Nini hasa maana ya utu?

Nini hasa maana ya utu?

Najua kuna watu watataka kujua what is symbiosies, harmony and peace ila sitajibu. they too are things we can only define through their materialisation.

RR

Talking of materialisation !!! One is forced to ask what is materializing? UTU is a product of SOMETHING which has been there at the first place and then went some kind of process? I wish you could let me know what is that something ...AND as a Request ..Lol .. tuambie what is symbiosies and harmony! Which in your context still is the product of from materialisation of something! Alafau hiyo something amabyo hatimaye ndio ianjileza kama ... UTU ... Si ndio itakuwa msingi wa Definition ya UTU ..Hence ..Itawekwe kwenye katiba..
 
Mkuu hata tukitafakari utu kuwa kupitia matukio still bado tunaweza tusifikie the same conclusion. Kwa mfano, wako wataosema vitendo ya Osama Bin Laden vilikuwa sio vya kiutu. Lakini namini wapo watakaosema kuwa matendo yake yalikuwa na kiutu. Yalimtokea pia Mandela wakati wa ubaguzi wa rangi to the extent hata wakamwita ni gaidi. What might me a terrorist to one might be a freedom fighter to another. Hata tukichukua mfano wa juzi wa Gaddafi, bado tutatofautiana kama utu wake uliheshimiwa. Labda niseme kama ilivyo kwenye human rights, wapo wataokaosema vigezo vya utu ni universal wakati wengine watasema ni cultural relative?

Mkuu EMT

Bado nachelea kuudefine UTU! Ndio maana nimekubaliana na RR kuwa UTU NI UTU NA KILA MTU ANA WAKE!! Na kinachobakia NI KUUELELZA TU! Ila kitakacho amua kuwa Mtu kauleelza UTU ni watu wanaomzunguka ambao wanafaya Jamii yake. Kwa hiyo nakubalina kuwa watu wanaomzunguka meeleza Utu kwa kuwa nao wanatofautiana ..lazima kutakuwa na makubaliano tofauti ya kuwa hicho kilichoelezwa ni Utu au sio Utu na inapofikia hapo .. HOJA .. Hiyo tunaichia famili au Jamii husika!!
 
Mimi nakubali kuwa miongoni mwa hao waliokwisha kuupoteza utu wao wa asili; hivyo najipa haki ya kuuliza "utu ni nini?" @Azimio jipya

Na ikiwa utu wa taifa umeanza kupotea na wengi wanakufa wakiwa karibu na unyama kuliko utu, utamhukumu vipi mwenzio kwa kukosa utu?

Azimio jipya hebu nieleze kwa malezo mafupi

Utu ni nini? Unatokana na nini? na Unapimwaje?

Gaijin,

You know ..They are not that simple ...eh?

Soon am going to try get the answers for this as you know is the basis of this Thread..ingawa nafikiri umeshapata some of the answer kwa member wengine..but I will bring my version ...!

Na ninafikiri Kama anavyosema mara nyingi EMT ..kuwa ni sehemu muhimu sana inayokosekana kwenye katiba yetu!
 
Absolutely....ukimsoma mkuu EMT hapo juu anazungumzia kuwa kukua kwa "Utu"

Ukiniuliza mimi nitasema sio "kukua kwa Utu" ila "Kukua kwa Ufahamu wetu juu ya Utu wetu"....

Kwa nini nasema hivi? Hapa nitarudi kwa Mkuu Paulss anaposema "utu" wetu ni natural thing....Ulikuwepo na upo na utazidi kuwepo maadam mwanadamu anaendelea ku-exist, sema tu tatizo ni kuwa kuna mahali "TUNAPIGA UTASHI WETU KUFULI" na kuutupa utu wetu "hata mavumbini"

Mkuu Cathode Rays,

Lets face it ... ! Kwani what is the difference between UTU na UFAHAMU?
 
Mkuu RR hebu tendeeni haki hiki "KIGODA CHA UTU" kwa kukiweka kuwa Sticky thread ili iwasaidie hata wanaofanya review ya katiba wahakikishe angalau wanaweka tafsiri ya "utu" kwa lugha yetu kutusaidia hasa kwa kuzingatia mkuu Gaijin anapata tabu sana kukosekana kwenye tafsiri za sheria zetu na zaidi kwenye katiba
NI ombi

What a good name!!! ?? KIGODA CHA UTU...!!
AND As you can see the request has been Granted ..That is Thanks ..To RR!
 
