Nini kilimfanya Benjamin Mkapa ashindwe kuchapa Taazia ya muasisi wa TANU Abdul Sykes katika magazeti ya chama?

Hata Yesu alilia na kulalamika msalabani:- Eloi Eloi lamasabchtan.

Yaani; Ewe Mungu, ewe Mungu mbona waniacha.

Kama Yesu pamoja na utukufu na ukubwa wake wote alimlilia Mungu, vipi mimi mtu hohehahe nishindwe kulia???!!!.
Mokaze,
Angalia hiyo hapo chini:

file:///C:/Users/Administrator/Pictures/KLEIST%20SYKES%20DICTIONARY%20OF%20AFRICAN%20BIOGRAPHY.pdf_RFd14c353.TMP
 
Kuna siku kuna mtu aliuliza kwa nini watu kama Maria Nyerere wasiulizwe kama kunakuwa na utata wa baadhi ya matukio? Hii mada ilisubiri mpaka watajwa wafe?
Siku akifa Maria Nyerere tena atawekewa maneno maneno mdomoni. Nafkiri kuna haja ya kuyaweka haya mambo bayana kabla baadhi ya watu hawajafa. Naona Mzee Saidi anakichaka cha kujificha kuendesha agenda zake.
 
Aende akawaulize wakiwa hai hataki anasubiri mpaka wafe,unfortunately siku wakitutoka Mzee Mwinyi au Dk Jakaya tuyategemee haya yakitokea laah haijawa hivi basi zitakuwa zimewabeba imani zao coz huyu ataandika anavyoandika but akiwa ni mrengo anaoamini yeye hutamuona akiwazungumzia vibaya wahusika kasheshe uwe upande wa pili basi utajuta.
 
James...
Kuna mambo inaelekea huyajui katika uandishi wa historia ya.TANU.

Mimi nimeanza kuandika historia hii kuanzia mwaka wa 1929.

Nyerere hayuko Dar es Salaam.

Nimemtia Abdul Sykes katika historia ya TANU 1942 wakati wa Vita Vya Pili Vya Dunia yuko Burma 6th Battalion na yuko Kalieni Camp Bombay mwaka wa 1945 baada ya vita kumalizika.

Abdul hajafahamiana na Nyerere.

Nimemtia Abdul katika historia ya TANU mwaka wa 1950 sasa yuko Dar es Salaam.

Nimewatia Abdul na Nyerere katika historia ya TANU mwaka wa 1952 baada ya hawa wawili kufahamiana.

Kama kuijua TANU basi Mwalimu hapa ndipo alipojua kuwa ipo mipango ya kuunda chama cha siasa.

Sasa mimi niwazulie watu maneno kwa kutafuta nini?

Haya yote yanafanyika babu ya na baba yangu wako Mtaa wa Kipata jirani na nyumba ya Kleist Sykes na baba yangu na Abdul wanasoma shule moja darasa moja Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Muslim School.

Wala simlazimishi yeyote kuamini niliyoandika katika kitabu cha Abdul Sykes.
 
I think, this is the agenda. MS hakuna anayebisha ushiriki wa mtu mmoja mmoja ktk Uhuru wa Tanganyika. Inshu kubwa hapa Nguruvi aliipambanua ni wewe kumpa jina baya Nyerere!
 
Sir...
Fanya staha.

Mama Maria hakuna haja ya kumuingiza katika kuitafuta historia ya TANU.

Ikiwa kama yeye mwenyewe anapenda kukumbuka historia ya siku za mwanzo walipofahamiana na Abdul Sykes, Mama Daisy, Bi. Chiku bint Said Kikusa na wanae Bi. Sakina na Bi. Fatna ataeleza.
 
I think, this is the agenda. MS hakuna anayebisha ushiriki wa mtu mmoja mmoja ktk Uhuru wa Tanganyika. Inshu kubwa hapa Nguruvi aliipambanua ni wewe kumpa jina baya Nyerere!
James...
Wahariri wasingethubutu kuniachia nimpe Nyerere, "jina baya."

Hiki kitabu walishakiona umuhimu wake, "as corrective history."

Kitabu kinasahihisha history ya uhuru wa Tangamyika kitasomwa na kufundishwa vyuo vikuu.

Kuandika upuuzi kitaua kitabu chao.
 
Asante.
Mzee Mohamedi niseme kwanza ni kweli mengi siyajui na kiukweli huwa ninajitajidi kufatilia maandiko yako humu. Lakini kuna vitu vinabangua bongo zangu. Nguruvi ameuliza juu ya kupokelewa Nyerere na Sykes ? Kuwa umempa jina baya Nyerere kwanini useme alipokelewa na Sykes wakati alifundisha Pugu siku nyingi ?

