Nini kilimfanya Benjamin Mkapa ashindwe kuchapa Taazia ya muasisi wa TANU Abdul Sykes katika magazeti ya chama?

Nini kilimfanya Benjamin Mkapa ashindwe kuchapa Taazia ya muasisi wa TANU Abdul Sykes katika magazeti ya chama?

Of course hayawezi kuwa na maana kwako kwasababu hayalingani na lengo lako.
Haya ninayoandika yanamaana sana kwa wasomaji.

Nina uhakika Prof Shivji na Prof Saida, watakaa kitako kufikiri ikiwa kauli waliyosoma kwako kwamba Abdul alimpokea Nyerere ni upotofu . Sidhani kama wanaweza kusimama mahali na kuitetea!
Wewe unaweza kwasababu huna aibu, sijui kama wao wanaweza

Kwa Wanajamvi, hasa vijana haya yana maana sana kwao.
Kwanza , wanajifunza kusoma kwa kufikiri na kuunganisha mtiririko wa habari
Pili, inawakinga kumeza uongo bila makosa , kwamba, umri wao unatumika tu kuwa 'exploit'

Tatu, inasaidia pia 'wafuasi' wako wasome maandishi kwa uangalifu, kinyume chake wanaweza kuangukia pua
Sasa kama umeshindwa kuthibitisha uwepo wa katiba ya AA na TAA ya Abdul, wao wanaweza nini?

Muhimu zaidi ni kueleza jinsi Abdul Sykes alivyokuwa overrated na vitabu vyako katika jitihada za kumdunisha Nyerere. Kwa vigezo vyote Nyerere atabaki kuwa Nyerere na sifa zake na Abdul atabaki kuwa na sifa zake.
Huwezi kumfanya Abdul awe zaidi kwa kumnyanyasa au kumdhalilisha Nyerere

Nyerere anatetewa na historia, ambayo haiandikwi , kubumbwa au kufinyangwa. Ni historia inayojidhihiri kwa muda na matokeo. Ndiyo maana miaka 20 tangu afariki bado '' historia inamtetea'' akiwa amelala kaburini tuli

Kwamba alilishwa mayai kwa Sykes, na alivaa Kaptula au alipewa pesa za kununua ng'onda, au alikwenda sokoni na kikapu bila pesa, hayo hayaondoi ukweli mwingine wowote kuhusu aliyofanya katika kuongoza harakati za uhuru

Ni Nyerere aliyebadilisha siasa za barazani na kuzipeleka majimboni , Tanganyika na UN. Siyo Abdul Sykes
Tena tukichamba zaidi, kubwa la Abdul ni kuongoza genge la wahuni kwenda kutandika wazee wake ili achukue utawala wa baba yake. Hakuandika Katiba wala baba yake hakuandika. Hawakupeleka siasa mikoani zaidi ya Tandamti na Agrey.

Historia si hisia, tenzi au simulizi. Si mahoka au ngano, ni mtiririko wa matukio usiohitaji nakshi au uvumba.

Nawahi Magila, leo tunamuoza mtoto wa baba shangazi.
Nguruvi...
Unayoandika yana maana sana kwangu na nayasoma na nakujibu kwa adabu.

Nimekwambia unanifurahisha sana.

Hakika naamini watu wengi wanatusoma na wananufaika na majadiliano yetu.
 
Nguruvi...
Unayoandika yana maana sana kwangu na nayasoma na nakujibu kwa adabu.

Nimekwambia unanifurahisha sana.

Hakika naamini watu wengi wanatusoma na wananufaika na majadiliano yetu.

HISTORIA YA TANU KUTOKA NYARAKA ZA SYKES

KISA CHA ALLY SYKES, DENIS PHOMBEAH NA KENNETH KAUNDA TANGANYIKA NA MKUTANO WA WAPIGANIA UHURU KUSINI YA SAHARA 1953

SEHEMU YA KWANZA

Mwaka wa 1953 Harry Nkumbula alikuwa amechaguliwa rais wa African National Congress (ANC) na Kenneth Kaunda aliteuliwa Katibu Mwenezi wa Jimbo la Kaskazini, Northern Rhodesia sasa Zambia.

Mwezi Agosti Kaunda akawa Katibu Mkuu wa ANC. Haukupita muda Kaunda akaanza kupeleka barua Nairobi, Dar es Salaam na Johannesburg akiitikia rai ya Kenya African Union na chama cha African National Congresss (ANC) cha Afrika ya Kusini kualikwa vyama vya ukombozi kuja Lusaka kwenye mkutano wa vyama vya siasa vya wazalendo kutoka nchi zilizo Kusini mwa Sahara.

