Nini kilimuua Mehmed II aliyetaka kuufuta ukristo/dola ya kirumi ulaya ??

Nini kilimuua Mehmed II aliyetaka kuufuta ukristo/dola ya kirumi ulaya ??

zitto junior

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2013
Posts
20,537
Reaction score
31,729
unnamed (1).jpg
images (12).jpg
Habari za mchana wakuu kama kichwa cha thread kinavyosema kwenye historia ya ulaya na kiislam kulikuwa na mfalme wa Ottoman empire dola ya kiislam hii iliyovamia ulaya kutokea mashariki ya kati na asia kwa sababu za kupanua utawala wao na dini pia.

Katika miaka ya 1400 walifanikiwa kuikamata constantinople iliyokuwa makao makuu ya byanztium empire ambayo ilikuwa ndio tawi la Dola ya kirumi mashariki ya ulaya na ilikuwa chini ya wakristo ila Mehmed II alifanikiwa kukamata mji huu na kufuta ukristo na kuifanya dini ya kiislam kushamiri mpaka leo yaani uturuki ya sasa na nchi za jirani.

Sasa baada ya kumalizana na tawi hili la mashariki Mehmed II hapo kati aliteka miji mingi tu ya ulaya ila mwishoni kabisa alielekea kuvamia makao makuu ya dola ya kirumi yani Rome ili kuitawala na penginepo kufuta ukristo ulaya nzima maana kama makao makuu ya wakatoliki wakisilimu je nchi gani ya ulaya ingebaki na ukristo??

Alianzia mji wa Otranto hapo italia kwa kuwavamia na kutaka wasilimu walivyogoma alichinja mji mzima na alikuwa amepanga sasa kuelekea Roma na alikua ameagiza majeshi zaidi yatiririke ili kufanikisha adhma yake.... ila usiku mmoja kabla ya kuanza vita ya kuelekea Roma alifariki ghafla na hivyo mpango huo ukafia naye na tokea hapo hakuwahi patikana mtawala wa ottoman mwenye dhamira na uwezo wa kuvamia Roma tena.

Sasa wajuvi wa mambo naomba mtujuze je nini hasa kilimuua Mehmed II aka Mehmet the conqueror shujaa huyu wa kiislam je aliwekewa sumu?? Alisalitiwa?? Aliuawa na wakatoliki ?? Na kivipi jemedari huyu masaa machache kabla ya tukio la kihistoria afariki ghafla maana wajuzi wa mambo wanasema kma sio kifo chake leo hii ulaya nzima ingekuwa imesilimu

Naomba kuwasilisha

Cc Palantir Malcom Lumumba Eiyer MSEZA MKULU na wanajukwaa wote

NB: Mods naomba uzi huu msiufute maana huwa mnazimoderate then mnazifuta hii inavunja moyo sana watu kuanzisha thread za kufikirisha jukwaa hili maana wanatumia muda kutafiti alafu tafiti zao zinaishia kutupwa kapuni.....
 
Hongera kwa kuanzisha uzi murua kabisa.

Hemed II kimsingi aliugua na kufariki dunia mwaka 1481 akiwa katika kampeni ya kivita huko Italy, japo mpango ulikuwa pia kuikamata Misri.

Ugonjwa uliomuua mpaka leo haujafahamika.
Lakini kabla ya mauti yake alikuwa mtu anayesumbuliwa sana na magonjwa ya viungo kwa muda mrefu hali iliyopelekea mpaka mguu wake mmoja kuharibika kabisa(kuwa deformed), pia alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa gout.

Siku mbili kabla ya kifo chake aliugua ugonjwa wa tumbo na hakuweza kabisa kutokea kwenye ukaguzi wa vikosi vyake kama ilivyo ada ya wababe wa kivita kwa wakati huo.

Lakini taarifa za siri kutoka Ottoman Empire zinasema aliwekewa sumu na mtoto wake wa kwanza ambaye alikuwa pia mrithi wake mtarajiwa aliyejulikana kwa jina la Bayezid kwa sababu ya uchu wa madaraka.

Ikumbukwe kuwa Hemed II alikuwa na miaka 49 tu wakati mauti inampata, kwa picha hio ina maana kuwa alikuwa bado na safari ndefu sana ya kutawala, almost miaka 40 mbele, kitu ambacho dogo aliona kama "kinamchelewesha", ikabidi amuwahishe baba mapema.
 
Hongera kwa kuanzisha uzi murua kabisa.

Hemed II kimsingi aliugua mwaka 1481 akiwa katika kampeni yake huko Italy, japo mpango ulikuwa pia kuikamata Misri.
Ugonjwa uliomuua mpaka leo haujafahamika.

Lakini taarifa za siri kutoka Ottoman Empire zinasema aliwekewa sumu na mtoto wake wa kwanza ambaye alikuwa pia mrithi wake mtarajiwa aliyejulikana kwa jina la Bayezid kwa sababu ya uchu wa madaraka.

