Nini kimeiua CHADEMA? Walikosea wapi? Vyama vingine vya upinzani vijifunze kuepuka kibri cha kupendwa

Nini kimeiua CHADEMA? Walikosea wapi? Vyama vingine vya upinzani vijifunze kuepuka kibri cha kupendwa

Tofautisha chama kushika madaraka na mtu mmoja kushika madaraka. Na chama cha siasa ni taasisi ya umma, huwezi sema ifanye inachotaka kwa sababu hakipo bungeni na serikalini. Unafiki mkubwa ni kudhani kuwa udikteta ni mbaya ukifanywa na wengine, ila mzuri tukifanya sisi.

Chama sio mali ya umma acha uongo, chama ni mali ya wanachama. Wanachama ndio huamua chama kiendeje.

Unafiki ni kutetea CCM kukaa madarakani kwa muda wote huo kupitia wizi wa tume ya mahera lakini kukasirika wanachama wa Chadema kuchaguwa mwenyekiti wao kwa muda.

Hiyo ni mbinu pia ya kupambana na mitego ya ccm . Ona kundi la Zitto lililotaka kuiongoza CHADEMA kipindi hicho lipo wapi? Wote wanerudi CCM. Hivi unadhani Zitto angechaguliwa mwenyekiti wa chadema kipindi kile mambo yangekuwaje?
 
Tatizo Tz hamna upinzani uliosimama haswa watu wanaona bora tu wawaachie tu ma ccm yani upinzani uliponichosha haswa ni pale wlipomuachia Lowassa agombee, yani mnamuingiza tena adui na kumpa cheo aisee [emoji23][emoji23] ila tukiongea ukweli Nan wa upinzani anafaa kupewa nchi??? Wote hawana misimamo
Mi pale ndio nikavua gwanda na zote nikazigawa. Nikaona kwa sasa nitakuwa naangalia mtu mwenye uwezo na maono nitamsapoti. Awe wa ccm, CUF, ACT, CHAUMA au Chadema.

Na nikapata nafasi nzuri ya kumsapoti Magu na sio CCM.

Kwa sasa nipo nipo tu. Sisapoti yoyote na sijajua kama 2025 nitapiga kura.
 
Nani kataka kumaliza upinzani? Usije kuwa wewe unajiita upinzani ndiye hutaki kusikia upinzani, maana hutaki kusikia kuwa
vyama vya upinzani ni vya kihuni na kidikteta.

Vyama vya upinzani vilimfanyia nani udikteta?. Kwenye kugombea uenyekiti wagombea ni zaidi ya mmoja na kwenye kugombea urais mgombea ni zaidi ya mmoja, shida ipo wapi?

Kwa CCM mgombea uenyekiti ni mmoja tu na hakuna mwingine na kwenye awamu ya pili mgombea urais ni mmoja tu. Membe alitaka kugombea urais akanyofolewa uanachama.

Anza kwanza na CCM ndio uje upinzani. Ndoa yako kila siku magomvi, ila kutwa kusema ndoa za wengine.
 
Yaani wewe ni [emoji706][emoji706][emoji706]sana. Mtu anapiga risasi wapinzani na kuwafunga jela, anapiga marufuku mikutano ya kisiasa halaf unasema chadema imekufa! Idiot!
Ukitaka maendeleo ya kweli hakikisha umenyamazisha wapinzani wako.

Wapinzani wapo kwa ajili ya kupewa asali tena kila wanapotaka. Siku ukiwanyima wanakuchafua na watasema ulikuwaga unawapa asali kuwafunga mdomo.
 
Chadema bado kipo sana na kitaendelea kuwepo.
The funny shit ni kwamba aliyetumia nguvu nyingi na kila ya recourses kukiua amekufa yeye na Chadema kiko hai.

Mkuu ili jambo watu wengi wanajifanya kulipotezea, ila kuna fundisho nyuma yake. Mimi nilimchukia magufuli moja kwa moja baada ya ule uchaguzi wa 2020.

