Nini kipo nyuma ya ukuaji na ongezeko la watu wasiokuwa na dini?

Nini kipo nyuma ya ukuaji na ongezeko la watu wasiokuwa na dini?

Kuna gaps nyingi kwenye hizo taarifa zako, hujapata taarifa kamili kukusaidia kujudge na kuamua juu ya jambo hili vema, wote hatujui lakini maandiko ya biblia takatifu yalimnukuu YESU mwenyewe akisema
" MWAPOTEA KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO. WALA UWEZA WA MUNGU"

Tatizo ndio lilipo hapo mkuu, hatujifunzi maandiko wenyewe , kama tunavyotakiwa kufanya tunadhani kumsikiliza muhubiri ibadani inatosha kuelewa mambo haya vizuri,

No research , no right to speak.
unataka kuniambia nilichoandika hapo ni uongo kuwa mtu huchomwa moto milele hata kama kaishi maisha ya dhambi kwa miaka 25? Ni ukweli mtupu nilioandika hapo juu aiseh!!!
 
Mimi ninaamini Mungu yupo, ila hizi njia za binadamu za kuabudu ndio sizikubali,zina uongo mwingi.

Kuna Nabii aliwahi kudai kuwa ameupasua Mwezi vipande viwili kitu ambacho ni hakiwezekani.

Kwa maelezo yako yasiyompendeza Mungu haitakiwi kuyafanya. Au kwa ufupi dhambi hazimpendezi na hatutakiwi kuzifanya na roho ndo anayongoza katika hayo maamuzi
Ni sahihi.Na dhambi basically ni disobedience.Mungu akikupa Muongozo wake kupitia Roho wake ukipuuza thats disobedience therefore it amounts to Sin.
 
Dah!. Binafsi naamini Mungu yupo na ndio aliyenibariki nipo na maisha mazuri kwa Sasa.
Ila sijaenda kanisani miaka na miaka ( Mimi ni RC). Tatizo kwa kweli zile sanamu na mipicha tunayoambiwa ni yesu Kule kanisani zinanikwaza sana.

Yaani mtu kachonga mjisanamu wake na mti wa mpingo Leo hii naambiwa kuwa niheshimu kuwa ni mfano wa yesu!!?. Nimeshafafanuliwaga na watu mbali mbali kuhusu hizo sanamu Ila sikuwaelewa hata kidogo.

Nimejaribu kusali makanisa mbali mbali Ila kote kumenishinda. Ila Kama sio sanamu na mipicha picha kanisani, basi RC is the best.
😀😀😀😀😀😀😀
 
Bado ni mkanganyiko mkubwa kwenye haya mambo ya Dini!!!Imani kama imani tu bila uwezo wa kutafakari na kung'amua uhalisia!!!KWA HIO TUKUBALIANE HAPA!MUNGU ALIMUUMBA SHETANI AKAMFANYA KUA SHETANI ILI ATUDANGANYE TUKACHOMWE MOTO?KUMBUKA KULIKUWA HAKUNA SHETANI KABLA YAKE WALA MWENYE KIBURI!!!KWAHIO SHETANI ALIKITOA WAPI KIBURI KAMA KULIKUA HAKUNA SHETANI MWINGINE???????Najua utaishia kusema mengine tutajua tukifika huko kwake!!Lakini ikumbukwe mjinga huamini kila neno bali mwerevu hulijaribu neno!!!
Mungu alimuumba Malaika na Free will(kama ambavyo alimuumba mwanadamu na free will).Kuwa na Free will maana yake Mungu anataka umwabudu kwa kupenda ndo maana Mungu hakuumba Robots tu na kuziprogram kumpenda na kumwabudu.

Lakini kuwepo kwa Free will kunakwenda sambamba na kuwepo Consequences.Kila choice utayofanya inakuwa na matokeo ambayo unfortunately hayako kwenye maamuzi yako.Mfano una hiyari ya kuweka kidole kwenye moto au kutokuweka (umeexercise free will) lakini kuungua au kutokuungua sio maamuzi yako (Consequences).