Hapa mtu anaweza kusema vile vile kama ulivyosema kwa Mkapa kuwa mwandishi nguli wa historian ya Tanganyika usingeweza kusahau taarifa muhimu kama hiyo juu ya rais wa kwanza wa Tanzania kwa kuwa wewe siyo zuzu.
Au kubali kuwa ulifanya kosa
 
James...
Mimi si mtu wa ubishi kwani ubishi haujengi mjadala bali unabomoa.

Hivi kwa nini wewe ushughulishwe na jambo la kupokelewa?

Kwani lina kipi kikubwa sana?

Kubwa kwa Nyerere wakati ule ni yeye kupelekwa na kujulishwa kwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na Abdul Sykes.

Hili ndilo kubwa katika historia ya Nyerere.
 
MS kama akibadilisha mrengo wa maandishi yake atapata recognition kubwa sana.... lakini kwasababu yuko kwenye mission ya kupush ajenda ngoja tuone ..... mi nashangaa kweli ilikuwaje tena Mkapa akaja kwenye ajenda hizi.... au ndio kutafuta uhalali wa ajenda zenyewe
 

Mwezi October 1999 nilikuwa Dubai na nikikaa Carlton Hotel.

Siku moja jioni simu yangu ikalia.

Walikuwa BBC London Idhaa ya Kiswahili wanataka kunihoji kuhusu Mwalimu Julius Nyerere ambae wakati ule alikuwa amelazwa St. Thomas Hospital, London.

Ulikuwa mwaka wa pili toka kitabu changu, ‘’The Life and Times of Abdulwaid Sykes (1924- 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika,’’ kichapwe na kitabu hiki kikawa kimenifanya nifahamike na sababu kubwa ni kuwa kilikuja na historia mpya ya yeye Mwalimu Nyerere mwenyewe, historia ya TANU na historia nzima ya kudai uhuru wa Tanganyika.

Kitabu kilimweeleza Mwalimu Nyerere kwa namna ambayo hakuna mwandishi alipatapo kufanya hivyo.

Hii nadhani ndiyo ikawa sababu ya BBC kutaka kunisikia nikimzungumza Mwalimu Nyerere.

BBC wakawa wanataka tuzungumze kidogo kuhusu Mwalimu na jinsi Watanzania walivyoathirika na ile hali ya Mwalimu kuwa kwenye matibabu Uingereza.

Katika kipindi kile cha maradhi ya Mwalimu akiwa hospitali kila siku habari ya hali yake ilikuwa inatolewa na kwa kweli sote tukifuatilia kwa karibu sana hadi pale alipofariki tarehe 14 Oktoba 1999.

Kishindo chake kilikuwa kikubwa hakijapatapo kutokea na mazishi ya Mwalimu hayapata kutokea halikadhalika simanzi iliyoonyeshwa na Watanzania haijapatapo kutokea.

Umma mkubwa usio na kifani ulijitokeza kupokea jeneza lake Uwanja wa Ndege na maelfu ya watu walijipanga pembeni ya barabara kutoa heshima zao wakati jeneza lake lilipokuwa linapita kuelekea nyumbani kwake Msasani.

Mimi nilikuwa Tanga nikifuatilia kwenye TV na binafsi fikra nyingi zilipita katika kichwa changu.

Mimi sikupata kujuana na Mwalimu lakini katika utafiti wangu wa maisha ya Abdul Sykes na harakati za uhuru nimemjua kwa karibu Mwalimu Nyerere kushinda wale waliokuja kuwa karibu na yeye baada ya uhuru.

Katika utafiti nimekutana na Mwalimu Nyerere ndani ya Nyaraka za Sykes na ndani ya nyaraka hizi nimesoma barua zake akiwa Rais wa TAA na kisha TANU katika miaka ya mwanzoni ya 1950, nimezungumza na Ally Sykes na Dossa Aziz na Mama Daisy (mke wa Abdul Sykes) watu waliokuwanae toka siku ya kwanza wanaanza mapambano ya kudai uhuru.

Katika mikoa ya Tanzania nilikokwenda kwa utafiti nimekutana na kuzungumza na watu waliokuwanae bega kwa bega katika siku hizo za mwanzo wakati Mwalimu Nyerere ndiyo anaanza harakati za kudai uhuru wa Tanganyika akiwa kijana wa miaka 30.