Pasco said:
.......Utu wa mtu, hauna uhusiano na kitu, mtu muone kama mtu sio mpaka awe na kitu!.

Pasco naomba nitofautiane na wewe
Naona unaongelae nadharia au unaongea kama tunavyoambiwa hali ya mambo yatakavyokuwa kuwa huko mbinguni. Hapa duniani utu wa mtu unaweza kufungamanishwa vitu, tabia, mali, vyeo, jamii, dini,elimu, etc
  • Kinadharia utu wa mtazamaji na utu wa Riais kikwete au PM Pinda mbele ya jamii ni sawa lakini hapa duniani hali halisi ni tofauti
  • Kinadahria mmasai asili mwenye ng'ombe 3 na yule mwenye ng'ombe 50 ni sawa lakini kimila za kimasai kwa kigezo cha mifugo mmasai mwenye ng'ombe 70 mbele ya jamii ya kimasai atathaminiwa zaidi ya yule mwenye ng'ombe 3
  • Mtu asiye kuwa na dini na wenye dini utu wao unaakiwa uwa sawa akini jamii nyingi tunawaon watu wasiomani uwepo wa mungu kama hawana utu fulani na thamani ya utu wao kupungua. Wengine wanana jpo wanaamini mungu ile kuwa dini tofauti ni kigezo cha imani tu........
  • Wasuk-uma naambiwa kimila msichana mweupeposa yake ni kubwa zaidi kuliko yule mweusi. Unaweza ukaona hapo utu unathaminishwa wa vitu tofauti tofauti
  • Utaona kuna watu wanaheshimika na wanasiikilizwa (utu wao) sababu ya uzee wao na wengine wanadaharulika sababu ya ujana wao. Hivyo hivy ukija wenye mamb kama elimu jamii inaweza kuthaminisha utu wa mtu kulingana na elimu tu.
Ukitaka kuna complexity ya utu na defition zetu anagalia baadhi ya viongozi waliotumikia wakati wa nyerere . Wanachekwa kuwa hawana kitu. Utu wao unashushwa . Wakati huo huo sasa kuna kizazi cha viongozi wa sasa wananunua majumba UK, wanajilibiizia mali . Hatuwezi kusema hawa wana utu kuliko wale wanaochekwa kwa kutokuwa na kitu.

Kwa hiyo kuna mambo yapo yanafanya yawepo madaraja ya utu.Kuna mambo na mifumo yap mtazamaji hawezi kuwa na utu sawa na EMT au waziri XYZ mbele au machoni pa jamii.

Kwa hiyo ingekuwa utu haufungamani na vitu au mambo fulani tungepata jibu moja duniani ote kama lile jibu la 1+1=2
 
Mkuu Kahanga

Mada zilikuwa nzuri sana!

LAKINI: HIvi kulingana na Falsafa ya UTU ...kwa nini Ufisadi unachukuliwa kuwa SIO UTU!!

Katika mafundisho yetu ya falsafa ya UTU tunataja kwamba misingi ya utu ni[U.M.U.H.I.M.U.W.A.K.E.]
U
mojawapo katika kifupisho hicho inamaanisha Uadilifu. Fisadi si mwadilifu.

 
quote_icon.png
By Didia

Tunaweza kusema mtu kakosa "utu" kwa kufanya kitendo ambacho kwa hali ya kawaida binadamu aliye na akili timamu asingeweza kufanya. Tunaweza kulinganisha utu na kukosa huruma kwa binadamu wenzako kwa kufanya matendo yanayoweza tafsiriwa kuwa binadamu hapaswi kumtendea mwingine.

Kutafsiriwa na nani? Nani mwenye haki ya kutafsiri kwa niaba ya wengine?

Kesi ya Mbunge wa Arumeru VS wanajimbo inaonyesha dhahiri kuwa tafsiri zinatofautiana baina ya watu na watu. Wapo wanaotafsiri tendo moja kuwa ni la kiutu na tendo jengine ni la kukosa utu.

Nani tafsiri yake ndio inakubalika?
 
Kutafsiriwa na nani? Nani mwenye haki ya kutafsiri kwa niaba ya wengine?

Kesi ya Mbunge wa Arumeru VS wanajimbo inaonyesha dhahiri kuwa tafsiri zinatofautiana baina ya watu na watu. Wapo wanaotafsiri tendo moja kuwa ni la kiutu na tendo jengine ni la kukosa utu.

Nani tafsiri yake ndio inakubalika?

Wewe tafsiri yako ya 'utu' ni nini?
 
