Nini kilimfanya Benjamin Mkapa ashindwe kuchapa Taazia ya muasisi wa TANU Abdul Sykes katika magazeti ya chama?

Nini kilimfanya Benjamin Mkapa ashindwe kuchapa Taazia ya muasisi wa TANU Abdul Sykes katika magazeti ya chama?

Ninachokiona kwenye uzi huu ni ubinafsi uliopitiliza. Pande zote hazitumii hoja bali ni hisia zimewatala. Kila mtu anataka kuona kile anachodhani ni ukweli kinawateka wasomaji. Hili si jambo zuri sana katika uanazuoni.
 
Sheikh Mohamed Said kwa faida ya vizazi vilivyozaliwa era ya mzee Mwinyi kupanda juu unaonaje ukawafanyia hisani ya kuweka kitabu cha kina Sykes na Historia ya TANU ktk PDF form ili wenye kupenda kuchimbua wapate mwanga halisi na kuepuka hii mikanganyiko isiyokua ya lazima ambayo wenye kuuibua ni wachanga wa historia? Asante
 
Sheikh Mohamed Said kwa faida ya vizazi vilivyozaliwa era ya mzee Mwinyi kupanda juu unaonaje ukawafanyia hisani ya kuweka kitabu cha kina Sykes na Historia ya TANU ktk PDF form ili wenye kupenda kuchimbua wapate mwanga halisi na kuepuka hii mikanganyiko isiyokua ya lazima ambayo wenye kuuibua ni wachanga wa historia? Asante
Horse...
Kitabu kimechapwa na publisher Minerva Press London (Kiingereza) na Phoenix Publishers Nairobi (Kiswahili)kwa nia ya kukiuza.

Hawezi wakakitoa bure kwa PDF.
 
Mtafiti...
Nimeandika historia ya wazee wangu katika kukabiliana na ukoloni.

Vyanzo vyangu katika mwanzo wa kuunda African Association ni mswada alioandika Kleist Sykes kabla hajafariki.

Mswada huu upo Maktaba ya Chuo Kikuu Chs Dar es Salaam East Africana na uliwasilishwa na Daisy Sykes mjukuu wa Kleist kama seminar paper mwaka wa 1968.

Seminar paper ikawa katika kitabu kilichohaririwa na John Iliffe, "Modern Tanzanians," mwaka wa 1973.

Pamoja na mswada huo nilifunguliwa Sykes Papers zenye historia ya TAA na TANU kuanzia miaka ya 1920 hadi uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961.

Pamoja na hao tena nilifanya mazungumzo marefu familia ya Sykes na wakanieleza yale waliyofanya wakati wa kuunda TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

Nilipita mikoani ambako nilizungumza na wazalendo waliokuwa hai na nilikusanya nyaraka na picha na kupata maelezo ya historia ya uhuru.
Ninachokiona kwenye uzi huu ni ubinafsi uliopitiliza. Pande zote hazitumii hoja bali ni hisia zimewatala. Kila mtu anataka kuona kile anachodhani ni ukweli kinawateka wasomaji. Hili si jambo zuri sana katika uanazuoni.
 
Ninachokiona kwenye uzi huu ni ubinafsi uliopitiliza. Pande zote hazitumii hoja bali ni hisia zimewatala. Kila mtu anataka kuona kile anachodhani ni ukweli kinawateka wasomaji. Hili si jambo zuri sana katika uanazuoni.
Umeshasoma mada ngapi za huyu Mzee? Nahisi humfahamu huyu mfia dini wa pwani
 
Hatuhitaji nyaraka za vikao au mialiko n.k

Tuletee nyaraka moja tu, Katiba. Iwe ya AA ya Kleist au TAA ya Abdul
Kama kuna kipande cha karatasi iwe robo au nusu tuwekee hapa

2. Tuonyeshe kiongozi mwingine wa siasa zaidi ya Mwl Nyerere aliyewahi kutangaza katiba achilia mbali kuwa nayo

3. Tuonyeshe ushiri wa Abdul kuandika katiba ya Seaton! kwa maana kama Abdul alikuwa na 'mkono' ukiachilia urafiki wake na Seaton katika chai na makaimati.

