuliza hivi, yeye aliporudi nchini alifanya nini? Upi mchango wake mkubwa baada ya kurudi nchini kutoka Ubelgiji ambao tunaweza sema Tundu Lissu aliyeondoka ndiye huyu aliyerudi.
Aligombea uchaguzi. Aliposhindwa yeye na wenzake wakatangaza maandamano. Wakati wenzake wanashughulikiwa yeye akakimbilia Ubelgiji.
Mimi niko huku nilisikia haya
1. Tumesikia alikutana na Abdul nyumbani kwake arudishiwe fedha zake za maribabu nje ya utaratibu. Inakuwaje mpokea rushwa ni Wenje sio yeye au kwa sababu hakupata fedha hizo ndio kageuka?
1.Lissu alisema Wenje aliongozana na Abduli ili wamhonge. Akasema walimtajia viongozi wengine ambao waliisha pokea mzigo. Mpaka leo hajawataja hao viongozi. Yericko alisema kuwa mashtaka yaliletwa kwenye Kamati Kuu lakini alishindwa kutoa ushahidi. Sasa hivi anasema aliyempa ushahidi hayupo tena duniani. So convenient. Kuthibitisha kuwa alikuwa hasemi ukweli wameweka clip akisema Wenje alimtaarifu kuhusu uwezekano wa kumpigia kifua kwa mama yake. Akasema pia kuwa Abduli alienda na Wenje nyumbani akampa document husika za madai yake. Akasema pia kuwa alimwambia Abduli kuwa akifanikisha malipo yake atakuwa rafiki yake milele! Anasema haya kuhusu mtu ambae amedai kuwa ni corrupter in chief wa mama yake.
2. Tulisikia CCM wakimchagia kupata gari lake na akasema wakimpa atalichukua, ilitokeaje?
Na kwa mtu anaetaka uwazi kuhusu mapato na matumizi ya chama chake mpaka leo hajatoa mchanganuo wa kiasi kilichopatikana. Alichofanya ni alitoa a general figure baada ya kuhisi litakuwa tatizo.
3. Tundu Lissu akiwa Ubelgiji alimuomba Mama Samia kumlipa hela zake nje kabisa ya mfumo wa malipo ya fedha na akalipwa.
Katika fikra za kawaida utajiuliza Je, Mama Samia alitaka nini kutoka kwa Lissu mpaka akampa fedha hizo nje ya utaratibu wa Bunge?
Atakwambia zilikuwa stahili yake.
Nina hakika angekuwa Kiongozi mwingine yeyote Tundu Lissu asingemuacha.
Lissu alimpigia debe sana Msigwa katika uchaguzi wa Ziwa Nyasa. Akatahadharisha umma kuwa kuna pesa za Abduli zimeingizwa kuinfluence uchaguzi. Rafiki yake aliposhindwa akabaki kusema kuwa alionewa. Na bado anamtetea huyo rafiki hata baada ya kuhamia kwa mama Abdul. Siku hizi anavaa nguo zenye picha za mama Abdul. Hivi angeshindwa Sugu halafu angehamia kwa mama Abduli baada ya kushindwa angemuacha salama? Huyo huyo kada wa CCM sasa hivi anampigia debe wazi wazi. Angalau Heche aliyesema kuwa hana mpango na Msigwa baada ya kuhamia CCM na kufanya jitihada za kuibomoa CDM.

Lema anajitahidi kumsafisha Msigwa na Lissu amekaa kimya kabisa! Nakumbuka vile vile kuwa kuna kada wa CCM aliyesema mazungumzo na Msigwa yalianza zamani tuu! Bila shaka wakati wakifanya mpango wa kumpindua Mbowe.

Hawa hawaitakii mema Chadema.

Amandla...
 
Rais Yoweri Kaguta Museveni " kotapini kwenye baiskeli inaingia kwa nguvu na inatolewa kwa nguvu ."
 
Back
Top Bottom