Nini kimetokea mpaka kufa kwa uzalishaji wa Ngano hecta 350,000 kule Bassotu Manyara?

Nini kimetokea mpaka kufa kwa uzalishaji wa Ngano hecta 350,000 kule Bassotu Manyara?

Unasema nmc ilifirisika ambacho ni chombo cha serikali lakini unapinga serikali ilishindwa kununua ngano hivi unajielewa.
Ningekuelewa kama ungesema nmc ilishindwa kununua ngano sababu ilifirisika.
Andika Kiswahili viuri kabla hujaanza ubishi wa kijinga.

1990 haikuwepo NMC sasa itashindwa ipi kununua? Una akili kweli kichwani mwako? Au maika inakupiga chenga? Sikushangai ikiwa huelewi hata kwenye maandiko L uiweke wapi na R uiweke wapi.
 
Katika vitu huwa vinaniuma ni hili la kulima unakuta watu wanahamasishana walime Mihogo, au mtu akipata Hela kiasi tu anakimbilia kujenga frames...

Yaani tunatoka kulima Ngano tunarudi kwenye Mihogo, hii inaonesha namna gani sisi kama watu wa nchi hatujajua high values assets...
 
Andika Kiswahili viuri kabla hujaanza ubishi wa kijinga.

1990 haikuwepo NMC sasa itashindwa ipi kununua? Una akili kweli kichwani mwako? Au maika inakupiga chenga? Sikushangai ikiwa huelewi hata kwenye maandiko L uiweke wapi na R uiweke wapi.
Nilichogundua mwalimu wako alikuwa na shida sana.
 
Power nyingine Mkoloni aliyotumia na bado anaitumia ni elimu na technology. Wakati mkoloni anatutawala alitumia kilimo cha kisasa kulima mashamba, pamoja na kutumia Rasilimali watu kwa ujira mdogo pia alitumia mashine za kisasa kwa wakati ule.

Alifanya tafiti nyingi na kupata matokeo. Leo hii huko London na Berlin wanajua sehemu zote zenye madini Tanzania. Wanaweza kupanga mbinu yeyote ya kuyapa wakati sisi hatujui kinacho endelea.
It's seems like you have something uncommon, Please ongea zaidi Kuhusu hili
Kuna mahali nilishafanya kazi na mzungu alikua na shamba ila Ni porini alikua anayajua maeneo yale kuliko hata wenyeji pia alikua anajua sehemu karibia zote zenye BICON tofauti na sie mpaka uzione, Inawezekana alishafafanuliwa jinsi ya kuzisoma zile BICON... Kwasasa yupo Germany na nadhani ni tajiri sana maana nilikuja kugundua mwishoni kwamba HE WAS AFTER GOLD kilimo ilikua ni gelesha.
 
Ni kweli kabisa mkuu hii mada ingepelekwa pia kule Twitter ili Mhe Husein Bashe aione yuko very positive and open minded Kwenye issues kama hizi...
Hujui unachokiongea, you better keep quiet, tusianzishe mengine hapa [emoji275]
 
Hii tabia ya kuendekeza wanyonge ni utoto,kila mtu amesoma the so called agrarian revolution ilivyoleta mapinduzi..

Mpango wa kilimo kwanza ulikuwa unaenda kuanzisha mashamba makubwa ya mabepari au ushirika wa kibepari Ili kuleta tija kwenye kilimo..

Unfortunately kila kitu kimekufa.
Habari njema ni kwamba aliyeleta wazo la kilimo kwanza yupo, hopefully atamshauri bi mkubwa vyema

Mungu ibariki nnji yangu "mrema"
 
Wajapan si wakikuja wakaqatengenezea mradi wa kapunga,wakawachia...ehe nini kilifata

Ova
Hahaha umenikumbusha mbali sana, project ya kapunga, hapo ndipo nilipoamini hii nchi kila mtu anapiga anapopata nafasi, shamba la bibi
 
Katika vitu huwa vinaniuma ni hili la kulima unakuta watu wanahamasishana walime Mihogo, au mtu akipata Hela kiasi tu anakimbilia kujenga frames...

Yaani tunatoka kulima Ngano tunarudi kwenye Mihogo, hii inaonesha namna gani sisi kama watu wa nchi hatujajua high values assets...
Dira ya taifa hakuna...
 
Umekumbusha mbali sana. Ni maeneo yaliyokuwa mazuri sana miaka ya mid 80 hadi mwishoni mwa miaka ya 90. Kulichangamka sana kwa biashara, watu toka kila pembe ya nchi n.k.

Ngano iikuwa inalimwa sana, kama sikosei mashamba ya Basuto yaliongoza Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Kuna Setcheti, Basuto, Gawali, Murijanda, Gidagamowdi, Mulbadow n.k. Kateshi ilichangamka haswa, hata Mwagitu, Kendabi, Nangwa n.k.

Kuna mameneja/meneja wasaidizi kama Mzee Mndeme, Kimaro, Shetui, Koopa n.k walikuwa wanachapa kazi sana.

Jandu plumbers ndio aliyevuta maji kutoka Kindabi (mlima Hanang) na kuyasambaza kwenye hayo mashamba.

Wengi waliokuwa mameneja na wasaidizi wao walisoma Canada.

Ila wengi walikufa na ukimwi sana. Halafu wengi wao hawakuwekeza , ukikutana nao sasa hivi wamepigika kimaisha na utawaonea huruma. Walipenda sana starehe maeneo ya Arusha, Katesh, Babati na Basuto Central.

Kulikuwa na wanawake wengi sana wazuri kutoka kila pembe ya Tanzania ukijumlisha na dada wa Kiiraq, ilikuwa burudani haswa.

Karibuni Katesh, Kindabi, Mwagitu, Hydom, Masakta, Endasaki, Dareda Centre na Mission, Balang'ida Lalu na Dirima, Milima ya Logia, Gendii, Bonga, Managha, Galapo, Maweni, Maisaka, Murara, Magugu n.k.

Saitaaaaa/Gabaseyuuu.

Maisha yalikuwa mazuri sana..
Nikiwa darasa na kwanza 1987 nilifuatwa na school bus hadi mlangoni na kurudishwa hadi mlangoni.. baba alikuwa mfanyakazi katika moja ya shamba. Tulisoma na watoto wa kizungu. Life was good
 
Gharama ya kulima Tanzania ni kubwa kuliko kununua mazao nje,ukitaka kuamini hvyo angalia mafuta ya alizeti yanayotengenezwa Tanzania na mafuta ya alizet yanayokuwa import bei zake
Serikali za nchi zilizo endelea zinawaruzuku wakulima zaida ya dollar bilioni 250 kwa mwaka ,hivyo mkulima anaweza kuuza mazao yake kwa bei pungufu ukilinganisha na gharama halisi ya uzalishaji. Farm subsidies ulaya inaua kilimo uswahilini.
 
Rodrick mahenge wa iringa alikuwa analima ngano ambayo mavuno yake serikali ilikuwa inashindwa kuyanunua
Je huyu Rodrik Mahenge bado yuko hai?

Nakumbuka Rais Mwinyi aliwahi kumpa zawadi ya pickup truck mwanzoni mwa miaka ya 1990s
 
Kuna wazungu wamechukua hilo shamba la basuto wanafukua barabara zote za shamba ili kuanza kilimo cha ngano,bila shaka mwaka kesho wataanza kilimo....shamba limeharibika sana mpka waweke miundombinu sawa
Wakiona shamba limeanza kukaa vyema wananchi watalalamika kuporwa maeneo yao watakwenda kuvamia eneo
 
Back
Top Bottom