Hatuhitaji kitu kingine chochote kile, ni hayo matatu tu hapo juu
Unampa jukumu zito sana huyu Mzee na asiyoiweza, anachoweza ni kutunga stories za uongo na kupost humu.
 
Zamani nikiandika tanzia. Abdilatif Abdallah mtaalamu wa Kiswahili akaniambia hicho ni Kiswahili cha bara.

Sisi watu wa pwani tunasema "taazia," kwa kuwa neno lenyewe asili yake ni Kiarabu.

Kwahiyo wewe unaona Kiswahili cha bara ni haramu bali kile unachokiita cha Pwani, ilimradi kwa asili ni Kiarabu!!!
 
"Mohamed Said, post: 36271731, member: 12431"]
Nimeandika historia ya wazee wangu katika kukabiliana na ukoloni.
Wanajamvi, hapa MS anasema ameandika historia ya Wazee wake. Hilo si tatizo kabisa na ni haki yake na awaye akitaka naye pia atende.
Mohamed anasema hakuandika historia ya Watu wa Tanganyika, bali sehemu ya watu ambao ni wazee wake.
Pamoja na mswada huo nilifunguliwa Sykes Papers zenye historia ya TAA na TANU kuanzia miaka ya 1920 hadi uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961.
Sina shaka ulizisoma zote na hakuna mahali ulipata ushahidi wa uwepo wa katiba ya AA au TAA.

Je, kadi ya uanachama ya Kleist ya AA 1929 ilikuwa namba ngapi?
Je, kadi ya uanachama wa Abdul Sykes ya TAA ilikuwa namba ngapi?
Umetueleza kadi ya Abdul ya TANU ni Namba 3, Nyerere ni 1.
Pamoja na hao tena nilifanya mazungumzo marefu familia ya Sykes na wakanieleza yale waliyofanya wakati wa kuunda TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.
Jitihada za kum-sideline Nyerere zinaanza.
MS anaonyesha kuwa TANU iliundwa na Familia ya Sykes.
Ukweli ni kuwa TANU iliundwa na watu wengi akiwemo Nyerere.
Kama Nyerere hakuwepo Mohamed thibitisha

Lakini pia ni makosa kusema Familia ya Sykes iliyoingia nchini kama Mamluki wa kupigania na si kupinga ukoloni ilipigania Uhuru. Tunaweza kuona haya kwa ushahidi kuwa hakuna mahali popote Abdul Sykes au baba yake Kleist walikwenda mikoani kwa shughuli za siasa ukiacha Tandamti, Agrey , New street na kidongo chekundu.
Nilipita mikoani ambako nilizungumza na wazalendo waliokuwa hai na nilikusanya nyaraka na picha na kupata maelezo ya historia ya uhuru.
Well, nyaraka nyingi zinamusu Nyerere wakati akisambaza TANU.Huenda Mohamed ukawa na nyaraka za Kleist na Abdul Sykes mikoani, na hilo lingetufariji tukiziona
 
Wanajamvi, hapa MS anasema ameandika historia ya Wazee wake. Hilo si tatizo kabisa na ni haki yake na awaye akitaka naye pia atende.
Mohamed anasema hakuandika historia ya Watu wa Tanganyika, bali sehemu ya watu ambao ni wazee wake.
Sina shaka ulizisoma zote na hakuna mahali ulipata ushahidi wa uwepo wa katiba ya AA au TAA.

Je, kadi ya uanachama ya Kleist ya AA 1929 ilikuwa namba ngapi?
Je, kadi ya uanachama wa Abdul Sykes ya TAA ilikuwa namba ngapi?
Umetueleza kadi ya Abdul ya TANU ni Namba 3, Nyerere ni 1. Jitihada za kum-sideline Nyerere zinaanza.
MS anaonyesha kuwa TANU iliundwa na Familia ya Sykes.
Ukweli ni kuwa TANU iliundwa na watu wengi akiwemo Nyerere.
Kama Nyerere hakuwepo Mohamed thibitisha

Lakini pia ni makosa kusema Familia ya Sykes iliyoingia nchini kama Mamluki wa kupigania na si kupinga ukoloni ilipigania Uhuru. Tunaweza kuona haya kwa ushahidi kuwa hakuna mahali popote Abdul Sykes au baba yake Kleist walikwenda mikoani kwa shughuli za siasa ukiacha Tandamti, Agrey , New street na kidongo chekundu. Well, nyaraka nyingi zinamusu Nyerere wakati akisambaza TANU.Huenda Mohamed ukawa na nyaraka za Kleist na Abdul Sykes mikoani, na hilo lingetufariji tukiziona
Nguruvi...
Unanifurahisha sana kwa maswali yako kwa kweli unanifanyia ikhsani kubwa sana.