Nchi zingine ubunge wanawaachia wananchi waamue kwenye urais ndio wanaiba. Yeye kaiba kila kitu kuanzia uwenyeviti, udiwani ,ubunge na urais. Lakini akafa ndani ya miezi minne baada ya wizi
 
Kwanini mnakuwa na hasira hebu weka point tano tu kwanini niwachague Chadema? wana nini wanataka kutu offer mimi kama mwananchi wa kawaida tu, vitu vitano tu

Vitu vitano?. Hivyo vitu vitano kawaambie CCM waliopo madarakani.
 
Mwana uchumi kweli unaamini kabisa Chadema wanaweza kutawala? Chadema kama mchezaji mpira kwenda Kagera au Mtibwa kutengeneza jina akipata ndoto kwenda Simba au Yanga. Akikosa huko ndio utamkuta Lindi au Singida united.

Kwanini chadema wasiweze?. Mwaka 2015 walipata asilimia 40 ya kura za urais, ina maana walibakia asilimia 10 tu wafikishe 50. Hivi chama chenye margin ya asilimia 10, hakiwezi kupewa madaraka?. Yani pamoja na tume ya uchaguzi kuwa ya rais na upendeleo kuwa wa wazi, bado chadema ilifanikiwa kuzoa asilimia 40.

Hivi fikiria kwanini mwaka 2020 mizengwe ilikuwa mingi dhidi ya chadema? Issue ni kwamba ukiachia chadema nafasi ikafanya siasa kwa uhuru , tume huru hakuna kubambikiana kesi, utakuja kuniambia. Mazingira ya sasa yana ifavour CCM sana.
 
Wamejiua wenyewe kwa tamaa zao
  1. Mbowe
  2. Lissu
  3. Lema
  4. Msigwa
  5. Mnyika
Walisimama majukwaani kusema Lowasa fisadi papa, ndimi hizohizo zikaja kusema Lowasa safiiiii👍🤣

View attachment 2480444
Utamwamini mtu wa hivi?
Utamuelewa?

Kwa hivyo Lissu na mbowe ni mahakama? Lazima uelewe wale ni wanasiasa, na siasa ni dynamic. Alikuwa fisadi au hakuwa fisadi, hilo sio issue, ila cha muhimu Lowassa na Chadema walimpa headache magufuli mpaka kufuta mikutano ya hadhara.
 
Chama sio mali ya umma acha uongo, chama ni mali ya wanachama. Wanachama ndio huamua chama kiendeje.

Unafiki ni kutetea CCM kukaa madarakani kwa muda wote huo kupitia wizi wa tume ya mahera lakini kukasirika wanachama wa Chadema kuchaguwa mwenyekiti wao kwa muda.

Hiyo ni mbinu pia ya kupambana na mitego ya ccm . Ona kundi la Zitto lililotaka kuiongoza CHADEMA kipindi hicho lipo wapi? Wote wanerudi CCM. Hivi unadhani Zitto angechaguliwa mwenyekiti wa chadema kipindi kile mambo yangekuwaje?
Umma maana yeke watu wengi. Ndiyo maana kuna umma wa waislamu nk. Kitu kama hicho hakiwezi kuendeshwa kwa kidikteta kampuni ya mtu binafsi. Ikitokea kimeendeshwa kwa udikteta basi ni makosa. Zitto angepata uenyekiti chama kingeweza kuwa vizuri kuliko kilivyo sasa. Ni unafiki mkubwa kuona ubaya wa udikteta wanapofanya wengine na kushangilia unapofanya wewe.
 
Vyama vya upinzani vilimfanyia nani udikteta?. Kwenye kugombea uenyekiti wagombea ni zaidi ya mmoja na kwenye kugombea urais mgombea ni zaidi ya mmoja, shida ipo wapi?

Kwa CCM mgombea uenyekiti ni mmoja tu na hakuna mwingine na kwenye awamu ya pili mgombea urais ni mmoja tu. Membe alitaka kugombea urais akanyofolewa uanachama.

Anza kwanza na CCM ndio uje upinzani. Ndoa yako kila siku magomvi, ila kutwa kusema ndoa za wengine.
Hao unaosema wamekuwa na mgombea mmoja wamebadilisha wenyeviti mara nne ndani ya miaka 20. Vyama vya upinzani vipo na watu walewale, Mbatia, Lipumba, Mbowe, Mrema nk nk. Wenyeviti wa vyama vya siasa vya upinzani ni madikteta wakubwa. Bahati mbaya wafuasi wao wamejaa mahaba kiasi kwamba hawaoni udikteta huo. Lazima kuwe na ukomo wa mtu kuongoza, tofauti na hapo ni kuanzisha mazalia ya madikteta.
 
