Nini kimeiua CHADEMA? Walikosea wapi? Vyama vingine vya upinzani vijifunze kuepuka kibri cha kupendwa

Nini kimeiua CHADEMA? Walikosea wapi? Vyama vingine vya upinzani vijifunze kuepuka kibri cha kupendwa

Hao unaosema wamekuwa na mgombea mmoja wamebadilisha wenyeviti mara nne ndani ya miaka 20. Vyama vya upinzani vipo na watu walewale, Mbatia, Lipumba, Mbowe, Mrema nk nk. Wenyeviti wa vyama vya siasa vya upinzani ni madikteta wakubwa. Bahati mbaya wafuasi wao wamejaa mahaba kiasi kwamba hawaoni udikteta huo. Lazima kuwe na ukomo wa mtu kuongoza, tofauti na hapo ni kuanzisha mazalia ya madikteta.

Mbona unajicontradict. Unasema wafuasi wao wana mahaba ya kutaka waongoze. Hivi kuna ubaya gani wafuasi na wanachama wa upinzani wakimpenda mwenyekiti wao na kutaka aongoze.

Hao CCM unaowasema, huwa wanachaguliwa kwa mahaba au itifaki. Yani ukishakuwa rais lazima uwe mwenyekiti wa CCM wanakupenda au hawakupendi. Sasa kwa upinzani ni tofauti, wanachama wakikupenda unachaguliwa tu.

Udikteta upo CCM ambapo Rais Anakuwa Mwenyekiti bila kushindanishwa na yeyote. Na kura inapigwa kiitifaki maafisa usalama wakiwa wamejaa kwenye mkutano.
 
Mali

Nimekuambia umma ni jumla ya jamii yote, lakini wanachama ni specific. Ndio maana mambo ya CCM yanawahusu wanachama wa CCM pekee. Sasa kulazimisha maamuzi ya CHADEMA kuwa ya watanzania wote unakosea sana. Wanaotakiwa kulalamika ni wanachama wa chadema sio wengine.

Zitto yupi? Huyu aliye ambulia kura za urais elfu tisini nch nzima mwaka 2015? Kipindi hicho ACT ipo hot kabisa. Mwaka 2020 wakashindwa hata kumcontrol mgombea wao wa urais?. Kama Zitto kashindwa kukiamsha chama kipya kama ACT angeweza kwa CHADEMA?. Yupo wapi msando, Dr Kitila, Pamba, et al?. Wote walirudi CCM. Sasa jiulize walitaka kuiongoza chadema kwanini kama ACT iliwashinda.
ACT ni chama kipya hauwezi tegemea kiwe na nguvu kama CDM hata kama Zitto ni nguli wa siasa.

Kila mtu ana haki ya kulalamikia utendaji wa chombo cha wengi kama chama cha siasa. Hata dini zikitenda ndivyo sivyo zitalalamikiwa na waumini wao na wasio waumini wao.

Hao wamerudi CCM baada ya kuona chama kinachojiita cha demokrasia hakina demokrasia yoyote ndani yake. Kupitia udikteta mwenyekiti alimpitisha Lowassa kugombea mwaka 2015. Mtu mwenye akili na anayesimamia principle hawezi kaa kwenye taasisi ya namna hiyo.
 
ACT ni chama kipya hauwezi tegemea kiwe na nguvu kama CDM hata kama Zitto ni nguli wa siasa.

Kila mtu ana haki ya kulalamikia utendaji wa chombo cha wengi kama chama cha siasa. Hata dini zikitenda ndivyo sivyo zitalalamikiwa na waumini wao na wasio waumini wao.

Hao wamerudi CCM baada ya kuona chama kinachojiita cha demokrasia hakina demokrasia yoyote ndani yake. Kupitia udikteta mwenyekiti alimpitisha Lowassa kugombea mwaka 2015. Mtu mwenye akili na anayesimamia principle hawezi kaa kwenye taasisi ya namna hiyo.

Labda umesahau nikukumbushe mambo mawili, hao akina kitila, mwigamba, msando, Anna mghwira et al, walihamia CCM wakitokea ACT sio CHADEMA usipotoshe.