Ningeweza kukuwekea mengi hapa lakini natayarisha kipindi cha kesho asubuhi na nimeweka hapa tangazo.

Naingia break kwa muda In Shaa Allah kukuwekea haya:

Sijui kama umepatapo kusoma habari hizi hapo chini:

Mohamed Said: TANGANYIKA POLITICAL INTELLIGENCE SUMMARY, MARCH 1952

"Tanganyika Political Intelligence
Summary, March 1952":

"...it is reported that the Secretary of the Association, Abdul Wahid Sykes has
dispatched letters to all branches asking members for suggestions under
the following heads for a memorandum to be prepared for the Royal
Commission..."

“...Abdul Wahid Kleist Sykes, Secretary of the African Association who, as
reported in last month's summary (paragraph 20) was going on safari up
country, visited Mwanza, where he met Paul Bomani, President of the
Bukoba African Association, and accompanied him to Bukoba. Sykes then
visited Kampala alone.....on 8th March, a secret meeting was held, attended
by leading members of the Mwanza Branch...”

(Hizi ni taarifa kutoka Rhodes House Library, Oxford kutoka majalada ya
kikachero ya Waingereza baada ya miaka 50 yanawekwa wazi kwa mtafiti
yeyote kuyasoma na kufanya nakala akipenda).
 
Nguruvi...
Unanifurahisha sana kwa maswali yako kwa kweli unanifanyia ikhsani kubwa sana.

Ningeweza kukuwekea mengi hapa lakini natayarisha kipindi cha kesho asubuhi na nimeweka hapa tangazo.

Naingia break kwa muda In Shaa Allah kukuwekea haya:

Sijui kama umepatapo kusoma habari hizi hapo chini:

Mohamed Said: TANGANYIKA POLITICAL INTELLIGENCE SUMMARY, MARCH 1952

"Tanganyika Political Intelligence
Summary, March 1952":

"...it is reported that the Secretary of the Association, Abdul Wahid Sykes has
dispatched letters to all branches asking members for suggestions under
the following heads for a memorandum to be prepared for the Royal
Commission..."

“...Abdul Wahid Kleist Sykes, Secretary of the African Association who, as
reported in last month's summary (paragraph 20) was going on safari up
country, visited Mwanza, where he met Paul Bomani, President of the
Bukoba African Association, and accompanied him to Bukoba. Sykes then
visited Kampala alone.....on 8th March, a secret meeting was held, attended
by leading members of the Mwanza Branch...”

(Hizi ni taarifa kutoka Rhodes House Library, Oxford kutoka majalada ya
kikachero ya Waingereza baada ya miaka 50 yanawekwa wazi kwa mtafiti
yeyote kuyasoma na kufanya nakala akipenda).
Mimi ninapokushangaa ni pale unapoulizwa jambo halafu unajibu kitu kingine
Mara nyingi nimekuwa najiuliza, hivi unaelewa swali au huelewi au swali halieleweki?

Kusafiri si kufanya mkutano, mbona Abdul alikwenda Ukerewe kama unavyosema na sijawahi kukuuliza?

Pili, nimekuuliza katika mkabrasha ya AA kadi ya Kleist ilikuwa namba ngapi?
Tatu, katika TAA, kadi ya Abdul sykes ilikuwa namba ngapi?
Nne, Je, TANU ikiundwa Nyerere hakuwepo? Alipataje kadi namba 1 kwa chama kilichoundwa mwaka 1929?
 
hivi mwaks 1929 nyerere alikuwa na miaka mingapi?
 
Mimi ninapokushangaa ni pale unapoulizwa jambo halafu unajibu kitu kingine
Mara nyingi nimekuwa najiuliza, hivi unaelewa swali au huelewi au swali halieleweki?

Kusafiri si kufanya mkutano, mbona Abdul alikwenda Ukerewe kama unavyosema na sijawahi kukuuliza?