Hivi ndivyo ilivyokuwa kuwa ujumbe wa watu watatu wa TAA ukaalikwa na Kenneth Kaunda, kuhudhuria mkutano wa Pan African Congress (ANC) mjini Lusaka.

Mwezi wa Novemba, 1953 Ally Sykes alipokea barua kutoka kwa Kaunda akimwalika kuhudhuria mkutano huo.

Wakati ule ANC ilikuwa na manung'uniko kadhaa dhidi ya Waingereza na ilikuwa imeamua katika mapambamo yake kutumia njia za amani ambayo katika barua ambayo Kaunda alimpelekea Ally Sykes aliielezea njia hizo za amani kama hivi, ‘’Hutashirikiana na mtu yoyote katika shauri lolote litakalokuwa na madhara kwa maslahi ya Waafrika.’’

Waafrika nchini Rhodesia Kaskazini walikuwa wanapambana dhidi ya mfumo wa kura tatu ambao baadaye ulitwishwa Tanganyika na Gavana Edward Twining wa 1958.

Baadhi ya malalamiko ambayo Kaunda na ANC iliyoyaona kuwa ni madhara kwa maslahi ya Waafrika ilikuwa uendelezaji wa mashamba na nyumba za Wazungu katika nchi yao.

Lakini suala lililokuwa likiwashughulisha sana watu wengi lilikuwa ni ule msimamo dhidi ya muungano wa nchi yao yaani Northern Rhodesia na Southern Rhodesia.

Kaunda alikuwa akifanya mpango wa kuchukua hatua dhidi ya muungano huo kwa kuwaondosha wafanyakazi wa Kiafrika kutoka kwenye mashamba ya Wazungu na makandarasi wa ujenzi waliokuwa wakifanyakazi za ujenzi wa nyumba za walowezi.

Halikadhalika Kaunda alikuwa akifanya kampeni dhidi ya ubaguzi wa Waafrika.

Kaunda na chama cha ANC kilikuwa kinakusudia kuziunganisha jumuiya zote za Waafrika zilizokuwa zinapinga ukoloni na kuunda Baraza la Waafrika wote kwa ajili ya Afrika iliyo Kusini mwa Sahara ili kuwa na nguvu za umoja wa Waafrika.

Katika kutayarisha mkutano huo mkuu Kaunda alipanga kuvishirikisha Chuo Kikuu cha Makerere Uganda, Achimota Ghana, Fort Hare Afrika ya Kusini na baadhi ya vyuo vikuu nchini Uingereza, India na Marekani.

ANC ilikuwa na mpango wa kuyashughulikia maswala saba katika mkutano huo.

Katika kutayarisha mkutano ule Kaunda alifanya kazi na Rev. Michael Scott na pia alikuwa akitafuta msaada wa Canon Raven wa Maddingley Hall Cambridge na Arthur Lewis, mchumi kutoka Chuo Kikuu cha Manchester.

Baada ya kupokea mwaliko ule tarehe 12 Novemba, Ally Sykes alimwandikia barua Kaunda akimthibitishia kushiriki kwa chama Tanganyika African Governemt Servant Association (TAGSA) na TAA kwenye mkutano huo.

Denis Phombeah na Bhoke Munanka, katibu wa TAA Jimbo la Ziwa walikuwa walichaguliwa kuwa wawakilishi wa TAA.

Tarehe 1 Desemba, Alexander Tobias aliyekuwa katibu wa TAA alimwandikia barua Kamishina wa Kazi, G, A. Bennet akimuombea ruhusa Ally Sykes ahudhurie mkutano huo wa Lusaka.

Bhoke Munanka alinyimwa pasi ya kusafiria na serikali na kwa hivyo hakuweza kusafiri. Tarehe 10 Desemba, Ally Sykes na Phombeah baada ya kupewa ruhusa na serikali kuhudhuria mkutano huo waliondoka kwa ndege ya aina ya Dakota ya Central African Airways kwenda Lusaka kupitia Salisbury, Southern Rhodesia.

Ally na Phombeah walikuwa ndiyo Waafrika pekee ndani ya ndege hiyo.

Walikuwa wasimame Salisbury na kisha waondoke kwenda Lusaka siku iliyofuata.

Wazalendo hawa wawili wajumbe wa mkutano ule walikuwa wamepanga kufikia Ambassador Hotel, Salisbury, kwa usiku ule na hoteli ilikuwa imethibitisha kuwa imekwisha tayarisha malazi yao.


