Nini kingetokea kama Mwl. Nyerere angestaafu Urais mwaka 1971 na Oscar Kambona kuvaa viatu vyake hadi mwaka 1981?

Weka nyama kidogo hapo kwa kimbia kwa kambona
Kambona alikimbilia uhamishoni Uingereza baada ya kukosana na Nyerere kisa kupinga ujamaa mwaka 1969. Lakini tutengeneze imagination au mabunio kuwa hawakugombana na hatimaye 1971 kuachiwa nchi. Sasa watu wanachomekea kipindi hicho tayari ni mkimbizi, nalijua hilo, tusiliangalie.
 
Naona umejikuza sana!!
Kwani wewe ni nani?
Kwanini maoni yako kuhusu utawala wa nchi hii yawe ndiyo kipimo cha ubora au ubovu wa uongozi au utawala?

Unaweza kumgeuka sababu ya ubinafsi endapo maslahi yako binafsi hayajapewa kipaumbele au umedhibitiwa uovu(ufisadi) , au umenyimwa ulaji.
 
Inaonekana na sasa mwanae kaporwa mali na kuachiwa akili asake mali zingine!!!
Haya ndio maajabu ya dunia
 
Kwa mara ya kwanza na bila unafiki na kupepesa macho Rais Mtaafu wa Awamu ya 2 Mh Alhaj Ally Hassan Mwinyi anasifiwa na kuenziwa kama Baba wa Tanzania ya Leo ya Uchumi wa Soko Huru.Akiwa Rais wa SMZ wa Bara walikuwa wakifurika Zanzibar kununua bidhaa huku Bara tukikumbwa na Uhaba wa kila kitu.
 
Lakini Nyerere ameacha GDP ya Tanzania ilikuwa juu ya ile ya Kenya mwaka 1984. Fanyeni reference mjue kuwa Nyerere hakuwa mbovu kama mnavyotaka watu waliozaliwa baada ya utawala waamini. Kenya imetupita kipindi cha Mwinyi. Pamoja na reform zake Mshahara Wa Mwalimu uliweza kununua godoro tu. Na baiskeli ya swala kiwanda cha Tanzania usingeinunua kwa mshahara mmoja. Ni kweli Nyerere aliacha akiba BOT ni zero lakini kama sio vita ya Kagera he was doing good ingawa hapo ndipo wakenya walianza kutunyemelea wakatupita 1985 Mwinyi alipotawala.
 
Nimekulewa. Ukitaka kufanya research ya vitu kama hivyo unasoma resources nyingi na kuongea na watu mbalimbali. Hukimbilii kusoma gazeti moja na ukaja na conclusion. Anyways mimi nilitaka tu kutahadharisha wachangiaji wote kwani Tanzania mara nyingi utakuta watu hawafanyi bidii yoyote wanapotaka kujua nchi yetu ilikotoka wanapokuwa na uhitaji na badala yake wana-argue kuwa hawakuwepo kipindi hicho. Hivyo siyo kwamba nimekunanga. BTW hata ulivyoulizia pia njia moja ya ku-reserch.
 
sahihi kabisa. In short nilichomaanisha pia kwa wakati huo, hakukuwa na media huru/binafsi zilizokuwa na uwezo wa kuweka wazi kilichokuwa kinaendelea. Kumbuka maendeleo ya mawasiliano hayakuwa kama ilivyo leo. Kama tujuavyo, mfumo wa uchumi ulikuwa centralized kwa maana ya centralized. Kila mtanzania alikuwa limited na habari za kutoka RTD na "hotuba kwa wazee wa mzizima". Huhitaji takwimu kujua uchumi ulikuwaje kama kulangua pakti ya sigara ilikuwa "uhujumu uchumi". Halafu leo anakuja mtu anakwambia katika miaka yake 23, Tanzania ilikuwa ikinawiri.
 