Pili, nimekuuliza katika mkabrasha ya AA kadi ya Kleist ilikuwa namba ngapi?
Tatu, katika TAA, kadi ya Abdul sykes ilikuwa namba ngapi?
Nne, Je, TANU ikiundwa Nyerere hakuwepo? Alipataje kadi namba 1 kwa chama kilichoundwa mwaka 1929?
Nguruvi...
Ahsante ndugu yangu.

Sote tunashangaana.

Katika kitabu "Ben Hur The Tale of the Christ" kilichoandikwa na Lew Wallace, Messala anamwambia Juda Ben Hur, "Nakuonya."

Ben Hur akamjibu, "Tunaonyana."

Unanishangaa mimi kuwa sijibu maswali yako wakati mimi najibu zaidi ya maswali yako.

Hizo nilizokuwekea ni taarifa za Special Branch.

Hizi taarifa ninazo kadhaa nimeletewa na vijana kutoka Ulaya na Marekani wanaokuja kunihoji kwa ajili ya thesis zao za Ph D na wao kwa kule sasa kumjua Abdul Sykes wamefanya utafiti zaidi juu yake.

Hayo niliyokuwekea hayamo katika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes.

Kwa upande wangu mimi pia hujiuliza kuhusu wewe kuwa hii ni hasad au kitu gani?

Ni hasad kwangu au kwa Abdul Sykes?

Ndipo nikauliza vipi mzalendo kama Abdul Sykes na yake yote yale akafutwa katika historia ya TANU?
 
hivi mwaks 1929 nyerere alikuwa na miaka mingapi?
Ofisa...
Hii Ofisa ni lakabu ya Rashid Sisso aliyopewa na Julius Nyerere wakati wa kupigania uhuru.

In Shaa Allah nikipata nafasi nitakuwekea hapa historia yake.

Alikuwa mtu muhimu sana katika propaganda.

Kujibu swali lako ni kuwa Nyerere alikuwa na miaka 7 Abdul 5.
 
Nguruvi...
Ahsante ndugu yangu.

Sote tunashangaana.

Katika kitabu "Ben Hur The Tale of the Christ" kilichoandikwa na Lew Wallace, Messala anamwambia Juda Ben Hur, "Nakuonya."

Ben Hur akamjibu, "Tunaonyana."

Unanishangaa mimi kuwa sijibu maswali yako wakati mimi najibu zaidi ya maswali yako.

Hizo nilizokuwekea ni taarifa za Special Branch.

Hizi taarifa ninazo kadhaa nimeletewa na vijana kutoka Ulaya na Marekani wanaokuja kunihoji kwa ajili ya thesis zao za Ph D na wao kwa kule sasa kumjua Abdul Sykes wamefanya utafiti zaidi juu yake.

Hayo niliyokuwekea hayamo katika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes.

Kwa upande wangu mimi pia hujiuliza kuhusu wewe kuwa hii ni hasad au kitu gani?

Ni hasad kwangu au kwa Abdul Sykes?

Ndipo nikauliza vipi mzalendo kama Abdul Sykes na yake yote yale akafutwa katika historia ya TANU?
MOHAMED NA MOHAMED SOMO NA SOMO: GUMZO LA MOHAMED GHASSANI

Huwezi kuchoka kumsoma wala huwezi kuchoka kumsikiliza Mohamed Ghassani.

Kipindi chake ''Gumzo la Mohamed Ghassani'' kina wafuatiliaji wengi wakimsikiliza akieleza historia yetu kwa mtazamo tofauti kabisa wa ule uliozoeleka wa kuisomesha historia kutokana na historia rasmi.

Fuatilia ukurasa huu usikilize mahojiano aliyonifanyia somo yangu akitaka nimueleze chimbuko la siasa za ukombozi wa Tanganyika kama mimi nilivyopokea kutoka kwa wazee wangu walioishi Dar es Salaam ya karne ya 19 na kutoka katika tafiti nilizofanya.

Somo yangu ametaka nimrudishe nyuma sana karne ya 19 nimueleze historia ya wazalendo wa nyakati hizo ambao alama zao tunaweza kuziona hivi leo karne ya 21 sasa zaidi ya miaka 100.

Nimemchagulia somo yangu Kleist Abdallah Sykes ambae alizaliwa karne ya 19, yeye mwenyewe kaacha mswada alioandika kabla ya kufariki katika karne ya 20.

