Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani?

Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?

Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.

Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.

Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.

Maasalam.
Mkongwe mwenzangu, habari ya kuadimika ndugu Mkandara ?
Karibu tena barazani hapa.

Kwani kuna mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani au ni uchaguzi kutimiza demokrasia ukizingatia CHADEMA ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo!!??
Iweje kutimiza suala la kidemokrasia uwe mpango ( ambao kwa mujibu wa maandishi yako ni mpango wenye nia ovu)!!??
 
Unashangaza aisee, unauliza kwanini siyo mwaka jana au juzi kwani mwaka jana au mwaka juzi kulikuwa na uchaguzi mkuu wa chama!? Kwa mujibu wa katiba yao hiki ndo kipindi cha uchaguzi kwahiyo ndo nafasi pekee ya maamuzi. Hata hivyo kwa akili ya kawaida tu nikuulize: unahisi Mbowe hata akiachwa/Akishinda uchaguzi anaweza kuiongoza CHADEMA kuitoa CCM madarakani kwenye uchaguzi wa mwaka huu? Zoezi hilo chini ya Mbowe limeshashindikana na mbaya zaidi graph inazidi kushuka hivyo chama kinahitaji hamasa na uongozi mpya usio na makando kurudisha imani kwa Watanzania.
Inabidi umsome mtu kwanza uelewe anasimamia wapi. Hoja za kwa nini Lissu anagombea Uenyekiti ndizo nimezungumzia. Tuhuma.ntingi zimesemwa ambazo zingeweza kuzunfumzwa toka 2021 na hata kuweka katazo la.Mbowe kuendelea na Uenyekiti.
Usichukulie Uenyekiti kama ni Urais. Mwenyekiti anasimamia tu Chama hana madaraka ya Urais wala Uchief. Hata Uchaguzi ndani ya Vyama.vya Siasa sii lazima kwa sababu ni kazi ya kujitolea hawalipwi mshahara. Kwa hiyo ukiwasoma jamaa hawa unaona kabisa tatizo ni NJAA. Akili yao Mwenyekiti ana source za kucuta mkwanja na Mbowe kavuta sana CCM. Sasa ni zamu yao na wao wavute!. Ikiwa sivyo walivgodhani unadhani Chadema itapona? Yaliwakuta NCCR na CUF kwa mtindo huu huu, ugonvi juu ya UENYEKITI leo wako wapi?
 
Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?

Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.

Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.

Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.

Maasalam.
Ccm wameweza kumingia Mbowe wakifikiri wakisha muweka Mbowe mfukoni hata Chadema itakuwa imeingizwa mfukoni. Kitu ambacho ccm hakutegemea ni mbowe kupoteza ushawishi na kuaminika kwa wanachadema.

Sasa tegemeo la ccm ni kumfanya Mbowe aendelee kuwa mwenyekiti kwa njia za mahakama au kutumia nguvu ya serikali.
Bila hivyo Mbowe anakaa pembeni . Chaema chini ya Tundu Lissu na heche ccm watajuwa kuwa hawajui ndani ya mwaka mmoja tu. Watu ccm ilio waandaa kuanzisha vyama vya upizani wanaanza kuisha taratibu.
 
Sheria ya Bunge inasemaje ikiwa mbunge akifutwa Ubunge?

Hayo ni madai ya Lissu anatapatapa tu. isikilize vizuri hotuba yake kisha jiulize what if ni Wenje aloomba ushauri kugombea, ulitaka Mbowe aseme usigombee? Kwani nafasi hiyo imezuiwa kugombewa isipokuwa Lissu peke yake?
Na kwa nini Lissu aseme Mbowe alimtuma agombee nafasi yangu basi na mimi nagombea nafasi ya huyo alomtuma!
Huoni kama ni Uchizi huo?
kuhusu sheria ya bunge inasemaje, iwe ilisema hatakiwi kupata au anapata, cha muhimu ni kwamba Lisu alikuwa anajiuguza kila mtanzania anajua, na kile alichopewa na samia haikuwa hisani, ilikuwa haki yake kiubinadamu. sasa mtu ukimpa haki yake unataka akulambe miguu tena, au hujui maana ya haki?
 