Sio kweli, mambo yaliharibika kabla ya vita ya Kagera. Baada ya nationalization, ni kweli miaka michache iliyofuatia output iliongezeka sana, kumbe ilikuwa ni just "counterfactual" kwani muda mfupi baadaye inefficiency ilianza. Mambo yalianza kwenda kombo mwanzoni miaka ya 70. Kama mambo hayakuharibika katika kipindi chake, jiulize economic recovery program ilianza lini? Na kwanini iwe "recovery"? Ilikuwaje nchi ikose hata sabuni. Labda ungetueleza kwa namna gani vita ya mwaka mmoja ikafanye uzalishaji wa viwandani ufe kabisa.
Nyerere was so good or call him best at its gudos, lkn kuna mengi kwenye uchumi na demokrasia alichemka.
 
Sasa hapo mambo kabla ya kuharibika Mara paap anaingia Kambona, tungekuwaje?
 
Sasa hapo mambo kabla ya kuharibika Mara paap anaingia Kambona, tungekuwaje?
Hahaha, naamini kiuchumi tungekuwa pazuri ya hapo ilipo. Kwasababu, kambona alikuwa against na sera za kijamaa. Kwa kifupi policy failure ya Nyerere haikuwa tofauti na Mugabe. Wote wamefanya nationalization, mmoja kwenye njia zote za uzalishaji na mwingine kwenye kilimo. Ujamaa kama ule tuliokuwa nao sisi unapingana hata na nature ya bianadamu.
 
Je huyu kambona alifanikiwa kurudi nchini?
 
Hapa tunatengeneza mabunio/imagination, tuseme hawakugombana na Kambona kaendelea kuwa na ushawishi na hatimaye kuachiwa nchi.

Kambona kama wangeendana kifikra na Nyerere, pengine nchi ingekuwa tofauti kabisa
 
HABARI.
Mimi nadhani Kungekuwa na Watu wachache tu wasiozidi elfu 5 ndio wangekuwa wanamiliki zaidi ya asilimia 50 ya aridhi yote yenye rutuba Tanzania.Tungekuwa tunasikia Tanzanite ni miliki ya ukoo flani au kikundi cha watu mererani yote ingekuwa ni miliki ya watu wachache au ukoo.Hiyo ni mifano michache ongeza na ya kwako.

LUMUMBA
 
No kweli Kambona aliendekeza ubepari na tayari nasikia alikuwa milionaire miaka hiyo ya 1960's. Je ni kweli angewadhulumu mamilioni ya Watanzania kiasi hicho uwazacho?
 
No kweli Kambona aliendekeza ubepari na tayari nasikia alikuwa milionaire miaka hiyo ya 1960's. Je ni kweli angewadhulumu mamilioni ya Watanzania kiasi hicho uwazacho?
HABARI,
Ndugu jaribu kusoma kwa kina tabia za mabepari na ufikiria kama miaka ya 1960 alishakuwa milionaire alikuwa anafanya biashara gani?
Hapo ndio tungejikuta kunakoo chache ni mabilionaire wanaondesha Nchi watakavyo kuanzia kuchagua viongozi wa kuongoza na mambo mengine ni hatari sana hiyo.Sisi kwetu hapa hata ukienda Njombe utakuta aridhi ya kutosha na hapa kwetu bado tumelala hatujapata shida hasa kwenye ukali wa maisha ndio maana hata hizo aridhi siko tu hata ukitaka heka 30 unapata kwa bei rahisi hapo kwenye kungekuwa kuna mkoa kama njombe na mikoa mingine yanya halinzuri kwa kilimo na ufugaji ungekuta ni matajiri 10 ndio wenye miliki ya ardhi yote wote mko chini yao.
Kenya pale kunawatu wanaardhi ambapo hata serikali haiwezi kuigusa kwasabau ya ubepari wao sasa fikiria miaka 30 ijayo idadi ya watu inavyoongezeka itakuwaje.Hapo ndipo yatatokeo kama ya zimbabwe .

LUMUMBA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…