Karne ya 20 mwaka wa 1968 Kleist Sykes alikuwa tayari yuko ndani ya Maktaba ya University of East Africa, East Africana akisomwa ndani ya Seminar Paper Idara ya Historia iliyoandikwa na mjukuu wake Aisha ''Daisy'' Sykes na mwaka wa 1973 alikuwa ndani ya kitabu alichohariri John Iliffe, ''Modern Tanzanians.''

Karne ya 21 mradi wa Harvard na Oxford University Press wa kuandika wasifu wa watu mashuhuri Afrika walimtia katika kamusi maarufu kwa jina la Dictionary of African Biography (DAB) ( 2011) yenye volume 6.

Usikose In Shaa Allah kupita hapa kuangalia kipindi hicho.
 
"Mohamed Said, post: 36275788, member: 12431"]
Unanishangaa mimi kuwa sijibu maswali yako wakati mimi najibu zaidi ya maswali yako.
Mohamed ukiulizwa kitu unajibu ulichoulizwa. Nadhani hili halina shida labda kama tunalifanya shida bila sababu

Ukiniuliza, Abdul Sykes alikuwa mtoto wa Kleist? Jibu langu ni ndiyo au hapana kutegemeana
Ukiniuliza Sheikh Chambera anafahamiana na Abdul Sykes? Nitakujibu sijui au najua abcd

Nitakuwa wa ajabu kidogo ukiniuliza habari za Sheikh Chambera na Abdul halafu nikakuletea maelezo mengi na marefu ya uhusiano wa Chambera na Nyerere na alivyokwenda Lindi baada ya mwaliko.

Umeona kwanini ninashangaa?
Hizo nilizokuwekea ni taarifa za Special Branch.
Mfano mzuri huu hapa. Mimi sijahoji source ya taarifa zako na kwamba zimepatikana wapi.
Nilichokihoji ni kitu kimoja, niwapi na ni lini Abdul Sykes alihutubia mkutano nje ya Tandamti na Kipata? Sijauliza aliwahi kusafiri kwenda wapi kumbuka hilo

Nikauliza, kadi ya Kleist Sykes ya AA ilikuwa namba ngapi? Sijauliza special branch wanasemaje
Nikauliza kadi ya Abdul Sykes ya TAA ilikuwa namba ngapi? Sijauliza special branch wanasemaje

Nimeuliza haya kwasababu wewe umebahatika kusoma makabrasha kwa mujibu wako.

Halafu nikauliza, kama TANU iliundwa 1929 na Familia ya Sykes na nadhani Nyerere alikuwa na miaka 7 Butiama, iweje basi kadi yake ya TANU iwe namba 1 na Abdul Namba 3.
Hizi taarifa ninazo kadhaa nimeletewa na vijana kutoka Ulaya na Marekani wanaokuja kunihoji kwa ajili ya thesis zao za Ph D na wao kwa kule sasa kumjua Abdul Sykes wamefanya utafiti zaidi juu yake.
Sawa sawa wanatoka Ulaya, sisi ni wa hapa nyumbani na unaweza kuwatumia kutusaidia ndio maana tunahitaji ufahamu.
Kutokujua haijawa dhambi au kosa lakini kutotaka kujua au kujua kwa kububusa ni hatari kuliko kutojua.
Tuache ya Ulaya tuendelee na mnakasha
Hayo niliyokuwekea hayamo katika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes.
Hakuna aliyeyahitaji.
Kwa upande wangu mimi pia hujiuliza kuhusu wewe kuwa hii ni hasad au kitu gani?
Hapana sina husda kabisa na sina sababu za kuwa na husda, nina sababu za kukemea husda
Ni hasad kwangu au kwa Abdul Sykes?
Hapana si kwenu, ni mnakasha tu. Sifa moja ya usomi ni uvumilivu wa kazi unazofanya. ukishajipambanua kama mwana historia basi daraja lako ni la juu, lakini pia daraja hilo haliji bila chujio.