Image may contain: 2 people, people sitting, text that says 'LIFE'
 
"WE MZEE!" LUGHA YA DHARAU, KEJELI NA VITISHO

Baada ya uhuru zilipoanza kauli ya kukashifu TAA na yeye mwenyewe Abdul kuwa hakuwa anaongoza chama cha siasa bali chama cha starehe mmoja wa marafiki zake aliyekuwa anaumizwa na maneno yale alikuwa Ahmed Rashad Ali.

(In Shaa Allah nitaweka historia ya Ahmed Rashad hapa kwa faida yetu sote).

Ahmed Rashad akawa anamuomba Abdul aeleze historia ya TANU kuanzia jinsi baba yake alivyoanza harakati kupitia African Association mwaka wa 1929.

Abdul Sykes alikataa akimwambia kuwa kama tatizo ni nani kaunda TANU yeye hilo halimshughulishi na hakika Abdul hakufungua kinywa chake hadi anaingia kaburini.

(In Shaa Allah nitakuwekeeni hapa yale aliyoandika Daisy kuhusu vipi baba yake alikabiliana na fitna hii katika kipindi hiki).

Nilipokuwa nasafiri kuwatafuta hawa wazalendo ilikuwa tukimaliza mazungumzo nataka kunyanyuka kuondoka wananambia nisubiri tupige fatha, yaani tufanye dua.

Wakisema kuwa hili jambo nililokuwa nalifanya ni kubwa sana linahitaji msaada wa Allah.

Baadhi ya wazee hawa wengi walifariki kabla kitabu hakijatoka na wengine nilibahatika kuwapa nakala ya kitabu kwa mkono wangu ingawa kilikuwa kwa Kiingereza na wasingeweza kukisoma.

Moyoni walikuwa wanasononeka kuwa mchango wao katika kupigania uhuru haukuzaa matunda waliyotegemea.

Leo nafarajika ninaposoma jina la Abdul Sykes lililofutwa katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika lilivyorejea na sasa limekuwa maarufu watu wakibishana kuhusu yeye.

Kleist Sykes mtoto wa Abdul Sykes alikuja ofisini kwangu Tanga kunishukuru baada ya baba yake na baba yake mdogo Ally Sykes, kutunukiwa Medali ya Mwenge wa Uhuru kwa mchango wao katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Kleist alinipa mkono huku akibubujikwa na machozi.

Leo ninaposona lugha za "We mzee," lugha za dharau na kejeli na wakati mwingine vitisho dhidi yangu sikasiriki.

Wale wazee waasisi wa TANU walinambia hii kazi niliyoamua kufanya ni nzito.

Daisy anaeleza chokochoko zilizivyoanza karibu ya kupata uhuru na zikaendelea baada ya uhuru:

‘’...uhuru ulipokuwa dhahiri sasa unapatikana na ulipopatikana ulikuja na changamoto nyingi ambazo naamini baba hakuzitegemea.

Haitakuwa sawasawa ikiwa sitaeleza upeo wa juu wa baba yangu katika wema, huruma na unyofu aliokuwanao.

Hata nilipokuwa mtoto nilipata kushuhudia na kuona chokochoko na chuki dhidi yake bila shaka kwa ajili ya hasad kwani baba kwa kiwango chochote kile alikuwa mtu aliyefanikiwa na kwenye ngazi nyingi wengi hawakuthubutu hata kuota kukanyaga, lakini sikumuona baba kukasirika wala kutaka kulipiza kisasi.

Katika unyofu wa hali ya juu aliendelea na maisha yake...’’

Katika kipindi hiki Abdul Sykes alikuwa anatembelea Mercedes Benz 220 SE.

Kijana mwingine Dar es Salaam aliyekuwa na gari kama hii alikuwa kijana wa Kiarabu Abbas Abdulwahab.

Huenda maisha kama haya ndiyo yaliyosababisha hasad na wivu dhidi yake na Abdul alikuwa hata hajafikisha miaka 35.

Kuna msemo wa Kiarabu unaosema kuwa, ''Sababu huondoa ajabu.''

Jibu tunalo kwa nini magazeti TANU ya chama alichoasisi na kukifadhili kwa miaka mingi hayakuweza kumpa Abdul Sykes ile heshima ndogo aliyostahili katika umauti wake.

Kuchapa taazia yake ndani ya magazeti ya Uhuru na The Nationaist na kueleza yale aliyoyafanya kwa Nyerere na TANU wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika ilikuwa ni kumnyanyua juu katika sifa na heshima isiyo kifani.