Ikumbukwe kuwa Hemed II alikuwa na miaka 49 tu wakati mauti inampata, kwa picha hio ina maana kuwa alikuwa bado na safari ndefu sana ya kutawala, almost miaka 40 mbele, kitu ambacho dogo aliona kama "kinamchelewesha", ikabidi amuwahishe baba mapema.
mkuu habari...nimepndezwa mnooo na hili jibu lako "" lakini kwann usianzie mwanzo ili tusiomfahamu vyema huyo Jamaa kabla yakuja kuingia Roma hayo madaraka yake aliyatoa wapi na aliyapata vipi ...yaani tupate full package ya maisha ya huyo mtu ""
maana sisi wengine hatumjui ati
 
Mtu aliekuwa anachinja watu ili wafuate dini yake... Nilazima tu alimuudhi Mungu wa kweli! Alilaaniwa kilichomuua ni laana tu!
Ila mkuu haya mambo sio ya kuangalia upande mmoja hata hao wakatoliki walivamia nchi za ulaya mashariki kama poland hungary na bulgaria wakiwataka wabatizwe waliokataa walichinjwa hiyo ni miaka ya 1000 hivi hivyo miaka zamani dini zote zilitumia mbinu hii

Ila huyu kidogo ilishtua wengi maana alifariki masaa machache kabla hajaenda kufuta dola ya kirumi ndio maana nimekuja kuuliza huku tupate habari za chini ya kapeti isije kuwa alipigwa kipapai na papa
 
Hongera kwa kuanzisha uzi murua kabisa.

Hemed II kimsingi aliugua na kufariki dunia mwaka 1481 akiwa katika kampeni ya kivita huko Italy, japo mpango ulikuwa pia kuikamata Misri.

Ugonjwa uliomuua mpaka leo haujafahamika.
Lakini kabla ya mauti yake alikuwa mtu anayesumbuliwa sana na magonjwa ya viungo kwa muda mrefu hali iliyopelekea mpaka mguu wake mmoja kuharibika kabisa(kuwa deformed), pia alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa gout.

Siku mbili kabla ya kifo chake aliugua ugonjwa wa tumbo na hakuweza kabisa kutokea kwenye ukaguzi wa vikosi vyake kama ilivyo ada ya wababe wa kivita kwa wakati huo.

Lakini taarifa za siri kutoka Ottoman Empire zinasema aliwekewa sumu na mtoto wake wa kwanza ambaye alikuwa pia mrithi wake mtarajiwa aliyejulikana kwa jina la Bayezid kwa sababu ya uchu wa madaraka.

Ikumbukwe kuwa Hemed II alikuwa na miaka 49 tu wakati mauti inampata, kwa picha hio ina maana kuwa alikuwa bado na safari ndefu sana ya kutawala, almost miaka 40 mbele, kitu ambacho dogo aliona kama "kinamchelewesha", ikabidi amuwahishe baba mapema.
Duh naweza kukubaliana na jibu lako hili lakini je kwanini iwe wakati wa kwenda kuifuta Roma?? Kwanini kijana asingesubiri baba yake amalize ulaya nzima ili hata akija kutawala asipate upinzani kipindi akipata madaraka ?
 
Duh naweza kukubaliana na jibu lako hili lakini je kwanini iwe wakati wa kwenda kuifuta Roma?? Kwanini kijana asingesubiri baba yake amalize ulaya nzima ili hata akija kutawala asipate upinzani kipindi akipata madaraka ?
Kuna kitu inaitwa ambition mkuu, kumbuka Hemmed alichukua madaraka akiwa na umri wa miaka 21 tu na akawa tishio kubwa sana.

Aliuwawa wakati akiwa Roma si kwa sababu ya conspiracy yoyote toka kwa wazungu wa Ulaya ila ilikuwa ni "inside job".
Tayari kulikuwa na internal conflict kubwa sana ndani ya familia yake, hasa baada ya jamaa kupenda kuoa wake kutoka Ulaya na kuzaa watoto machotara.

Wahafidhina ndani ya utawala wake hii hawakulipenda.

Baada ya kifo chake wazungu walishangilia sana maana walikuwa washakata tamaa ya kumshinda huyu jamaa, kitu kilichofanya siku taarifa ya msiba wake imeingia Ulaya misa zilifanyika "kujipongeza" na "Kumshukuru" Mungu kwa kuwaondolea adui yao namba moja.
 
Kuna kitu inaitwa ambition mkuu, kumbuka Hemmed alichukua madaraka akiwa na umri wa miaka 21 tu na akawa tishio kubwa sana.

Aliuwawa wakati akiwa Roma si kwa sababu ya conspiracy yoyote toka kwa wazungu wa Ulaya ila ilikuwa ni "inside job".
Tayari kulikuwa na interbal conflict kubwa sana ndani ya familia yake, hasa baada ya jamaa kupenda kuoa wake kutoka Ulaya na kuzaa watoto machotara.

Wahafhinina ndani ya utawala wake hii hawakuipenda.

Baada ya kifo chake wazungu waishangilia sana maana walikuwa washakata tamaa ya kumshinda huyu jamaa, kitu kilichofanya siku taarifa ya msiba wake imeingia Ulaya misa zilifanyika "kujipongeza" na "Kumshukuru" Mungu kwa kuwaondolea adui ya namba moja.
Na najiuliza kwanini tokea hapo hakutokea mfalme mwingine wa ottoman aliyekuwa na nia ya dhati ya kuvamia Roma..... Nini kilikuwa kikwazo
 
Back
Top Bottom