Nini kimemkuta Waziri wa zamani na Wakili Msomi, Lawrence Masha hadi kufika kwa “Kiboko ya Wachawi”?

Nini kimemkuta Waziri wa zamani na Wakili Msomi, Lawrence Masha hadi kufika kwa “Kiboko ya Wachawi”?

Nini kimemkumba Lawrence Masha? Nimeshangaa sana kukutana na hii video ikizunguka mtandaoni eti yupo kwa huyu anayejiita Pastor, Kiboko ya Wachawi sijui.

Naelewa kwenye maisha kuna kupanda na kushuka lakini inakuwaje mtu msomi kama Masha mwenye Shahada ya Uzamili ya Sheria (LL.M) kutoka Kituo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Georgetown na Shahada ya Kwanza ya Sheria (LL.B Hons) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, anaishia kwenye masuala kama haya!

Je, anatumiwa na huyu anayejiita mchungaji au ni tangazo hili?


Masha alikuwa mtu mzito sana kwa kweli. Amewahi kuwa Mwenyekiti wa Lyson Law Group na Tanga Cement, Managing Partner Gabriel & Co na IMMMA , Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Nyamagana. Lakini pia alikuwa Mwenyekiti Mtendaji wa FastJet pamoja na nyadhifa nyingine nyingi alizokuwa nazo.

Pia soma;
1. Lawrence Masha: Kutoka Uwaziri hadi kukusanya takataka Dar
2. Lawrence Masha amiliki asilimia 68 ya hisa Kampuni ya Fastjet Tanzania
3. Lawrence Masha! Mpambanaji anayekaribia kupoteza pambano
4. Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha akamatwa na Polisi
5. Logical conclusion ni kuwa Lawrence Masha siyo msafi
6. Lawrence Masha ajivua uanachama wa CHADEMA. Adai hawana nia ya kushika dola!
Hii ya kuwataja wake za watu madhabahuni imekuwa fasheni, kuna mwingine alifannya kitu kama hiki Arusha siku si nyingi
 
Ktk hali ya kawaida ingetarajiwa mwanamke kumpa mumewe faraja na kumtiamoyo wakati Mwanaume anapofilisika na kukosa kazi, au kupitia mitihani ya mambo magumu
Lakini badała yake imekuwa kinyume chake,
Mke ndio anakuwa sababu ya mume kukosa usingizi, kukosa amani, kuugua presha na kisukari kwa Maneno na kelele zidizoisha usiku na mchana na kutishia kuachana 👌👌👌

Inasikitisha sana .

Usiombe kupitia hali hiyo.
Na wengi tunapitia hapa
 
Nini kimemkumba Lawrence Masha? Nimeshangaa sana kukutana na hii video ikizunguka mtandaoni eti yupo kwa huyu anayejiita Pastor, Kiboko ya Wachawi sijui.



Naelewa kwenye maisha kuna kupanda na kushuka lakini inakuwaje mtu msomi kama Masha mwenye Shahada ya Uzamili ya Sheria (LL.M) kutoka Kituo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Georgetown na Shahada ya Kwanza ya Sheria (LL.B Hons) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, anaishia kwenye masuala kama haya!



Je, anatumiwa na huyu anayejiita mchungaji au ni tangazo hili?






Masha alikuwa mtu mzito sana kwa kweli. Amewahi kuwa Mwenyekiti wa Lyson Law Group na Tanga Cement, Managing Partner Gabriel & Co na IMMMA , Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Nyamagana. Lakini pia alikuwa Mwenyekiti Mtendaji wa FastJet pamoja na nyadhifa nyingine nyingi alizokuwa nazo.



Pia soma;

1. Lawrence Masha: Kutoka Uwaziri hadi kukusanya takataka Dar

2. Lawrence Masha amiliki asilimia 68 ya hisa Kampuni ya Fastjet Tanzania

3. Lawrence Masha! Mpambanaji anayekaribia kupoteza pambano

4. Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha akamatwa na Polisi

5. Logical conclusion ni kuwa Lawrence Masha siyo msafi

6. Lawrence Masha ajivua uanachama wa CHADEMA. Adai hawana nia ya kushika dola!

Masha, nadhani ni mmoja wa watu waliokuwa na 'bahati mbaya' sana na serikali ya awamu iliyopita. Mwingine jamaa anaitwa Gonzaga, yule 'mtoto wa mjini' kwa wanaomjua.



Gonzaga alipewa kesi ya kudukua mifumo ya TRA, akatupwa mahabusu na kesi yake ikawa haiendi. Sijui hadi sasa imefikia wapi, naye sijui yuko nje au mahabusu.



Hawa wawili walidaiwa 'kuichezea' ile kesi ya 'samaki wa pombe'. Kwamba waliwaonesha njia na kutoa msaada wa kisheria hadi jamaa wakashinda kesi na kulipwa fidia.



Hao watu wawili kwa nyakati tofauti walifuatwa na Pombe akiwa Waziri wakati huo, na kuombwa waiache hiyo kesi, kwani ni turufu yake akiwa katika wizara hiyo.



Wakati huo alikuwa Wizara hiyo kama 'adhabu' baada ya 'fujo' alizowafanyia viongozi wenzake akiwa Ujenzi. Hivyo, Uvuvi nako alitaka afanye 'maajabu' pia ili kufunga watu midomo.