Na si wote tunaoweza kumeza bila kutafuna, la hasha! si wote tunaovumilia kusikia mpapai unazaa maembe. Tutauliza, umepandikizwa ? na kwa njia gani maana chungwa na limao ni ndugu!
Ndipo nikauliza vipi mzalendo kama Abdul Sykes na yake yote yale akafutwa katika historia ya TANU?
Hapana usiwe na shaka hawezi kufutwa, mbona umejitahidi kumdunisha na kumdhalilisha Nyerere lakini kila siku anazungumzwa? Hata wangeungana woote wa Mzimama kila mmoja ana nafasi yake, na hili la husda dhidi ya Mwalimu linakera. Najiuliza hivi husda dhidi ya Nyerere ni kwa lipi?

Hii mada si ya Mkapa, Marehemu ametumika kama daraja.

mlengwa hapa ni mzee mla Mayai kwa Sykes, Mwl Nyerere! Kambarage anayekwenda sokoni bila pesa
 
Mohamed ukiulizwa kitu unajibu ulichoulizwa. Nadhani hili halina shida labda kama tunalifanya shida bila sababu

Ukiniuliza, Abdul Sykes alikuwa mtoto wa Kleist? Jibu langu ni ndiyo au hapana kutegemeana
Ukiniuliza Sheikh Chambera anafahamiana na Abdul Sykes? Nitakujibu sijui au najua abcd

Nitakuwa wa ajabu kidogo ukiniuliza habari za Sheikh Chambera na Abdul halafu nikakuletea maelezo mengi na marefu ya uhusiano wa Chambera na Nyerere na alivyokwenda Lindi baada ya mwaliko.

Umeona kwanini ninashangaa? Mfano mzuri huu hapa. Mimi sijahoji source ya taarifa zako na kwamba zimepatikana wapi.
Nilichokihoji ni kitu kimoja, niwapi na ni lini Abdul Sykes alihutubia mkutano nje ya Tandamti na Kipata? Sijauliza aliwahi kusafiri kwenda wapi kumbuka hilo

Nikauliza, kadi ya Kleist Sykes ya AA ilikuwa namba ngapi? Sijauliza special branch wanasemaje
Nikauliza kadi ya Abdul Sykes ya TAA ilikuwa namba ngapi? Sijauliza special branch wanasemaje

Nimeuliza haya kwasababu wewe umebahatika kusoma makabrasha kwa mujibu wako.

Halafu nikauliza, kama TANU iliundwa 1929 na Familia ya Sykes na nadhani Nyerere alikuwa na miaka 7 Butiama, iweje basi kadi yake ya TANU iwe namba 1 na Abdul Namba 3.Sawa sawa wanatoka Ulaya, sisi ni wa hapa nyumbani na unaweza kuwatumia kutusaidia ndio maana tunahitaji ufahamu.
Kutokujua haijawa dhambi au kosa lakini kutotaka kujua au kujua kwa kububusa ni hatari kuliko kutojua.
Tuache ya Ulaya tuendelee na mnakashaHakuna aliyeyahitaji.Hapana sina husda kabisa na sina sababu za kuwa na husda, nina sababu za kukemea husdaHapana si kwenu, ni mnakasha tu. Sifa moja ya usomi ni uvumilivu wa kazi unazofanya. ukishajipambanua kama mwana historia basi daraja lako ni la juu, lakini pia daraja hilo haliji bila chujio.

Na si wote tunaoweza kumeza bila kutafuna, la hasha! si wote tunaovumilia kusikia mpapai unazaa maembe. Tutauliza, umepandikizwa ? na kwa njia gani maana chungwa na limao ni ndugu! Hapana usiwe na shaka hawezi kufutwa, mbona umejitahidi kumdunisha na kumdhalilisha Nyerere lakini kila siku anazungumzwa? Hata wangeungana woote wa Mzimama kila mmoja ana nafasi yake, na hili la husda dhidi ya Mwalimu linakera. Najiuliza hivi husda dhidi ya Nyerere ni kwa lipi?

Hii mada si ya Mkapa, Marehemu ametumika kama daraja.

mlengwa hapa ni mzee mla Mayai kwa Sykes, Mwl Nyerere! Kambarage anayekwenda sokoni bila pesa
Nguruvi..
Huyo ndiyo Abdul Sykes...

Kadri itakavyokuwa.

Ukimfuta kwenye historia ya TANU unafuta historia kubwa katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kivukoni wamejaribu na matokeo yake ndiyo haya.
 
Back
Top Bottom