Shetani Lucifer ambaye alikuwa ni sehemu ya Malaika akatamani yeye kuwa katika nafasi ya Mungu hivyo akastage rebelion Mbinguni na theluthi moja ya malaika wakaungana naye.
Na Mungu akamfukuza Mbinguni.

Binadamu pia aliwekewa free will,kama Mungu angemwekea binadamu options zilizonjema tu mbele yake tungesemaje palikuwa na uwezo wa kuexercise free will?Maana yake ni kwamba kama pangekuwa hakuna choices tofauti tungesemaje kuwa tumemchagua Mungu?

Pia choices za kutenda uovu zilikuwepo kabla Shetani hajaja kumshawishi mwanamke (Mti wa ujuzi wa mema na mabaya ulipandwa na ulikuwepo bustanini).Shetani alikuja kumshawishi mtu kuchagua kula tunda(hakuleta tunda).

Hivyo hatuwezi kumlaumu Mungu kumwekea Shetani Free will pia hatuwezi kumlaumu Mungu kutuwekea Free will.Lakini we are nothing compared to him hivyo hatuwezi kumpangia what will happen kama tukimkataa atufanye nini au nini kitokee.
 
Yes kwa wanaoongozwa na Sheria.But No kwa wanaoongozwa na Roho.Kwa wanaoongozwa na roho dhambi ni kudisobey sauti ya Mungu ndani yako.
Mbona unajichaganya sasa?
Mkristo ukizini umetenda dhambi au hujatenda?
Kama hujatenda sawa.
Ila kama umetenda, dhambi si ni uasi wa sheria?
Kutokusikiliza sauti ya Mungu ndani yako na ukaenda kinyume si ndo kutenda dhambi? Na adhabu si ipo?
 
Habari 👋🏾

Nimefanya tafiti katika vipindi, nyakati na maeneo tofauti na inaonekana wazi ushawishi wa dini unapungua kwa kasi kubwa sana.

Inaonekana wengi kutokuwa na hakika katika dini mbalimbali na wengi wao bado wanajaribu kujionesha katika ngwe hiyo kwa sababu kadhaa ikiwemo kutokataliwa na jamii hizo.