Maadui wa Abdul Sykes walitaka jina lake lipotee kabisa katika ramani ya historia ya Tanzania.

Lakini Brendon Grimshaw alipochapa taazia ya Abdu Sykes katika Sunday News (20 October, 1968) kichwa cha taazia ile ilikuwa katika wino mweusi uliokoza: ''ABDUL SYKES WAS A TANU PIONEER.''

Hiyo picha ni siku watoto wa Abdul Sykes waliponiita nikaione Medali aliyotunukiwa baba yao (posthumous) katika kumbukumbu ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika.

Aliyevaa nguo nyekundu ni Daisy na kushoto wa kwanza ni Kleist.
Basi kijana unapoanza kuandika anza na introduction siyo unarukia katikati kama kila mtu anajua unachoandika ni nini.
 
Basi kijana unapoanza kuandika anza na introduction siyo unarukia katikati kama kila mtu anajua unachoandika ni nini.
Kiranga,
Mimi ni mtu mzima ujana nimepita miaka mingi nyuma.

Mjadala umetoka mbali bahati mbaya wewe umeukuta kati ndiyo maana unauliza utangulizi.
 
Kiranga,
Mimi ni mtu mzima ujana nimepita miaka mingi nyuma.

Mjadala umetoka mbali bahati mbaya wewe umeukuta kati ndiyo maana unauliza utangulizi.
Mimi naongelea bandiko lako la kwanza kwenye uzi huu.

Yani umeanza kuendesha gari mwanzo ghafla bin vuu spidi ya maili 120 kwa saa.

Unaandika ukiwa unakimbizwa?
 
Mimi naongelea bandiko lako la kwanza kwenye uzi huu.

Yani umeanza kuendesha gari mwanzo ghafla bin vuu spidi ya maili 120 kwa saa.

Unaandika ukiwa unakimbizwa?
Kiranga,
Mbona lugha kali?

Nifahamishe tu unachotaka kufahamu kwa taratibu In Sha Allah nitakueleza.
 
Ha ha ha.
Abdul Sykes anajulikana JF. Povu la nini sasa?
Hahaha...hicho mnakisoma na kukiamini ninyi huko misikitini, madrassat na kwenye mikutano yenu ya kidini

Ila LEGACY ya Mwl. J.K Nyerere haitofutika wala kufutwa asilani.

Huyo Abdul Sykes anajulikana JF tu kwa watu wachache, tena haaminiki.
 
Kiswahili hujui Madam.
Tatizo bibie una mdomo ningekufunza kiswahili.

Kufananiza ndio nini?

Wewe usiyejua kuandika kama Mtume wako Muhammad (S.A.W) ulipaswa ukajifinze kwanza kuandika vizuri kabla ya kuja kumtetea Muumin mwenzio
 
Yego...
Akiwa na ghadhabu mtu hawezi kufikiria vizuri.

Nyerere alikuwa Pugu akisomesha na alipelekwa na Joseph Kasella Bantu nyumbani kwa Abdu Sykes.

Mwalimu alipoacha kazi ndiyo akahamia Dar es Salaan na kupokelewa na Abdul Sykes.
Nilikuja hapa kucheka na kweli nimecheka sanaaa.
 
We mzee,
Baada ya kugundua hila ovu katika maandishi yako, nayapuuza. Huwa nakuja hapa kuwatahadharisha wasio tambua hila zako.
Hapo ulivyomuovu unasubiri kwa watu usiowapenda wafe uendelee na hila zako! Uombe mungu wako safari hii usife wewe kwanza!
Anachokitafuta siku zote bahati mbaya sana kiko mbele yake kwa mabilioni ya Miles!
 
M...
Zamani nikiandika tanzia. Abdilatif Abdallah mtaalamu wa Kiswahili akaniambia hicho ni Kiswahili cha bara.