Kelele nyingi, huyo Lowassa si yupo CCM mbona hamjamshtaki? Na mmempa mwanae ubunge?.

Chadema walipata kura milioni sita na wabunge wa kutosha. Hilo kwenye siasa ndilo la maana. Mbona magufuli alikuwa na kashfa ya ufisadi ya kuuza nyumba za serikali kwa hawala yake?. Lakini akateuliwa kuwa rais?. Lowassa alikuwa anaenda kutoa shukrani mpanda baada ya uchaguzi akakamatwa na polisi na mikutano ikazuiliwa.
 
Kuna wengi sn wanaweza kufikiria nini kilisababisha anguko la Chadema wapo wachambuzi wengi wa masuala ya siasa wanaweza Kuja kuelezea mengi Sana yaliyosababisha anguko la kilichokuwa chama kikuu cha upinzani zifuatazo ni baadhi ya hoja zinazotoa ushahidi juu ya kiini cha anguko la Chadema

Udikteta: Pamoja na kujitabanaisha kama chama kikuu cha upinzani lakini Chadema kilikumbwa na tafsiri batili ya Jina na matendo yake, Chama cha kidemokrasia kinachoendeshwa kidikteta kwa kung'ang'aniwa na mtu mmoja kukiongoza kwa muda mrefu na kukifanya chama kama Mali binafsi ya Familia kwa mfano Mbowe amekuwepo madarakani toka enzi za Mzee mkapa, mkapa aliondoka akamuacha Mbowe kama mwenyekiti baadaye akaja kikwete akamuacha Mbowe kama mwenyekiti

akaja Magufuli akamuacha Mbowe kama mwenyekiti na sasa ni Samia, kwa lugha nyingine ni kwamba CCM imepata wenyeviti wanne tofauti lkn Chadema kikiwa na mwenyekiti mmoja tu naye ni Freeman Alkael Mbowe

Ni kosa kubwa sana kuruhusu mawazo ya mtu mmoja anayekosea Mara kwa Mara kutowajibika pale anaposhindwa
uchaguzi wa Mwaka 2005 ulitosha kabisa kumuondosha Mbowe kama mwenyekiti wa Chadema

Lakini ameng'ang'ania madaraka tu utazani kupe na hatimaye America chama kwa kunyonya damu yote

Mbowe Hana Mamlaka ya kudai katiba mpya kwa sababu yeye mwenyewe ni mvurugaji namba moja wa katiba ndani ya chama chake

tutaendelea kujadili udikteta kama kigezo cha anguko la Chadema namba 2
Una chuki na Mbowe na si vinginevyo,ukweli uko pale pale CHADEMA haijafa na haiwezi kufa kwa mawazo yako.
 
Kuna wengi sn wanaweza kufikiria nini kilisababisha anguko la Chadema wapo wachambuzi wengi wa masuala ya siasa wanaweza Kuja kuelezea mengi Sana yaliyosababisha anguko la kilichokuwa chama kikuu cha upinzani zifuatazo ni baadhi ya hoja zinazotoa ushahidi juu ya kiini cha anguko la Chadema

Udikteta: Pamoja na kujitabanaisha kama chama kikuu cha upinzani lakini Chadema kilikumbwa na tafsiri batili ya Jina na matendo yake, Chama cha kidemokrasia kinachoendeshwa kidikteta kwa kung'ang'aniwa na mtu mmoja kukiongoza kwa muda mrefu na kukifanya chama kama Mali binafsi ya Familia kwa mfano Mbowe amekuwepo madarakani toka enzi za Mzee mkapa, mkapa aliondoka akamuacha Mbowe kama mwenyekiti baadaye akaja kikwete akamuacha Mbowe kama mwenyekiti

akaja Magufuli akamuacha Mbowe kama mwenyekiti na sasa ni Samia, kwa lugha nyingine ni kwamba CCM imepata wenyeviti wanne tofauti lkn Chadema kikiwa na mwenyekiti mmoja tu naye ni Freeman Alkael Mbowe