Pia, nikukumbushe jambo moja, kwanini Lowassa alipewa kugombea urais chadema. Mpango ulikuwa Lipumba, Dr Kulangwa wa NCCR na Dr Slaa wakae pamoja wakubaliane nani agombee urais. Wakashindwa kukubaliana kwenye vikao vyote kila mtu akitaka awe mgombea.

Sasa Chadema walipoamua kumpitisha slaa, siku waliyopanga kumtangaza Slaa akagoma akasema anatakiwa kutangazwa kwa tukio kubwa. Sasa baada ya kuona mbwembwe ni nyingi ndio likatokea suala la Lowassa, . Lowassa ilikuwa last resort na Dr Slaa hakuwa na nguvu ya kupambana na Magufuli.
 
Mbona unajicontradict. Unasema wafuasi wao wana mahaba ya kutaka waongoze. Hivi kuna ubaya gani wafuasi na wanachama wa upinzani wakimpenda mwenyekiti wao na kutaka aongoze.

Hao CCM unaowasema, huwa wanachaguliwa kwa mahaba au itifaki. Yani ukishakuwa rais lazima uwe mwenyekiti wa CCM wanakupenda au hawakupendi. Sasa kwa upinzani ni tofauti, wanachama wakikupenda unachaguliwa tu.

Udikteta upo CCM ambapo Rais Anakuwa Mwenyekiti bila kushindanishwa na yeyote. Na kura inapigwa kiitifaki maafisa usalama wakiwa wamejaa kwenye mkutano.
Madikteta wote husema kuwa wanaongoza kwa mandate ya watu. Hukuna dikteta atakayekuambia kuwa anaforce kuongoza. Na vibaraka wa madikteta nao hutoa hizi kauli,
"Hivi kuna ubaya gani wafuasi na wanachama wa upinzani wakimpenda mwenyekiti wao na kutaka aongoze."
Hata Idi Amin alisema anaongoza kwa matakwa ya watu na anapendwa na watu. Hata Nyerere angeamua ile 1985 achaguliwe aendelee na urais angechaguliwa na kuendelea. Lakini aliamua kutoka na kuweka ukomo, kitu ambacho hawa madikteta kwenye vyama vya siasa hawataki kabisa.

Huko unakosema kuna udikteta wanabadilisha wenyeviti wa chama kila miaka kumi.
 
Kuna wengi sn wanaweza kufikiria nini kilisababisha anguko la Chadema wapo wachambuzi wengi wa masuala ya siasa wanaweza Kuja kuelezea mengi Sana yaliyosababisha anguko la kilichokuwa chama kikuu cha upinzani zifuatazo ni baadhi ya hoja zinazotoa ushahidi juu ya kiini cha anguko la Chadema

Udikteta: Pamoja na kujitabanaisha kama chama kikuu cha upinzani lakini Chadema kilikumbwa na tafsiri batili ya Jina na matendo yake, Chama cha kidemokrasia kinachoendeshwa kidikteta kwa kung'ang'aniwa na mtu mmoja kukiongoza kwa muda mrefu na kukifanya chama kama Mali binafsi ya Familia kwa mfano Mbowe amekuwepo madarakani toka enzi za Mzee mkapa, mkapa aliondoka akamuacha Mbowe kama mwenyekiti baadaye akaja kikwete akamuacha Mbowe kama mwenyekiti

akaja Magufuli akamuacha Mbowe kama mwenyekiti na sasa ni Samia, kwa lugha nyingine ni kwamba CCM imepata wenyeviti wanne tofauti lkn Chadema kikiwa na mwenyekiti mmoja tu naye ni Freeman Alkael Mbowe

Ni kosa kubwa sana kuruhusu mawazo ya mtu mmoja anayekosea Mara kwa Mara kutowajibika pale anaposhindwa
uchaguzi wa Mwaka 2005 ulitosha kabisa kumuondosha Mbowe kama mwenyekiti wa Chadema

Lakini ameng'ang'ania madaraka tu utazani kupe na hatimaye America chama kwa kunyonya damu yote

Mbowe Hana Mamlaka ya kudai katiba mpya kwa sababu yeye mwenyewe ni mvurugaji namba moja wa katiba ndani ya chama chake

tutaendelea kujadili udikteta kama kigezo cha anguko la Chadema namba 2

Nimechy, eti CDM imekufa. Haya ndio matamanio ya kila mwanaccm. Siku 2 tatu CDM wakianza mambo yao utasikia vilio vya wanaccm kuwa CDM wanaharibu amani ya nchi. Na ikifika uchaguzi CCM ndio wanageuka vituko kwa kupora chaguzi kwa mbeleko ya vyombo vya dola.
 