Sisi watu wa pwani tunasema "taazia," kwa kuwa neno lenyewe asili yake ni Kiarabu.
Na ukaamua ukariri alivyokuelekeza hivyo au sio? Wazanzibar na hata vijana wengi wa wenye elimu ya dini hupenda kuongea , kuandika kiswahili kwa namna flani wao kuonekana waarabu! Inastaajbisha maneno ya kiarabu yaliyoletwa kuwa ya kiswahili hayo tayari yapo katika kiswahili na haina haja ya kuyatamka, ama kuyaandika kwa namna ya lafudhi za kiarabu. Utasikia
1. Nadhwifu badala ya nadhifu
2.taazia- Tanzia. nb
 
Na ukaamua ukariri alivyokuelekeza hivyo au sio? Wazanzibar na hata vijana wengi wa wenye elimu ya dini hupenda kuongea , kuandika kiswahili kwa namna flani wao kuonekana waarabu! Inastaajbisha maneno ya kiarabu yaliyoletwa kuwa ya kiswahili hayo tayari yapo katika kiswahili na haina haja ya kuyatamka, ama kuyaandika kwa namna ya lafudhi za kiarabu. Utasikia
1. Nadhwifu badala ya nadhifu
2.taazia- Tanzia. nb
Sela...
Naam.
 
KWA NINI BENJAMIN MKAPA ALISHINDWA KUCHAPA TAAZIA YA ABDUL SYKES KATIKA THE NATIONALIST BRENDON GRIMSHAW AKACHAPA "OBITUARY" YA ABDUL SYKES KATIKA SUNDAY NEWS (TANGANYIKA STANDARD)?

Mgogoro wa EAMWS nimeueleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Vyombo vilivyohusika katika mgogoro ule kuanzia gazeti la Uhuru na The Nationalist Mkapa akiwa Mhariri, Radio Tanzania Dar es Dalaam Martin Kiama akiwa Mkurugenzi, Polisi Geofrey Sawaya akihusika na Usalama wa Taifa alikuwapo Rashid Kayugwa.

Wote hawa walikuwa wakiamrishwa kutoka juu wengine wameyasema haya kwa kujuta kabla ya kufa kwao.

Hakika ni mkasa wa kusisimua.

Nataka nikupe mfano mmoja.

Kifo cha Abdul Sykes katikati ya mgogoro wa EAMWS maziko yake yalikuwa hayajapata kuonekana Dar es Salaam.

Mazishi yale yalikuwa habari kubwa kutokana na mchango wa Abdul Sykes katika TANU na uhuru wa Tanganyika achilia mbali kuwa yeye ndiye aliyempokea Nyerere Dar es Salaam namkuishinae nyumbani kwake Mtaa wa Aggery na Sikukuu.

Haya hakuna aliyekuwa hayajui haya na hii ndiyo ilikuwa sifa yake kubwa akitambulika kama mwezeshaji wa mambo yote ya TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Sasa jiulize vipi magazeti ya TANU chama alichounda Abdul yasimwandike inavyostahiki?

Mkapa kama mwandishi bila shaka alijua uzito wa stori iliyokuwa mbele yake na pengine kwa kufahamu uhusiano wa Abdul na Nyerere alimtaka Nyerere mwenyewe amwandikie rafiki yake taazia kwa mkono wake au amhoji (exclusive interview).

Yawezekana kuwa Mkapa aliyataka yote haya kwa Mwalimu na yeye akakataa?

Hapa ndipo panapoumiza kichwa.

Kuamini kuwa Mkapa kwa kutaka kwake tu aliamua kupuuza kifo cha Abdul Sykes huu ni muhali mkubwa sana.

Mwandishi mpumbavu peke yake.ndiye anaeweza kuchagua uamuzi wa kijinga kama huu.

Benjamin Mkapa hakuwa mtu zuzu.

Kama ulivyohitimisha kuwa Allah ni mjuzi wa siri na dhahiri nami nasema hivyo hivyo.

Yapo mengi Mkapa aliyafanya hata alivyokuwa rais lakini kwa hali ya siasa zetu Tanzania, alijikuta mikono yake imefungwa na si kufungwa tu bali imefungwa nyuma ya mgongo wake.

Hapo chini ni taazia ya Abdul Sykes katika Sunday News la 20 October, 1968.

Lakini taazia hii ilileta mgogoro mkubwa ofisi ya TANU New Street.

Kuna baadhi ya viongozi ndani ya TANU walikerwa na taazia hii.

Hapo chini kuna Kumbukumbu ya Abdul Sykes kama zilivyochapwa na magazeti ya Chama na Serikali Uhuru na Daily News ya tarehe 12 Oktoba 1988.

Kumbukumbu hizi nazo zikafikwa na mkasa pia.
Wahariri walitishika na waliyoyasoma wakasema hawatachapa hadi wamepata kibali kutoka Dodoma.

Walipopewa ruhusa ya kuchapa Kumbukumbu ya Abdul Sykes yale yote muhimu katika kumuelewa Abdul Sykes yaliondolewa.
Ilikuwaje ukashindwa kuuliza mhusika akiwepo?
 
Back
Top Bottom