Nini kilikufanya ukaacha ajira ya serikalini ukaingia sekta binafsi?

Nini kilikufanya ukaacha ajira ya serikalini ukaingia sekta binafsi?

Macbook pro

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2020
Posts
722
Reaction score
1,030
Habari zenu ndugu zangu na wanajamvi letu pendwa la HHM.

Nimekuja kwenu tena kama mwanajamvi kujifunza kitu kutoka kwenu.

Kama utafuatilia hapo nyuma niliweka uzi wangu juu ya kukosa morali na mvuto na ajira yangu. Labda niweke hivi, Kabla sijaingia kwenye ajira nilikuwa na kibiashara changu ambacho kimenisaidia sana na mpaka ajira zinatoka kwamba nimepangiwa huku Mtwara nilikuwa nimeifikisha nyumba yangu katika hatua ya Mwisho kabisa. Na Biashara ipo bado inaendelea so mimi nikawa nimeiacha Biashara nikamwacha mdogo wangu wakisaidiana na mrs kusimamia biashara yetu. Yeye mdogo wangu huwa namlipa mshahara kama mfanyakazi maana natambua yeye sio mmiliki wa Biashara ila ni ndugu na anafanya vizuri.

Baada ya kuwa nimekuja huku kusema ukweli mipango yangu na mategemeo yangu yanaelekea kukwama. Suala la uhamisho ni ngoma nzito mana hizi Halmashauri hawapitishi uhamisho kama huna wa kubadilishana naye. Na sina connection ya simu moja ambayo inaweza kunisaidia kusukuma mchakato wa kuomba kuhama nirudi nikajumuike na familia. Nahisi kukata tamaa na kuchoka kuishi mbali na familia. Sokilicho tawala akili yangu ni mawazo ya kuachana na hii kazi nirudi nijumuike na familia yangu na nikaendelee kusimamia Biashara yangu na kuachana na ajira za utumishi.

Nataka kusikia kutoka kwenu, wale ambao mmewahi kuachana na ajira za serikali na kujitegemea au kufanya kazi kwenye mashirika binafsi, Ni nini ilikuwa sababu kubwa kwako hadi kuwaza kuondoka huko na nini ilikuwa changamoto baada ya wewe kuachana na ajira ya utumishi wa umma. Naomba tusaidiane mawazo.
 
Mimi bwana nilikua na mawazo ya kuajiriwa sana lakini baada ya kumaliza na kuangalia kozi niliyosoma nikaona tayari nimeingia cha kike hivyo nisifanye ujinga mwingine kwenda kujifunga kijijini nikaua ndoto zangu. Mwanzo mama yangu hakunielewa kabisa alitamani niombe kazi serikali na niajiriwe ila kwa sasa anaelewa nilichokua napigania.

Hivyo mkuu pima hasara na faida sio lazima wote tuingie serikalini hasa kwa wale wenye ndoto kubwa na wapambanaji.

NB:kama huna roho ngumu mtaani hakukufai nenda serikalini.
 
Mimi bwana nilikua na mawazo ya kuajiriwa sana lakini baada ya kumaliza na kuangalia kozi niliyosoma nikaona tayari nimeingia cha kike hivyo nisifanye ujinga mwingine kwenda kujifunga kijijini nikaua ndoto zangu. Mwanzo mama yangu hakunielewa kabisa alitamani niombe kazi serikali na niajiriwe ila kwa sasa anaelewa nilichokua napigania.

Hivyo mkuu pima hasara na faida sio lazima wote tuingie serikalini hasa kwa wale wenye ndoto kubwa na wapambanaji.

NB:kama huna roho ngumu mtaani hakukufai nenda serikalini.
Nashukuru umerudia kuisoma tena ikaeleweka.
 
Ujinga wako kivipi ? Kipi unakikosa kwenye sekta binafsi na kipi hasa hasa unajutia ?
Kule serikalini kuna likizo ya mwaka siku 28, na katika kila likizo za miaka miwili, mojawapo mtumishi analipwa nauli yake na ya familia yake pamoja na mizigo. Huku private sector havipatikani kwa utaratibu, inategemea na huruma ya Management.