Mkongwe mwenzangu, habari ya kuadimika ndugu Mkandara ?
Karibu tena barazani hapa.

Kwani kuna mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani au ni uchaguzi kutimiza demokrasia ukizingatia CHADEMA ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo!!??
Iweje kutimiza suala la kidemokrasia uwe mpango ( ambao kwa mujibu wa maandishi yako ni mpango wenye nia ovu)!!??
Uchaguzi sina tatizo nalo isipokuwa ukiwasikia madai yao ndio utajua ni kampeni. Mgombea ni Lissu kwa nini kila mtu anataka Mbowe aondoke, sijui asigombee, mara mla rushwa, Mbowe ni CCM!
Kweli ndio denokrasia inavyotakiwa? Kwa nini Tundu Lissu asingeweka nia ikaisha bila kuwa na kundi la washabiki nyuma kummaliza kisiasa hata kabla ya Uchaguzi wenyewe? Halafu yanayozungumzwa sii kwamba mapungufu ya itikadi, sera wala misimamo ya Chama bali MBOWE hafai, Mbowe CCM, mzee n.k. Chama cha Siasa hakiongozwi kwa mihemko ya Wanaharakati bali huongozwa na Wanasiasa. Kugombea Urais shauri jingine lakini sio timu moja kumnanga captain wenu. Lissu anazungumza kama Wakili mwanasheria na kesi ya Mbowe ipo mahakamani, kitu ambacho kinaharibu kabisa Demokrasia

.
 
Tumestuka

Lakini pia ungemuuliza museveni, nini hasa lilikua lengo lake kutaka kumuondoa Lissu kwenye nyazifa zote na kukataa asigombee Uraisi?
Sisi huu mpango tuliujua kutoka mwaka 2022 mwishoni. Mbowe aliandaa mazingira mazuri kwa mama Abdul
 
Waswahili wanasema "Akili ni nywele kila mtu ana zake" Najiuliza hii timing ya Mgogoro wa Chadema inaashiria nini wakati kumebakia miezi 10 tu kufikia Uchaguzi Mkuu wa Taifa?

Nini hasa lengo la harakati hizi za kumuondoa Mbowe madarakani wakati ambao Chama kinatakiwa kuwa pamoja wakipanga mikakati ya Uchaguzi Mkuu ujao?

Kama Mbowe mzee na hafai kuongoza, wamejua haya toka lini? Kwa nini sasa hivi sio mwaka juzi, jana ila leo ndio imekuwa hoja ya msingi kufanya mabadiliko ndani ya Chama. Hivi wakimundoa Mbowe madarakani ndio wataweza kumkabiri vema Mama Samia na CCM hiyo November 2025 kupitia sera gani? Maana Kama Chadema haikufanya vema chini yake, je wale Wagombea Urais waloshindwa walikuwa Chaguo la nani, Mbowe?

Nikiitazama safu ya wapambe wa Tundu Lissu ni kundi la wanaharakati wanaodai TANGANYIKA HURU kwa sababu hawaridhiki na Uongozi wa Mama Samia. Na wala tusidanganyane ya kwamba mpango wa kumuondoa Mbowe madarakani umetokea ghafla.

Nina hakika Ulikuwepo na ulipangwa sawa kabisa na ule wa kina Zitto 2013. Tofauti ni kwamba kina Zitto waligunduliwa mapema na hawa kwa usiri mkubwa wameweza fikia hatua ya mwisho. Pengine walijifunza yalowakuta kina Zitto na Kitila.

Niliwahi kusema rasimu ya Warioba ilishindikana kutokana na madai ya Serikali 3. Na nazidi kusisitiza kuwa haitawezekana kurudiwa Rasimu ya Warioba kupitia madai yale yale ya Kudai Serikali ya Tanganyika. Kama Chadema itasambaratika basi Tanzania itabakia imara kwa kulindwa na KATIBA hii hii.

Binafsi sielewi kina Lissu na Heche wana Mpango gani lakini niseme tu kwamba sasa hivi CCM wanatafuna popcorn huku wakisukumiza na juice baridiii kwa mrija. Sinema ya Mdudu ndio kwanza imeanza.