Katika mafundisho yetu ya falsafa ya UTU tunataja kwamba misingi ya utu ni[U.M.U.H.I.M.U.W.A.K.E.]
U
mojawapo katika kifupisho hicho inamaanisha Uadilifu. Fisadi si mwadilifu.

Katika mada ambayo inaendelea hapa kwa muda sasa, utaona hoja na michango mbalimbali imesha fanyika tayari. zaidi ya kwamba utaendeela kudadavua na kuweka in put yako ... utaona tuna utata mkubwa wa kukubalina wote (Universally) maana ya UTU! Mimi kwa sasa hilo niliache kwani nina hakika una mchango wako. Kwa sasa hebu tuangalie ....Hivi kwa nini tunafikiri uadilifu ni UTU?
 
Katika mada ambayo inaendelea hapa kwa muda sasa, utaona hoja na michango mbalimbali imesha fanyika tayari. zaidi ya kwamba utaendeela kudadavua na kuweka in put yako ... utaona tuna utata mkubwa wa kukubalina wote (Universally) maana ya UTU! Mimi kwa sasa hilo niliache kwani nina hakika una mchango wako. Kwa sasa hebu tuangalie ....Hivi kwa nini tunafikiri uadilifu ni UTU?
Mfano rahisi,
Rejea jinsi nafsi yako ilivyo na utambuzi wa jema na baya. Ukidondosha hela kwa bahati mbaya, mtu akaziokota akakuletea utajua kafanya jambo jema, lakini ukipita mtaa fulani, matharani kariakoo, mtu akakuchomolea hiyo hela mfukoni, unajua kafanya jambo baya. Alichochukua si chake, hajapewa, si halali yake n.k. Wawili hawa waweke katika mizani ya uadilifu na utu.
 
Asha dii unajaribu kusema nini dada yangu, bado sijakusoma uzuri


Paulss In brief nilikua na maanisha kua ni members tofauti wamechangia hapa kuelezea Utu na kila mmoja kaja na maana yake thou zooote zina msingi mmoja; kama vile ya Ubuntu, Desmond na Mandela zilivo tofauti yet similar...
 
Mkuu unajua ni kweli ni ngumu kupata tafsiri ya moja kwa moja ya maana ya hili neno (yaani universal definition and SI unit ya hili neno na likawa applicable kote). Nadhani ndiyo maana General Assembly ya UN kwenye ile UNIVERSAL DECLARATION OF HUMAN RIGHTS wamejaribu kuweka set of common standards values ambazo kimsingi kila mtu ana haki nazo ili kuondoa ule mkanganyiko wa tafsiri ya "yule ambae kwako ni gaidi, kwangu ni shujaa" ikiwamo na kuwepo kwa Mahakama ya Kimataifa (Japo hapa napo maswali ni mengi zaidi ya majibu

The question still is how common and standards are these "common standards of achivements" ???



Naomba jibu hapo toka kwa members for i am interested on how different or Similar itakua for most members hapo.... Hasa wewe mwenyewe Cathode Rays....
 
Wewe tafsiri yako ya 'utu' ni nini?


Nimesoma posts zoote, na I like the answers ya most hasa tokana na constructive questions za Gaijin,

@Gaijini hata mimi ningependa your Definition of Utu ....
 
Nimesoma posts zoote, na I like the answers ya most hasa tokana na constructive questions za Gaijin, hata mimi ningependa you your Definition of Utu Gaijini....

Aisee alter...hebu rekebisha kidogo hiyo sentensi ipate kusomeka vizuri..
 
Wewe tafsiri yako ya 'utu' ni nini?

@Gaijini hata mimi ningependa your Definition of Utu ....

Mimi sina tafsiri wala definition ya utu. Siijui. Na siondoi uwezekano wa kuwa huo utu wenyewe sina au ulishapotea kitambo.

Ninachosema mimi ni kuwa hakuna universal definition ya utu. Kila mtu anaejua tafsiri au definition ya utu, anayo yake kwa sababu ya athari ya vitu vilivyomzunguka katika maisha yake.

Chukulia mfano huu: Mnyama akiuguwa akawa anateseka na hakuna uwezekano wa kupona, ni utu kumuuwa haraka iwezekanavyo lakini tunaambiwa si utu kumuuwa binaadamu anaeteseka kwa maradhi licha ya kuwa hakuna uwezekano wa kupona. Tunaambiwa kuwa ni utu zaidi kumuacha akiteseka kwa vile utu wetu unataka tuweke matarajio kuwa atapona

Utu ni nini?



 
Back
Top Bottom