Je, ni ipi sababu ya ukuaji wa kiwango hiki cha watu kutokuwa na dini kama ilivyozoeleka?
1. Ukisoma biblia kwa mfano, utaona kuwa hili si jambo geni kwa watu 'kuacha njia ya kweli' na kuanza 'kutangatanga'. 2 Anza na Adam na Eva bustanini Eden - Mungu aliwapa kila kitu, lakini hawakuridhika. 3. Nenda wakati wa Nuhu. 4. Nenda kwenye Mnara wa Babeli. 5. Nenda Sodoma na Gomora... 6. Nenda kwa waana wa Israeli katika safari yao kuelekea nchi ya ahadi. 7. Nenda enzi za nabii Amos na Hosea mambo yaliyokuwa yakitendeka. 8. Nenda wakati wa nabii Ezekieli, Danieli na Yeremia. 9. Nenda wakati wa Yesu, hata watesi wake kuamua kumtesa na kumuua kwa kuona heri aachiwe huru mhalifu, lakini mwenye haki auawe. 10. Nenda wakati wa Matendo ya Mitume - wale wafuasi wa Yesu walivyokuwa wakikatazwa kuhubiri habari za Yesu, wengine kama Stephano kupigwa mawe hadi kufa, na Saulo alivyokuwa akiwatesa na kuwaua Wakristo kabla ya kuongoka kwake...11. Ukimaliza hapo sasa njoo wakati wetu huu, ambapo watu tunahangaika na maisha zaidi na kusahau hata kumjulia hali jirani yetu anayeumwa na tuko radhi kumwibia mtu kuliko kumwambia 'umeangusha hela au simu yako'...12. Bila shaka unakumbuka kipindi ndugu zetu albino walivyokuwa wakiwindwa kama wanyama kwa kudhani viungo vyao vina nguvu za kimuujiza za kuleta utajiri na baadhi yao waliuliwa na wengine kukatwa viungo na kuachwa wafe au wauguze majeraha waliyosababishiwa...13. Kuna watu wanalawiti watoto, wanafanya mapenzi na wazazi au ndugu zao, wengine wanabaka na wengine wanafanya mapenzi na wanyama, wakidai wamezidiwa na tamaa...14. Yote haya kwangu ni matendo yanaonyesha kuwa tumemwacha Mwenyezi Mungu - yaani tumeachana na njia sahihi na kuamua kwenda kivyetu vyetu (ovyo ovyo) na huenda ndilo swali unalouliza hapo juu. Kwa kifupi sana 'we are lost' kama ilivyo ile stori ya 'mwana mpotevu' kwenye Injili ya Luka 15:11-32 na unaweza kujiuliza Yesu alikuwa na maana gani? 1) kwa yule mwana aliyeenda kutapanya mali na baadaye kutubu na kurudi na kisha kupokelewa na baba yake na kufanyiwa sherehe kubwa ndiye 'mwana mpotevu' au 2) yule mwana mwaminifu siku zote, lakini alikataa kuingia kwenye sherehe iliyoandaliwa na baba yake kwa madai kwamba baba yake amempokea ndugu yake aliyerudi na kumfanyia sherehe kubwa, wakati yeye ambaye amekuwa mwaminifu siku zote hajawahi kumkosea baba yake hajawahi kufanyiwa sherehe kama hiyo? Ukiona dalili hizo zinazokufikirisha hivyo, ujue ndiyo muda hasa tunaomhitaji Mwenyezi Mungu kuliko muda mwingine wowote na hata hao wanaohama dini na kusema hawamwamini Mungu: jiulize, kwa nini wakati ule waliamua kuwa waumini na kwa nini sasa wameamua kwenda kivyao vyao? Lini walikuwa sahihi: wakati ule au wakati huu? Kama wanadai walipotoshwa au walibatizwa kwa kufuata imani ya wazazi/walezi wao ni mambo mangapi ya wazazi wao wameachana nayo? Kama wakati ule hawakuwa sahihi, wanajuaje kwa sasa ndiyo wako sahihi - na ni kigezo gani wanachotumia?
 
Mbona unajichaganya sasa?
Mkristo ukizini umetenda dhambi au hujatenda?
Kama hujatenda sawa.
Ila kama umetenda dhambi si ni uasi wa sheria? Kutokusikiliza sauti ya Mungu ndani yako si ndo kutenda dhambi?
Tatizo ndugu yangu huelewi kuhusu mambo ya sheria na pia huelewi kuhusu mambo ya neema(kuongozwa na roho).

Unanifanya nianzie mbali sana.
Watu wanaotumia Biblia kama muongozo wako makundi mawili.Kundi la kwanza ni lile kundi linalofuata agano la Mungu na wanawaisrael Sinai.Kundi hili ni lile ambalo linatambua dhambi kwa kupitia amri ambazo Musa alipewa mlimani sinai. Kundi hili linaamini kuhesabiwa haki na Mungu kunapatikana kwa kuepuka kutenda yale yaliyokatazwa na Mungu kupitia Musa. Well wako sahihi lakini je inawezekana kumpendeza Mungu kwa kuzishika AMRI zake?(Hili ndo kundi unalolitambua wewe)

Kundi la pili ni la wale ambao wapo chini ya Agano la Neema.Watu hawa wametambua kuwa ni impossible kuzishika hizo AMRI ili upate kuhesabiwa haki.Namna pekee ya kumpendeza Mungu ni kumruhusu yeye mwenyewe akuongoze kwenye kila maamuzi unayokutana nayo mbele yako. Na kundi hili ndilo haliongozwi na sheria.Linaongozwa na Roho wa Mungu ndani yao.

Nakupa mfano

Jamaa mmoja (John) alikuwa na familia yake lakini alikuwa mlevi mbwa na hataki kununulia hata watoto wake nguo.Jirani yake (Chale) akachukua pesa za jamaa bila jamaa kujua akawanunulia nguo watoto wa jamaa na kuwalipia ada.