Kule nilikuwa napata allowance za semina, wakati mwingine semina ya siku mbili inarefushwa hadi siku saba, ya siku saba inaenda siku 14. Hata kama ilikuwa inawezekana kufanyika ndani ya chumba kimojawapo ofisini, itapelekwa nje ya mkoa ili perdiem zisomeke sh. 150,000/= kila siku, local transport (taxi) 30,000/= kila siku na transport ya bus itategemea. Huku sector binafsi, semina ya siku tatu inafanyika kwa siku moja na hakuna malipo.

Kule nilikuwa naweza kuomba study leave na nikaendelea kulipwa kila kitu ikiwa pamoja na ada plus stipends, huku ukitaka kusoma uache kazi, au tafuta programme za nje ya muda wa kaxi kwa gharama zako.

Kule nikifiwa na mtoto au mzazi, nitapewa kila kitu cha mazishi ikiwa na usafiri wa Coaster iwapo nitahitaji kusafirisha popote. Huku nitatumiwa mjumbe asome salamu za rambirambi.

Kule nikipata mauti kwa ajali nikiwa kazini, njiani kwenda kazini au njiani kurudi kutoka kazini, basi familia yangu itaendelea kupata 70% ya mshahara niliokuwa ninaupata hadi siku ambayo ningestaafu kisheria. Huku familia itasomewa salamu za rambirambi na mwakilishi.

Kule nilikuwa napanda cheo kila baada ya miaka mitatu, na nyongeza ya mshahara ya mwaka. Huku hata cheo nilichopewa hakiko katika mfumo maalum
 
Kule serikalini kuna likizo ya mwaka siku 28, na katika kila likizo za miaka miwili, mojawapo mtumishi analipwa nauli yake na ya familia yake pamoja na mizigo. Huku private sector havipatikani kwa utaratibu, inategemea na huruma ya Management.

Kule nilikuwa napata allowance za semina, wakati mwingine semina ya siku mbili inarefushwa hadi siku saba, ya siku saba inaenda siku 14. Hata kama ilikuwa inawezekana kufanyika ndani ya chumba kimojawapo ofisini, itapelekwa nje ya mkoa ili perdiem zisomeke sh. 150,000/= kila siku, local transport (taxi) 30,000/= kila siku na transport ya bus itategemea. Huku sector binafsi, semina ya siku tatu inafanyika kwa siku moja na hakuna malipo.

Kule nilikuwa naweza kuomba study leave na nikaendelea kulipwa kila kitu ikiwa pamoja na ada plus stipends, huku ukitaka kusoma uache kazi, au tafuta programme za nje ya muda wa kaxi kwa gharama zako.

Kule nikifiwa na mtoto au mzazi, nitapewa kila kitu cha mazishi ikiwa na usafiri wa Coaster iwapo nitahitaji kusafirisha popote. Huku nitatumiwa mjumbe asome salamu za rambirambi.

Kule nikipata mauti kwa ajali nikiwa kazini, njiani kwenda kazini au njiani kurudi kutoka kazini, basi familia yangu itaendelea kupata 70% ya mshahara niliokuwa ninaupata hadi siku ambayo ningestaafu kisheria. Huku familia itasomewa salamu za rambirambi na mwakilishi.

Kule nilikuwa napanda cheo kila baada ya miaka mitatu, na nyongeza ya mshahara ya mwaka. Huku hata cheo nilichopewa hakiko katika mfumo maalum
A very detailed Response, Ahsante sana chief. Nimejifunza kitu ahsante mno kwa kutoa muda wako
 
Binafsi niliachana na kazi ya kuajiriwa baada ya kuchoka kuhama kila mradi mradi mpya unapoanza,boss anaweza jiskia kukuhamisha tu maksudi na hulipwi pesa ya usafiri..leo uko tabora baada ya mqaka upo Tanga hujasettlo vizuri upo singida..nkaona huu ujinga imetosha kujiajiri ..nitulie nifanya plan c d na e ..maisha yanasonga..nabiashara,nalima nafuga kwenye siasa pia nipo.nilijiuliza lini nitasettle na familia yangu?ntalipa kodi za nyumb mpk lini akati nimejenga?safari za kila mwezi kuona familia umri unaenda familia inaongezeka hivo..nkaachana na hizo mambo.
 
Back
Top Bottom