Wakati naangalia TV usiku mmoja wakionyesha ndege ya Air Tanzania Corporation (ATC) iliyokwenda kuchukua mwili wa Mwalimu Nyerere London camera ikapita kwa Abbas Sykes kwa haraka lakini nilimtambua bila wasiwasi wowote kuwa ndiye yeye.

Wakati ule yeye alikuwa ndiye Mwenyekiti wa ATC nafasi aliyoteuliwa na Rais Benjamin Mkapa.

Nilikuwa na kawaida kila nikija Dar es Salaam kutoka Tanga lazima nipite ofisini kwa Bwana Ally Sykes kumjulia hali kisha niende nyumbani kwa Balozi Abbas Sykes.

Safari hii nilikwenda kwa Balozi Sykes kwa nia khasa ya kutaka kujua safari yake ya London kwenda kuchukua mwili wa Mwalimu Nyerere.

Bwana Abbas tukiwa mimi nimekaa kwenye kiti changu ninachokipenda ndani ya ukumbi wake, kiti ambacho kinanipa mandhari ya mchanga mweupe wa bahari na bahari yenyewe na yeye kama kawaida amekaa kwenye kiti cha baba mwenye nyumba kwani huwa siku zote ndicho kiti chake nilianza mazungumzo kwa kumpa pole kwa msiba wa Mwalimu Nyerere.

Balozi Sykes akaitikia ile pole yangu kisha akasema, ‘’Unajua mimi kama Mwenyekiti wa ATC nilitiwa katika msafara wa kwenda kuuchukua mwili wa Nyerere.

Ingekuwa si hii nafasi yangu ya uenyekiti nisingepata fursa na heshima ile kwani hawa viongozi walioko madarakani hawajui kuwa Nyerere sisi ni ndugu yetu.’’

Nilijua bila ya kuuliza kuwa ile, ‘’sisi,’’ Balozi alikusudia wao Sykes Brothers.

Nilikuwa sijapatapo kumsikia Bwana Abbas akijinasibisha udugu na Nyerere.

Mara zote alipokuwa akieleza harakati za kudai uhuru alikuwa akimweleza Nyerere katika nafasi ya urafiki wake na kaka yake Abdul na kama kiongozi wa TANU, hili la udugu ndiyo siku ile nalisikia kwa mara ya kwanza.

‘’Mimi nimejaaliwa kumuona Nyerere siku ya kwanza kaja kwetu pale Mtaa wa Stanley na Sikukuu kaja kumuona Bwana Abdul akiwa kaongozana na Joseph Kasella Bantu na kuanzia hapo tukawa kama ndugu mama yake Bi. Mugaya akafahamiana na mama yetu na akawa anamtembelea mama nyumbani kwake pamoja na Sophia dada yake Nyerere.

Nikajuana na Joseph mdogo wake na Mama Maria Nyerere ambae alikuja kuwa shoga mkubwa wa Mama Daisy.’’

Bwana Abbas alipomaliza utangulizi huu na hapa alinistua kwani ingawa vifo siku zote vinatokea lakini huwa hatupendi kusikia vile vitu vya karibu vinavyomgusa maiti kama jeneza sanda na kadhalika.

Bwana Abbas akanieleza hali ilivyokuwa ndani ya ndege, ‘’Mohamed Nyerere nimejuananae kuanzia mwaka wa 1952 mimi kijana wa miaka 23 mdogo sana hata Bwana Abdul alikuwa mdogo kwa Nyerere.

Ndani ya ndege tuliweka sanduku lililokuwa na mwili wake mbele kabisa tumelifunika na bendera ya Tanzania.

Ilikuwa tabu sana kwangu kukwepa kulitazama sanduku lile lenye mwili wa Nyerere.

Kila mara fikra zinakwenda mbele na kurudi nyuma zinakwenda mbele zinarudi nyuma namkumbuka Nyerere kijana na Bwana Abdul kijana wote vijana wako pale nyumbani kipindi kile ameacha kazi na siku za mwanzo za TANU.

Endapo mtu angelinambia kwa wakati ule kuwa Nyerere atakuja kuwa kiongozi mkubwa barani Afrika ingekuwa tabu kwangu kuamini kuwa mambo yale waliyokuwa wanayanzungumza wakipanga na kupangua yatakuja kuwa makubwa kwa kiasi kile kilichofikia.

Nimekuwa na Nyerere kwingi Ulaya katika mikutano na nimeshuhudia kwa macho yangu viongozi wenzake na watu maarufu duniani wanavyokuwa wakiwa mbele yake.

