Nini kipo nyuma ya ukuaji na ongezeko la watu wasiokuwa na dini?

Kutokuwa na dini sio kwamba hawaamini Mungu yupo. Dini ni taasisi tu ambazo siku hizi zimekuwa zikichukua pesa kwa waumini hadi anatoka damu. Dini na madhehebu yanatofuautiana taratibu, sala, miongozo, matumizi ya sadaka lakini Mungu ni mmoja na habadiliki. Kuliko kunyonywa hivi ni bora ubaki huna dini utajuana na Mungu siku ikifika. Dini sio Mungu na Mungu sio dini. Dini ni sawa na chama cha siasa tu
 
Kumsifia jewellery?
 
Dini ni uongo kama uongo mwingine,ipo kwa ajiri ya CODE OF CIVILIZATION tu.
 
Dini ililetwa na mzungu, kwanini mpaka leo bado kuna watu hawajielewi wakati walioleta dini kwa asilimia kubwa wameisha itupa kule
Siyo kuitupa tu. Bali kubadibadili yale maandiko yakidhi haja zao za kibinadamu kwa pande zote iwe Uislamu au Ukristo…
 
Siyo kuitupa tu. Bali kubadibadili yale maandiko yakidhi haja zao za kibinadamu kwa pande zote iwe Uislamu au Ukristo…
Lete uthibitisho kua Waislamu wamebadilisha maandiko
 
Baada ya kugundua kwamba dini ni madili ya watu. Mungu hayupo kwenye hizo dini, watu wameamua kumtafuta Mungu wa kweli. Turudi kwanza kwenye mila zetu za asili na kutafakari kwa makini. Hakuna imani ya asili inayoamini Mungu alimtoa mwanae sadaka.
 
Sio umasikini kwani, masikini anafikia mwisho wa upeo wa kufikiria, na kuamini kuwa kuna maisha baada ya kifo. Chukuwa utafiti utagundua masikini ndio washika dini duniani. Ulaya makanisa yamegeuka kuwa baa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…