Maasalam.
Sasa wewe kwa Akili zako unadhani CCM wamemtuma nani Kati ya hawa wote wanaogombea nafasi pale CHADEMA wasaidie watanzania wenzako tena ukiwa na Akili TIMAMU kabisa isiyo na chembe ya uchawa wa mtu yeyote.
 
Ccm wameweza kumingia Mbowe wakifikiri wakisha muweka Mbowe mfukoni hata Chadema itakuwa imeingizwa mfukoni. Kitu ambacho ccm hakutegemea ni mbowe kupoteza ushawishi na kuaminika kwa wanachadema.

Sasa tegemeo la ccm ni kumfanya Mbowe aendelee kuwa mwenyekiti kwa njia za mahakama au kutumia nguvu ya serikali.
Bila hivyo Mbowe anakaa pembeni . Chaema chini ya Tundu Lissu na heche ccm watajuwa kuwa hawajui ndani ya mwaka mmoja tu. Watu ccm ilio waandaa kuanzisha vyama vya upizani wanaanza kuisha taratibu.
Mbowe aloiongoza Chadema kwa miaka 20 na miaka yote watu wamekuwa wakisema Mbowe ni CCM. Mbona Chadema imekuwa chama Kikuu cha Upinzani kwa miaka yote hakijashuka? LIssu mwenyewe kaingizwa Chadema na Mbowe na kumwingiza moja kwa moja Kamati kuu. Mbowe wa CCM angetaka kuona watu kama Lissu, Wangwe, Heche, Wenje, Lema, Zitto, dr.Slaa, Msigwa, Sugu, Kina Halima Mdee na wengine wote woitikisa CCM ambao hawakuwepo miaka ya nyuma? Acheni matusi jamani Mbowe kawapokea kawavusha leo hana maana yoyote..
 
Inabidi umsome mtu kwanza uelewe anasimamia wapi. Hoja za kwa nini Lissu anagombea Uenyekiti ndizo nimezungumzia. Tuhuma.ntingi zimesemwa ambazo zingeweza kuzunfumzwa toka 2021 na hata kuweka katazo la.Mbowe kuendelea na Uenyekiti.
Usichukulie Uenyekiti kama ni Urais. Mwenyekiti anasimamia tu Chama hana madaraka ya Urais wala Uchief. Hata Uchaguzi ndani ya Vyama.vya Siasa sii lazima kwa sababu ni kazi ya kujitolea hawalipwi mshahara. Kwa hiyo ukiwasoma jamaa hawa unaona kabisa tatizo ni NJAA. Akili yao Mwenyekiti ana source za kucuta mkwanja na Mbowe kavuta sana CCM. Sasa ni zamu yao na wao wavute!. Ikiwa sivyo walivgodhani unadhani Chadema itapona? Yaliwakuta NCCR na CUF kwa mtindo huu huu, ugonvi juu ya UENYEKITI leo wako wapi?
Wakati mbowe anavuta huo mkwanja chadema haikufa ila chadema ikiwa chini ya lissu itakufa ila uchawa mwingine pumzika mzee ulee wajukuu
 
Wakati mbowe anavuta huo mkwanja chadema haikufa ila chadema ikiwa chini ya lissu itakufa ila uchawa mwingine pumzika mzee ulee wajukuu
Upuuzi kama huu ndio ulonifanya nipumzike #Jamiiforums kwa sababu hamsomi content mkazielewa bali mnakurupuka na kutukana watu wazima pengine wazazi wanu. Na ndio.maana sidhangai kuona watu kama wewe mnashangilia Lissu bila kujiuliza uwezo wake bali kwa sababu analipiza kisasi.
 