Kwangu mimi ile ilikuwa historia inafunguka mbele ya macho yangu ya mtu niliyemuona akitembea kwa miguu mitaa ya Gerezani akiwa na mimi au na Bwana Abdul wakienda kumuona huyu au yule.
 
Matu...
Umeeleza sivyo ungeniuliza kama nimepata ''recognition,'' nikuambie kuwa sijapata ndiyo unipe ushauri uliokusudia.
''Recogntion,'' nimepata.

Mkapa kaingia kwa kuwa baada ya kufa Abdul Sykes kukawa katika duru za rafiki zake masikitiko jinsi magazeti ya TANU yalivyoshindwa kumuadhimisha Abdul Sykes.

Mhariri wa magazeti yake alikuwa Benjamin Mkapa kwa hiyo lawama zote zikaelekezwa kwake.

Ndipo katika kuandika taazia yake nikauliza vipi Mkapa alishindwa kuchapa taazia ya Abdul Sykes katika ''The Nationalist?''
 
Muheshimiwa una ujasiri mzuri wa kuhoji japo intention yako sijajua, isije kuwa ndio hidden agenda kama anayotuhumiwa Mohamed said ya kutetea dini yake "jambo ambalo sioni ubaya wake". Hivi kweli hushangazwi na ziada ya majibu ya bwana moh
 
Ni sawa na kuhoji kuonekana kwa Philip mangula majukwaani ili kuvunja hoja ya anae eleze umashuhuri wake kwenye siasa kwa miongo hii, kisha badae ukaja kuwapa mfano wa bashiru Ally kakulwa anavyo spit majukwaani
 
Muheshimiwa una ujasiri mzuri wa kuhoji japo intention yako sijajua, isije kuwa ndio hidden agenda kama anayotuhumiwa Mohamed said ya kutetea dini yake "jambo ambalo sioni ubaya wake". Hivi kweli hushangazwi na ziada ya majibu ya bwana moh
Mkwavingwa,
Tatizo ni kuwa namna yangu ya kujibu maswali ni kuongeza mengi ambayo wao hawayajui.

Hiki kitu kinawapa sana shida wangependa nijibu swali kwa namna ya wao majibu yangu tayari wanayo vichwani mwao.
 
Mokaze,
Angalia hiyo hapo chini:

file:///C:/Users/Administrator/Pictures/KLEIST%20SYKES%20DICTIONARY%20OF%20AFRICAN%20BIOGRAPHY.pdf_RFd14c353.TMP


Shukrani mkuu, lakini kwenye Cm yangu hiyo link haifunguki.
 
Mkwavingwa,
Tatizo ni kuwa namna yangu ya kujibu maswali ni kuongeza mengi ambayo wao hawayajui.

Hiki kitu kinawapa sana shida wangependa nijibu swali kwa namna ya wao majibu yangu tayari wanayo vichwani mwao.
Lakini naona ni prestige kwako kwani mijadala yako ni ya wazi na huwafokei kama namna ya wao wakufokeavyo kiasi unatambua kabisa wamekasilishwa either na ukweli au jingene
 
Mkwavingwa,
Tatizo ni kuwa namna yangu ya kujibu maswali ni kuongeza mengi ambayo wao hawayajui.

Hiki kitu kinawapa sana shida wangependa nijibu swali kwa namna ya wao majibu yangu tayari wanayo vichwani mwao.
Lakini naona ni prestige kwako kwani mijadala yako ni ya wazi na huwafokei kama namna ya wao wakufokeavyo kiasi unatambua kabisa wamekasilishwa either na ukweli au jingene
 
Lakini naona ni prestige kwako kwani mijadala yako ni ya wazi na huwafokei kama namna ya wao wakufokeavyo kiasi unatambua kabisa wamekasilishwa either na ukweli au jingene
Mkwaviga,
Tatizo ni hili.

Uhuru ulipokuwa unakaribia kupatikana baada ya Uchaguzi wa Kura Tatu mwaka wa 1958, waliingia katika TANU watu wengi wapya na katika hawa wako waliokuja kushika nafasi za uongozi katika chama na wengine kushika nafasi za juu katika serikali iliyokuwa inaongozwa na Nyerere.

Kundi hili halikuwa linajua historia ya TANU na lilianza kuwapiga vita wale waliowakuta katika chama.

Tatizo hapa ndipo lilipoanza.

TANU haikuwa tena inahitaji msaada ule uliokuwa ukipokea kwa watu kama Abdul, Dossa, Rupia na wengine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…