Kwa watu wanaoongozwa na sheria Chale amefanya dhambi,ingekuwa ni heri kwa chale awaache tu watembee uchi kuliko alichokifanya maana ameiba hivyo ametenda dhambi.

Kwa watu wanaoongozwa na Roho chale hakufanya dhambi kwa sababu upendo kwa wale watoto umemsukuma kufanya alilofanya ili kwasitiri wale watoto.(Note Chale amewasaidia hawa watoto kupata haki yao kutoka kwa baba yao)

Kwenye Biblia Daudi alikula mikate ya hekaluni ambayo kwa sheria ya Musa lilikuwa ni kosa kubwa sana lakini hakuhesabiwa dhambi kwa sababu alifanya jambo kubwa zaidi la kuokoa uhai wake na wa wale aliokuwa nao.Kama angeamua kuongozwa na sheria basi pengine angelikufa na njaa.Lakini aliamua kuongozwa na roho wa Mungu ndani yake akala yeye na watu wakaokoka.

Kuasi ni kudisobey sauti ya Mungu ndani yako.Sio kudisobey sheria.

Nimeongea kwa ufupi sana.Hii opic ni kubwa mno.
 
Mbona unajichaganya sasa?
Mkristo ukizini umetenda dhambi au hujatenda?
Kama hujatenda sawa.
Ila kama umetenda, dhambi si ni uasi wa sheria?
Kutokusikiliza sauti ya Mungu ndani yako na ukaenda kinyume si ndo kutenda dhambi? Na adhabu si ipo?
Kuzini ni dhambi sawa,na tumejua kupitia amri za Mungu zilizotolewa Sinai sawa,ngoja nikuulize kabla Amri hazijatolewa Sinai hapakuwa na Uzinzi?Au watu walijuaje kama hii ni dhambi na hii sio dhambi? Au unataka kusema hapakuwa na dhambi?

Nakuuliza haya kwa sababu unasisitiza kutokutii sheria ndiyo dhambi. Sasa tangu Adam,Nuhu,Abrahamu na wanaye mpaka wanawaisrael kabla ya kushushiwa sheria sinai walikuwa hawafanyi dhambi?kama walikuwa wanafanya niambie wamekiuka sheria zipo hizo?
 
Mungu alimuumba Malaika na Free will(kama ambavyo alimuumba mwanadamu na free will).Kuwa na Free will maana yake Mungu anataka umwabudu kwa kupenda ndo maana Mungu hakuumba Robots tu na kuziprogram kumpenda na kumwabudu.

Lakini kuwepo kwa Free will kunakwenda sambamba na kuwepo Consequences.Kila choice utayofanya inakuwa na matokeo ambayo unfortunately hayako kwenye maamuzi yako.Mfano una hiyari ya kuweka kidole kwenye moto au kutokuweka (umeexercise free will) lakini kuungua au kutokuungua sio maamuzi yako (Consequences).

Shetani Lucifer ambaye alikuwa ni sehemu ya Malaika akatamani yeye kuwa katika nafasi ya Mungu hivyo akastage rebelion Mbinguni na theluthi moja ya malaika wakaungana naye.
Na Mungu akamfukuza Mbinguni.

Binadamu pia aliwekewa free will,kama Mungu angemwekea binadamu options zilizonjema tu mbele yake tungesemaje palikuwa na uwezo wa kuexercise free will?Maana yake ni kwamba kama pangekuwa hakuna choices tofauti tungesemaje kuwa tumemchagua Mungu?

Pia choices za kutenda uovu zilikuwepo kabla Shetani hajaja kumshawishi mwanamke (Mti wa ujuzi wa mema na mabaya ulipandwa na ulikuwepo bustanini).Shetani alikuja kumshawishi mtu kuchagua kula tunda(hakuleta tunda).