Kwa hiyo, kwa Masha baada ya IMMA kupigwa bomu, ilikumbana na vita nyingi za kikodi hadi ikatetereka hasa. Na kutimuliwa kwa Fast Jet kulimaliza vingi kwake kiuchumi.



Kwa mtu kama Masha kupitia hayo, ni pigo kubwa kwake. Amepoteza vingi na mapato yake yameshuka sana, na nadhani hilo lilimletea shida ya kindoa pia na mkewe Stellag
Masha, naweza kusema yeye na Gonzaga (yule mtoto mjini, kwa mnaomfahamu) walikuwa na 'bahati mbaya' na serikali ya awamu iliyopita iliyohitimishwa na msiba.

Gonza alipewa kesi ya kudukua mifumo ya kodi na kuwa akiingiza hela 'ndefu' kwa kila dakika. Alikuwa ni mtu wa mwanzoni sana kudakwa na kutupwa mahabusu na kesi yake ikawa haiendi.

Hawa watu wawili, walikuwa wakidaiwa kuwahi 'kuchezea' kesi ya 'Samaki wa Pombe', hadi kufanya serikali ishindwe na kulipa fidia. Ni kesi iliyoibuliwa na Pombe akiwa Waziri kwenye Uvuvi.

Kwa wakati huo Pombe, kama alikuwa kwenye 'adhabu' kwenye Uvuvi, baada ya kutibuana sana na viongozi wenzie alipokuwa Waziri kwenye Ujenzi. Kwa sifa za Ujenzi, alitaka aje nazo Uvuvini.

So, kesi ya samaki Ilikuwa ndiyo turufu yake, kwani kupandisha nauli za vivuko na kuileta boti isiyoweza kutia nanga bandarini, haikuwa sifa nzuri, japo boti ilikuwa ya ruti za nyumbani kwa Rais.

Inaelezwa kuwa, aliwafuata kwa nyakati tofauti hao jamaa wawili kuwaomba waiache hiyo kesi ili 'atoboe' nayo impe sifa. Lakini, jamaa waliendelea kutoa msaada wa kesi na serikali ikaanguka.

Masha, IMMA yake mbali na kupigwa bomu la kutupa kwa mkono, lakini kulikuwa na vita nyingine za bwana kodi, kabla Fast Jet kutimuliwa nchini. Hapo Masha, akalazwa chali.

Baada ya uchumi kuyumba na siasa kumsahau, nadhani kwake tukio hili ni kama kiki yake ya kurejea vichwani mwa watu, hasa ukizingatia mwaka ujao tuko kwenye uchaguzi mkuu.

Na kwa hiki kilicho kwenye hii video, nadhani ni namna ya kumwonesha Mwenyekiti wa CCM kuwa asimsahau, naye yupo.

Ova
 
Tumpe pole tu kijana watu. Tumuombee arudi kwa Mwenyezi Mungu, ajiondowe huko kwa wapigaji, hao ndiyo wanammaliza kabisa sasa.
 
Mimi ndiyo maana nikimuona mtu anaenda kwa hao wapigaji wala sihangaiki nae kumzuia maana huwa kwa uwezo wake wa kutambua vitu aliopewa anakuwa amefika mwisho kifikra so nachofanya namuacha aendelee kujifunza in hard way

Kwa msomi level ya huyu jamaa kufikia kwenda Buza huko ndani ndani kwenye banda la mabati kwa so called mtume kutabiriwa unaweza ukaona jinsi maisha yakimpiga mtu yanavyoondoa ufahamu wake.
Kama kaenda kwa utashi wake na siyo kutafuta kiki za kisiasa basi kaingia chaka, hakuna nabii hapo....

Wife huwa anapenda kuweka chaneli ya vipindi vyake usiku, ukisikia maongezi anayofanya kwenye simu na watu wanaojifanya kumpigia, kwa akili ya kawaida utagundua mapema ni usanii na utapeli tu unaoendelea pale, wengi wanaompigia wanakuwa wamefiwa muda huo wanaompata hewani.

Igizo huwa linaanzia kwa nabii kiboko ya wachawi kutaja majina na tarehe za kuzaliwa za wahusika, kumtaja mchawi aliyemuua marehemu ambaye mara nyingi ni mmoja wa wafamilia hasa mama, kumtishia mchawi aseme ukweli au afe, na linaishia kwa kumfufua marehemu.......lakini ukisubiri kesho yake usikie habari mtaani kujua kama kuna mtu alikufa na kufufuliwa na kiboko wa wachawi hutasikia hata moja pamoja na marehemu kama wanne kufufuliwa usiku huo mmoja.

Hawa matapeli wanaojiita manabii na mitume wanapotosha sana watu hasa wanawake wasiotaka kuumiza akili zao kutafakari mambo.​
 
Natamani walokole wanijibu haya maswali:
1. kuna umuhimu gani wa nabii mfukuza wachawi kulindwa na bodigadi?
2. Hivi ukiwa mlokole ni lazima uwe maskini (angalia hali za waumini wake!)?
3. Hivi nabii hawezi kuwa kiboko ya umaskini? ukiwa muumini wake wewe ni mwendo wa utajirisho tu?

Halafu na ninyi wachawi mmekosa uzalendo na utaifa, Unahangaika kuroga Choka mbaya
si watafute kina GSM, MO, BAKHRESA, ROSTAM
 
Back
Top Bottom