Ni kosa kubwa sana kuruhusu mawazo ya mtu mmoja anayekosea Mara kwa Mara kutowajibika pale anaposhindwa
uchaguzi wa Mwaka 2005 ulitosha kabisa kumuondosha Mbowe kama mwenyekiti wa Chadema

Lakini ameng'ang'ania madaraka tu utazani kupe na hatimaye America chama kwa kunyonya damu yote

Mbowe Hana Mamlaka ya kudai katiba mpya kwa sababu yeye mwenyewe ni mvurugaji namba moja wa katiba ndani ya chama chake

tutaendelea kujadili udikteta kama kigezo cha anguko la Chadema namba 2
Magufuli alitaka kuua CHADEMA lakini alikufa yeye tarehe 17/03/21. Yule kichaa alipopewa madaraka ya kuwa Rais October 2015 akapagawa akajiona yeye ni mungu.

Akataka kumuua Lissu na kumzika Ikungi chapchap tarehe 17/09/2017 baada ya kumshambuliankwa risasi, lakini Mungu wetu aliyejuu akasema wewe ni nani mpaka uamue nani Aishi na nani afe. Mwishowe akafa mwenyewe.

Usijidanganye kuwa CHADEMA imekufa hata kwa 1%, instead nakuhakikishia CHADEMA imekuzwa na vitendo viovu vya magufuli pengine kwa 300%
 
Ukitaka maendeleo ya kweli hakikisha umenyamazisha wapinzani wako.

Wapinzani wapo kwa ajili ya kupewa asali tena kila wanapotaka. Siku ukiwanyima wanakuchafua na watasema ulikuwaga unawapa asali kuwafunga mdomo.

Upinzani ni hoja pana sana. Tatizo tunadhani upinzani ni CHADEMA tu. Kipindi cha Nyerere alinusurika mara mbili kupinduliwa na ulikuwa mfumo wa chama kimoja. Nyie bakieni kudhani Upinzani ni mbowe na Lissu.

Magufuli alidhani wapinzani wake ni chadema, lakini kipindi anakufa chadema ndio walipaza sauti kuhusu kifo chake mpaka ilipotangazwa rasmi.
 
Chadema haijafa bado ipo hai ila moja ya sababu kubwa inayopelekea Chadema kuwa chama dhaifu ni pale walipoamua kuukana ukweli wao wenyewe kwakutaka kumsafisha fisadi waliyezunguka Nchi nzima kumtukana!!. Ujio wa Eddo 2015 ndani ya chadema uliondoa uaminifu hasa kwa watu wenye uelewa mpana juu ya siasa zetu wakaona Chadema na viongozi wao wakuu hawapo kwaajili ya Tz bali wao kwanza, mpaka Leo ukimfuata mwanachadema ukamuuliza ni sababu zipi ziliifanya Chadema kumpokea Eddo hawawezi kukupa... Kuanzia hapo watu timamu wakaona hamna la maana zaidi ya ubabaishaji mtupu.
Sababu nyingine ni utawala wa Magufuli na uchaguzi wa 2020, magufuli alikuwa na nia hasa yakuiondoa Nchi kwenye mfumo wa vyama vingi kuipeleka chama kimoja. Siku zote uhai wa chama cha siasa ni kufanya siasa na kuuza sera zao kwa wananchi, Chadema na wapinzani wengine hawakupata tena hiyo fursa automatically Nchi ikabaki kusikia sifa na mapambio yanayoimbwa juu ya chama kimoja Cha CCM chini ya Magufuli.
Pia kutokuwa na ukomo wakiuongozi kwa kiongozi mkuu wa chama, hii inadhoofisha na inaondoa uhalisia wa chadema na wanachokipigania hasa ni Demokrasia ipi wanayoitaka wao?, Haiwezekani mtu mmoja ndio akawa Bora kwa vipindi vyote vya zaidi ya miaka 15 bila kuachia ngazi ili Chadema ipate kiongozi mwingine ambaye nae atatoa dira na mwenendo mpya kuhakikisha wanachukua dola.
Ukiwasililiza Chadema wanavyoimba suala la kujenga taasisi imara za kiuongozi kuliko kumjenga mtu au kimtegemea mtu imara kwa mbaali utawaona wapo siriasi lakini hebu tafakari wao Wana hizo taasisi imara? Kama wanazo Kwanini FAM haachi uongozi?, Jibu lao ni jepesi sana eti mwamba tuvushe!! Mara eti hanunuliki kinachoshangaza ni Kumbe Chadema sio chama cha kitaasisi bali ni chama kinachotegemea maamzi ya mtu mmoja. Ili Chadema ichukue dola inahitaji ipate kiongozi kijana tena asiyemwoga.... Huyu Mbowe ni mandonga mtupu aliyepata umaarufu kupitia mgongo wa Dr slaa na kazi nzuri za vijana wa chadema.
Dr Slaa huyu huyu zuzu asiyejielewa? Angekuwa na msima walau 10% ya Mbowe angalau angekuwa 'mtu', mtu kadindisha kuunga mkono 'juhudi' licha ya kuharibiwa na kufilisiwa investments kibao unadhani ni wangapi wanaliweza hilo.
Lowassa businesses zake zimeguswa kidogo tu kaufyata na kurudi tena akapokelewa kwa bashasha ikulu Jiwe akiuhesabu kuwa ni ushindi wa ndugu.
 