Hivyo hatuwezi kumlaumu Mungu kumwekea Shetani Free will pia hatuwezi kumlaumu Mungu kutuwekea Free will.Lakini we are nothing compared to him hivyo hatuwezi kumpangia what will happen kama tukimkataa atufanye nini au nini kitokee.
hizo ni ngonjera za kuhalalisha uongo mkubwa!!Eti free will ya rebellion wakati hakuwepo shetan mwingine hiyo tamaa ya madaraka itatokea wapi kama wazo la uovu halipo akilini????Chenga za mwili hizi!!!!HATA SASA HAKUNA FREE WILL ZAIDI YA USHETANI NA UUNGU UNAO TAWALA KWENYE ULIMWENGU WA KIROHO TUNAOPAPASA KUUJUA!!!
 
hizo ni ngonjera za kuhalalisha uongo mkubwa!!Eti free will ya rebellion wakati hakuwepo shetan mwingine hiyo tamaa ya madaraka itatokea wapi kama wazo la uovu halipo akilini????Chenga za mwili hizi!!!!HATA SASA HAKUNA FREE WILL ZAIDI YA USHETANI NA UUNGU UNAO TAWALA KWENYE ULIMWENGU WA KIROHO TUNAOPAPASA KUUJUA!!!
Kama huelewi concepts za FREE WILL na kama unakataa uwepo wa FREE WILL na unaita ngonjera basi hakuna namna utaelewa.

Your Cup is Full Already.
 
Kama huelewi concepts za FREE WILL na kama unakataa uwepo wa FREE WILL na unaita ngonjera basi hakuna namna utaelewa.

Your Cup is Full Already.
Haiwezekani free will ikachagua uovu wakati shetani hayupo na mungu yupo tayari!!!!Kumbuka shetani hakuwepo bali mungu!!sasa nafsi ya malaika mkuu inachaguaje uovu wakati chanzo cha uovu hakipo??kwann asichague mema tu ambayo huyo mungu yupo ndio anaesimamia kila kitu????Ndio maana nasema Ni Ngonjera tupu hizi mambo!!!And i can assure you that my cup is fullest and dusted done!!!
 
Haiwezekani free will ikachagua uovu wakati shetani hayupo na mungu yupo tayari!!!!Kumbuka shetani hakuwepo bali mungu!!sasa nafsi ya malaika mkuu inachaguaje uovu wakati chanzo cha uovu hakipo??kwann asichague mema tu ambayo huyo mungu yupo ndio anaesimamia kila kitu????Ndio maana nasema Ni Ngonjera tupu hizi mambo!!!And i can assure you that my cup is fullest and dusted done!!!
Tatizo kaka unalazimisha kuwa chanzo cha uovu ni shetani kitu ambacho sio cha kweli. Mungu ametuumba kwa mfano wake na tunatambua kuwa Mungu anataka heshima,kupendwa,kuabudiwa na kutukuzwa. Basi kama tumeumbwa kwa mfano huo its natural kutambua kuwa hiyo haja na sisi tumeirithi(angels included). Na haja hiyo ndiyo iliyomprompt shetani kuasi.(Alitamani kuwa kama Mungu).He was with God so he understand the Beauty of being God himself he didn't need anybody kumshawishi. So he sinned against God.

Humans was happy with what they have.Lucifer came to try to stir them into sinning.He tried to make them feel that they can fulfil that desire from inside,desire of being respected and worshiped.If you remember correctly Shetani aliwaambia wanaweza kuwa kama Mungu.That wasn't new desire to humans its was just domant.He actived that desire by making it seem possible.

So my friend Lucifer didnt need anyone to stir him into rebelion.That innate nature made him exrcise his will and went against God. And Later Lucifer used that same innate nature humans have to stir them into exercising their free will to sin against God.
 
Kuzini ni dhambi sawa,na tumejua kupitia amri za Mungu zilizotolewa Sinai sawa,ngoja nikuulize kabla Amri hazijatolewa Sinai hapakuwa na Uzinzi?Au watu walijuaje kama hii ni dhambi na hii sio dhambi? Au unataka kusema hapakuwa na dhambi?