Madikteta wote husema kuwa wanaongoza kwa mandate ya watu. Hukuna dikteta atakayekuambia kuwa anaforce kuongoza. Na vibaraka wa madikteta nao hutoa hizi kauli,

Hata Idi Amin alisema anaongoza kwa matakwa ya watu na anapendwa na watu. Hata Nyerere angeamua ile 1985 achaguliwe aendelee na urais angechaguliwa na kuendelea. Lakini aliamua kutoka na kuweka ukomo, kitu ambacho hawa madikteta kwenye vyama vya siasa hawataki kabisa.

Huko unakosema kuna udikteta wanabadilisha wenyeviti wa chama kila

Dikteta ina apply kwenye nchi kwa sababu una kamata dola yote na kuwabagua usiowataka. Lakini kwenye vyama huwezi fanya hivyo maana hakuna dola na wananchama wana uhuru wa kuhama ukizingua. Udikteta ni kuagiza undercover kumlima risasi mbunge kwenye makazi yake.
 
Madikteta wote husema kuwa wanaongoza kwa mandate ya watu. Hukuna dikteta atakayekuambia kuwa anaforce kuongoza. Na vibaraka wa madikteta nao hutoa hizi kauli,

Hata Idi Amin alisema anaongoza kwa matakwa ya watu na anapendwa na watu. Hata Nyerere angeamua ile 1985 achaguliwe aendelee na urais angechaguliwa na kuendelea. Lakini aliamua kutoka na kuweka ukomo, kitu ambacho hawa madikteta kwenye vyama vya siasa hawataki kabisa.

Huko unakosema kuna udikteta wanabadilisha wenyeviti wa chama kila miaka kumi.

Mbona unatoa mifano ya marais wa nchi? Wakati wewe unalalamikia viongozi wa chama?. Hakuna udikteta kwenye level ya vyama , udikteta upo kwenye level za nchi.
 
Walivyo na mihemko kama wajumbe wa VICOBA vya uswahilini sijui kama mtaelewana😂😂😂😂

Ukimgusa tu mtu wa chama hicho anapayuka kama yuko kwenye sinagogi:
 
Walivyo na mihemko kama wajumbe wa VICOBA vya uswahilini sijui kama mtaelewana😂😂😂😂

Ukimgusa tu mtu wa chama hicho anapayuka kama yuko kwenye sinagogi:

Chadema imetabiriwa kufa tangu 2019 mpaka leo waliotaka kuiua wanakufa wao wanaiacha.
 
Madikteta wote husema kuwa wanaongoza kwa mandate ya watu. Hukuna dikteta atakayekuambia kuwa anaforce kuongoza. Na vibaraka wa madikteta nao hutoa hizi kauli,

Hata Idi Amin alisema anaongoza kwa matakwa ya watu na anapendwa na watu. Hata Nyerere angeamua ile 1985 achaguliwe aendelee na urais angechaguliwa na kuendelea. Lakini aliamua kutoka na kuweka ukomo, kitu ambacho hawa madikteta kwenye vyama vya siasa hawataki kabisa.

Huko unakosema kuna udikteta wanabadilisha wenyeviti wa chama kila miaka kumi.

Huwezi kuwa dictator bila nguvu ya vyombo vya dola. Inaonekana ww ni bendera fuata upepo na huu uzi umeshakuzidi pumzi, hivyo unarukia kila neno unalosikia ili ujiokoe.
 
Labda umesahau nikukumbushe mambo mawili, hao akina kitila, mwigamba, msando, Anna mghwira et al, walihamia CCM wakitokea ACT sio CHADEMA usipotoshe.

Pia, nikukumbushe jambo moja, kwanini Lowassa alipewa kugombea urais chadema. Mpango ulikuwa Lipumba, Dr Kulangwa wa NCCR na Dr Slaa wakae pamoja wakubaliane nani agombee urais. Wakashindwa kukubaliana kwenye vikao vyote kila mtu akitaka awe mgombea.