Uchaguzi sina tatizo nalo isipokuwa ukiwasikia madai yao ndio utajua ni kampeni. Mgombea ni Lissu kwa nini kila mtu anataka Mbowe aondoke, sijui asigombee, mara mla rushwa, Mbowe ni CCM!
Kweli ndio denokrasia inavyotakiwa? Kwa nini Tundu Lissu asingeweka nia ikaisha bila kuwa na kundi la washabiki nyuma kummaliza kisiasa hata kabla ya Uchaguzi wenyewe? Halafu yanayozungumzwa sii kwamba mapungufu ya itikadi, sera wala misimamo ya Chama bali MBOWE hafai, Mbowe CCM, mzee n.k. Chama cha Siasa hakiongozwi kwa mihemko ya Wanaharakati bali huongozwa na Wanasiasa. Kugombea Urais shauri jingine lakini sio timu moja kumnanga captain wenu. Lissu anazungumza kama Wakili mwanasheria na kesi ya Mbowe ipo mahakamani, kitu ambacho kinaharibu kabisa Demokrasia

.
Unamshauri lissu atukalipie siye wafuasi wake tusimseme mbowe ni mzee
 
Upuuzi kama huu ndio ulonifanya nipumzike #Jamiiforums kwa sababu hamsomi content mkazielewa bali mnakurupuka na kutukana watu wazima pengine wazazi wanu. Na ndio.maana sidhangai kuona watu kama wewe mnashangilia Lissu bila kujiuliza uwezo wake bali kwa sababu analipiza kisasi.
Mzee pumuzika lea wajukuu umepitwa na wakati nyie ndiyo wazee mmeifikisha nchi namna hii ya ovyo bado unatetea uzee wako.
Nani amekuita urudi
 
Nimegundua baadhi ya watanzania wanapenda sana ugomvi.Lisu amefanikiwa kukuza kisasi chake na Mbowe na kila mtu asiyetafakari anafurahia kila anachosema Lisu.Hii ni hatari
 
This is too low... nina wasiwasi kama wewe ni Mkandara yule yule wa zamani wa UD au ID imehackiwa... Kama ni wewe basi kama nchi tuna shida mahali, na kama JF tuna shida zaidi ya kupoteza GT tuliowategemea zamani.

Nikuombe Mkuu rudia kusoma hii post


Shallow questions... hoja hizi zinaibuka sasa kwa sababu ndio wakati wake (election) hujui hilo??
Nyuma ya Lissu kuna wanaharakati wa kudai Tanganyika, how sure is this, any proof?? Hata kama ndio, je kuna ubaya/kosa gani kisiasa? Ni sawa na mtu akisema nyuma ya Mbowe kuna CCM, utakataa???

SIASA NZURI SIO ZENYE DEMOKRASIA PEKEE, MAANA DEMOKRASIA KILA NCHI INA TAFSIRI YAKE, BADALA YAKE NI SIASA ZENYE FAIR PLAY GROUND... TENGENEZA CONTENT YA FAIR PLAY GROUND UKIWA KAMA PROFFESSIONAL POLITICAL (ANALYST) "EXPERT"..

Wasaaalam

...Ni Hayo Tu!!
MKuu kilichonifanya niandike makala hii ni kuitakia mema Chadema badala ya kushughulika na Mbowe. Chama ni kikubwa kuliko Mbowe ama hiyo nafasi ya Uenyekiti.
Wakati huu Chadema ya Wanasiasa wangekaa na kutunga mikakati ya kuiondoa CCM madarakani, na wale Wanaharakati wangepiga majungu Serikali ya Mama Samia toka wakati huu ili ikifika November wamevuta hisia za Wapiga kura zaidi, badala yake Chadema wanaanza kupotezana wenyewe.

Jiulize kwa nini? Kaanzisha nani hizi tuhuma jambo ambalo walitakiwa tu kutangaza Uchaguzi wao Mkuu tukasubiri kuona Wagombea. Infact nilisikia Mbowe hakutaka kugombea tena Uenyekiti isipokuwa Lissu ndiye kaingia na gia kwamba Mbowe kamtuma Wenje agombee nafasi yake na hivyo yeye atagombea nafasi ya Mbowe!