Mali
Umma maana yeke watu wengi. Ndiyo maana kuna umma wa waislamu nk. Kitu kama hicho hakiwezi kuendeshwa kwa kidikteta kampuni ya mtu binafsi. Ikitokea kimeendeshwa kwa udikteta basi ni makosa. Zitto angepata uenyekiti chama kingeweza kuwa vizuri kuliko kilivyo sasa. Ni unafiki mkubwa kuona ubaya wa udikteta wanapofanya wengine na kushangilia unapofanya wewe.

Nimekuambia umma ni jumla ya jamii yote, lakini wanachama ni specific. Ndio maana mambo ya CCM yanawahusu wanachama wa CCM pekee. Sasa kulazimisha maamuzi ya CHADEMA kuwa ya watanzania wote unakosea sana. Wanaotakiwa kulalamika ni wanachama wa chadema sio wengine.

Zitto yupi? Huyu aliye ambulia kura za urais elfu tisini nch nzima mwaka 2015? Kipindi hicho ACT ipo hot kabisa. Mwaka 2020 wakashindwa hata kumcontrol mgombea wao wa urais?. Kama Zitto kashindwa kukiamsha chama kipya kama ACT angeweza kwa CHADEMA?. Yupo wapi msando, Dr Kitila, Pamba, et al?. Wote walirudi CCM. Sasa jiulize walitaka kuiongoza chadema kwanini kama ACT iliwashinda.
 
Usijisahaulishe kwamba magu aliwazuia chadema kufanya siasa miaka mitano. Uchaguzi wa 2019 na 2020 ulitia fora. Unaenguaje robo tatu ya wagombea wa chadema? Halafu siku ya kupiga kura akazima na mitandao ya internet ili aibe vizuri.

Magu alikosea sana, huwezi wazuia chadema wasifanye mikutano miaka tano halafu muda wa uchaguzi unafanya ujinga kama ule. Ule uchaguzi ndio chanzo cha kifo cha magufuli.
Haya mikutano mmeruhusiwa tuone kama mtashindaa
 
Chama sio mali ya umma acha uongo, chama ni mali ya wanachama. Wanachama ndio huamua chama kiendeje.

Unafiki ni kutetea CCM kukaa madarakani kwa muda wote huo kupitia wizi wa tume ya mahera lakini kukasirika wanachama wa Chadema kuchaguwa mwenyekiti wao kwa muda.

Hiyo ni mbinu pia ya kupambana na mitego ya ccm . Ona kundi la Zitto lililotaka kuiongoza CHADEMA kipindi hicho lipo wapi? Wote wanerudi CCM. Hivi unadhani Zitto angechaguliwa mwenyekiti wa chadema kipindi kile mambo yangekuwaje?
Zitto au Slaa wangefanikiwa kuongoza CDM leo hii kingeshageuka na kuwa tawi la CCM na kisingekuwa kinapigiwa kelele na supporters wa CCM.
 
Back
Top Bottom