Sasa Chadema walipoamua kumpitisha slaa, siku waliyopanga kumtangaza Slaa akagoma akasema anatakiwa kutangazwa kwa tukio kubwa. Sasa baada ya kuona mbwembwe ni nyingi ndio likatokea suala la Lowassa, . Lowassa ilikuwa last resort na Dr Slaa hakuwa na nguvu ya kupambana na Magufuli.
Huko ni safari ya kisiasa, kwanini wakina Msando walitoka CDM kwanza. Tuangalie kiini. Na hiyo habari ya Slaa kugoma sababu ya kutaka mbwembwe nyingi ni porojo tu zisizoingia akilini mwa mtu mwenye akili timamu. Na hata kama angetaka mbwembwe nyingi, ilishindikana vipi? Upitishwaji wa Lowassa ulikuwa wa kidikteta usiofuata misingi. ndiyo uliowakimbiza Slaa chamani, na hilo linaingia akilini.
 
Chadema imetabiriwa kufa tangu 2019 mpaka leo waliotaka kuiua wanakufa wao wanaiacha.
Kumbe bado iko hai? Sasa walivyokua wanalilia uhuru wa kutoa maoni, walivyokua wanalalamika demokrasia hamna mbona saizi uhuru wanao na hali ni mbaya zaidi ila siwaskii wakisema. Ufisadi umezidi, maisha yamepanda bei, tozo kila kona ila yameufyata.

So shida yao ilikua uhuru wa kuzungumzia nini haswa? Au uhuru wa kutukana rais! How pathetic
 
Chadema kama Mandonga tu maneno mengi utadhani wako serious hawana wanachogambania kama Mandonga yeye mechi za kirafiki tu hawana sera wanafuata trending kama Mandonga tu anaalikwa kupigana kama sherehe ya harusi tu. Miaka yote hiyo mpaka leo hujui wanasimamia nini tofauti na CCM.

Hoja yako hapa ni ipi, ni CDM au Mandonga?
 
Huwezi kuwa dictator bila nguvu ya vyombo vya dola. Inaonekana ww ni bendera fuata upepo na huu uzi umeshakuzidi pumzi, hivyo unarukia kila neno unalosikia ili ujiokoe.
Kuwa dikteta chamani huhitaji vyombo vya dola. Unahitaji vibaraka, ulaghai na kuhonga vyeo au pesa. na nikuambie tu, nguvu ya madikteta wote duniani haipo kwenye vyombo vya dola, ipo kwa vibaraka.
 
Kumbe bado iko hai? Sasa walivyokua wanalilia uhuru wa kutoa maoni, walivyokua wanalalamika demokrasia hamna mbona saizi uhuru wanao na hali ni mbaya zaidi ila siwaskii wakisema. Ufisadi umezidi, maisha yamepanda bei, tozo kila kona ila yameufyata.

So shida yao ilikua uhuru wa kuzungumzia nini haswa? Au uhuru wa kutukana rais! How pathetic

Kupanda kwa bei unasubiri CDM wakusemee, sema ww maana hakuna aliyekuzuia. Au umekaa mahali unasubiri kusemewa na wengine?
 
Mbona unatoa mifano ya marais wa nchi? Wakati wewe unalalamikia viongozi wa chama?. Hakuna udikteta kwenye level ya vyama , udikteta upo kwenye level za nchi.
Nakupa 101 za Udikteta. Udikteta si kwa nchi tu, unaweza tokea ndani ya taasisi yoyote ile. Kama unadhani udikteta ni mpaka aufanye urais bado huijui siasa, na ndiyo maana unatetea udikteta wa wazi.
 
Kuwa dikteta chamani huhitaji vyombo vya dola. Unahitaji vibaraka, ulaghai na kuhonga vyeo au pesa. na nikuambie tu, nguvu ya madikteta wote duniani haipo kwenye vyombo vya dola, ipo kwa vibaraka.

Udictator ni matumizi ya nguvu, na sio ulaghai au kuwa na wapambe. Unapokuwa bendera fuata upepo hizi ndio huwa hoja.
 
Back
Top Bottom