Think my brother, kwa hiyo ndio tuseme kama Mbowe asingemtuma Wenje ina maama Mbowe angebakia mru safi, Mwenyekiti hana udhoofu wanao usema leo? Lissu ana run kuwa Mwenyekiti sii kwa sababu ya kuongoza Chama bali kumkomoa Mbowe! Does this this sound right?
Well, kuhusu Kundi la watu wanaotaka Tanganyika, nenda vijiwe vyao utajua nasema nini. Binafsi niliwahi kuwepo huko nikaona chuki na upuuzi mtupu unaoendelea.
Kama sababu ya kudai Tanganyika ni Mama Samia sio Katiba basi dawa ilikuwa kuhakikisha anaondoka yeye, sio kumjengea hoja ambayo pengine yeye Rais anataka kuigawa Tanzania. Hizi ndizo Siasa za haki na kujenga na sii kubomoa.

Nguvu kubwa ya Chadema ingewekwa kwenye Upinzani wa itikadi, sera na sheria zinazowakwaza Watanzania ili ifikapo November, Chadema inajiweka katika.nafasi ya Ushindi lkn msikie vema Lissu ni ugonvi tu nani agombee Urais, nani awe Mwenyekiti nani Makamu na nafasi zote anataka yeye! Demokrasia ipi unayozungumzia?
 
Kwani hujui kuwa uchaguzi wa mwenyekiti CHADEMA ni mwaka huu?

Ulitaka wamuondoe mwenyekiti bila kufuata katiba kabla ya mwaka wa uchaguzi?

Katiba ya CHADEMA haina option ya recall.
Uchaguzi ungefanyika pasipo haya madudu ya kudhalilishana maana wote wako timu moja, sijui kama unanielewa? Hapakuwa na sababu wala haja ya Mimi kujua kinachoendelea huko Chadema. Aidha tungesikia wagombea kina nani kisha matokeo maana ni jambo lao - Upo?

Hata kama Mwenyekoti angekuwa Lissu halafu Mbowe akaibuka na hoja kama hizi na wapambe zake ningempinga na kuandika haya haya nayo andika leo. Wrong move is wrong haijalishi nani kafanya.

Leo hii mimi nasikia za ndaaani kabisa msemo wa Kadomomo. Hii ni vita vya ndani ya Chama kama ilivyokuwa kule NCCR na CUF inanipa hofu ya matokeo hili naliweka wazi na mtakuja nambia. Historia ipo wazi Yuko wapi Mbatia NCCR na Lipumba CUF leo hii wamebakia historia. Huko ndiko Chadema inakoelekea
 
Uchaguzi ungefanyika pasipo haya madudu ya kudhalilishana maana wote wako timu moja, sijui kama unanielewa? Hapakuwa na sababu wala haja ya Mimi kujua kinachoendelea huko Chadema. Aidha tungesikia wagombea kina nani kisha matokeo maana ni jambo lao - Upo?

Hata kama Mwenyekoti angekuwa Lissu halafu Mbowe akaibuka na hoja kama hizi na wapambe zake ningempinga na kuandika haya haya nayo andika leo. Wrong move is wrong haijalishi nani kafanya.

Leo hii mimi nasikia za ndaaani kabisa msemo wa Kadomomo. Hii ni vita vya ndani ya Chama kama ilivyokuwa kule NCCR na CUF inanipa hofu ya matokeo hili naliweka wazi na mtakuja nambia. Historia ipo wazi Yuko wapi Mbatia NCCR na Lipumba CUF leo hii wamebakia historia. Huko ndiko Chadema inakoelekea
Sehemu ya demokrasia ni uwazi, wanatekeleza jina la chama chao.

Tatizo ni uongo tu, kama jambo kweli uwazi si tatizo katika demokrasia.
 
Sehemu ya demokrasia ni uwazi, wanatekeleza jina la chama chao.

Tatizo ni uongo tu, kama jambo kweli uwazi si tatizo katika demokrasia.
Uwazi kwa wahusika tu, hata ukiwa na mkeo unafunga milango na madirisha, uwazi unabakia kwenu pekee 😁😁
 
Uwazi kwa wahusika tu, hata ukiwa na mkeo unafunga milango na madirisha, uwazi unabakia kwenu pekee 😁😁
Kama unaona habari hazikuhusu zipotezee tu. Hujalazimishwa kuzifuatilia.

Wanaoona zinawahusu watafuatilia.

Hizi ni habari za kuendesha chama cha kitaifa, si habari za mke na mume kulala.

You are comparing apples to oranges.
 
Back
Top Bottom