Nakuuliza haya kwa sababu unasisitiza kutokutii sheria ndiyo dhambi. Sasa tangu Adam,Nuhu,Abrahamu na wanaye mpaka wanawaisrael kabla ya kushushiwa sheria sinai walikuwa hawafanyi dhambi?kama walikuwa wanafanya niambie wamekiuka sheria zipo hizo?
Kasome biblia yako na historia ya imani yako vizuri.

Sheria zilikuwepo tangu uumbaji. Na kuzivunja ilikuwa dhambi kama ilivyo sasa.

Kabla ya musa palikuwepo sheria kama sheria ya kutokula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Wakati wa Musa zilikuwepo amri kumi za Mungu na mpaka sasa hizo sheria zipo.

Kinachokuchanganya wewe ni uhusiano wa uwepo wa sheria, kuokolewa kwa Neema na uwepo wa roho mtakatifu.

Sheria zipo, hazijawahi kuondoka. Zitakuwepo hata huko mbinguni unapotaka kwenda.
 
Kasome biblia yako na historia ya imani yako vizuri.

Sheria zilikuwepo tangu uumbaji. Na kuzivunja ilikuwa dhambi kama ilivyo sasa.

Kabla ya musa palikuwepo sheria kama sheria ya kutokula tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

Wakati wa Musa zilikuwepo amri kumi za Mungu na mpaka sasa hizo sheria zipo.

Kinachokuchanganya wewe ni uhusiano wa uwepo wa sheria, kuokolewa kwa Neema na uwepo wa roho mtakatifu.

Sheria zipo, hazijawahi kuondoka. Zitakuwepo hata
Sheria zipi unazozizungumzia wewe?ndo nakwambia Sheria kwa mara ya kwanza zimeletwa Kwenye mlima Sinai.Paliletwa Amri 10 na Ceremonial laws nyingine kama 600 hivi.Thats the Bible. Go and study all books of Moses (Torah) you will see what i am talking about.God never gave them rules or laws before Sinai.He guided their steps and let them exercise their free will.Those who chose wisely became great men of the Old and those who ignored well we know how the end was.

Najaribu kukufahamisha kuwa kilichokuwa kinamfanya mwanadamu atambue kipi cha kutenda na kipi cha kuacha sio sheria alizowekewa bali Roho wa Mungu alikuwa anaongoza hatua zao.

Kilichofanya wahesabiwe makosa ni kutokuitii ile sauti ya Mungu inayosema ndani yao.That is why tangia mwanzo nakuambia dhambi ni matokeo ya kutokutii sauti ya Mungu ndani yako.
 
Sheria zipi unazozizungumzia wewe?ndo nakwambia Sheria kwa mara ya kwanza zimeletwa Kwenye mlima Sinai.
Si kweli, labda kama hujui tafsiri ya neno sheria.

Sheria ya kwanza ni lile katazo la matunda ya mti wowote waweza kula, isipokuwa mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Hapo ndo mara ya kwanza binadamu anakutana na sheria na kuivunja.

Sheria ni mfumo wa kanuni, katazo, sharti, amri, maelekezo ambayo kwa kawaida hutekelezwa na jamii, taasisi, nchi, au kundi kupitia seti ya taasisi maalumu.

Sheria za MUNGU hazijawahi kutokuwepo, kilichoongezeka ni sheria kuu ya kwanza na ya pili, hukumu kupitia neema na roho mtakatifu kuongoza wakristo katika kuzifata sheria. FULL STOP.

37 Yesu akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’ 38 Hii ndio amri kuu, tena ni ya kwanza. 39 Na ya pili inafanana nayo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’ 40 Amri hizi mbili ndio msingi wa sheria zote na Maandiko ya manabii.”
 
Kukua kwa teknolojia ya mawasiliano kumewafanya watu kuwa wadadisi, kuweza kupata taarifa na mawazo tofauti nje ya dini zao na kuweza kufahamu uongo na utapeli mwingi uliopo kwenye dini. Pia kuna mikanganyiko mingi ndani ya maandiko ya kidini ambayo sio rahisi kusuluhishwa na wanaoitwa "wanazuoni".
 
Back
Top Bottom